Wamama wananguvu kubwa ya ushawishi kwa watoto, kuwa makini kama umezaa na mwanamke ambaye hauishinaye

Wamama wananguvu kubwa ya ushawishi kwa watoto, kuwa makini kama umezaa na mwanamke ambaye hauishinaye

IKUMBUKWE NYAKATI ZIMEBADIRIKA SANA,
ZAMANI WATU WALIKUA WANAZAA WATOTO WENGI ILI WAJE KUPATA USAIDIZI UZEENI.
ZAMA HIZI, WATOTO NDIO WANAWEZA KUHITAJI USAIDIZI WA WAZEE WAO!
MWELEZE MTOTO WAKO BABA YAKO NI SHETANI, MBWA, NYOKA, MAREHEMU, NK NK.
HALAFU UNAKUJA KUKUTA HUYO HUYO MZEE ANA UCHUMI MZURI, CHEO KIKUBWA,KIASI WEWE NDIO WA KUMTEGEMEA!

Mithari 18: 20-23 Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi.
Ndo maana inatakiwa tuoe wanawake wenye dini hapa maandiko Yana maanisha afya njema ya akili
 
Zama zimebadilisha live your own life hata ukiwa nao karibu lakini usiweke mategemeo nao.
Ukiwa masikini hata wanao na mkeo watakutenga.
 
Zama zimebadilisha live your own life hata ukiwa nao karibu lakini usiweke mategemeo nao.
Ukiwa masikini hata wanao na mkeo watakutenga.
Ni kweli usemalo maana hata maandiko yanasema mtu maskini atatengwa hata na ndg zake . Lakini jambo la muhimu ni kuithamini damu hako usiruhusu watoto wateseke wakati uwezo wa kuwahudumia unao
 
Ili kuepuka yote hayo muwe mnalea watoto sio kuwatelekeza baadae wakiwa na mafanikio mnajisogeza
 
Labda wa kwako ndugu hawatakutafuta ila hata ikiwa umebebesha mimba na kupotea iko siku utatafutwa tu, whatever ulitoa au hukutoa matunzo.

Kitanda hakizai haramu.
Sasa hata akikutafuta unadhani itabadili nini? Kama hukuwahi kutengeneza bond wakati akiwa mdogo unadhani utaweza wakati akiwa mkubwa? Kwanza unakubali vipi mwanao afundishwe maadili, Mila na desturi na baba mwingine? Atakapokuja kila mtu atamuona mwenzake stranger na hapo ili mambo yende inabidi wewe baba ndio uwe mpole!
 
Labda wa kwako ndugu hawatakutafuta ila hata ikiwa umebebesha mimba na kupotea iko siku utatafutwa tu, whatever ulitoa au hukutoa matunzo.

Kitanda hakizai haramu.
atakutafuta aone hilo sura lako limekaa kaa kivipi baba mwenye roho mbaya wewe! Halafu atapotea kabisa. Labda kama ndugu zake watampokea ndiyo anaweza kujiunga nao kifamilia.
 
Haijalishi unaishi nae ama huishi nae. Unataka watoto wakuseme vizuri lazima mama yao awe anakusema vizuri kwao.

Mwanaume hakikisha una vitega uchumi vyako mwenyewe vya kukufanya uishi kama mwanaume hata ukiwa na miaka 100 watoto watakuheshimu tu hata kama hauishi na mama yao.
 
Kwa wewe ambaye umezaa na wanawake/ mwanamke ambaye hauishinaye inakupaswa ufahamu wamama wananguvu kubwa ya ushawishi kwa watoto kuliko wababa.

Kama hauna maelewano mazuri na huyo mwanamke uliyezaanaye usitegemee watoto watakuja kukutambua.

Nafahamu sio wababa wote ambao hawatoi huduma wanamatatizo kuna mambo huwa yanapelekea kufanya hivyo. Tumia tu busara hasira zako kwa mwanamke usipeleke kwa watoto, watoto wanawezwa kujazwa maneno ya uadui na wasikutambue
Hili halina ubishi...
 
atakutafuta aone hilo sura lako limekaa kaa kivipi baba mwenye roho mbaya wewe! Halafu atapotea kabisa. Labda kama ndugu zake watampokea ndiyo anaweza kujiunga nao kifamilia.
Pole kwa kukimbiwa na babako, naona umekuja na povu kumalizia hasira kwangu.
 
Kuna jamaa yangu mwaka jana alipata kazi kampuni kubwa sana alinipa story yake nilishangaa sana.

Ananambia katika maisha yake mama yake alimuaminisha kwamba baba yake ni mbaya mpaka ikafikia hatua baba akawa anakosa ujasiri wa kumshauri au kumwambia chochote jamaa. Lkn nyuma ya pazia kumbe jamaa alivyokuwa Primary baba ndo alimlipia ada na kila kitu cha shule. Lkn alivyofika sekondary mzee akaona ili isilete ugomvi huku kwenye familia yake (baba tayari alikua ameshaoa mke mwingine) na wakati mwingine kuna kukosa pia ili mwanaye asikwame ada akamfungulia mama biashara nzuri ya mtaji mkubwa tu. Na akamwambia kabisa kwamba hii biashara ni kwa ajili ya mwanangu asikwame ada

Jamaa anasema katika kukua kwake amemkuta mama anafanya hyo biashara na jamaa anasema nilikua nikimuona mama anatoa hela kwenye hyo biashara analipa ada. Jamaa anasema yeye pia amekua akihusika kwenye hyo biashara na mama yake anamkandia sana mzee kwamba hamsaidii chochote. Na jamaa anasema kweli nikiangalia ni mama ndo anakomaa na biashara ananilipia ada. Kumbe kuna ukweli ambao mama hakumwambia mtoto.

Sasa funga kazi jamaa alipigiwa simu na mtu mmoja akamwambia kuna kazi kampuni flani jaribu utume maombi, akamtumia na tangazo. Jamaa ananambia hakutaka hata kujua aliyemtumia hlo tangazo ni nani maana mchongo wa kazi ukishakuja mezani kikubwa ni kufanya application.

Kumbe huyo alomtumia hlo tangazo alitumwa na baba yake. Baba kumbe ashasuka mchongo kila kitu, kama mnavyojua kazi za mjini wakati mwingine inabidi upasuke ili uipate. Mzee kumbe kashatoa hela kibao kwa ajili ya kumsafishia njia mwanaye. Jamaa ananambia anashangaa namna interview ilivyokua kuna namna flani mambo yalikua smooth mchizi kaingia kazini.

Jamaa anasema alikaa miezi sita hajamwambia mzee kama amepata kazi na wala hajamtumia chochote mzee kwa kuamini kwamba mzee anazingua maana kapambaniwa na na mama yake mpaka amepata kazi kwa hustle zake binafsi.

One day walienda Arusha kikazi huko walikutana staff kutoka branches za nchi nzima. Ananambia HR mmoja yeye yuko branch ya Dodoma alipata taarifa kwamba anamuulizia. Walivyokutana ndo akamuuliza wew ni mtoto wa fulani? Jamaa akasema ndiyo unamfahamu? katika story story ndo akaja kujua kwamba mzee ndo alisuka mchongo mzima na hata lile tangazo la kazi alotuma ni yule HR. Ndo jamaa ikabidi agutuke akaona pengine baba kuna vitu vingine anaweza kuwa amefanya kimya kimya bila yeye kujua.

Jamaa ananambia alikuja kujua vitu vingi ambavyo mzee alikua anamfanyia lkn kwa kupitia kwa mama wala hakutaka kuonesha kwamba amefanya.

Jamaa alinia?ambia alimtafuta mzee akamuomba msamaha sana. Mzee alisema mimi nilishakusamehe hata kabla hujanikosea kilio changu ilikua ni kuona wew una maisha mazuri na kazi nzuri. Mengine namuachia Mungu tu ndo anajua ukweli.

Hii scenerio ya huyu jamaa ilinifundisha sana. Yani jamaa anakwambia wanawake siwaamin aisee. Yani hata girlfriend wake huwa anamuangalia ananambia hata huyu kuna siku atanigeuka huyu .😀
We acha tu!
 
Ili kuepuka yote hayo muwe mnalea watoto sio kuwatelekeza baadae wakiwa na mafanikio mnajisogeza
Kosa kubwa tunafanya wanaume ni kuacha mwanamke! Unatakiwa mwanamke akuache yeye, hapo hakutakuwa na shida. Ila ukimuacha wakati bado anakutaka, hakuna rangi hutaaacha kuiona hapa duniani, na hata ukifa kaburi lako akiliona lazima alichape na fimbo.

Si wote hatutoi matunzo, tunatoa hadi wanafika 20 years ila shida ipo pale pale. Ukizaa na mwanamke unalo hilo hadi Golgota.
 
Inatokea lakini mara chache sana , kama mama mtu alikukandia kwa mtoto wake ile sumu inakuwepo kwa mtoto ni ngumu kukutafuta
akiwa bado mdogo mama anaweza kumlisha sumu za maneno kadri awezavyo. Lakini mtoto akikua akawa mtu mzima akaweza kupambanua mambo na kujua kati ya baba na mama ni nani mjenzi wa familia na ni nani hubomoa familia. Hapo ndipo mtoto hufuta maneno ya mama yake kichwani na kumuuliza baba yuko wapi mama nipeleke kwa baba!
 
Pole kwa kukimbiwa na babako, naona umekuja na povu kumalizia hasira kwangu.
Baba yangu mimi hakupotea bali alifariki nilipokuwa na umri wa miaka 7. Lakini kwa hiyo miaka michache niliyokuwa naye alitupenda sana na kutushughulikia kwa kila hali.

Unaweza kuamini kuwa katika miaka ya sitini kabla ya kufariki sisi tayari alikuwa ametufungulia account bank, kila mtoto na account yake, kila mwezi deposit Shilingi 5 kwenye kitabu (zilikuwa nyingi sana enzi zile). Mungu akupe baba wa aina gani tena? Ni bahati mbaya kwamba alifariki wakati sisi tukiwa wadogo lakini mimi namshukuru Mungu na kumuombea dua ya kumpa malazi mema peponi.

Hao mababa wa design za generation Z ndiyo munaohangaika hivyo.
 
Kwa wewe ambaye umezaa na wanawake/ mwanamke ambaye hauishinaye inakupaswa ufahamu wamama wananguvu kubwa ya ushawishi kwa watoto kuliko wababa.

Kama hauna maelewano mazuri na huyo mwanamke uliyezaanaye usitegemee watoto watakuja kukutambua.

Nafahamu sio wababa wote ambao hawatoi huduma wanamatatizo kuna mambo huwa yanapelekea kufanya hivyo. Tumia tu busara hasira zako kwa mwanamke usipeleke kwa watoto, watoto wanawezwa kujazwa maneno ya uadui na wasikutambue
Kama baba alikimbia mimba na malezi mtoto akiwa mdogo sioni haja ya mtoto kumtambua. Ila kama baba aliwajibika mwanamke anaemjaza mtoto upuuzi wa kumfanya amchukie baba ni shetani mkubwa.
 
Back
Top Bottom