Wananchi mkoani Arusha waandamana kupinga Ushoga

Wananchi mkoani Arusha waandamana kupinga Ushoga

Maandamano hayo yaliongozwa na viongozi wa dini, na wananchi walijitokeza kwa wingi kupinga matendo ya mapenzi ya jinsia moja.

Hali hii imetokana na baada ya vikundi vya kutetea mapenzi ya jinsia moja duniani kuzidisha kasi na msukumo wa kuhalalisha matendo hayo.

Tuliona presha nchi ya Qatar iliyopigwa wakati wa kombe la dunia.

Tukashuhudia vitabu vinavyofundisha mambo hayo vikisambazwa ktk shule za watoto.

Tumeshihudia shule fulani ambayo watoto wanafundishwa kufanyana kinyume cha maumbile.

Huko Kenya mahakama ya juu ikaruhusu uanzishwaji wa NGOs za kutetea ushoga ktk nchi hiyo.

Na kuna baadhi ya madhehebu ya dini duniani yameanza kurasimisha ndoa za jinsia moja na kuna Mengine yamebaki na msimamo uleule wa toka zamani wa kukataa mambo hayo machafu.

Kwa mfano hapa Tanzania Kanisa la Anglican la Tanzania limekataa katakata kukubaliana na kanisa la Anglican la Uingereza kuruhusu ndoa za mashoga. Katika barua ambayo uongozi wa kanisa la Anglican la Tanzania limeliandikia kanisa mama la Anglican la uingereza, Limegoma kabisa kukubaliana na msimamo wa kanisa hilo la Uingereza kuhusu kuruhusu ubarikio wa ndoa hizo.

Kwa bahati mbaya pia, kanisa la Kikatoliki huko Ujerumani limepiga kura kuruhusu ubarikio wa ndoa za Jinsia moja kuanzia mwaka 2026. Hii inafuatia kauli ya Papa ya kuwatakia "Rehema( Grace)" watu wote hata wale wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja.

Hapa chini ni video ya wananchi huko Arusha kuandamana kupinga mambo ya ushoga.

View attachment 2547164

View attachment 2547165
Papa kuombea Neema kwa maana ya neno ulilotumia (grace) haina tatizo lolote na haina maana ya kuunga mkono ushoga. Tunapowaombea wadhambi neema ya msamaha haimaanishi kuunga mkono dhambi. Ni kuomba Neema ya Mungu iwafikie waweze kuongoka na kuwa watu bora katika maisha.

Pili, pamoja na maandamano ya kupambana na ushoga, pia kunahitaji mikakati mipana zaidi ya hilo ili kuinua nguvu ya kupinga na kufifisha nguvu ya uungaji mkono.

Ushoga uko sponsored na unaendeshwa na watu ambao wanatambua nguvu ya fikra (mind). Hivyo wanatumia akili katika fikra pana sana na uko katika program endelevu iliyosukwa kwa ubora. Hapa panahitaji kufikiria vizuri kunielewa maana ukifikiria katika mipaka ya kihisia, kikanda, kiimani, kitamaduni n.k. utafikiri na mimi nataka kusupport ushoga.

Jiulize, je tangu ushonga umeanza kusikika ukianzia huko ulaya na kwingineko, haukupingwa? Je, ulipoanza kuingia Africa na Tanzania, haukupingwa? Je, sheria hazitungwi kuupinga? Lakini je kati ya tunaopinga na tunaunga mkono, ni upande upi unaoonekana kusonga mbele kila siku? Enzi hizo kwa Tanzania, mtu kujulikana ni shoga tu ilikuwa ni aibu lakini siku hizi tuko nao, tunakula nao, ni rafiki zetu, kwenye kamati za harusi, VIKOBA, kwenye dini zetu, wengine wanatufadhili na kutupa mitaji au kutusaidia kwa njia mbalimbali na tunawajua. Wanatupikia vyakula kwenye mahotel, tunapeana mikono ya jambo nao kila siku, hawa wanazidi kusonga mbele.

Swali ni je, maandamano haya na mengine yataweza kuzuia ushoga na mashoga wasizidi kusonga mbele? Kisaikolojia, kuna mambo ambayo kwa kadiri unavyopaza sauti ya kuyazuia ni kama maji ndivyo unavyoyapa nguvu ya kusikika na kuwafikia na kuvutia wengine zaidi. Hivyo mashoga hawatishwi sana na maandamano, zaidi wanaona hiyo ikiwa fursa kwao kwamba ushoga sasa unasikika na kuzungumzwa kila kona ya dunia kama jambo la kijamii, sio la aibu tena kuzungumzwa. Hii kwao ni mafanikio.

Je, nataka kusema tuache tusiseme au kuupinga ushoga? La hasha, lakini tunauzuiaje, tunaupingaje kwa mbinu zipi na vichocheo vyake ni vipi?

Haya ni ya kujiuliza kwa kina na kuwa na njia bora na mathubuti. Kujipanga wengi bondeni kunaweza kusiwe njia bora sana ya kuzua mkondo wa maji kupita au hata kuwasomba kama kusimama kwenu hakutaungamanishwa na njia nyingine za kimkakati zaidi na zenye kuimarishwa kimifumo katika jamii nzima.

Tusitumie mihemko, tujue mbinu na tutumie mbinu, kwa sauti tu za mihemko hakika hii vita itakuwa ngumu na hata waandamanaji wa leo tusishangae kesho tukiwaona wakiandamana kuomba haki ya upande wa pili.

TUTAFAKARI VYEMA
 
Malezi yalishatetereka leo kinachoonekana ni matokeo ya kutofundisha watoto wetu kuwa na mipaka na kiasi katika kila jambo
 
Zipo kwa PC anguu zimejaa kibao,

Siku nikipoteza PC au kuibiwa, cjui ntaweka wapi uso wangu.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
[emoji23] kumbe unaogopa tena..
 
Je hayo maandamano yatazuia ushoga?

Mashoga wanaingiliwa na wanawake??? Hao hao waandamanaji ndio mashoga buyers
 
Wanaandamana kwa ajili ya nani,ujumbe wao wamelenga kumfikishia nani
 
Back
Top Bottom