Wanaume tupeni majibu sahihi kwanini mnapenda kuwachumisha wengine dhambi?

Wanaume tupeni majibu sahihi kwanini mnapenda kuwachumisha wengine dhambi?

We we we!!!!! usikanyage huko, ujue mke wa mtu mimi, na huko mme wangu anashinda sasa jitupe mkajibizane nae.

hahahhaa................. The Dealer uwe machom usije tolewa utumbo huko
 
Last edited by a moderator:
Dada zangu kabla hamjatulaumu sisi wanaume...ingekuwa vyema kwanza na nyinyi mkajitathmini kwa namna moja au nyingine...ukiangalia katika jicho la tatu utagundua kuwa wanawake wa karne hii wamepoteza sifa za kuolewa kwa sababu ya tabia zao mbovu....wengi wao wanasifika kwa kuwabambikia mimba wanaume....wengi wao wanasifika kwa kuwagonganisha wanaume....katika hali kama hiyo nani atakuwa na amani na kuwajibika katika ujauzito ambao una mashaka nayo....hakuna mwanaume aliyetimamu wa akili ambaye atakuwa na amani kulea mimba ya mwanamke ambae mara kibao alikuwa anamfumania....
 
unless hujanielewa nilimaanisha kwamba kwann akina baba hawaoni hayo uliyoyasema mwanzoni.............
ndo mana nikauliza kwann hamlioni hili mnaishia kuzitenda familia zenu hasa watt?

Wanayaona isipokuwa wanakatishwa tamaa na tabia zenu za kuwabambikia waume zenu mimba.....
 
dada zangu kabla hamjatulaumu sisi wanaume...ingekuwa vyema kwanza na nyinyi mkajitathmini kwa namna moja au nyingine...ukiangalia katika jicho la tatu utagundua kuwa wanawake wa karne hii wamepoteza sifa za kuolewa kwa sababu ya tabia zao mbovu....wengi wao wanasifika kwa kuwabambikia mimba wanaume....wengi wao wanasifika kwa kuwagonganisha wanaume....katika hali kama hiyo nani atakuwa na amani na kuwajibika katika ujauzito ambao una mashaka nayo....hakuna mwanaume aliyetimamu wa akili ambaye atakuwa na amani kulea mimba ya mwanamke ambae mara kibao alikuwa anamfumania....

nimekuelewa kabisa kaka/mdogo wangu.
Lakin naomba nikuambie kwamba huyu mbaba ambaye anao uhakika na watoto wake mathalan mtu umemzalisha mkeo watt 3 ama 2 afu unamtelekeza kwa miaka kadhaa unakuja kurudi kwake tena ukiwa umechoka magonjwa yanakusumbua ahivi wewe unakuwa unawaza nini?

Manake kama umenifumania ukaniacha basi usirudi tena kwangu kinachokurudisha ukiwa mgonjwa ni kitu gani?
 
Hivi kama mimi sijafanya hili,naweza kujibu hili swali kweli?

By the way,hili ni tatizo kama lile la wanawake kutojua wanachokihitaji kwenye mahusiano

Tatizo ambalo hata kwa wanaume lipo vile vile,kama.vile ambavyo hilo lako lilivyo kwa wanawake vile vile

Kimsingi kila mtu anaweza kuwa na sababu zake za kufanya jambo hivyo jibu linaweza kuwa tofautu kati ya mtu na mtu!
 
mie ilo la kusema wanalogwa najiliza kwanza unalogwa wewe ulikuwa wapi??
uliyumwa uanze ukaribu na mtu asiyekuwa jamaa yako?
wee kilichokupeleka kula kwa watu kitu gani?

Dunia hadaa...
Chanzo cha yote tamaa..
Kimada anapewa chapaa..
Mke ananyimwa dagaa...
Watoto wanaranda kitaa...
Mama anachoka chakaa..
Watoto wanalia njaa..

Ndoa imekua kichaa..
Shetani kati kakaa...
Usije ikatia tamaa..
Mpinge kwa sala duwaa..
Nayo itatengemaa...

Samehe saba sabini!
Usihoji chanzo kilikuwa nini!
Maana jibu li wazi,shetani!
 
sasa Mungu anajiinua mkiwa na matatizo ndo mnakumbuka wtt mliowatelekeza na wtt hao hao Mungu kashawainua ndo inakuwa mwanangu nisaidie! !! kasaidiwe ulikokuwa mtt akisusa mdo watu mnaibuka dhambi .mlikuwa wapi kumwambia baba yake dhambi alipotelekeza familia? alieuwa kwa upanga nae atauwa kwa upanga
 
Kwahili, Mtuombee tu sisi wachache wetu tusiwe hivyo.
 
Let me ask you, yaani niishi kwa mateso ambayo hayavumiliki kwa mtu ambaye hana muelekeo? Sikua kabisa radhi mtoto kuondoka lakini kwa kuwa ni mzazi mwenzangu kaenda home na wanamjua akasema anakwenda likizo atamrejesha na amegoma kumleta labda wewe unashauri nifanyaje? Nikamuoe?

Hilo ni gunia l msumari ukimuoa ni kuongeza matatizo n kukosa furaha y ndoa kma uliishi nae ukaona hakufai ukirudi hpo stress zitakuua.mimi nlipitia maisha hyo ila nlionyesha msimamo wng mtoto naishi nae mama yke alinisumbua ikafikia mahali ningepata murder case ila mungu aliniepusha
 
Dada zangu kabla hamjatulaumu sisi wanaume...ingekuwa vyema kwanza na nyinyi mkajitathmini kwa namna moja au nyingine...ukiangalia katika jicho la tatu utagundua kuwa wanawake wa karne hii wamepoteza sifa za kuolewa kwa sababu ya tabia zao mbovu....wengi wao wanasifika kwa kuwabambikia mimba wanaume....wengi wao wanasifika kwa kuwagonganisha wanaume....katika hali kama hiyo nani atakuwa na amani na kuwajibika katika ujauzito ambao una mashaka nayo....hakuna mwanaume aliyetimamu wa akili ambaye atakuwa na amani kulea mimba ya mwanamke ambae mara kibao alikuwa anamfumania....

Ndugu uko na umri gani? Wanaume kutelekeza wake na watt haikuanza hii karne ilianza toka enzi na enzi sidhani kama kuna sababu ya maana zaidi ya kuwa ni laana.
 
My hakuna limbwata wala nini, wanaume wengi wanatamaa sasa anapojikuta kampa mimba mwanamke ambaye sio chaguo lake anaweza kumlazimisha bint atoe na akikataa anatoka nduki mita 1000, hapo hata mtoto hana habari nae. siku zote wanawake kwa hili ni wahanga kabisa.

Usemalo ni kweli ila huwezi lazmisha roho impende mtu kma humpendi toka rohoni,kufake furaha n jambo gumu sana ni bora uwe muwazi kumweleza 2 kua nitalea mtoto kukuoa cwezi.kulazmisha furaha ni ngumu sana mana furaha inakuja automaticaly rohoni mimi n muhanga w jambo hilo i
 
Ndugu uko na umri gani? Wanaume kutelekeza wake na watt haikuanza hii karne ilianza toka enzi na enzi sidhani kama kuna sababu ya maana zaidi ya kuwa ni laana.

Na matukio ya wanawake kuwasingizia mimba wanaume hayakuanza leo....
 
Upo sahihi sana ila ukijaribu kuchunguza kabla ya baba kuacha watoto unakuta huko ndan ya nyumba yao kulikuwa na sinto fahamu ya muda sana na wanaume unajua tunanyanyaswa sana siku hizi ni kina mama yaan ni siri yetu, Na unakuta mwanamke anakuletea mapozi kisa tu mmeshafunga ndoa ataleta timbwili kila kukicha inafikia had haki ya ndoa tunanyimwa hafu ukimwangalia mwanamke mwenyewe ukimuamilia hata dk achukue kabla hujamharibu sura na hapo watoto wako kwenye age ya kisheria kuwa inatakiwa wawe chin ya uangalizi wa mama...unadhan nin kinafuata hapo?

Hapo hakuna sababu bado ya kutelekeza damu yako kuna sheria zipo watt watabaki na mama angalia jinsi ya kuwasaidia hao watt lakini ati ugombane na mke ususie na damu yako. Kuna wanaume wanaoa wake kama mashetani lakini utaona atahakikisha watt wake wanapata mahitaji kutoka kwake yeye baba na nikauambia mtt akipendwa na baba na baba akawa ni mzuri hata mama aongee uovu gani kuhusu baba yao watt watampenda baba yao tu! So hakuna sababu ya kutelekeza damu yako.
 
Na matukio ya wanawake kuwasingizia mimba wanaume hayakuanza leo....

Hayakuanza leo lakini zamani kulikuwa na traditions kali. Unataka kuniambia unaacha mke na watt zaidi ya wawili wote hao unasema umesingiziwa? Na kama umesingiziwa mbona uzeeni unarudi utanataka wakusaidie? Mjaribu kureason kama binadamu na si mbwa ambaye hajui hata alizalisha nani na wtt waliishia wapi.
 
Mtoa mada salute cc vjana Wengi sana maarufu Leo Na wengne tupo serikalini ktk vtengo vya maana ukchunguza tumelelewa tu Na mother ding tumewajua miaka hii ya 2000 wameanza kujipendekeza Baada yakusikia tupo mavyuo dats why m/ mungu huwahukumu at the end of a day wamechoka Na vsukari wanakujaa kuomba msaada. Nakwambia kutoka rohoni namsiklizia tu ding azeeke astaafu kaz aanze blah bla za uzee kudeka kwa kdume mm kwakweli ntakuwa realistic
 
Hayakuanza leo lakini zamani kulikuwa na traditions kali. Unataka kuniambia unaacha mke na watt zaidi ya wawili wote hao unasema umesingiziwa? Na kama umesingiziwa mbona uzeeni unarudi utanataka wakusaidie? Mjaribu kureason kama binadamu na si mbwa ambaye hajui hata alizalisha nani na wtt waliishia wapi.

Sifa ya kiume sio kurudia matapishi yako...
 
Dada zangu kabla hamjatulaumu sisi wanaume...ingekuwa vyema kwanza na nyinyi mkajitathmini kwa namna moja au nyingine...ukiangalia katika jicho la tatu utagundua kuwa wanawake wa karne hii wamepoteza sifa za kuolewa kwa sababu ya tabia zao mbovu....wengi wao wanasifika kwa kuwabambikia mimba wanaume....wengi wao wanasifika kwa kuwagonganisha wanaume....katika hali kama hiyo nani atakuwa na amani na kuwajibika katika ujauzito ambao una mashaka nayo....hakuna mwanaume aliyetimamu wa akili ambaye atakuwa na amani kulea mimba ya mwanamke ambae mara kibao alikuwa anamfumania....

Mbona hata mkioa wenye tabia njema huwa mnarudi kwa wenye hizo tabia ambazo unasema hawafai kuolewa?

Point ya msingi ni malezi kwa watoto. Mtoto ni baba na mama, tabia mbaya ya mama ndio mtoto akose hata matibabu au sare ya shule?
 
Back
Top Bottom