Wanaume wenye watoto tupeni uzoefu wenu. Mara ya kwanza unampelekea Mwanamke wako hospitali kujifungua, hiyo siku ilikuwaje?

Mtoto wa kwanza ...ni...liambiwa uchungu bado nikaelekezwa kwenda kununua vidonge vya uchungu nikampelekea....siku ya kwanza hola...siku ya pili akaambiwa afanye mazoezi kupanda na kushuka ngazi za pale kwa Kariuki hosp..mi njikaenda kupiga vombo.....nimeibuka alfajiri hospitali niko bwii,,nikamkuta mama watoto ameshajifungua,,,,nikakabeba katoto nusura nianguke nako...but was ok
 
Asante sana Hannah naamini kabisa wewe ni mama bora pia na uko na baba bora pia.
Ukweli wakati mwanamke anahangaika na uchungu mwanaume pia anakuwa na mahangaiko makubwa sana , hakai sawa kabisa hadi mama awe ametoka chumba cha kujifungulia, anafanya kila harakati kuhakikisha mwanamke anakuwa na utulivu wakati wa ujauzito kujifungua na uzazi, hata kama hakuwahi kuingia jikoni kupika au kufua anakuwa mwepesi sana kwa hilo.

Pongezi kwako hannah, yote mema kwako na mwana.
 
Mtaani kwetu kuna demu kajifungua kwa njia ya operesheni mara 3 kwahiyo watu wanadai wanakulana nyuma ndio maana mke hazai kawaida
 
Kama kiasi gani uwe nacho?
 
Mtaani kwetu kuna demu kajifungua kwa njia ya operesheni mara 3 kwahiyo watu wanadai wanakulana nyuma ndio maana mke hazai kawaida
Kuna mijadala kama hiyo mitaani hasa hawa shombe shombe lkn huenda hakuna ukweli wowote

Na hata hao ambao wanafanya michezo hiyo nasikia wanahospital zao maalum ambazo wanafichiana aibu zao huko

Anyways lililokubwa zaidi wengine nyonga zao hazifunguki hivyo kushindwa kuzaa kwa kawaida,mfano mama watoto wangu mimba ya kwanza ilikuwa operation,,ya pili walimchelewesha kidogo kuona kama atazaa kwa njia ya kawaida lkn ikashindikana so wakaamua kumpiga kisu,kwahiyo watoto wote watatu ni kwa operationi,,ishu ni kimaumbile zaidi na si habar za mtaani
 
Hili ni jambo la kujifunza sasa ukikataa watajifunzia wapi? Maana hata huyo Dr alikuwa mwanafunzi akajifunzia kwa wagonjwa akajua je na wao wangekataa ingekuwaje kwa mkeo?
Madam ishu hapa si kujifunza bai ishu ni wanafunzi wengi kuingiza mikono kwa my baby mama

Ingekuwa mmoja au wasio zidi wawili ningeelewa lkn sijui wanafunzi wengi hapana

Wasubiri kesi kama hiyo itokee tena wafanye mazoezi huko
 
pole sana mkuu uliyopitia hayatofautiani na ya kwangu, leo binti yangu anatimiza miaka minne kikubwa ni kusema alhamdulillah
 
Sintosahau ile siku ya uchungu kwa kweli. Kila kitu nilikichukulia mzaha sana maake mimi na mke wangu tumeishi kwenye mazingira ya utani na vimbwanga sana. Kuna ka system kaliingia ka baba kwenda kumtazama mkeo akijifungua. Kiufupi nilinaswa kofi nene na daktari msaidizi

Sijawahi fika wodi ya ujauzito hadi hii leo tena
 
Sure Mkuu.
Ujue wanasema mwanamke anabeba ujauzito kwenye tumbo lake wakati huo huo mwanaume amebeba huo ujauzito kichwani kwake. Mwanamke na mwanaume wote wanakuwa wameubeba huo ujauzito.

Mungu awabariki wanaume wote walio pamoja na wake zao sambamba katika hatua zote za ujauzito hadi kujifungua.
 
Sku naambiwa hongera Sasa unaitwa baba kwa njian ya sms , ilikua niko first year nko kwenye kipind Cha medical psychology hakika kile kipind sikukielewa nikaamua nikalale kwanza hostel nilijawa na wenge la hatari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…