Wanajeshi 60 wa Tanzania huko Afrika ya kati kurejeshwa nyumbani kwa tuhuma za unyanyasaji wa kingono

Wanajeshi 60 wa Tanzania huko Afrika ya kati kurejeshwa nyumbani kwa tuhuma za unyanyasaji wa kingono

Graduate wote huwa ni commissioned officers jeshini

Labda wale waliojiendeleza umri ukawatupa mkono

Maana monduli kule niliwahi sikia mwisho ni 32 years kupiga kozi ya cadet.

Lakini lazima wapate man power jeshini ndio hao askari wa kawaida ambao sio maafisa

At least useme wachukie high school underperformers at least div 3/4
Muulize huyo Graduate anauvumilivu wa kuburuzwa kama Ng'ombe...???
Ana uthubutu wakukaa maporini (mpakani) kwa kushindia mkate na Maji.
Wasilete Graduate na mambo ya maisha na kujitoa kwa elimu zao za kuunga na mikopo ya kununula mihogo na kugongea malaya.
Ni mpuuzi mmoja tuu anae weza kuongea Nerg kwenye Jesh
 
Wacha kutetea ushenzi wewe hii ni tabia ya Tanzania ngono ndio kipaumbele hata maofini ni mchezo huu umeshamiri kwa hiyo usiseme majeshi yote kuwa na nyenge hahukupi ruhusa kubaka watoto chukua sabuni piga punyeto
Acha ushamba na kukurupuka.
 
Acheni ubakaji,kama unampenda demu basi "ongea naye mpaka mwisho ni mia tano" in Masai voice
Nalog off
Kasome kanuni za ulinzi wa Amani, chini ya UN, utaona mlinzi wa amani, haruhusiwi kufanya mapenzi hata kwa hiari na mtu anaemlinda, kufanya hivyo inahesabiwa umebaka.

Inachukuliwa umetumia shida zake kumrubuni, hivyo hairuhusiwi, kufanya mapenzi na unaemlinda, ni sawa kwa Tanzania, mtu mzima kufanya mapenzi na mtu ambae hajatiza miaka 18 hata kama alihiari, uhesabika umebaka.

Hivyo hao wanajeshi, ukute hao wanawake walihiari na kuhongwa wamehongwa, na kinachowakamatisha ni mimba.
 
Walinda amani wa Tanzania kurejeshwa nyumbani kutokana na madai ya utovu wa nidhamu CAR


9 Juni 2023Haki za binadamu

Mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati (MINUSCA) chenye makao yake makuu mjini Bangui, kimetangaza uamuzi wa Sekretarieti, kuwarudisha nyumbani kikosi cha wanajeshi 60 wa Tanzania, waliokuwa wametumwa katika kambi ya muda ya operesheni katika eneo la magharibi mwa nchi hiyo kufuatia madai makubwa ya matendo ya unyanyasaji wa kingono yanayodaiwa kutekelezwa na walinda amani hao, msemaji wa Umoja wa Mataifa amewaeleza walinda waandishi wa Habari hii katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa, jijini New York, Marekani.

Msemaji wa Katibu Mkuu wa UN, Stéphane Dujarric, amesema, "Uamuzi huo unakuja baada ya uchunguzi wa awali ambao ulipata ushahidi wa kuaminika kwamba walinda amani 11 wa kitengo hicho walidaiwa kujihusisha na unyanyasaji wa kingono kwa waathirika wanne.”

Akifafanua zaidi Dujarric amesema, “Waathiriwa waliotambuliwa wanapatiwa matunzo na usaidizi kutoka kwa wadau wa operesheni za kibinadamu. MINUSCA pia imetuma timu ili kuzungumza zaidi na jamii.

Tanzania imetuma wachunguzi

Kwa mujibu wa Dujarric, “Mamlaka za Tanzania zimearifiwa rasmi na zimetuma maafisa wa uchunguzi wa kitaifa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati. Katika kuthibitisha dhamira yao ya kutovumilia kabisa unyanyasaji wa kijinsia na kingono, mamlaka za Tanzania zilibaini uzito wa tuhuma hizo na wamejitolea kuchukua hatua zinazohitajika kushughulikia masuala haya.”

Msemaji huyo amesema, “Kikosi kimehamishwa na kupelekwa katika kambi nyingine huku uchunguzi ukiendelea, na wahusika wa kitengo hicho wamezuiliwa kwenye kambi, hii ni kwa ajili ya kuwalinda waathirika na bila shaka uadilifu wa uchunguzi. Kikosi hicho kitarejeshwa nyumbani pindi ambapo uwepo wao hautahitajika tena kwa wachunguzi.”

Vilevile Dujarric ameeleza, “Uamuzi wa Sekretarieti kurudisha kikosi hiki ni kwa mujibu wa azimio namba 2272 la Baraza la Usalama, ambapo Baraza 'linaidhinisha uamuzi wa Katibu Mkuu wa kurudisha nyumbani kikosi fulani cha kijeshi au kuunda kitengo cha polisi cha kikosi wakati kuna ushahidi wa kuaminika wa unyanyasaji wa kingono ulioenea au wa kimfumo unaofanywa na kitengo hicho'.

Msemaji huyo wa Umoja wa Mataifa amesisitiza kuwa, "Umoja wa Mataifa unasalia na nia ya kutekeleza kwa dhati sera ya Katibu Mkuu ya kutovumilia kabisa unyonyaji na unyanyasaji wa kijinsia."
Bado vijana wa kike wa JKT wanawabaka sana pia, tunashauri rais Dkt Samia aingilie kati vijana wa kike wananyanyasika mno huko JKT.
 
Acha ushamba na kukurupuka.
Anaekurupuka ni wewe unaebaka haki za watu na hutaki ukweli ujulikane Tanzania ngono ndio kipaumbele na ukimwi umeshamiri ndio nchi ya wajinga mpaka leo bado wanaanbukizana ukimwi wakati duniani kote maambukizi yamepungua
 
Sio kwamba wanabaka directly Mzee..once ukitoka uku kwenda kulinda amani hutakiwi kufanya mapenzi na raia yeyote wa kule ata kama mmekubaliana inahesabika umebaka,ikijulikana au ukionwa tu kibarua huna tena uko Kwa taratibu zilivyo
Kwahiyo wanajitibuje ugwadu wa mwaka mzima?

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
NINA WASIWASI NA HII TAARIFA.
HAIWEZEKANI IDADI YA WATU WENGI KIASI HICHO IFANYE UBAKAJI.

Labda wahuni watatu watano.
wamebaka wanasingizia WATU wote.

Hii ni aibu KUBWA kwa JESHI letu.
HAO wanajeshi WANATAKIWA wapelekwe mahakamani.
Waliobakwa watoe USHAHIDI.

JESHI LIMEPAKWA MATOPE.


au ndio kututoa kwenye Reli msaada wa Bandari.
# SAMIA AMEUZA BANDARI
 
jeshi la nchi za kiarabu misri algeria sudan uae kuweit yemen rusia saudia china korea wapi ulisikia jeshi la nchi hizi zinabaka wanawake?
Waondoe Warusi ni Mashetani wanachofanya Ukrain wanabaka watoto wadogo sana tena mbele ya wazazi wao hao sio binadamu ni wanyama
 
Pamoja na kuikomboa Uganda, lakini jeshi letu lilijizolea sifa ya ukwapuaji huko Uganda . Nilidhani waliacha
 
Ilitakiwa wamalizane kiutu uzima, shida wanawarusha hata kile kidogo wanachawaahidi, Wacha TU wachafuke, mtu unalipwa Kwa dola, unatembea na Binti unashindwa kumfariji Kwa vijisenti!? Kwa nini wasiwaripoti sehemu husika!?
Hivi wewe una akili timamu??
 
Wametumwa wakalinde amani wao wameenda kunyandua!!anyway wametuwakilisha!!!
 
Daah aisee hatari kabisa kwa hiyo wanarudi home kwenye familia zao kwa kosa la Tupac..
 
Back
Top Bottom