Wanaume wenzangu fanyeni mazoezi acheni kula chips yai

Wanaume wenzangu fanyeni mazoezi acheni kula chips yai

Niajee wakuu,

Mazoezi ni muhimu sana.

Shauri yenu!!!

Mwanaume ata kupiga push ups 10 huwezi, kukimbia nayo huwezi, ata kutembea mdogo mdogo km ½ nayo huwezi.

Achaneni na chips yai wazee pigeni tiz(mazoezi ya viungo).

Hivyo vitambi waachieni wake zenu.

Mazoezi kwa afya bora.
We unapata wapi ujasiri wa kupangia watu maisha? Janabi atupelekeshe na wewe nae utusumbue, aaaghhhh
 
Mkuu umegusa penyewe...yaani kwenye msosi hapo umesahau kuongeza kitimoto rost na Castle lite baridi
Acha tu nibaki na kitambi changu mimi siwezi kwenda gym kunyanyua mavyuma mazito yaani nijitese utadhani niko kwenye mafunzo ya kijeshi?
Kwanza sisi vibonge wenye vitambi tunaaminika sana mitaani tunaonekana hatuna njaa
Mimi huwa nawala sana mademu wa chuo hapa Dom wengi wakiona body langu wanaamini nna maokoto ya kutosha halafu ni mtu wa serikali kumbe muuza majeneza tu!
Kuleni misosi vijana mnenepe acheni kujitesa mazoezi waachieni wacheza mpira na walinzi wa club
Maisha yenyewe tunayoishi ni magumu kuzidi hata hayo mazoezi yenyewe bado ukajitese kukimbia 5km na kubeba vyuma halafu unakuta unashindia chapati mbili na supu ya pum. bu au mapupu! Mtakondeana mpaka mkufwe!!
Watu wanajibana sana sijui wanataka kuanza kuishi lini wakifurahia maisha. Misosi hawatupilii, maji wanakunywa kwa kujibana na bia mbili nazo hawazitaki, mwishowe wanaona maisha magumu.
 
Back
Top Bottom