Wanaume, watoto wako hawawezi kukugeuka ikiwa ulishiriki malezi Yao tangu mwanzo

Wengine hata huyo dingi hatujui kama kafa au yuko hai.

Nadhan mfumo wa maisha hasa mjini baba harakati nyingi, kutoka kumi na mbili kurudi night kali madogo washalala, wanaishia tu kujua ni baba ila time nao hana.
Ni mbaya sana sana hii kitu, baba unakua upo kama haupo vile.
 
Subiri wa kiume wamalize shule uone kali yake!
 
Grahams babu vipi watoto wako Huwa unafanyaje kuwaonyesha wewe ndio mzee wao
Huwa nashiriki kwenye malezi yao tangu wakiwa mimba...

Unaposhiriki malezi tangu wakiwa tumboni then hata baada ya Kuzaliwa kwao, hutengeneza bond baina yao na Mimi.

Kingine, nawajibika. Mimi ni Baba ninayependa kuwajibika Kwa malezi na makuzi ya watoto wangu. Kuwajibika huku ni pamoja na kuwafanya watoto waone hakuna Baba mzuri na anayeweza kuwahudumia Kwa chochote zaidi yangu.

Kingine wanapotaka hela ya shopping nampa Mama yao hela mbele yao

Bila kusahau kuwashirikisha Mipango yetu ya maendeleo. Mfano Kuna Kiwanja nataka kuanza Ujenzi huwa nawaambia.

Nikiwa napitia kipindi kigumu cha kifedha, huwa nawaambia na huishia kuniambia Baba tunakuombea uwe na hela kama Jana 🤗🙏🙏
 
Subiri wa kiume wamalize shule uone kali yake!
Unataka kusema atanimind,,,nadhan inategemea na malezi ya mama yao,lakini mama yao yupo smart sana na anajali makuzi ya wanae,,,wamama wabaya ni wale ambao wanapandikiza chuki kwamba baba yenu mbaya na mambo kama hayo
 
mimi mzee hata kula nae meza moja ni kipengele.. sijui alikua na shida gani mbinafsi balaa
Mi mzee alikuwa sio mbinafsi, ila akianza kutoa kichapo utatamani kuhama maskani. Ukizua mambo ya skuli akikupeleka anakusulubu mboko mpaka waalimu wanakuombea msamaha hata kama ilikuwa wakuadhibu.
 
Wewe ni baba Bora sana
Waje wachukue notes hapa
 
Duh! Stori za humu zinanitisha.

Mimi baba yangu alitujali sana. Anatupeleka shule na gari yake na kisha anapitia kazini kwake.

Muda wa kurudi nyumbani dereva wake anatufuata au tunarudi wenyewe. Wakati wa kula familia tunakula pamoja mezani na mzee alikuwa na tabia kama mboga (nyama) mama alikuwa anamwekea za kwake maalumu. Baba yetu alikuwa anatoa za kwake na kutugawia tena sisi watoto. Mama utamuona anamwambia sasa wewe utakula nini? baba anamwambia; waache bhana watoto hawa.

Siku ya jumamosi na jumapili muda wa jioni anakaa na watoto wake ana kaa karibia na eneo la parking kuna mahali pa kupumzika tunakaa tunapiga naye stori.

Muda wa mpira tunaangalia naye wote. Nilikuwa namtania nacheka kama yeye anavyocheka ataniangalia basi mama atacheka mpaka bhasi!

Kwenye mipango yake ya biashara alitushirikisha. Kwa ufupi alitujali sana! Yeye na mama walitujali sana na tulipokesea waliturekebisha.

Kwa sasa nina umri wa miaka 31. Baba yangu ameshatangulia mbele ya haki. Kila siku kila baada ya swala huwa namuombea kwa Mungu. Na kila baada ya wiki moja au mbili huwa nafanya dua maalumu ya kumuombea.

Nawapenda wazazi wangu wote wawili. Na huwa sipendi kabisa kusikia mama yangu ana tabu. Akiwa na changamoto yoyote chapu kwa haraka naishughulikia.
 
Sisi baba yetu siku za jumamosi au jumapili asubuhi utamuona anatengeneza mkate wa kukaanga ana kaanga na mayai. Basi mama anamwangalia tu!

Utamsikia baba anasema hii ni tamu sana! Halafu anaonja mwenyewe utamsikia ewaaaa! Hii safi kabisa! Mtaipenda.

Kingine amenifanya kwenye chai au uji naweka asali badala ya sukari. Ndiyo ilikuwa tabia yake sukari kwake hapana.
 
Kila siku nashukuru kwa kuwa na baba huyu niliyenayee, huwa nawaza je angekua mwingine ingekuaje kwa upande wangu?

Baba angu nampenda kuliko chochote, nae ananipenda na ananithaminiii, Nafurahia uwepo wake na aishi miaka mingi zaidi ili niendelee kufaidi matunda yakee.

[emoji120][emoji120][emoji120]
 
Thanks for sharing madam, kuna vitu nimevinote nitavi apply..
 
Mungu amtunze sana 🙏
 
Kma nakuona unavodekaga 😃😃
 
Wale wanaodanyana kwa harakati uchwara za KATAA NDOA waisome
 
Usiongee ukamaliza
Hizi fikra mimi nazikataaga

Kupata watoto wema ni tawfiq ya Allah kwa hiyo Allah anawachagulia watu fulani wawe na watoto wabaya na wengine wawe na watoto wazuri ?

Hizi ni itikadi zisizokuwa na mashiko kabisa ambazo binafsi nazipiga vita,LAZIMA UFANYE JUHUDI NA UTUMIE AKILI ALIYOKUPA ALLAH KULEA WATOTO.

Kulea sio kupeleka watoto shule na madrasa pekee,kulea kuna mambo mengi na ukiyakosea lazima upate toto ovu na wala jambo hilo halihusiani na tawfiq ya Allah.

Tunamsingizia sana Allah kwa mambo ambayo yapo mikononi mwetu.

وما أصابكم من مصيبة فبما كسبت أيديكم ويعفو عن كثير

[ ASH-SHUURA - 30 ]
Na misiba inayo kusibuni ni kwa sababu ya vitendo vya mikono yenu. Naye anasamehe mengi.
 
Shukrani mkuu
Kumradhi km neno haiwezekani huenda nimelitamka sehemu isiyo sawa
Kukugeuka nimemaanisha kwenda kinyume na wew lakin pia sikumaanisha ni Kwa watu wote Iko hivo inategemea na moyo pia wa mtoto hakuna mzazi asiempenda mwanae ila changamoto ni kuwajibika na kusimama km baba
Fuatilia watu wengi tunajifunza tukiwa wadogo sana na chanzo Huwa ni familia,shule na vitu vingine ni ziada ila Huwa tunajifunza kuanzia nyumbni
Mtoto aliefanyiwa ukatili akiwa mtoto kuwa mwema ni kitu kigumu

Mtoto alieonyeshwa upendo kuwa na upendo ni rahis japo pia sio wote pia
Ukimkuta mtu hajali chochote kuhusu wengine ukimuuliza sabbu hawez kukosa kusema nae hakuthaminiwa hivo Hainamaana kujali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…