Uchaguzi 2020 Walioshinda kura za maoni na kukatwa, msikubali ujinga huu

Uchaguzi 2020 Walioshinda kura za maoni na kukatwa, msikubali ujinga huu

Ulikuwa mshindi halali kura za maoni, lakini Watawala wajuu wakakukata jina lako na kumuweka mtu wanayemtaka.

Kisha mliokatwa mkaambiwa muwapigie kampeni hawa mahasimu wenu, kwa ahadi kwamba mmeshafanyiwa vetting mtateuliwa kwenye nafasi zingine.

Kataeni ujinga huo, yani aliyekukata usigombee, baadaye aje akuteue?

Inakuingieni akilini kweli, kwanini asinge mteua huyo aliyempenda na kumpa nafasi yako uliyopewa na wananchi?

Wanasema mlitoa rushwa, sasa kama hilo ni doa tayari huo uteuzi mtaupataje?

Fanyeni maamuzi sasa, nendeni vyama vingine mkagombee kama mnaamini mlishinda na mtashinda nafasi za kuchaguliwa.

Kumbukeni hizi za kuteuliwa ni kama mwanamke anyechumbiwa, hana uhakika wa kuolewa mpaka siku ya kufunga ndoa.

Na ndio maana huona wanawake hulia siku ya ndoa, hawaamini wamefikia hatua hiyo.

Jitoeni CCM nendeni Chadema au ACT, mkathibitishe hamjatoa rushwa, na mlionewa ili wananchi wachague, huko CCM hata mkibaki mneshatuhumiwa kwa rushwa, sasa mtateuliwa vipi?

Muda ndio huu msichelewe kwa ahadi hewa mtajuta.
Uchadema utakuua
 
Uchadema utakuua
Hahaha sasa kuwashauri wagombea waliochaguliwa na wananchi kihalali na wakaporwa ushindi wao, nakufa vipi?!

Basi niseme wasiende Chadema waende hata TLP, as long as wao ndio chaguo la wananchi watashinda tu.

Kuwaambia waende Chadema na ACT ilikuwa kuwarahisisia choices, ni sawa na maswali ya multiple choice, ungeweza kupewa swali hilo hilo bila majibu bado ulitakiwa ujaze jibu sahihi.

Vipi hapo, bado nitakufa?!
 
Hahaha kubaki ccm kwa ahadi ya cheo ni ujinga lakini, hulioni hilo, kwamba aliyekukataa leo eti kesho akuteue, how?!
Baki CCM kwa kuwa unakipenda chama. Ukibaki kwa matumaini ya kuteuliwa unaweza kuambulia frustration.
What is a probability for you to be selected out of 10K people? Virtually zero!
 
Ccm imedhiirishia dunia kuwa haina wala haitambui mfumo wa demokrasia.
Hahaha wao wameshazoea kuteuliwa watatambuaje haya maswala ya kuchaguliwa , tena kuchaguliwa na wananchi?!

Kwao ccm wananchi ni takataka tu, iweje wawaamulie wao watawala ni nani wanayemtaka?!

Yani kwasababu wanatawala, wanadhani hata maamuzi yetu ni ya kijinga isipokuwa yao wao watawala?!

Halafu, kuna watu wanasubiria kuteuliwa na hao hao walio wakata.
 
Baki CCM kwa kuwa unakipenda chama. Ukibaki kwa matumaini ya kuteuliwa unaweza kuambulia frustration.
What is a probability for you to be selected out of 10K people? Virtually zero!
Hahaha chama ukipende ili iweje?!

Chama kina wenyewe tayari, hata ukikipenda unapoteza muda, unatakiwa uwapende wenye chama na wao wakupende zaidi.

Wenye chama hawakupendi, na wameshakuonyesha hawakupendi, sasa unataka frustration zaidi ya hiyo?

Solution ni kuondoka tu.
 
Mkisusa wenzenu wanakula, vita haiishi ukipigwa risasi, bali ukifa.
Mkikubali kuonewa mtafanya ni amini mlitoa rushwa.

Na nitashauri msiteuliwe popote.

Msiwe kama mlichanjwa chanjo ya kuwa wajinga.
Wameshaambiwa na half rey kuwa ccm ni tajiri wa vyeo maskini wa ajira....na kwa mtazamo wa half rey na ccm cheo si dhamana,weledi au taaluma ...kwao cheo ni asante,kujipendekeza na unafique
 
Wameshaambiwa na half rey kuwa ccm ni tajiri wa vyeo maskini wa ajira....na kwa mtazamo wa half rey na ccm cheo si dhamana,weledi au taaluma ...kwao cheo ni asante,kujipendekeza na unafique
Hahaha huyo anawachuuza. Ngoja uchaguzi uishe utasikia tuliwafunza adabu wala rushwa.

Sijui chanjo ya ujinga ccm inayowachanja wanachama wake waliitoa wapi?!

Yani wanawajinga wengi hadi nawaonea wivu.
 
Mimi namuonea huruma yule dogo wa Kawe [emoji16][emoji16][emoji16]

Sent from my SM-G928F using JamiiForums mobile app
Yule hata yeye bado hajui alishindaje, kaahidiwa atateuliwa baada ya uchaguzi.

Wale ccm walijua wangempa ushindi mtu mwenye akili timamu ingekuwa ngumu kumpora, wakaona wamsukumizie mtu hata asiyejulikana ili iwe rahisi kumpora.

Yule dogo hata kura moja hakupata.
 
Back
Top Bottom