Walinzi wa rais wetu fitness yao vipi?

Walinzi wa rais wetu fitness yao vipi?

Nani kakwambia ni wazembe??? Usidharau mtu kwa muonekano...dont judge a book by its cover my friend..hao watu wameiva wanajua ukujaribu utabroo...na Rais ana mambo mengi sio kila unauona hapo ni mlinzi wengine wana ditect hatari na wengine wanalinda sio kama mnavyodhani nyie
mwambie akawajaribu alete mrejesho
 
Toka lini walinzi wa Rais wakakimbizana na wahalifu?

Kumlinda Rais kunahitaji ukakamavu wa misuli?

Kumlinda Rais kunahitaji akili na Intellijensia ya hali ya juu basi. Hivyo vingine ni mbwe mbwe tu.
Kwahiyo kwa wenzetu ni mbwembwe ila sisi ndo tunajua?
 
Kwahyo unataka tuamini mtu mwenye kitambi na ambae umri wake umesogea kama hawa jamaa wetu ni wepes mno kuliko watu wasio na vitambi na wenye mazoezi?umeanza vizuri lakini umemaliza kienyeji sana Kwa mtazamo wako binafsi tu tena dhaifu ambao Haujazingatia data za kitaalam kama ulizotoa huko juu
Tofautisha mwili mkubwa na kitambi kitambi hata watu wenye mwili wa kawaida wapo wengine wana vitambi , pia unatakiwa kujua unapozungumzia ulinzi (protection) na usalama(security) unazungumzia matumizi ya AKILI,SILAHA NA MWILI

AKILI hapa ndio zinatumika zile zinazoitwa hisia 6 au "sixth sense"

Kila binadamu ana body sensitivity 3 ila wanausalama wanakwenda kusomea zingine tatu ndo inakuja kuwa 6 kwani unatakiwa kujua duniani kuna aina tatu za elimu

1 Elimu ya kidini
2 Elimu ya kidunia hii ndio tunafundishwa mashuleni
3 Elimu ya utambuzi elimu hii wanafundishwa watu wachache ambao wanakuwa trained kwa ajili ya kudeal na watu wenye elimu hzo mbili yani ya dini na kidunia

nikutajie kuanzia hisia ya 4 mpka 6 kwa ufupi
4 Ni uwezo wa kumsoma mtu kwa sura yake
kwa kumwangalia tu tutakubaliana ya kuwa sura inaongea sura inaweza elezea kila kitu kinachotokea ndani ya mwili wako mfano furaha,huzuni,shauku,hofu,jazba na kukata tamaa

5 Ni uwezo wa kumsoma mtu kupitia moyo wake hapa napenda kuwaelezea kidogo na kuwapa mfano juu ya usomaji wa moyo mtu aliyeiva ktk maswala ya ujasusi anauwezo mkubwa wa kujua ata anapomtongoza mwanamke anajua atajibu nini au anawaza nini kihisia juu yake kwan lipo somo maalumu kwa ajiri ya wanawake ktk tasinia ya ujasusi inamtambua mwanamke kama ni silaha ya maangamizi ( Weapons of Mass Distraction)

6 Ni uwezo wa kumsoma mtu ndani ya ubongo pia tunatakiwa kujua ubongo ndio command center ya mwili wa kila mwanadamu command zote zinatoka ndani ya ubongo na ukiweza kufuzu vizuri somo ili ambazo pass mark zake ni 70% utakuwa unawezo mkubwa sana wa mambo wa ujasusi

SILAHA hapa inatakiwa kujua matunizi sahihi ya silaha za aina 5 tofauti pili huwe na uwezo wa kulenga shabaha kwani kila risasi utakayo piga ni lazima uhit target , kwani kazi yako unaifanya kwenye mikusanyiko ya watu wengi kwani mara nying viongozi huwa kwenye mikusanyiko ya watu so ni lazima adui tu ndie adhibitiwe si watu wasio na hatia


MWILI hapa ndo linapokuja swala fitness ya mwili na fitness inapatikana kwa kufanya mazoezi ya ukakamavu si mazoezi ya kujaza au kupunguza mwili sasa ninaposema wepesi inatakiwa huwe mwepesi wa mwili na akili (smart thinker) na ndo maana nakwambia hakuna kipengere kinachosema mlinzi wa viongozi ni lazima huwe ni mwembamba au mwili mkubwa ila unatakiwa huwe mkakamavu na utayali wa kukabili tukio lolote kwa wakat wowote
 
Halafu kuna hili la askari polisi hao wapya wanaorandaranda mitaani na kuongoza magari, mbona wana miili kidogo sana maumbo yao ni madogo mno , sidhani kama wataweza kumdhibiti mtu mwenye kilo tisini wale, sijui kwa nini wale maaskari polisi wa miaka ile ya themanini na mwanzoni mwa tisini kama watakuwepo tena, hawa wa sasa niliwaona huko TZ, mpaka wanangu wakawa wanawashangaa eti ndio askari wetu mbona wadogo hivyo.
Hilo kweli linasikitisha maumbo yamekuwa madogo sana enzi zile anakuja askari unapigwa tanganyika jeki (tanganyika jack )unatembelea vidole jamaa walikuwa mapande ya watu akikwambia ongoza kituoni unaenda .Sasa hawa inabidi tu atumie diplomasia kuwa mzee eti eti nimetumwa eti eti Ocs anakuhitaji pale kituoni huku kaweka mikono kichwani.
 
acheni ujuaji kwenye ulinzi wa mkuu wa nchi,
mleta mada elewa kuwa ulinzi wowote hasa wa mtu mhimu kama rais uko katika ringi 'ring' kuu tatu mhimu hasa kulingana na mazingira aliyopo mlindwa(esp.rais)
1.Ringi ya tatu.
hii ni ringi ya nje ambayo ndio nguzo mhimu kabisa kwenye ringi zote zilizobaki, ringi hii inajumuisha nguvu kazi ya wanausalama hasa wa intelijensia ambao kazi yao kuu ni kunasa au kupeleleza usalama wa mazingira yaliyo karibu na rais na kutuma taarifa kwenye ringi ya kwanza na ya pili kupitia redio maalum za kiusalama ( huonekana wazi kwenye sikio mojawapo kwa walinzi kama earphone hivi) katika hali tulivu ringi hii haijumuishi silaha nzito bali ni nyepesi kama bastola n.k ila ktk hali isiyo salama huhusisha silaha nzito za kujihami aghalabu submachines kama UZI, AKs (fupi sana) n.k

2.Ringi ya pili
hii ni co-ordination ring kati ya ringi ya tatu na ya kwanza, ringi hii huundwa na kikosi cha kujihami na kushambulia chenye nguvu kazi ya maafisa wachache wenye uwezo wa juu kimapambano ( ELITE PERSONNELS), kazi kubwa ya ringi hii ni kupokea taarifa kutoka C yaani ringi ya 3 na kuzifanyia kazi iwapo inahitajika, mfano mhalifu anaweza kuhisiwa na ringi ya 3 na hivyo ringi ya 2 hujulishwa ili kuchunguza au kureact directly kwa adui, mfano adui anapohisiwa mkutanoni ambapo rais anahutubia nguvu kazi kutoka ringi ya pili humsogelea adui na kukaa naye karibu( kwenye kundi la watu) ili kuweka urahisi wa ku intercept mashambulizi kutoka kwa huyu adui, hii huundwa na nguvu kazi yenye uwezo mkubwa katika medani za kivita na intelijensia mf commandos.

1.Ringi ya kwanza,
Ringi hii ndio iliyozoeleka kuonekana machoni pa wengi, ni ringi inayojumuisha wanaoitwa 'VIP BODYGUARDS' ringi hii humjumuisha mpambe wa rais yaani ADC na nguvu kazi ya wabobezi wa close combat ambao ni commandos, kazi yao kubwa kudhibiti any physical contact kwa rais, wako alerted sana na hupokea miongozo toka kwa wanausalama toka ringi ya 2, na 3, kupitia redio,
Pia iwapo kutatokea fujo au jaribio kumdhuru kiongozi ringi hii hufanya kazi ya uokoaji ( rescue unit) na kumuondosha rais eneo hilo huku wakijbu mapigo na kuondoka nae huku wakiiacha ringi ya pili ikiendelea kudhibiti tishio kwa mapigano ya silaha, endapo mapigano hayo yatakuwa magumu ringi ya pili huhitaji msaada kutoka vyombo vingine vya usalama kama polisi na jeshi.
ikumbukwe kuwa ringi hii ya kwanza pia hubeba silaha ndogo(portable) zenye ufanisi zaidi.
ULINZI WA RAIS SI SUALA JEPESI WALA NADHARIA ZA KISIASA, NI UTENDAJI HALISI

Nb; RINGI HIZI NI KULINGANA NA HALI, SIFA, YA ENEO HUSIKA INAWEZA IKAZIDI HAPO

THAKS, HAVE IT THOUGH SOME OF IT!
 
Mkuu huwezi kukimbia intelijensia uliopo hapo Huwezi kimbia maana eneo lote unaloona liko open na magari yamepaki kuna watu mule ogopa kuona gari tinted limepaki kwene sehemu hizo wanausalama wanaratibu eneo zima kwamfano hapo kwa shoe shine anaeshangaa kule kwene gari uyo sio mtu wakawaida wote na yule pili yke pia anaonekana kama mtu anashangaa shangaa tu wote wapo kazini wale mkuu japo kwa haraka haraka huwezi jua... sasa kwastairi iyo utakimbilia wapi mkuu kama mbio ndio hoja yako Mkuu...
 
acheni ujuaji kwenye ulinzi wa mkuu wa nchi,
mleta mada elewa kuwa ulinzi wowote hasa wa mtu mhimu kama rais uko katika ringi 'ring' kuu tatu mhimu hasa kulingana na mazingira aliyopo mlindwa(esp.rais)
1.Ringi ya tatu.
hii ni ringi ya nje ambayo ndio nguzo mhimu kabisa kwenye ringi zote zilizobaki, ringi hii inajumuisha nguvu kazi ya wanausalama hasa wa intelijensia ambao kazi yao kuu ni kunasa au kupeleleza usalama wa mazingira yaliyo karibu na rais na kutuma taarifa kwenye ringi ya kwanza na ya pili kupitia redio maalum za kiusalama ( huonekana wazi kwenye sikio mojawapo kwa walinzi kama earphone hivi) katika hali tulivu ringi hii haijumuishi silaha nzito bali ni nyepesi kama bastola n.k ila ktk hali isiyo salama huhusisha silaha nzito za kujihami aghalabu submachines kama UZI, AKs (fupi sana) n.k

2.Ringi ya pili
hii ni co-ordination ring kati ya ringi ya tatu na ya kwanza, ringi hii huundwa na kikosi cha kujihami na kushambulia chenye nguvu kazi ya maafisa wachache wenye uwezo wa juu kimapambano ( ELITE PERSONNELS), kazi kubwa ya ringi hii ni kupokea taarifa kutoka C yaani ringi ya 3 na kuzifanyia kazi iwapo inahitajika, mfano mhalifu anaweza kuhisiwa na ringi ya 3 na hivyo ringi ya 2 hujulishwa ili kuchunguza au kureact directly kwa adui, mfano adui anapohisiwa mkutanoni ambapo rais anahutubia nguvu kazi kutoka ringi ya pili humsogelea adui na kukaa naye karibu( kwenye kundi la watu) ili kuweka urahisi wa ku intercept mashambulizi kutoka kwa huyu adui, hii huundwa na nguvu kazi yenye uwezo mkubwa katika medani za kivita na intelijensia mf commandos.

1.Ringi ya kwanza,
Ringi hii ndio iliyozoeleka kuonekana machoni pa wengi, ni ringi inayojumuisha wanaoitwa 'VIP BODYGUARDS' ringi hii humjumuisha mpambe wa rais yaani ADC na nguvu kazi ya wabobezi wa close combat ambao ni commandos, kazi yao kubwa kudhibiti any physical contact kwa rais, wako alerted sana na hupokea miongozo toka kwa wanausalama toka ringi ya 2, na 3, kupitia redio,
Pia iwapo kutatokea fujo au jaribio kumdhuru kiongozi ringi hii hufanya kazi ya uokoaji ( rescue unit) na kumuondosha rais eneo hilo huku wakijbu mapigo na kuondoka nae huku wakiiacha ringi ya pili ikiendelea kudhibiti tishio kwa mapigano ya silaha, endapo mapigano hayo yatakuwa magumu ringi ya pili huhitaji msaada kutoka vyombo vingine vya usalama kama polisi na jeshi.
ikumbukwe kuwa ringi hii ya kwanza pia hubeba silaha ndogo(portable) zenye ufanisi zaidi.
ULINZI WA RAIS SI SUALA JEPESI WALA NADHARIA ZA KISIASA, NI UTENDAJI HALISI

Nb; RINGI HIZI NI KULINGANA NA HALI, SIFA, YA ENEO HUSIKA INAWEZA IKAZIDI HAPO

THAKS, HAVE IT THOUGH SOME OF IT!
Majibu mazuri sana lakini je muonekano wa wale walinzi wanaomzunguka rais wa vitambi na wanaonekana umri wao umesogea kias unaweza kukidhi makabiliano ya Ana Kwa Ana inapotokea ringi ya kwanza na ya pili zimepenywa?au kwasababu ya mazoea ya amani na utulivu nchini suala la body fitness ya hawa walinzi wanaomzunguka rais halizingatiwi sana?Kwa muonekano wao unahisi wanaweza makabiliano ya kimapigano ya mwili Kwa uharaka unaohitajika kabla ringi ya pili na tatu hawajaingilia kati na kutoa fursa Kwa ringi ya kwanza kuondoka na rais?
 
MAGUFULI & KA.jpg


UKIONDOA RAIS KABILA, MAGUFULI NA MAMA SAMIA SULUHU, WENGINE WOTE NI WALINZI, PIA UKICHUNGUZA VIZURI HUYO KUSHOTO NYUMA YA RAIS MAGUFULI YUKO EQUIPPED KWA SILAHA ZA MOTO.
 
Majibu mazuri sana lakini je muonekano wa wale walinzi wanaomzunguka rais wa vitambi na wanaonekana umri wao umesogea kias unaweza kukidhi makabiliano ya Ana Kwa Ana inapotokea ringi ya kwanza na ya pili zimepenywa?au kwasababu ya mazoea ya amani na utulivu nchini suala la body fitness ya hawa walinzi wanaomzunguka rais halizingatiwi sana?Kwa muonekano wao unahisi wanaweza makabiliano ya kimapigano ya mwili Kwa uharaka unaohitajika kabla ringi ya pili na tatu hawajaingilia kati na kutoa fursa Kwa ringi ya kwanza kuondoka na rais?
Kwa ufupi tu nikujibu kuwa hao unaohisi si lolote kwa mionekano ya vitambi ni maasikarijeshi idara intelijensia na ulinzi, wana uwezo mkubwa na viwango vyao vinakidhi kumlinda rais in any cost, wako fit kuanzia hand to hand na matumizi ya silaha za moto, haingii akilini kama taifa letu licha ya kuwa na maasikari ( makomandoo) walioiva wawekwe watu wasiojiweza kumlinda mkuu wa nchi, hao ni moto wa kuotea mbali,
suala la umri, unachokisema hakiendani na uhalisia kwa kuwa:
1. hujui umri sahihi unaofaa kuanza kumlinda rais na kustaafu kazi hiyo,
2. hujui namna kazi hiyo inavyofanywa/kutekelezwa

swali kwako mkuu, hebu taja umri hasa ni upi unaofaa kuanza kumlinda rais na upi unafaa kustaafu kazi hiyo?
 
1 Elimu ya kidini
2 Elimu ya kidunia hii ndio tunafundishwa mashuleni
3 Elimu ya utambuzi elimu hii wanafundishwa watu wachache ambao wanakuwa trained kwa ajili ya kudeal na watu wenye elimu hzo mbili yani ya dini na kidunia

Unazungumziaje kibao alichopigwa Mwinyi?
 
rais mstaafu huyo hana ulinzi mkali kama wa rais awapo madarakani
 
Hii simple sana kupruvu kama wako fiti ama matumbo tu. Vizia rais akiwa sehemu halafu fanya uwezelo umtemee mate kishe uje uhitimishe mjadala wa uzi wako kwa kuweka hitimisho sahihi.
 
View attachment 465702

UKIONDOA RAIS KABILA, MAGUFULI NA MAMA SAMIA SULUHU, WENGINE WOTE NI WALINZI, PIA UKICHUNGUZA VIZURI HUYO KUSHOTO NYUMA YA RAIS MAGUFULI YUKO EQUIPPED KWA SILAHA ZA MOTO.
Yeah nikweli mkuu lakini hapa watu wengine ukiwaambia ivo wanaona kama vile askari ni wachache au ilo eneo ndo linalindwa na wanaoonekana tu kumbe wengine wako pembeni kabisa ila wao wanatambuana
 
Wapo vzur sana aiseee weweeeee acha kabsa walinzi wetu ni kiboko,
Maneno haya sio sawa na yale ya kusifia jeshi letu ni kiboko Africa wakati mara ya mwisho kupigana vita ilikuwa ni dhidi ya Iddi Amin, ambayo pasipo msaada wa wananchi wa Uganda ambao hawakuwa wanaridhika na utawala wake, pengine tungechezea kichapo.
 
Maneno haya sio sawa na yale ya kusifia jeshi letu ni kiboko Africa wakati mara ya mwisho kupigana vita ilikuwa ni dhidi ya Iddi Amin, ambayo pasipo msaada wa wananchi wa Uganda ambao hawakuwa wanaridhika na utawala wake, pengine tungechezea kichapo.
Thibitisha kua sio imara?
 
Halafu kuna hili la askari polisi hao wapya wanaorandaranda mitaani na kuongoza magari, mbona wana miili kidogo sana maumbo yao ni madogo mno , sidhani kama wataweza kumdhibiti mtu mwenye kilo tisini wale, sijui kwa nini wale maaskari polisi wa miaka ile ya themanini na mwanzoni mwa tisini kama watakuwepo tena, hawa wa sasa niliwaona huko TZ, mpaka wanangu wakawa wanawashangaa eti ndio askari wetu mbona wadogo hivyo.
40% ya watoto wanakabiliwa na utapiamlo kimo kitatoka wapi?
 
Hii simple sana kupruvu kama wako fiti ama matumbo tu. Vizia rais akiwa sehemu halafu fanya uwezelo umtemee mate kishe uje uhitimishe mjadala wa uzi wako kwa kuweka hitimisho sahihi.
Me nilidhani utamshauri amzabe kibao au ampige singi? Hapo itakuwa ni kipimo sahihi.Akifaulu inamaana hao jamaa ni maboya, kwani italeta picha kuwa hata kisu anaweza kuchomwa wakiwepo.
 
Kwa ufupi tu nikujibu kuwa hao unaohisi si lolote kwa mionekano ya vitambi...

Unataka kusema tangu anapitia mafunzo kitambi kilikuepo? Kama hakikuepo kwanini sasa hivi kipo?
Kama kilikuepo, inawezekana vipi mtu anayepitia mafunzo ya ufiti akatoka kitambi?
 
Back
Top Bottom