Wanasiasa wa Upinzani kuweni makini mnapofanya mahojiano na Media za Nje

Juzi tu alivyorudi alikuwa na maandamano.
Vikao vys chama vyote kulikuwa na msongamano, bado kampeni.
Chadema wamfunge speed governor bila hivyo kuna sehemu atawaharibia
Halafu mbaya zaidi mwezi ujao zinaanza kampeni vipi atahutubia wananchi kwa YouTube au atawakusanya tu na kuwatoa mhanga kwenye corona.?
 
..hivi CCM mmewahi kuwaunga mkono wapinzani ktk jambo gani?

..mbona kila siku mnawachafua na kujaribu kuwaaminisha wananchi kwamba wapinzani ni watu wabaya?

Hakuna mtu ambae amesema, au atasema wapinzani ni watu wabaya.

Ndio maana nasema kwa kutoa mifano nchi nyinigne wapinzani na serikali hufanya kazi pamoja kwenye jambo lolote linalohusu maslahi ya taifa.

Kwa mfano mimi ningekuwa Tundu Lissu kwenye issue ya COVID -19 ningeulizwa suali lolote lile nikiwa mpinzani ningesema

"Mpaka sasa hatuna taarifa zaidi kuhusiana na idadi halisi ya vifo kwa kuwa serikali haijatoa takwimu sahihi. Lakini tunajitahidi kuwabana serikali kupitia wizara ya Afya ili waendelee kutoa taarifa.

Lakini kama serikali inasema hakuna Corona nchini basi nisingependa kutoa taarifa ambazo sinazo."

Ukisema hivyo unaonekana ni kweli wewe umeiva kisiasa, kidiplomasia na hata kwenye kuchambua lipi useme na lipi uhifadhi kwani suala hilo ni kwa maslahi ya taifa.

Kuna mambo mengi yanahusika hapo uchumi, utalii na kadhalika.

lakini wapinzani si watu wabaya kabisa ila wamekosa weledi wa kukabiliana na serikali.

Na weledi huo si matusi, kejeli wala kashfa na lugha kali wala upotoshaji wa taarifa na mambo mbalimbali.
 
Wewe Una mapenzi na CCM
 
Mitano ya nduli makufuli inatosha, utawala wake wa mkono wa chuma sasa basi.
Utawala usiozingatia mifumo na sheria za nchi ni wa kienyeji sana, hatuwezi kwenda huko, mitano inatosha.
 
Kwa hiyo sisi Kama Kama corona free country tunafungulia mipaka kuruhusu wataliii watuletee micorona yao ili sisi tufe,

busara iko wapi kuzuia muingiliano na nchi waatbirika au kushangilia mapato ya utalii yatakayokuja na .maambukizi
 
Wakenya walimtibu kwa miezi 4 pale Nairobi na walimchangia damu kwa sana tu,kwa hio anawaona ni ndg.

Ni kweli kabisa kwenye hilo siwezi nikapinga.

Wakenya ni ndugu zetu na jirani zetu hivyo hatuwezi kuanza kuleteana vitendo vya kihuni.

Hayati Jomo Kenyatta na Hayati Mwalimu Nyerere walikuwa makomredi kwenye kutafuta uhuru tulo nao.

Ila uhuru huo si kuanza kuchokozana kwenye masuala ya msingi.
 
Tension ya kidiplomasia imeletwa na kiongozi mwenye mitazamo ya kichifu.
 
Mbona yy hachukui tahadhari yoyote kila nikimuona hajavaa mask, watu nyomi, pia kampeni afanye online ili kujikinga na corona kama anajali wayonge
 
Kwa hiyo sisi Kama Kama corona free country tunafungulia mipaka kuruhusu wataliii watuletee micorona yao ili sisi tufe,

busara iko wapi kuzuia muingiliano na nchi waatbirika au kushangilia mapato ya utalii yatakayokuja na .maambukizi

Lakini hao watalii wakija si hupimwa joto?

Isitoshe huko kwao wameambiwa wasisafiri isipokuwa kama ni necessary and essential.
 
Acha uzuzu wewe korona ipo sana nchini acheni siasa za kishamba hizo.
Zama za Nyerere Wazanzania ughaibuni walitembea kifua mbele wakijivunia nchi yao hadi raia wa nchi nyingine za Afrika zilizokuwa na matatizo wakawa wanajiita Watanzania au watoto wa Mwalimu. Sitashangaa kama Watanzania walioko ughaibuni wanaona aibu kujitambulisha na nchi yao badala yake wanajiita Wasomali maana hao ni majasiri kuliko Wabongo. WaTz hata akili za kutuwexesha kwenda ughaibuni kwa shughuli yoyote hatuna hata lughà za huko hatujui. Kenya ugonjwa wa Covid-19 unaenea kwa kasi sana na ili kutulinda sisi tusio na ugonjwa huo, walizuia ndege zetu zisitue nchini humo zisichukue coronavirus kuleta kwetu, Wakenya wakaambulia matusi wanazuia watalii wasije kwetu. Wafu wa Covid-19 hata Marekani hawazagai mitaani Bali wanazikwa na Serkali fasta bila hata ndugu kuwepo.
Acha uzuzu wewe korona ipo sana nchini acheni siasa za kishamba hizo.
 
Wengi ambao wamepata kufuatilia haya mahojiano walikuwa waki-base zaidi kwenye majibu ya Lissu lakini hawakutilia maanani sana katika maswali aliyokuwa akiulizwa.

Kitu kingine ni kuwa wengi hawafahamu kuhusu COVID-19 ndio maana imekuwa rahisi sana kwa wengi pia kusema kuwa haipo.

Kumekuwa na tahadhari kadha wa kadha ambazo zimekuwa zikitolewa na serikali nchini Tanzania kuhusiana na COVID-19, tahadhari ambazo nafikiri hata Lissu katika mahojiano hayo amezisema. Sasa kwanini tuchukue tahadhari hizo kama tatizo halipo?!

Wewe mleta uzi unapoulizia uwepo wa COVID-19 "kwa takwimu zipi?" pia usiache kuuliza kwanini serikali imekuwa ikitoa tahadhari kuhusiana na COVID-19 kama kweli haipo?
 

Ni lini na wapi raisi Magufuli alitamka hadharani kuwaambia wananchi wasichukue tahadhari ya ugonjwa wa COVID-19?

Tuende na vielelezo mkuu.
 
Kwenye familia yenu wamekufa wangapi kwa corona.?
Hili swali la kijinga hata KUKU wako hawezi kuuliza. Kwetu hakuna aliyewahi kufa kwa Ukimwi, narudia hakuna. Kwa hiyo Ukimwi umeisha?
 

..CCM ndiyo vinara kwa kuwachafua wapinzani.

..Jpm aliji-quarantine Chato kwa siku 30+, kwanini iwe nongwa kwa Mbowe kuji-quarantine kwa siku 14?

..lakini hivi tunavyofanya kuhusu covid19 nadhani tunatisha na kufukuza watalii kuliko kuwa-attract.

..Jpm na serikali hawajui PR ya huu ugonjwa wa covid19. Kuna nchi zina maambukizi kutuzidi sisi lakini raia wake wamefunguliwa milango na mataifa mengine.

..YES, hatujaathirika lakini ni lazima tuonyeshe kwamba tunachukua tahadhari, na pia tuonyeshe kwamba tuna uwezo wa kumsaidia mgeni yeyote yule ikiwa atapatikana na covid19 akiwa hapa nchini.
 
Shetani ni shetani tu, ukikaa vibaya anakumiminia risasi 38, ogopa shetani.

Hawa wapinzani tatizo hawajui wanachokisimamia, wanabweka hovyo hovyo tu kwa kila kilicho mbele yao bila mpangilio. Mbaya zaidi wanatengeneza mazombie huku uraiani yani ni balaa tupu. Watu wanaburuzwa tu hovyo hovyo bila kujitambua. Iko safari kubwa sana na ndefu hadi kufikia kuiondoa CCM.
 
....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…