Wanaume wenye watoto tupeni uzoefu wenu. Mara ya kwanza unampelekea Mwanamke wako hospitali kujifungua, hiyo siku ilikuwaje?

Wanaume wenye watoto tupeni uzoefu wenu. Mara ya kwanza unampelekea Mwanamke wako hospitali kujifungua, hiyo siku ilikuwaje?

Mtoto wa kwanza ...ni...liambiwa uchungu bado nikaelekezwa kwenda kununua vidonge vya uchungu nikampelekea....siku ya kwanza hola...siku ya pili akaambiwa afanye mazoezi kupanda na kushuka ngazi za pale kwa Kariuki hosp..mi njikaenda kupiga vombo.....nimeibuka alfajiri hospitali niko bwii,,nikamkuta mama watoto ameshajifungua,,,,nikakabeba katoto nusura nianguke nako...but was ok
 
Hongera sana mkuu wewe ni mume bora kabisa. Utakuwa baba bora pia.

Umenikumbusha kipindi changu, baba watoto alivyokuwa na heka heka safari za hospital -nyumbani kama zote. Akirudi nyumbani kufuata chakula akikuta mdada anazubaa zubaa anaingia jikoni mwenyewe anapika (ndio nilijua kumbe anajua kupika😂😂😂).
Asante sana Hannah naamini kabisa wewe ni mama bora pia na uko na baba bora pia.
Ukweli wakati mwanamke anahangaika na uchungu mwanaume pia anakuwa na mahangaiko makubwa sana , hakai sawa kabisa hadi mama awe ametoka chumba cha kujifungulia, anafanya kila harakati kuhakikisha mwanamke anakuwa na utulivu wakati wa ujauzito kujifungua na uzazi, hata kama hakuwahi kuingia jikoni kupika au kufua anakuwa mwepesi sana kwa hilo.

Pongezi kwako hannah, yote mema kwako na mwana.
 
Picha limeanza saa tisa usiku,,baby mama uchungu umempata na kumbuka baby mama wangu hujifungua kwa operesheni

So mwelekeo ni muhimbili na ndio mtoto wangu wa kwanza,nipo makazi africana mbezi,,mungu mkubwa nje kuna nissan march kadogo kadogo hivi ndio nikakapiga start hao muhimbili,,yaan baby mama anaugulia maumivu mwamba namtaja Allah kwa sana na kumtukuza atufikishe salama

Dah ilikuwa experience ya kipekee sana
Mtaani kwetu kuna demu kajifungua kwa njia ya operesheni mara 3 kwahiyo watu wanadai wanakulana nyuma ndio maana mke hazai kawaida
 
Inabidi ujipange haswa kwenye cash, endapo ikitokea ameshindwa kujifungua kwa njia ya kawaida anahitaji kisu, apo mzee wangu jipange kwa gharama ..pia madakitari watakuwa wengi sana kipindi icho mzeemama anajifungua😀😀(apa ni wale majirani, ndugu, marafiki) mambo mengine ni kawaida tu kumuhudumia mzazi. Apo Sasa ndo uanaume unaonekana..😂😂😂

Siyo powa brooo
Kama kiasi gani uwe nacho?
 
Mtaani kwetu kuna demu kajifungua kwa njia ya operesheni mara 3 kwahiyo watu wanadai wanakulana nyuma ndio maana mke hazai kawaida
Kuna mijadala kama hiyo mitaani hasa hawa shombe shombe lkn huenda hakuna ukweli wowote

Na hata hao ambao wanafanya michezo hiyo nasikia wanahospital zao maalum ambazo wanafichiana aibu zao huko

Anyways lililokubwa zaidi wengine nyonga zao hazifunguki hivyo kushindwa kuzaa kwa kawaida,mfano mama watoto wangu mimba ya kwanza ilikuwa operation,,ya pili walimchelewesha kidogo kuona kama atazaa kwa njia ya kawaida lkn ikashindikana so wakaamua kumpiga kisu,kwahiyo watoto wote watatu ni kwa operationi,,ishu ni kimaumbile zaidi na si habar za mtaani
 
Hili ni jambo la kujifunza sasa ukikataa watajifunzia wapi? Maana hata huyo Dr alikuwa mwanafunzi akajifunzia kwa wagonjwa akajua je na wao wangekataa ingekuwaje kwa mkeo?
Madam ishu hapa si kujifunza bai ishu ni wanafunzi wengi kuingiza mikono kwa my baby mama

Ingekuwa mmoja au wasio zidi wawili ningeelewa lkn sijui wanafunzi wengi hapana

Wasubiri kesi kama hiyo itokee tena wafanye mazoezi huko
 
Uzazi wa pili Kipindi kile corona imepamba moto 2020 ingawa ilikua vyepesi sana lakini kidogo akili iliyumba.

Uzazi wa kwanza ndio sita sahau!
Kwanza kabisa hospitali ya jirani walisema uzazi wa kwanza lazima mwananyamala ama sinza.
Nikaomba sinza tukaelekezwa maana tulikuwa wa geni dar, hatuna mwenyeji hata mmoja.
tukaenda, kipimo tukaambiwa kurudi tarehe fulani, siku hio tulivyorudi nikaambia anabaki nirudi nikaandae chakula na vinginevyo, bahati nzuri tulipewa abc za kujifungua so vifaa alikuwa navyo.
Siku ya kwaza ikakata, siku ya pilli nayo ikakata!
Nikashauriwa na daktari kwamba njia imekataa kufunguka inatakiwa dawa fulani kama kumbukumbu ziko vizuri ni dinoproston, bei 50,000 kidonge kimoja! Nilizunguka mji wa dar es laam karibu kila famasia hio dawa hamna, siku inayofuata nikarudi pale namwambia ness nimekosa akanijibu ongea na watu vizuri dawa ipo hapa hapa lete hela nikuchulie!
Nusu saa nyingi dawa ikapatikana!
Akapewa dawa hata haikusaidia, siku ya nne ikaisha , siku ya tano asubuhi na fika pale mtu wa kwanza naulizia mapokezi pale nikaambiwa bado, mwanamke alishuka gorofani maana sehemu ya kujifungulia pale sinza ipo juu, ile tunakutana alikua ana lia! Nilijikaza kiume ingawa machozi yalikua yananilenga mno! Tulivyo achana nisiseme uongo nilitoka nje nikalia kwa kweli! Akaja mama mmoja simjui ila alisha nisoma, akanipeleka kwenye mgahawa akanunua chai akanipa, akaniambia wewe ni mwanaume kuwa mwanaume!

Nikarudi nyumbani kuandaa chakula jioni nikaenda tena hali ni ile ile.

Mungu ni mwema asubuhi siku ya sita saa 12 asubuhi nafika pale nikajitambulisha nikaambiwa panda juu, kufika naonyeshwa mtoto mama bado hakaa sawa katika operation dakika kumi zilizopita, nilishukuru aisee mtoto wa kiume uzito kg 4.2.
pole sana mkuu uliyopitia hayatofautiani na ya kwangu, leo binti yangu anatimiza miaka minne kikubwa ni kusema alhamdulillah
 
Sintosahau ile siku ya uchungu kwa kweli. Kila kitu nilikichukulia mzaha sana maake mimi na mke wangu tumeishi kwenye mazingira ya utani na vimbwanga sana. Kuna ka system kaliingia ka baba kwenda kumtazama mkeo akijifungua. Kiufupi nilinaswa kofi nene na daktari msaidizi

Sijawahi fika wodi ya ujauzito hadi hii leo tena
 
Asante sana Hannah naamini kabisa wewe ni mama bora pia na uko na baba bora pia.
Ukweli wakati mwanamke anahangaika na uchungu mwanaume pia anakuwa na mahangaiko makubwa sana , hakai sawa kabisa hadi mama awe ametoka chumba cha kujifungulia, anafanya kila harakati kuhakikisha mwanamke anakuwa na utulivu wakati wa ujauzito kujifungua na uzazi, hata kama hakuwahi kuingia jikoni kupika au kufua anakuwa mwepesi sana kwa hilo.

Pongezi kwako hannah, yote mema kwako na mwana.
Sure Mkuu.
Ujue wanasema mwanamke anabeba ujauzito kwenye tumbo lake wakati huo huo mwanaume amebeba huo ujauzito kichwani kwake. Mwanamke na mwanaume wote wanakuwa wameubeba huo ujauzito.

Mungu awabariki wanaume wote walio pamoja na wake zao sambamba katika hatua zote za ujauzito hadi kujifungua.
 
Sku naambiwa hongera Sasa unaitwa baba kwa njian ya sms , ilikua niko first year nko kwenye kipind Cha medical psychology hakika kile kipind sikukielewa nikaamua nikalale kwanza hostel nilijawa na wenge la hatari
 
Back
Top Bottom