Wananchi wa wilaya ya Mlimba, Morogoro wachoma magari na vifaa vya wapima ardhi

Wananchi wa wilaya ya Mlimba, Morogoro wachoma magari na vifaa vya wapima ardhi

Hii kitu si nzuri kwa raia kujichulia sheria mikononi
Lakini pia huenda lile wimbi la UNANIJUA limerudi, wale wenye nacho wanapora kwa kutumia wale watu wanawalipa mshahara na ile Haki yako anapewa mwenye mrungula , uporaji wa ardhi kwa jina la uwekezaji ndio jina la mchezo wenyewe.

Watauawa
 
Kuwapiga risasi ndiyo kutamaliza mgogoro?
Hapana..lakini wakifanya vurugu katikati ya utatuzi wa huo mgogoro ambazo zina hatarisha uhai wa watu wengine lazima polisi waingilie kati hata kwa kuwavunja miguu.

Maana hao wanakijiji na wao kwa kuharibu mali na kuumiza watu sio kutatua mgogoro huo.
 
Wananchi wenye hasira wamewashambulia watumishi wa Ardhi kutoka wilaya ya Mlimba na kuchoma magari, pikipiki pamoja na vifaa vyao vingine wakati wakiendelea na zoezi la uhakiki wa mipaka ya mashamba yanayogambaniwa na muwekezaji na wananchi wilaya ya Mlimba, Morogoro.

Watumishi wa ardhi waliokua kwenye hilo zoezi wamejeruhiwa vibaya, japokua hakuna kifo kilichorpotiwa hadi sasa.

View attachment 1885041View attachment 1885043View attachment 1885046View attachment 1885047
washukuru MUNGU hawakuuwawa. Je wangeuwawa?

Mpaka kufikia hatua hii maana yake wananchi waliona upumbavu wanaofanyiwa umevuka mipaka, wakaona namna ya kutuliza ghadhabu na hasira zao na ili kuwepo kuheshimiana ni kutekeleza walichofanya.

Serikali itoe fundisho hapo, yasije yakatokea na ya kuzidi hayo yalotokea.
 
DC yupo, DED yupo, OCD yupo wote wanazingizia wananchi hawana matatizo huko Mlimba. Mlimba Kuna matatizo makubwa,badala ya kwenda kuwasikiliza wananchi watatumwa polisi kuwakamata.

Wananchi ni vichaa kwenda kuchoma magari moto? Iundwe time kuchunguza tukio hilo. Sio kuanza kamata kamata mkifanya hivyo mlimba nyumba zitabakia na yatima wananchi watatimkia mikoani serikali itaanza kupeleka misaada ya kwenda kutunza teza raia.
Nyie ndio mtu anaharibu mali za uma mnasema asikilizwe ana tatizo gani.

Umeshahalibu mali,utetezi hauna nafasi kwa wakati huo.
 
Walichofanya wananchi siyo kitendo kizuri, ila waliosababisha huo mgogoro wanapaswa kuwajibishwa zaidi kwa kuwa wao ndio sababu ya wananchi kujichukulia sheria mkononi.
Walichofanya wananchi ni makosa ya wale waliosababisha mgogoro katika eneo hilo, tungeanza kudili na wale waliosababisha haya yote kutokea, wananchi ni sehemu ya matunda ya mgogoro huo, tumalizane kwanza na mizizi ya mgogoro kisha turudi kwa wananchi waliosababisha hasara kwa wataalamu wasio kuwa na hatia.
Wananchi wakichoka kutumia akili basi watatumia nguvu na hakuna nguvu ya wananchi itakayoweza kumalizwa bila uwajibikaji.
 
Kuna watu wenye hasira walichoma kituo cha Polisi - Bunju DSM... kama masihara sasa watumikia kifungo cha maisha
Kuna wale walichoma Gari la Ardhi kule Dodoma na kuua wale wataaalam kwa kisingizio cha Wanyonya damu. Aysee walijuta mpaka leo Kijiji kizima wamebaki na makovu watalipa hizo gari mara tatu yake
 
Trust me , punde si punde kuna majitu yatalia na kusaga meno fasi ya mlimba wamechoma ndinga ya serikali, bodaboda ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania na tripod stand ya serikali pia wamewadunda watumishi wa umma wakiwa wanatimiza majukumu yao
Majukumu gani ya kuwahujumu wananchi na kumpendelea mchina?
Kwanini huyo muwekezaji asikwende kuwekeza kwao? Nyambafu
 
Sawa captain kinjekitile ngwale unaamini utaweza kupambana na mwenye bunduki wewe ukiwa na rungu,
Hapo najua lazima polis wataenda kutembezea jando wakaz wa hilo bushi ili next time wajue nini maana ya mali za serikali na watumishi wake
Wananchi wakiamua hizo bunduki wataziweka chini na kutimua mbio, hapa ni maamuzi tu. Wewe Kama ni mumoja wa hao wenye bunduki usijivune na kujiamini sana tenda haki. Maana usipotenda haki ipo siku bunduki unayoibeba ndiyo itakayokuua. Weka kumbukumbu ya maneno yangu dogo.
 
Kuna watu wenye hasira walichoma kituo cha Polisi - Bunju DSM... kama masihara sasa watumikia kifungo cha maisha
Walipangiwa hivyo pindi tu walipozaliwa. Kwa iyo huko kwenda kuchoma kituo cha polisi ni forces of nature iliwasukumiza hili jinsi walivyopangiwa watumike vifungo vya maisha itimie na itiki.

Jiulize wangapi wamechoma vituo vya polisi na hawatumikii vifungo vyovyote? Ni kwasababu hawakupangiwa.
 
Ndio mkuu inabidi iwe hivyo..yaani wewe mwananchi unaona polisi wenye silaha kali wanakuambia tulia wataalamu wafanye kazi lakini wewe kwa ujeuri wako hutaki,wewe unachotaka ni kuwavamia na kuwatwanga hao wataalamu..ni haki yako kula risasi ya kichwa.

Hatuwezi kuwa na Taifa ambalo kila raia ana uwezo wa kumvamia tu yoyote ili aonyeshe ana hasira..watumie njia nyingine.
Zingine Zimeshindikana wakaamua watumie hiyo nyingine
 
Back
Top Bottom