Waliomsindikiza Mwalimu Nyerere safari ya kwanza UNO 1955

Waliomsindikiza Mwalimu Nyerere safari ya kwanza UNO 1955

Mzee Mohammed hizi historia zako zilizoegemea upande wa waislamu sisi wengine hazitufai kabisa. Ingelikuwa sisi ni waislamu tungetumia maneno manne kama ilivyo ada kwenu (hii historia haramu kwetu).

Historia za Nchi yetu Tanzania hazijajengwa kwa misingi ya dini wala ukabila na hazitokaa zijengwe hivyo.
Leo nakukatisha tamaa hatuzihitaji historia zako tafuta kazi nyingine.
Takakeisho...
Wewe kama haikufai wako inaowafaa sasa hili ni somo yaani "field of enquiry," na yeyote ana haki ya kutafiti na kuandika anachopenda.

Wala hii si historia yangu kama ulivyoandika.
Hii ni historia ya uhuru wa Tanganyika.

Mimi nimeamua kuandika historia hii kwa kuona jinsi ilivyokuwa muhimu kuhifadhiwa na zaidi inawahusu wazee wangu ambao walikuwa mstari wa mbele kupambana na ukoloni.

Kitabu kimekuja na elimu mpya katika historia ya Tanganyika kwa kuandika historia za wazalendo ambao historia iliwafuta kabisa.

Wewe ulikuwa unaijua historia ya Sheikh Hassan bin Ameir au Hamza Mwapachu au Abdul na Ally Sykes na baba yao Kleist Sykes?

Umeghadhibika kwa kuwa historia inataja Waislam?
Unasema historia hii haramu kwenu ningependa kujua uharamu wake ni upi?

Historia iliyokuwa inafahamika ni ya Mwalimu Julius Nyerere peke yake.
Hii kwako ndiyo historia halali?

Ukiwa huipendi hujalazimishwa kusoma wala kununua kitabu.
Kitabu sasa kina miaka 21 na kinakwenda toleo la nne.

Hii maana yake ni kuwa kitabu kinapendwa.
 
Mzee Mohammed hizi historia zako zilizoegemea upande wa waislamu sisi wengine hazitufai kabisa. Ingelikuwa sisi ni waislamu tungetumia maneno manne kama ilivyo ada kwenu (hii historia haramu kwetu).

Historia za Nchi yetu Tanzania hazijajengwa kwa misingi ya dini wala ukabila na hazitokaa zijengwe hivyo.
Leo nakukatisha tamaa hatuzihitaji historia zako tafuta kazi nyingine.

ndio maana ni nadra sana sana kukuta kitabu au makala imeandikwa kichwa cha habari cha kibaguzi kama vile "Jinsi Mkiristo Nyerere alivyosaidia nchi nyingine za Afrika kudai uhuru" hizi lugha za kutumia neno Muislamu au Mkiristo ni kauli za kibaguzi na za kidini sana na ni hatari kwa taifa liliojijengea misingi ya kupinga udini, ukabila e.t.c
 
Basi haya tufanye hivi, kwenye hili bandiko lako kila penye jina Nyerere litowe uweke jina la muslim mwenzako maana naona utaki kulisikia hivyo jina la Nyerere kwa sababu hakuwa mwenzenu.

Hacha chuki za kinga wewe utakatifu wa kikatoliki una taratibu zake takatifu pia usiuweke kwenye mambo yako ya kijinga.

Kama vipi na wewe kajilipue huko upande wako watakupa tu utakatifu maana kujilipua ndiyo jihadi sala yenu kuu.
Hakuna kama Marehemu Nyerere. Au hupendi hilo?
 
Ndio utumie dini yao kuwasilisha historia zao kwa hadhira?
Ungepungukiwa nini usingetaja dini zao ukaeleza tu historia zao zilizotukuka?

Au nawe umekuwa mmisionari wa kueneza dini kwa njia yako maana wale wa zamani walitumia njia ya utumwa
Takakeusho,
Nimekueleza vizuri sina sababu ya kubishana hasa kwa kuwa kitabu hiki kimetoka toka 1998.

Kukizungumza leo kuna tija gani?
 
Mzee Mohammed hizi historia zako zilizoegemea upande wa waislamu sisi wengine hazitufai kabisa. Ingelikuwa sisi ni waislamu tungetumia maneno manne kama ilivyo ada kwenu (hii historia haramu kwetu).

Historia za Nchi yetu Tanzania hazijajengwa kwa misingi ya dini wala ukabila na hazitokaa zijengwe hivyo.
Leo nakukatisha tamaa hatuzihitaji historia zako tafuta kazi nyingine.

Mwambie huyu Mzee Mohamed Said anatuletea mambo ambayo hayajawahi kutokea kabisa na watu ambao hawajawahi kuwepo kabisa.

Takakeisho lete historia ya kweli tumnyamazishe kabisa maana huyu mzee "anazingua".
 
Sheikh nafikiri usingekuwa unakutana na hoja za watu kudai kwamba wewe ni Mdini kama makala zako zingebeba uwiano kwenye mizani ya makala yako, sidhani kama harakati za kupigania uhuru zilifanywa na waislamu pekee ingawa sikatai kwamba kwa miaka ya 1950s ukanda wa pwani ulijaa waisilamu lakini katika TANU kuna viongozi wengi tu wa dini na imani tofauti walipata kuwepo. suala la kitabu chako kuwepo mwaka wa 21 sasa na kufikia toleo la 4 ni jambo jema na linaloonesha kinakubalika na najua unafahamu vizuri wanunuaji wakubwa wa hicho kitabu ni watu wenye imani na dini fulani unayoifahamu.
 
Ndio utumie dini yao kuwasilisha historia zao kwa hadhira?
Ungepungukiwa nini usingetaja dini zao ukaeleza tu historia zao zilizotukuka?

Au nawe umekuwa mmisionari wa kueneza dini kwa njia yako maana wale wa zamani walitumia njia ya utumwa
Kwanza analeta dini zao kama vike walikuwepo. Mpe bwana ya wa dini yako aelewe kuwa walikuwapo na hamuwataji tu.
 
kwamba,"Mwalimu JULIUS NYERERE raisi wa kwanza wa nchi yetu alikuwa kiungo pekee kati ya chama na serikali na kanisa Katoliki. Uhusiano huo unaelezwa kwanza kama msingi wa kuelewa jinsi gani na kwa kiasi gani viongozi wa kanisa walivoingilia kati maendeleo ya siasa hapa Tanzania". Na kwa msingi huo viongozi wa kanisa wamekuja kuwa na nafasi ya pekee Tanzania na wamefanya hivyo wakizingatia kwa kukuwa Uislamu.''- DK.Sivalon ameelezea ndani ya kitabu chake
(kanisa katoliki na siasa tanzania.....................)

Kwa Hili Lazima awe Mtakatifu!!!!!!!!!!!!!!
Hili ndio tatizo lenu kubwa akina muhamad yaani mnaweka imani zenu pembeni mnaanza kupambana na imani zingine zisizowahusu. Bahati mbaya sana kwa sababu ya kuwajua kwamba nyinyi ni wajinga/punguani, hao mnajilazimisha kupambana nao mara zote wamekuwa wakiwadharau na kuwa-ignore, mwisho mnajikuta hamna jinsi.

Kwa kuwa mnakuwa mmeisha poteza mwelekeo kiimani basi mnajikuta mnapigana na ku-umizana wenyewe kwa wenyewe. Ndio maana nchi nyingi zenye waislamu wengi mara nyingi azikariki vizuri wanapigana wenyewe ni fujo kwenda mbele.

Sisi hatuna muda na huo ujinga wenu mnakaa huko mnawaza na kupanga jinsi ya kulipuana. Mkija kushtuka wenzenu wako mbali kimaendeleo, mnaanza ooh Nyerere, ooh serikali inapendelea wakatoliki, nk. Washenzi sana ninyi.

Sijui hamjatembea, Katoliki ni taasisi kubwa mno (simaanishi dini na dhehebu nyingine ni ndogo, itanisadia nini?) sio hapa tu Tanzania, tembea uone. Sasa kama kweli mkatoliki aliendelea kupitia mgongo wa huyo Nyerere basi nyerere aliongoza nchi ngapi?

Acheni fikra zenu hizo mgando hamtaweza kamwe kushindana na huyo mnayedhania kuwa ni adui yenu mkatoliki wakati yeye wala hajali anaendelea na mambo yake ya kiimani zaidi badala ya malumbano.

Kwahiyo achaneni na hivyo vihoja vyenu vya kiwivu wivu, pambaneni na hali zenu. Fanyeni kazi na mjitambue ni nini hasa mnachoamini kupitia dini yenu, hilo tu ndilo litakalo wakomboeni na siyo hizi porojo na kujitia kupambana na mnayemdhania ni adui yenu kumbe sio.

Jifunzeni ya kuwa yeye mkatoliki hana hata muda na nyinyi na ndio maana mwisho mnaishia kujilipua wenyewe kwa wenyewe. Nyambafuu.
 
Sheikh nafikiri usingekuwa unakutana na hoja za watu kudai kwamba wewe ni Mdini kama makala zako zingebeba uwiano kwenye mizani ya makala yako, sidhani kama harakati za kupigania uhuru zilifanywa na waislamu pekee ingawa sikatai kwamba kwa miaka ya 1950s ukanda wa pwani ulijaa waisilamu lakini katika TANU kuna viongozi wengi tu wa dini na imani tofauti walipata kuwepo. suala la kitabu chako kuwepo mwaka wa 21 sasa na kufikia toleo la 4 ni jambo jema na linaloonesha kinakubalika na najua unafahamu vizuri wanunuaji wakubwa wa hicho kitabu ni watu wenye imani na dini fulani unayoifahamu.
Samurai...
Tatizo ni kuwa historia ya TANU inawatisha lakini Uislam ulitumika sana wakati wa kudai uhuru.
Kwa kuwa naona hili limekuwa somo ambalo halijulikani nimeamua kutoa darsa maalum ili liwe msingi wa kuielewa historia ya uhuru wa Tanganyika kama ilivyokuwa:

DARSA NO. 1
Dini ilivyotumika kuwaunganisha watanganyika dhidi ya ukoloni sehemu ya kwanza: Mwanzo wa harakati 1950

Utangulizi

Nami nasubiri patulie In Shaa Allah nataka niandike jinsi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alivyochaguliwa kuongoza harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika katika kikao cha watu watatu Nansio, Ukerewe nyumbani kwa Hamza Kibwana Mwapachu mwaka wa 1953 na moja ya sifa kubwa iliyotajwa ni dini yake. Wazalendo hao wote watatu waliokubaliana kumkabidhi Baba wa Taifa uongozi walikuwa Waislam, mmojawapo akiwa Katibu wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Kisha nitaeleza vikao vyote vya dua alivyoshiriki Baba wa Taifa pamoja na Waislam katika kumlilia Allah awape msaada Watanganyika washinde dhulma zote za Waingereza na Allah alikubali dua ya wenye kudhulumiwa.

***

Mwaka wa 1950 uongozi wa TAA ulikuwa chini ya Dr. Vedasto Kyaruzi kama Rais na Abdulwahid Sykes akiwa Katibu na ikaundwa TAA Political Subcommittee (Kamati ya Siasa ya TAA) iliyokuwa na pamoja na Rais na Katibu, wajumbe hawa wafuatao: Sheikh Hassan bin Ameir aliyekuwa Mufti wa Tanganyika, Sheikh Said Chaurembo, Hamza Mwapachu, Steven Mhando na John Rupia,

Katika kipindi hiki cha mwaka wa 1950 Abdul Sykes alikuwa katika majadiliano na Chief David Kidaha Makwaia akimtaka aingie TAA wamchague kuwa rais kisha waunde TANU yeye akiwa rais wadai uhuru wa Tanganyika.

Kwa kuwa hapa tunazungumza nafasi ya dini katika historia ya uhuru wa Tanganyika napenda kueleza kuwa Chief David Kidaha Makwaia hakuwa Muislam ingawa alikuwa mtoto wa Chief Makwaia Mohamed Mwandu.

Wakati huu Abdul Sykes alikuwa mmoja wa viongozi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) lakini hili halikuingia katika fikra zake katika kumtaka Chief Kidaha Makwaia kuongoza harakati za kudai uhuru wa Tanganyika na uhuru ukipatikana awe Waziri Mkuu wa Kwanza wa Tanganyika.

Juhudi hizi hazikufanikiwa.

Mwaka wa 1951 Waingereza walimpa uhamisho Dr. Kyaruzi na kumpeleka Jela ya Kingolwira, Morogoro kisha wakamuhamishia Nzega.

Hamza Mwapachu yeye akahamishiwa Nansio, Ukerewe na yote hii nia ya Waingereza ilikuwa kuivunja nguvu TAA Makao Makuu, New Street kudhoofisha juhudi za kuunda chama cha siasa.

Mwaka wa 1952 Mwalimu Julius Nyerere alipelekwa kwa Abdul Sykes na Joseph Kasella Bantu.

Wakati huu Abdul Sykes alikuwa Kaimu Rais wa TAA na Katibu.

Picha hizo hapo chini aliyevaa kitenge ni Chief David Kidaha Makwaia, Hamza Kibwana Mwapachu, Abdulawahid Kleist Sykes, Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na aliyefunga kilemba cha Ki-Omani ni Chief Makwaia Mohamed Mwandu wa Siha.

Itaendelea...

DARSA NO. 2
DINI ILIVYOTUMIKA KUWAUNGANISHA WATANGANYIKA DHIDI YA UKOLONI SEHEMU YA PILI: UJIO WA MWALIMU JULIUS NYERERE DAR ES SALAAM 1952

Joseph Kasella Bantu ndiyo alimchukua Mwalimu Julius Nyerere kutoka Pugu na kujanae nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu kuja kumtambulisha.

Kupitia kwa Abdul Sykes Nyerere akajuana na watu mashuhuri wa mji na wenyeji wa Dar es Salaam.

Mapenzi makubwa yalijengeka baina ya Nyerere na Abdul Sykes na ndugu zake wawili Ally na Abbas ambae wakati ule alikuwa kijana mdogo.

Kufikia mwaka wa 1953 kuelekea uchaguzi wa TAA Abdul tayari alikuwa keshauona uwezo wa Mwalimu Nyerere kama kiongozi na jina la Nyerere lilitawala mazungumzo baina ya Hamza Mwapachu na Abdul Sykes.

Shajara za Abdul Sykes za nyakati hizi zipo nyingine zimeandikwa kwa hati za kawaida na nyingine kwa hati mkato bahati mbaya shajara hizi hazijatolewa hadharani kwa watafiti kuzisoma na mwandishi ingawa aliziona hakupewa idhini ya kusipitia lakini ni wazi zitakuwa zimejaa mengi katika viongozi kama Chief Kidaha Makwaia na Julius Nyerere waliotegemewa kuongoza mapambano ya kudai uhuru wa Tanganyika.

Nalisema hili kwa kuwa katika nyaraka zingine zipo taarifa za wanasiasa wengi kama Dr. Wilbard Mwanjisi, Dr. Michael Lugazia, Ali Migeyo na Rashid Kawawa kwa kuwataja wachache.

Miezi michache kabla ya uchaguzi wa TAA uliokuwa ufanyike mwezi Aprili, 1953 Abdul Sykes akiongozana na Ali Mwinyi Tambwe aliyekuwa Katibu wa Al Jamiatul Islamiyyya fi Tanganyika walikwenda Nansio kuonana na Hamza Mwapachu.

Abdul Sykes alikuwa anataka apate kauli ya mwisho kutoka kwa Hamza kuhusu jambo ambalo walikuwa wakilizungumza kuanzia mwaka wa 1950 nalo lilikuwa kuunda TANU na kudai uhuru wa Tanganyika.

Abdul alimuuliza Hamza Mwapachu kama msimamo wake bado ni ule ule kuwa yeye ampishe Nyerere kwenye nafasi ya urais wa TAA na mwaka unaofuatia, 1954 waunde TANU kama chama cha ukombozi kudai uhuru wa Tanganyika.

Ilikuwa muhimu kwa Abdul kumkubaii Nyerere kwani Nyerere alikuwa mgeni na hakuna aliyemjua Dar es Salaam kwa hiyo ikiwa Abdul atagombea nafasi ya rais ambayo alikuwa akikaimu toka mwaka wa 1951 kwa nia ya kupata ushindi, kwa umaarufu wake Nyerere hatoweza kumshinda Abdul Sykes.

Hamza Mwapachu alimwona kati ya Abdul na Nyerere, Nyerere alifaa zaidi katika kuongoza harakati za kudai uhuru chini ya chama cha TANU kuliko Abdul.

Zaidi, Nyerere alikuwa na shahada ya pili kutoka Chuo Kikuu Cha Edinburgh, Uskochi.

Lakini kubwa ambalo Hamza Mwapachu alisema kumwambia Abdul yalikuwa maneno haya, ''Abdul wewe ni Muislam na sisi tunakabilliana na Waingereza katika kudai uhuru wa nchi yetu. Ikiwa wewe utaongoza harakati hizi inaweza zikachukuliwa hizi kama vurugu za Waislam dhidi ya Waingereza. Nyerere ni Mkristo, Waingereza hawatotishika na Nyerere katika hili.''

Vita Vya Maji Maji vilikuwa bado viko katika kumbukumbu ya vijana wanasiasa wa wakati ule ambapo katika vita vile Waislam walikuwa mstari wa mbele.

Unyama ambao wananchi wa Tanganyika walifanyiwa na Wajerumani baada ya vita vile ulikuwa bado uko katika kumbukumbu mbaya sana katika historia ya nchi.

Majemadari zaidi ya 60 wa vita vile wengi wao Waislam walinyongwa na kuzikwa kwenye kaburi moja.

Hakuna aliyetaka ijengeke picha kuwa Waislam walikuwa wanjikusanya upya kwa mara ya pili kuoambana na Waingereza na hapa ndipo ilipoingia dini ya Nyerere.

Fikra ya Hamza Mwapachu ilikuwa dini ya Nyerere haitakuwa tishio kubwa kwa Waingereza.
Kazi iliyotakiwa ni kwa Abdul kuhakikisha kuwa Nyerere anashinda uchaguzi wa mwaka wa 1953 na mwaka wa 1954 wanaunda TANU na kuanzia hapo kazi itakayofuata ni kuwahamasisha wananchi wote wa Tanganyika kummunga mkono Nyerere, TANU na harakati za kudai uhuru.

Nyerere alipita kwa shida sana uchaguzi ule uliofanyika Ukumbi wa Arnautoglo tarehe 17 Aprili, 1953.

TAA ilipata viongozi hawa wafuatao hapo chini:
J. K. Nyerere, Rais, Abdulwahid Sykes, Makamu wa Rais; J. P. Kasella Bantu, Katibu Mkuu; Alexander M. Tobias na Waziri Dossa Aziz, Katibu wa pamoja wa muhtasari; Wajumbe wa Kamati: Dr Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said Tewa, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo na Patrick Aoko.

Picha hapo chini ni Dome Budohi, Joseph Kasella Bantu na Julius Nyerere.

DARSA NO. 3
DINI ILIVYOTUMIKA KUWAUNGANISHA WATANGANYIKA DHIDI YA UKOLONI SEHEMU YA TATU: KUUNDWA KWA TANU 1954


Chama cha TANU asili yake ni African Association iliyoasisiwa mwaka wa 1929 na mwaka wa 1948 African Association ikabadili jina ikawa Tanganyika African Association (TAA).

Mwaka wa 1933 Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ikaasisiwa na ikasadifu kuwa waasisi wa chama hiki cha Waislam Kleist Sykes na Mzee bin Sudi walikuwa pia katika uongozi wa African Association.

Ikawa sasa viongozi wa African Association ndiyo wale wale viongozi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na hii ndiyo sababu TANU ilipoasisiwa rais wake wa kwanza Julius Nyerere akajikuta amezungukwa na watu wa dini moja.

Lakini hii haikuwa tatizo kwani wakati wa ukoloni hapakuwa na ubaguzi baina ya wananchi kwa kubaguana wenyewe kwa wenyewe kwa misingi ya dini na hii ndiyo sababu kubwa ya Baba wa Taifa Julius Nyerere kuweza kuchaguliwa kwanza kuwa rais wa TAA mwaka wa 1953 kisha rais wa TANU mwaka mmoja baadae na wale waliomchagua wengi wao walikuwa Waislam.

Katika mazungumzo ya Nansio ya kupata kiongozi wa kuongoza harakati za kudai uhuru katika ya Abdul Sykes, Ali Mwinyi Tambwe na Hamza Mwaochu, rai aliyotoa Hamza Mwapachu ilikuwa Nyerere atakuwa kiongozi muafaka kwanza katika macho ya Waingereza na pili katika kuwavuta wasio Waislam kuiunga mkono TANU kwa kuwa ingawa wanachama wengi walikuwa Waislam lakini chama kilikuwa kinaongozwa na kiongozi ambae hakuwa Muislam na hili iitajenga umoja wa Waafrika wa Tanganyika.

Wanachama wa mwanzo wa TANU walitafutwa kutoka Rufiji sehemu ambayo wakazi wake walikuwa wengi wao ni Waislam.

Mwalimu Nyerere alipokwenda kusajili TANU, aliulizwa kama anayo rejesta ya wanachama na kwa bahati mbaya haikuwapo.

Alipokwenda kumfahamisha Abdul Sykes tatizo hili, Abdul alimuomba Said Chamwenyewe aende Rufiji akatafute wanachama.

Hivi ndivyo ikawa kuwa wanachama wa mwanzo wa TANU walipatikana kutoka Rufiji ambako Mufti Sheikh Hassan bin Ameir kama Khalifa wa Tariqa Qadiriyya alikuwa na murid (wafuasi) wengi.

Makao Makuu ya TANU New Street kulikuwa na Baraza la Wazee wa TANU ambalo baraza zima wajumbe wake 120 walikuwa Waislam lakini hili halikuwa tatizo kwa umoja wa wananchi na sababu yake ni kuwa azma kubwa ya viongozi wa TANU ilikuwa umoja wa wananchi wote.

Hii ndiyo ikawa sababu ya Iddi Faiz Mafungo aliyekuwa Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na Iddi Tosiri wakiwa wanachama wa mwanzo wa TANU wakamchukua Mwalimu Nyerere, mguu kwa mguu hadi Bagamoyo kwenda kumtambulisha kwa Sheikh Mohamed Ramia, Khalifa wa Tariqa Qadiriyya Bagamoyo.

Sheikh Mohamed Ramia alikuja TANU na kundi kubwa la murid na TANU Bagamoyo ikawa na nguvu sana.

Southern Province ni ngome kuu ya Kanisa Katoliki na TANU ilipata tabu kubwa kuingia khasa kwa kuwa kanisa lilikuw alikiwatisha waumini wake kuhusu makusudio ya TANU wakielezwa kuwa italeta vita nyingine ya Maji Maji.

Sheikh Mohamed Yusuf Badi wa Lindi alipoingia TANU mwaka wa 1956 na alipompokea Mwalimu Nyerere kwa zafa na dufu iliyopigwa na wanafunzi wa madrasa yake iliyokuwa mjini Lindi, kitendo hiki kilivunja fitna zote dhidi ya TANU na chama kikaenea kuanzia Masasi hadi Tunduru na Nachingwea.

Viongozi hawa Waislam wote kwa umoja wao walikuwa nyuma ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na hapa ndipo ulipojengwa msingi wa umoja wa Watanganyika.

Si wengi wanaojua kuwa kuiongoza TANU kiwe chama cha siasa cha kisekula kazi kubwa ilifanywa na Sheikh Hassan bin Ameir kwani alijua kwa jinsi TANU ilivyokuwa na wanachama wengi Waislam hii ingeweza kupelekea TANU kukwepwa na wale ambao hawakuwa Waislam.

Hii ingesababisha pengine kuanzishwa kwa chama kingine katika misingi ya dini kwa hofu ya kuogopa kumezwa na TANU chama cha Waislam.

Katika mikutano ya mwanzo ya TANU, pale Mnazi Mmoja, Mwalimu Nyerere alikuwa akipanda jukwaani na kutambulishwa na Sheikh Suleiman Takadir aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU.

Picha hapo chini inamwonyesha Mwalimu Nyerere akiwa na Baraza la Wazee wa TANU. Sheikh Suleiman Takadir wa pili kulia waliokaa chini, Mtu wa pili waliosimama ni Dossa Aziz,wa sita Mwalimu Nyerere akifuatiwa na John Rupia na tisa ni Said Chamwenyewe akifuatiwa na Mohamed Jumbe Tambaza na Mshume Kiyate.

Picha nyingine ni hiyo inayomwonyesha kulia Iddi Faiz Mafungo, Sheikh Mohamed Ramia, Julius Nyerere, Saadan Abdu Kandoro na Haruna Taratibu wakiwa Dodoma wakati wa kuitangaza TANU.

Kumbukumbu kubwa ya kujenga umoja huu ni mwaka wa 1956 pale Mwalimu Nyerere aliposhiriki katika hafla kubwa ya khitma kwenye shamba la Sheikh Abdallah Chaurembo, Mtoni.

Picha hiyo hapo chini inamwonyesha Baba wa Taifa akiwa na viongozi wakubwa wa Kiislam shambani kwa Sheikh Abdallah Chaurembo.

Picha ya mwisho inamwonyesha kulia Bi. Titi Mohamed, Clement Mtamila, Sheikh Suleiman Takadir, Julius Nyerere na nyuma ni Rajab Diwani, John Rupia na Mama Maria Nyerere.

MWISHO
 

Attachments

  • CHIEF MAKWAIA MOHAMED MWANDU.png
    CHIEF MAKWAIA MOHAMED MWANDU.png
    43.4 KB · Views: 2
  • DOME OKOCHI BUDOHI 1.jpg
    DOME OKOCHI BUDOHI 1.jpg
    646.3 KB · Views: 1
  • BARAZA LA WAZEE WA TANU.jpg
    BARAZA LA WAZEE WA TANU.jpg
    36.8 KB · Views: 2
Hakuna kama Marehemu Nyerere. Au hupendi hilo?
Hata hilo bado ujui?! Hilo liko wazi, siyo Nyerere tu, ni ukweli pia kuwa hakuna na hatakuwepo mtu mwingine kama wewe. Kila mtu ni wa pekee. Hivyo hata wewe kama alivyo Nyerere ni wa pekee.
 
Takakeisho...
Wewe kama haikufai wako inaowafaa sasa hili ni somo yaani "field of enquiry," na yeyote ana haki ya kutafiti na kuandika anachopenda.

Wala hii si historia yangu kama ulivyoandika.

Hii ni historia ya uhuru wa Tanganyika.

Mimi nimeamua kuandika historia hii kwa kuona jinsi ilivyokuwa muhimu kuhifadhiwa na zaidi inawahusu wazee wangu ambao walikuwa mstari wa mbele kupambana na ukoloni.

Kitabu kimekuja na elimu mpya katika historia ya Tanganyika kwa kuandika historia za wazalendo ambao historia iliwafuta kabisa.

Wewe ulikuwa unaijua historia ya Sheikh Hassan bin Ameir au Hamza Mwapachu au Abdul na Ally Sykes na baba yao Kleist Sykes?

Umeghadhibika kwa kuwa historia inataja Waislam?

Unasema historia hii haramu kwenu ningependa kujua uharamu wake ni upi?

Historia iliyokuwa inafahamika ni ya Mwalimu Julius Nyerere peke yake.

Hii kwako ndiyo historia halali?

Ukiwa huipendi hujalazimishwa kusoma wala kununua kitabu.

Kitabu sasa kina miaka 21 na kinakwenda toleo la nne.

Hii maana yake ni kuwa kitabu kinapendwa.
Sentensi ya mwisho nadhani haijakamilika vizuri, usi-generalize kinapendwa. Sema kinapendwa na akina nani? Mimi sikipendi. Malizia tu kuwa kinapendwa na hao ndugu zako waislam. Na hao obvisious lazima wakipende kwa kuwa uandishi wako (which is a good market target strategy) umelenga kuwalazimisha wao wakipende. Ukumbuke, ni huruka ya wanadamu tulio wengi kupenda kusifiwa. Nawe umewasifia ustadhi wenzako kwa nini wasikipende?!
 
Sheikh nafikiri usingekuwa unakutana na hoja za watu kudai kwamba wewe ni Mdini kama makala zako zingebeba uwiano kwenye mizani ya makala yako, sidhani kama harakati za kupigania uhuru zilifanywa na waislamu pekee ingawa sikatai kwamba kwa miaka ya 1950s ukanda wa pwani ulijaa waisilamu lakini katika TANU kuna viongozi wengi tu wa dini na imani tofauti walipata kuwepo. suala la kitabu chako kuwepo mwaka wa 21 sasa na kufikia toleo la 4 ni jambo jema na linaloonesha kinakubalika na najua unafahamu vizuri wanunuaji wakubwa wa hicho kitabu ni watu wenye imani na dini fulani unayoifahamu.
Tena haweki mizani kweli kweli kwani haelewi kuwa Waisiramu walikuwa kidogo sana halafu Miisiramu hata kusoma haijasoma itajuwa kudai uhuru?

Mpe bwana majina ya wapigania uhuru wa kweli apate kuuelewa ukweli.

Kwanza walikuwa hawajui kuwanwaru wanadai uhuru kazi yao kunywa kahawa na kucheza bao tu mpaka alivyokuja Nyerere ndiyo akawafundisha, hawajui hawa kama Nyerere alikuwa mwalimu.
 
Hata hilo bado ujui?! Hilo liko wazi, siyo Nyerere tu, ni ukweli pia kuwa hakuna na hatakuwepo mtu mwingine kama wewe. Kila mtu ni wa pekee. Hivyo hata wewe kama alivyo Nyerere ni wa pekee.

Aah usifananishe na Nyerere bwana, yule ni mtakatifu bwana kwa kuipatia Tanganyika uhuru "single handed".

Dunia hii bwana ni pekee yule, hakuna mtu dunia nzima aliyepata utakatifu kwa siasa isipokuwa yeye tu bwana.

Au wewe unamfahamu mwengine?
 
ndio maana ni nadra sana sana kukuta kitabu au makala imeandikwa kichwa cha habari cha kibaguzi kama vile "Jinsi Mkiristo Nyerere alivyosaidia nchi nyingine za Afrika kudai uhuru" hizi lugha za kutumia neno Muislamu au Mkiristo ni kauli za kibaguzi na za kidini sana na ni hatari kwa taifa liliojijengea misingi ya kupinga udini, ukabila e.t.c
Samurai...
Hapana sijaandika kwa namna hiyo.
 
Sentensi ya mwisho nadhani haijakamilika vizuri, usi-generalize kinapendwa. Sema kinapendwa na akina nani? Mimi sikipendi. Malizia tu kuwa kinapendwa na hao ndugu zako waislam. Na hao obvisious lazima wakipende kwa kuwa uandishi wako (which is a good market target strategy) umelenga kuwalazimisha wao wakipende. Ukumbuke, ni huruka ya wanadamu tulio wengi kupenda kusifiwa. Nawe umewasifia ustadhi wenzako kwa nini wasikipende?!
Profftobe,
Kitabu hiki baada ya kuchapwa Uingereza mwaka wa 1998 kilifanyiwa ''reviews,'' tatu na John Iliffe, Jonathon Glassman na James Brennan (unaweza ku-Google ikiwa huwajuwi hawa ni nani katika duru za historia ya Afrika) na zikachapwa katika Cambridge Journal African History.

Naamini unaijua University of Cambridge.

Baada ya hapo kitabu kikajulikana kwenye vyuo vingi Ulaya na Marekani katika Idara za African Studies na kuwa moja ya rejea kuhusu Tanzania.

Mwalimu akisomesha na kama anataka wanafunzi wake wamjue Julius Nyerere vipi alianza siasa na kupigania uhuru wa Tanganyika basi mwanafunzi atapewa rejea ya kitabu changu.

Gazeti la The East African (Nairobi) likafanya ''serialisation,'' tatu mwezi wa December 1998 na hii ikazidi kukipa kitabu umaarufu.

Kuna jambo lazima utambue.
Mwalimu Nyerere ni mkubwa sana.

Kitabu chochote kitakachoandika historia yake kitavutia wasomaji wengi.
Mimi nilikuwa nimefanya kile ambacho hakuna mtafiti yeyote ameweza kukifanya.

Nikitumia kumbukumbu na Nyaraka za Sykes nilikuwa nimeweza kuandika historia ya Mwalimu kwa ushahidi usio na shaka kutoka siku ya kwanza anakutana na Abdul Sykes mwaka wa 1952.

Sasa hapa ndipo palipowavutia wasomaji wengi kusoma kuwa Nyerere si aliyekuwa na ''blue print'' ya TANU bali kaikuta kwa Abdul na Abdul kapokea harakati zile kutoka kwa baba yake.

Yanayofuatia ni historia ambayo wengi sasa mnaifahamu.

Watu walikuwa hawajasikia majina ya wazalendo mashiekh na lile jeshi ambalo walilileta katika TANU.

Masheikh hawa walikuwa Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Suleiman Takadir, Sheikh Yusuf Badi kwa kuwataja wachache.

Historia hii ilivutia wengi.

Haya ndiyo yaliyowashangaza wasomaji wengi na kikafanya kitabu hiki kiwe cha pekee katika historia ya TANU, Nyerere na historia ya uhuru wa Tanganyika.

Kilichofuatia ni mialiko kutoka vyuo kadhaa Afrika, Ulaya na Marekani.
Unasema nimewasifia ''maustadhi,'' na ndiyo wakakipenda kitabu.

Nimealikwa Marekani na Ulaya kuzungumza kwenye vyuo vyao.
Hawa ni maustadhi?

Labda nikufahamishe.

Ningependa sana mimi kuwa ustadhi lakini bahati mbaya elimu yangu haijafikia kiwango hicho.
 
Samurai...
Hapana sijaandika kwa namna hiyo.
Hujanielewa sheikh, nilichomaanisha ni kwamba ni nadra kukuta John Robert kakamilisha jambo fulani halafu baadae akatumia neno kama vile, "mimi Mkristo John Robert ndio wa kwanza kufanya hivi au vile"
 
Tena haweki mizani kweli kweli kwani haelewi kuwa Waisiramu walikuwa kidogo sana halafu Miisiramu hata kusoma haijasoma itajuwa kudai uhuru?

Mpe bwana majina ya wapigania uhuru wa kweli apate kuuelewa ukweli.

Kwanza walikuwa hawajui kuwanwaru wanadai uhuru kazi yao kunywa kahawa na kucheza bao tu mpaka alivyokuja Nyerere ndiyo akawafundisha, hawajui hawa kama Nyerere alikuwa mwalimu.

Ningekujibu ila ngoja niku-Ignore
 
Hujanielewa sheikh, nilichomaanisha ni kwamba ni nadra kukuta John Robert kakamilisha jambo fulani halafu baadae akatumia neno kama vile, "mimi Mkristo John Robert ndio wa kwanza kufanya hivi au vile"
Samurai...
Ili kunifanya nielewe hebu niwekee hapa sentensi ambayo nimeandika hivyo niweze kukujibu.
 
Aah usifananishe na Nyerere bwana, yule ni mtakatifu bwana kwa kuipatia Tanganyika uhuru "single handed".

Dunia hii bwana ni pekee yule, hakuna mtu dunia nzima aliyepata utakatifu kwa siasa isipokuwa yeye tu bwana.

Au wewe unamfahamu mwengine?
Ooh samahani sikujua kama uelewa wako ni mdogo. Au ndio ile asili yenu ya ubishi usiokuwa na maana ndiyo unakufanya kujitoa ufahamu.

Wapi mimi nimekufananisha na Nyerere. Nimesema kila mtu hapa duniani ni wa pekee ukiwemo wewe na huyo Nyerere unaye muota/waza mchana na usiku.

Pole maana hata unachoandika "utakatifu" inaonekana kumbe ujui maana yake.
 
Back
Top Bottom