Wamasai Ngorongoro: Spika ataka 'aliyechukua clip' ashughulikiwe, taasisi zilizosajiliwa nchini kufata

Wamasai Ngorongoro: Spika ataka 'aliyechukua clip' ashughulikiwe, taasisi zilizosajiliwa nchini kufata

Waziri mkuu mh Majaliwa amesema Loliondo na Ngorongoro kote hali ni shwari kabisa na hizo clip zinazoonekana mitandaoni wamasai wakirusha mishale siyo HALISI ni uzushi na usanii tu.

Kufuatia taarifa hiyo Spika Tulia amemwomba Waziri mkuu kuwashughulikia wahuni wote wanaorusha hizo clip

Source Star tv bungeni
Si ndio huyu jamaa alisema Jiwe ni mzima anapiga kazi ofisini, wakati mtu alishakata moto?

Bado mnamuamini?
 
Huyu naye ovyo tu. Baadala aombe uchunguzi ufanyike, yeye anawatafuta wistleblowers.
 
Bunge linasimamia
Leo Bungeni baada ya Waziri mkuu kuongelea video inayosambaa kwamba kuna mapigano yameanza Ngorongoro, Spika Tulia Ackson ametoa maoni yake na kutaka mhusika ashughulikiwe na taasisi zilizosajiliwa nchini zifate.

======

Spika: Tupo kwenye vita ya kiuchumi na nchi zingine, tukiwaacha hawa wakaendelea kutumika, wale waliopo hapa nchini sheria zetu zichukue mkondo wake.

Kama mtu anafanya upotoshaji kama huyo ambae amechukua hiyo clip na inajulikana ameichukulia wapi, tunaweza kuanza na huyo halafu wengine watafata ikiwa ni pamoja na hizi taasisi ambazo zimesajiliwa hapa nchini kwetu tukifikiri kwamba zina lengo jema na sisi hapa nchini lakini kama zinafanya jambo tofauti pia sheria zichukue mkondo wake.

[Let

Bunge linalowakilisha wananchi lakini linawatishia wananchi.
 
Spika ameongea kitu cha maana sana. watu kama Tito Magoti, Maria Sarungi, Ole Ngurumo na type zake zooote hizo, wanaichafua sana nchi na wanatamani hata Masai mmoja tu afe ili wapate cha kuongea. Wadhibitiwe mapema, sio afya kwa taifa.

Tatizo mnataka wote waimbe wimbo mmoja. Yani ukweli ufichwe kwa maslahi ya wachache. Ruhusuni na wengine waeelezee Hali ya mambo ilivyo.
 
Safi sana tuna spika msomi na anayekwanda sambamba na maendeleo ya nchi yake, Maria aitwe apewe onyo maana anakoelekea ni kubaya.

Spika yupi huyo? Huyu aliyesema sio lazima serikali itekeleze ushauri wa Bunge. Sasa huwa najiuliza hiyo bajeti wanaijadili ya Nini?.
 
Dikteta unamuonea tu!

Malaika wako alikuwa na nafasi ya kumtoa pale ila kamrudisha kitini!

Na hata hivyo mama anafungua nchi,

Anawakomesha mataga na sukuma gang na kufuta legacy

Ana tufuta machozi sisi machadema baada y kuonewa sana kwa miaka 5View attachment 2256102

Ndio mlichobakiza. Kutengeneza katuni za kujifurahisha.
 
Wakati Magufuli anawapuuza hao wajinga, nyie mlikuwa mnakata viuno humu mkimuita dikteta na mshamba!

Ngoja sasa waanze kuwatia vidole kwenye macho ndio mtajua hamjui.

Tuondolee Magufuli wako hapa.
 
Waziri mkuu mh Majaliwa amesema Loliondo na Ngorongoro kote hali ni shwari kabisa na hizo clip zinazoonekana mitandaoni wamasai wakirusha mishale siyo HALISI ni uzushi na usanii tu.

Kufuatia taarifa hiyo Spika Tulia amemwomba Waziri mkuu kuwashughulikia wahuni wote wanaorusha hizo clip

Source Star tv bungeni
Wakati wa Kifo cha Magu alitudanganya hivihivi
 
Rais ni buheri wa afya,anachapa kazi😁😁😁
AAMYtl.jpeg
 
Back
Top Bottom