Tukio lilitokea lini? Muda gani? Kukuta tiketi yake sio uthibitisho kuwa alikuwa eneo la tukio. Bado polisi wanatakiwa kuthibitisha kuwa alikuwepo eneo la tukio. Tiketi inawezekana iliachwa hapo n mhalifu makusudi ili kuwapoteza polisi.Jamani, Jamani
Wapendwa wa humu narudia tena, Chana au haribu kabisa tiketi au karatasi yoyote yenye taarifa zako sahihi kwa usalama wako.
Niko hapa Police Kimara, rafiki yangu wa kiume amekamatwa na kuwekwa ndani baada ya tiketi yake ya ki-electronic ya basi moja kutoka Arusha kuja Dar kukutwa kwenye tukio la uhalifu Kimara Bucha.
Yeye rafiki yangu anasema baada ya kushuka Mbezi Magufuli stendi, aliamua kuikunja na kuitupa tiketi yake karibu na lango la kutokea na baada ya hapo akaendelea na safari ya kuelekea kwake Tegeta.
Anasema zilipita siku 2 akapigiwa simu na police kuwa anahitajika kituoni Kimara.
Anasema hakwenda kwa kuhofia huenda ni watu wasio wema kisha akazima simu.
Anasema kesho yake anashangaa kuona police wako nyumbani kwake na wakamuweka chini ya ulinzi kwa kosa la uhalifu uliotokea maeneo ya Kimara bucha.
Na anasema walihisi walimpata kupitia Facebook, (mutual friend mmoja akatafutwa kisha akawaelekeza kwake).
Rafiki yangu si mtu wa kujichanganya sana na watu. Iwe usiku au mchana, akiwa ndani hujui na wala akienda kibaruani hujui.
Anasema ahusiki na tukio na wala hajafanya uhalifu wala kuwa na rekodi yoyote ya uhalifu.
Hapa tunashindwa cha kufanya.
Hatujui kama kweli kahusika au lah!
Sisi tunajua ahusiki ila binadamu hubadilika.
Ila maadam iko mikononi mwa jeshi la polisi tutajua tu hatma yake na wahusika halisi
Chana au haribu kabisa karatasi/tiketi ya basi/meli/treni/ndege/CV/copy yako ya NIDA na nyinginezo zenye taarifa zako sahihi.
Kumbe mjeda😂Usimtetee sana....
kuna kesi ya dogo mmoja hivi, dem wake alikua anaapa viapo vyote "huyu hawezi kubaka namjua tangu utotoni bla bla anasali ni mpole bla bla blaaa" jamaa nmekaa nae mezani nkaongea nae vizuri tu " kuwa mkweli hili tukio umefanya au haujafanya" kwa kinywa chake akasema kafanya....kabaka.
Baadae kidem kinakuja vipi amesemaje, namie nkakipoza tu hajafanya.
Huyo jamaa yeye mwenyewe ndio anaujua ukweli
Aisee!Rafiki yangu si mtu wa kujichanganya sana na watu. Iwe usiku au mchana, akiwa ndani hujui na wala akienda kibaruani hujui.
Katika mambo ya investigation kitu chochote kinachokuwa eneo la tukio.lazima kifanyiwe kazi,iwe,leso kipande cha chupa hata kipisi cha sigara,humo zitapatikana alama za vidole,au chochote kile iwe nywele,mate nakadhalikaTiketi ya basi inahusiana vipi na uhalifu hata kama imekutwa eneo la uhalifu??
Anyway, tiketi za electronics huwa zinaacha footprint kwenye database husika iliyotumika kukata tiketi, mtandao wa simu nao hubaki na kumbukumbu...
Simu yake kama alisafiri inaacha alama za mahali alipotembelea kwenye database za mitandao ya simu...
Hakuna kesi hapo unless hii iwe togwa mixer alkasusu...
Haya, wewe na u-logical thinker wako utanisaidia nini kwenye hii ishu bhana?Tatizo ni kwamba you're not a logical thinker kama hao polisi tu, naona umeshindwa kuelewa comment yangu kwamba polisi hawajawaza nje ya boksi wametumia shortcut kama kawaida yao...
Yes, na ndio manaa leo tunasubiri kukuche vizuri ili tukajue kinachoendelea.Tukio lilitokea lini? Muda gani? Kukuta tiketi yake sio uthibitisho kuwa alikuwa eneo la tukio. Bado polisi wanatakiwa kuthibitisha kuwa alikuwepo eneo la tukio. Tiketi inawezekana iliachwa hapo n mhalifu makusudi ili kuwapoteza polisi.
Mtuhumiwa awaambie alikuwa wapi siku na muda ambao tukio linatokea. Na anaweza kutafuta ALIBI...wapo watu alikuwa nao,alikuwa kazini(miamala aliofanya itaonekana) na simu yake inaweza kutumika kuonesha alikuwa wapi siku hio.
Yeye ni mtuhumiwa tu na polisi inabidi wathibitishe,watansumbua tu ila kama hakupiga tukio itajulikana.
Tufanyaje ili wamuamini?
Yaani mkuu, kuna watu humu ndani sijui wanajikutaga wao nani.Katika mambo ya investigation kitu chochote kinachokuwa eneo la tukio.lazima kifanyiwe kazi,iwe,leso kipande cha chupa hata kipisi cha sigara,humo zitapatikana alama za vidole,au chochote kile iwe nywele,mate nakadhalika
Kuna tukio moja la mauji nadhan mwanza kuna mwanadada maarufu sana aliuwawa,bahati mbaya muuaji aliacha chupa ya soda eneo la tukio,basi ikapimwa DNA ikasoma,ikasaidia uchunguzi
Penye wengi pana mengi my dear,tuwavumilie tu wasije wakakuharibia siku yakoYaani mkuu, kuna watu humu ndani sijui wanajikutaga wao nani.
Yaani ni pointless kabisa.
Kasoma mada kuu bila kuichambua kaja kukimbilia ku-comment bila kufikiri.
Yote tuwaachie jeshi la police wa dili na mtu wao.
Wanaleta sana ujuaji wakati kichwani ni sifuri.
hawa ndo wanakuwaga mamafya..achunguzwe kwa kina japo kuna mawili huenda alihusika au hakuhusika.Aisee!
DuhMimi huwa nachana mikeka tu. Tiketi naacha kwenye basi
Katika nchi zenye tawala Bora na za kisheria sambamba na kuwa na Jeshi la Polisi lenye uadilifu, suala hili lingeweza kuwa rahisi sana. Lakini kwa kuwa Jeshi la Polisi lililopo halina sifa hizo za Uadilifu, basi huyo mtu anatakiwa ajipange sawa sawa, he should expect the worse to come. Namuonea huruma sana huyo mtu, tayari ameshaingia kwenye mtego mbaya wa hawa jamaa, huyo Sasa amegeuzwa kuwa fursa na hao Polisi waliomkamata.Jamani, Jamani
Wapendwa wa humu narudia tena, Chana au haribu kabisa tiketi au karatasi yoyote yenye taarifa zako sahihi kwa usalama wako.
Niko hapa Police Kimara, rafiki yangu wa kiume amekamatwa na kuwekwa ndani baada ya tiketi yake ya ki-electronic ya basi moja kutoka Arusha kuja Dar kukutwa kwenye tukio la uhalifu Kimara Bucha.
Yeye rafiki yangu anasema baada ya kushuka Mbezi Magufuli stendi, aliamua kuikunja na kuitupa tiketi yake karibu na lango la kutokea na baada ya hapo akaendelea na safari ya kuelekea kwake Tegeta.
Anasema zilipita siku 2 akapigiwa simu na police kuwa anahitajika kituoni Kimara.
Anasema hakwenda kwa kuhofia huenda ni watu wasio wema kisha akazima simu.
Anasema kesho yake anashangaa kuona police wako nyumbani kwake na wakamuweka chini ya ulinzi kwa kosa la uhalifu uliotokea maeneo ya Kimara bucha.
Na anasema walihisi walimpata kupitia Facebook, (mutual friend mmoja akatafutwa kisha akawaelekeza kwake).
Rafiki yangu si mtu wa kujichanganya sana na watu. Iwe usiku au mchana, akiwa ndani hujui na wala akienda kibaruani hujui.
Anasema ahusiki na tukio na wala hajafanya uhalifu wala kuwa na rekodi yoyote ya uhalifu.
Hapa tunashindwa cha kufanya.
Hatujui kama kweli kahusika au lah!
Sisi tunajua ahusiki ila binadamu hubadilika.
Ila maadam iko mikononi mwa jeshi la polisi tutajua tu hatma yake na wahusika halisi
Chana au haribu kabisa karatasi/tiketi ya basi/meli/treni/ndege/CV/copy yako ya NIDA na nyinginezo zenye taarifa zako sahihi.
Tiketi isafiri na upepo kutoka Mbezi hadi ndani ya duka ulikotokea uhalifu?Shida ipo Kwa hao polisi hapo pia, unaokotaje tu kikaratasi kinachoweza kusafiri hata na upepo ukaanza kufanya ndio ushahidi wa kumuweka mtu ndani?