Uchaguzi 2020 Wana JF, nipeni Pole. Msinicheke wala msinibeze; nimegombea ubunge Kawe kupitia CCM nimeambulia kura 1. Ama kweli CCM ina wenyewe!

Pascal siyo mjumbe!
Ni kweli kabisa Pascal Mayala sio Mjumbe wa Mkutano huo Mkuu wa Jimbo
na hata yeye amekubali hivyo kuwa kaambulia kupigiwa moja
 
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Yaani bwashee we ni mnafki sana,umeona uje kumsimanga Pascal Mayalla na kakura kake kamoja alikoambulia...
 
Ukiona hivyo ujue kati ya wana JF wrote wewe na Paskal Mayalla tu ndio ccm.
 
Yaani Pascal umevuna ulichopanda. Uliyemsapoti Kigamboni ndo hivyo tena. Ila hongera kwa kupata First.
 
Swali moja tuu@Pascal Mayalla ni kweli ulitoa ahadi ya Milioni kumi kwa kila kata. ? .

Je nini hasa lilikua lengo la hiyo ahadi. ? .

Polee, ccm Ina wenyewe hilo ulijue kwa vitendo.
 
Mkuu mimi sikupi pole bali hongera kwa uthubutu, maji umeyapima na umeona kina chake. Ni muda wa kujipanga tena kwa 2025, wewe ni mkongwe na mzee wa mikakati so hakuna litakaloshindikana 2025.
 
Na hasa amajitambulisha kwa vitendo kwa mtembea na vyeo mfukoni, mgaa gaa na upwa hali wali mkavu.

Naamini cv yake wameiona na kupokea

Pascal Mayalla
 
Na naaamni hili ndio lilikua lengo kuu la pasikali. Wajue tena kwa vitendo
 
Anko naomba Ku kuuliza ( sijui km umelizwa huko juu )

Mfano ikitokea Mh Rais Magufuli akakuteua kuwa mbunge wa kuteuliwa na rais , Utakubali ? Kwakua ushaonesha nia ya kutaka kuwa mbunge

Lkn nakumbuka uliwahi kusema humu kuwa huhitaji nafasi yoyote ile ya uteuzi ,je ikitokea itakuaje ?
 
Mayalla kwa lugha yetu ya kisukuma maana yake NJAA
 
Ila mimi naona umejitahidi manake kwa kupata kura moja, kama ingekuwa ndo NECTA ni kweli ingekuwa umepata F lakini sio Division Zero! Au mi ndo sielewi?
 
Kuna kitu nadhani hamkukizingatia kwenu ninyi watangaza nia.

Mlio wengi hamkupima upepo wa maeneo mnayoenda kugombania.

Mkuu unavyokubalika kutokana na taaluma yako ya uandishi, ungelienda eneo sahihi wewe si wa kuambulia kura1, haiwezekani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…