Walioitwa 'stupid' na Rais bado wapo ofisini wanakula kiyoyozi!

Walioitwa 'stupid' na Rais bado wapo ofisini wanakula kiyoyozi!

Magu naye alikuwa na majizi yake aliyoyapa ushirikiano. Kuna walioficha hela za plea bargaining, kuna waliopora mchana kina Sabaya na Makonda. Kuna Kakoko na yeye mwenyewe Magufuli.
Yeah alikuwa mwizi kupitia washkaji zake na vijana wake, binafsi nimeongelea ishu ya maamuzi ya hapo kwa papo aliyokuwa akiyafanya Kama CinC
 
Aliyewaita kuwa stupids kaishia hapo, wakati ana mamlaka ya mwisho kabisa kuwawajibisha. Kwanini wao wahangaike?

Huko walipo wanajifariji kinafiki kwamba sio Mimi ni Fulani, hivyo hawawezi hata kujisuta nafsini mwao, watawezaje kujiuzulu?

Rais wetu hana uwezo wakupambana na mafisadi. Angestaafu tu mwaka 2025. Adhabu ya fisadi Tanzania ni kuitwa stupid.
 
Btw, ununuzi wa ndege kama sijakosea ulihamishiwa ofisi ya Rais , tangu enzi za awamu ya Tano .Kwa hiyo, na hiyo inaweza kuwa kizungumkuti' aiseee...kaazi kwelikweli.

Ajiuzuru tu huyo mama. Kaniboa Sana. Mtu anaiba benki tano zote hata jina hamlijui. Umebaki kuita watu stupid halafu waendelee kuiba.
 
Wachache wataelewa hili

Huyo waziri wa fedha anajua fika kila senti inaenda wapi, gavana anajua yote
Mazuzu tunapelekwa kwenye ushindi tena
Tunajua uchaguzi una gharama nyingi sana lazima watu wabebe magunia ya hela kuwapa wenye tamaa

Na mwisho wengine wanaambulia hata kofia yenye chapa na t-shirt inayochapishwa China

Kama ni hivyo Basi wizi uhalalishwe. Kwamba ukiiba kwa ajiili ya CCM kubaki madarakani sio wizi. Sheria itambue hivyo.
 
Sio kila jambo la kiserikali linatangazwa hadharani.

Sio kwa serikali hii ya stupid. Mbona wametueleza hayo maripoti yao. Wangekaa nayo huko kwenye Siri. Mntuambia watu wamepiga bilioni 10 kwenye vishikwambi, halafu baadae mnakuja kusema sio kila Jambo la serikali linatangazwa Nani aliwauliza?
 
Sawa, ila tuwape kina nani sasa mzee baba, sbbu wengine tunaogopa watasaini makubaliano na LGBTQ...[emoji2960][emoji2960][emoji2960]

Wewe endelea kuogopa hujakatazwa. Huwezi kusign LGBTQ ukabaki salama Tanzania.
 
Nchi ya kisenge saana hii, usikute hao wezi ni watu wake wa ndani kabisa, akija gundua hana ujanja..

Wanatujua sisi watz ni mapoyoyo tunapiga kelele mtandaoni bila matendo, na huku mtandaoni keshokutwa tutaletewa habari diamond abadili dini au atamani angezaliwa mwanamke, habari ya CAG inayeyuka.
 
Ma.ma: You are our President, our guide and our leader. Tunakuamini na tunakukubali. Piga Kazi na usipuuze ushauri ushauri ila usiendekeze kila lisemwalo. They want to see you derail ili wafurahi....HASBIYA WALLAHI WANI' LMAL WAKIL...They will not succeed biidhnillah...RAMADHAN KARIM
Unaongelea derail?. Mbona kasha derail zamani Sana. Yani adhabu ya mwizi wa bilioni kumi za vishikwambi Ni stupid. Hizo ripoti zao wazisomee chumbani kwao.
 
Mimi kinachonishangaza ni ukimya wa vyo habari ..haya mambo ya auditing report y CAG hata hayawahusu

Vyombo vya habari vipo kwaajiri ya kupongeza na kusifu serikali. Umesahau yaliyomtokea Gerald Hando?
 
Naomba Nikuambie kuwa Ile Kauli ya Rais Kuwa "Watupishe" ni AMRI na hao wahusika kama bado hawajatupisha inamaanisha kuwa hawajaitii AMRI Ya Rais. Hivyo basi Vyombo husika vya kuwachomoa huko ofisini vinapaswa kufanya kazi yake labda kama pia vinadharau Hiyo AMRI Ya Rais.

Kile kipindi Cha EPA Rais Kikwete alitamka "Watupishe" na mara hiyo hiyo kina Tubaijuka "walitupisha".

Watupishe ndio Nini?. Akina Mbowe walitangzwa hadharani ni magaidi tena BBC, lakini wezi wa bilioni wanaambiwa stupid mtupishe. Serikali ya uonevu.
 
"stupid" ni tayar onyo wamepew sasa unatak wapew adhabu mara Ngap mkuu


Na hili mkalitazame[emoji1783]

Unampaje onyo mtu aliyeiba bilioni kumi ya vishikwambi?. Una maana asiibe Tena au asiibe pakubwa Kama mwanzo.
 
Maza aliwaomba watupishe ni uamuzi wao kutupisha au kuendelea kula mema ya nchi. Ombi sio amri.
 
Back
Top Bottom