WANAUME WENZANGU: Umewahi kufanya jambo ukaja kujuta baadae kama mimi ninavyojuta mpaka sasa?

WANAUME WENZANGU: Umewahi kufanya jambo ukaja kujuta baadae kama mimi ninavyojuta mpaka sasa?

Nikuulize kitu Kapeace

Wapi uliona vitabu vitakatifu vinazungumzia Karma?

Hizi ni mambo tu watu wamejitungia kutishana tu
Kula andiko hilo
``Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.
Luka 6:38
 
Yani we mkware wewe,, hebu punguza dhambi unaona unavyohangaika umeniquote mara mbili kwa comment moja,, karma ipo kaa kwa kutulia hasa kwa makosa ya kukusudia km ya mtoa mada kumzalisha na kumtelekeza dada wa watu, chozi na simanzi ya huyo dada iko juu yake
😄😄😄 ninachojua ni mtu mwenyewe ndiye huvuna matoķeo ya dhambi zake.
``Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.
Luka 6:38

Wagalatia 6:7-8

Neno: Bibilia Takatifu

7 Msidanganyike, Mungu hadanganywi. Kwa maana kila mtu ata vuna kile alichopanda


Waroma 2:6 BHN

6 Siku hiyo Mungu atamlipa kila mmoja kufuatana na matendo yake.
 
Hakuna binadamu aliyezaliwa na WEMA asilimia zote...
HAYUPO na sidhani kama atawahi kutokea,
Wakati unafikiria hilo pitia na hili kuwa hakuna bina aliyezaliwa na UBAYA wa aina yoyote ile.
Kwa maana hiyo kila jambo ni uamuzi tu.
Chanzo cha matatizo haya yote ni wewe kufanya maamuzi halafu ukakataa MATOKEO ya maamuzi,
Bro, mke wa kwanza ni kwanza haijarishi, yule ndiye amebeba baraka zako aisee mrudie not matter what FACT!
Au kama utashindwa kumrudia mpe imani kwanza kwamba ulikosea na unajutia, pili hamuwezi kurudiana, tatu mpe hata MTAJI aanzishe mambo yake..

Aisee nimechoka kuandika utanicheki hata DM nikutumie namba zangu tuongee zaidi.
Uzi wako umenifundisha jambo fulani, AHSANTE.
 
Ulikosea sana mtu uliyepaswa kumpa kipaumbele ni huyu ambaye umekwisha zaa nae... Wengine mnawezaje kukubali kuwa na watoto kutoka kwa mama tofauti tofauti aisee....
Hii ya kua nawatoto kutoka mamatofuati hua inatokea mara nyingine sio kupanga.kuna scenarios nyingi zenye kusabbaisha mwanaume kuzaa nawanawake tofauti ikiwemo ya mwanamke kujibebesha mimba nje ya makubaliano namwanaume.
 
Unateswa na guilt,siyo tukio lenyewe.
Ni moja wapo ya ugonjwa wa akili.
 
Na usikute daktari aliyemfanyia C-section hakuwa na experience kaacha bonge la mkovu huo kuanzia kona moja ya tumbo mpaka nyingine. Mwanaume akiuona tu anajisemea hapa nimepotea njia anasepa zake...

Binti atakuwa kwenye maumivu makali ajabu....

Halafu wanaume tunakaa hapa tunawasimanga singo mazazi kila leo kumbe mara nyingi tuliozingua ni sisi. Mungu na Atusaidie [emoji1545][emoji1545][emoji1545]
Msimamo ni ule ule hakuna Kuoa single Maza. Haijalishi ni single Maza wa namna gani.

Kwenye kuzingua hapo kila mmoja amezingua kwa namna yake mwanaume kwa tamaa zake na mwanamke kwa ujinga wa kuto chukua tahadhari.

Msimamo ni ule ule KATAA SINGLE MAZA.
 
Majuto ni kawaida kwa binadamu , Wewe siye unayefanya asiolewe ! Muda wake bado au hiyo point ya yeye kuwa na mtoto ndo anaifanya kisingizio ! Wanawake wangapi wana watoto wanaolewa vizuri tu tena kwa ndoa nzuri na za kudumu!

Humu JF ndo tunadanganyana tusioe single mother tu na kundi lililo humu ni dogo sana !!
Ungelaumiwa kama hutunzi mtoto wako vizuri !! Ila hiyo issue ya mama ni yeye tu anajiwekaje!

Huyo hujamuharibia maisha badilisheni mtazamo maisha yanatoa second chance !! Kweli mlikosea wote lakini sio kitu cha kujisononesha hata kama unaogopa kuhusu karma kwa binti yako mfundishe baada ya makosa ni kunyanyuka sio kuomboleza

! Usikute ana pigo za kifeminist wahuni wakitoroka anajificha kwenye mwamvuli wa Single maza !!

Single maza wanapata mahusiano mazuri tu kama raia wengine tena hata kuliko wasio na watoto ni suala la timing tu.
Wacha kujifariji.

Single Maza sio wa Kuoa.

Utaowaje mke wa mtu?

Msimamo ni ule ule KATAA SINGLE MAZA.
 
ajabu ni kwamba kuna male atasoma hichi kisa thereafter atarudia the same mistake
Kwani kuna kosa gani hapo? Kuto kuolewa kwa huyo mwanamke hakuhusiani na kuzalishwa. Ni matabia yake tu ya hovyo,asitafute mchawi.mbona kuna wadada kibao tu walizaa na waliolewa vizuri tu.
 
Operation inazuia nini kwani? Halafu huwa mnasema humu waliopasuliwa ndo safi kei inakuwa vilevile
Hata mimi nilisema huko juu mbona kati ya hivyo hakuna kinachozuia binti kuolewa ? Wamekazana eti wanaume wanamuacha kwa sababu ana mtoto eti mwingine alimuacha kwa sababu ya mshono !! Ni wakati wake tu haujafika , au hana bahati au mienendo tu !!
Kwani kuna kosa gani hapo? Kuto kuolewa kwa huyo mwanamke hakuhusiani na kuzalishwa. Ni matabia yake tu ya hovyo,asitafute mchawi.mbona kuna wadada kibao tu walizaa na waliolewa vizuri tu.
 
Habari wana Jf nipo na ID nyingine niliifungua karibu siku 26 zilizopita. Twende kwenye mada.

Mimi nina umri wa miaka 35 kwa sasa nina watoto 3. Nimeoa na nina mke nimezaanae watoto 2. Mtoto wangu wa kwanza nilizaa na dada mmoja chuoni. Mama yake sikumuoa nilioa mwanamke mwingine ila mtoto ninaishi nae mimi. Kitu hiki ndo kinanifanya kuwa na majuto kitendo nilichomfanyia mama yake. Daa kinaniumiza sana sometime nawaza bora ningemuoa mama yake.

Kipindi nipo chuo mwaka wa 3 naingia. Mwaka wa kwanza ndo walikuwa wanafika chuoni. Sasa si unajua mambo ya chuo mabinti wapya kutoka form 6 ndo wanakuja. Vijana mambo ya chuo naamini mnaelewa. Sasa nikamuona binti mmoja, nikaanza kumvizia sana, nakumbuka kipindi kile na rafiki zangu tulikuwa tunagawana mabinti, mimi huyu wewe yule.

Nilizoeana nae na kuanza kumfuata ili kuanzisha mahusiano nae. Nilijitahidi kuvizia na kupeana mbinu wa friends. Wenzangu walifanikiwa baadhi hadi kuwa nao first year. Ila mimi bado ananiangaisha.

Yeye alisema issue ya mahusiano hapana labda kuwa friends kawaida tuu. Mimi nikaona poa ila bado namvizia yule dada. Japo alikuwa mgumu sana.

Siku moja chuoni night watu walikuwa wanafanya discussion. Sasa nilikuwa na yule binti night siku ile tulipiga story kadhaa. Nilipanga kusex nae anytime nitakapo pata chance.

Siku ile nilipanga leo ni leo nitafanikiwa. Nakumbuka niseme kwa kifupi tuu nilimlaghai sana kwa kumshika shika akawa anasema tuu acha. Baadae akatoka akaamua kuondoka kurudi hostel, mimi nilikuwa sikai mbali na chuoni ghetto langu ni maeneo hayo ya chuoni tuu.

Nilimshikashika mpk akasema usinishawishi kuzini mimi siitaji.

Niliendelea tu.

MWISHOWE alilainika na akajikuta anakubali , nilienda nae ghetto tukasex na alilala mpk morning.

Asubui anashituka daa nikamkuta analia sana na kunilaumu, aliondoka na kwenda hostel .

Hatukuwa karibu kama 2 weeks hivi. Baada ya wiki 3 na siku kadhaa akaniambia siku zake haziona. Mimi eeeeeee. Nilishituka sana. Kumbe siku ile alikuwa siku zake za hatari . Nikili tuu nilitake risk sikutumia condom.

Niliisi kama kuchanganyikiwa hivi nikaona au ananimbambikizia nini. Niliwaeleza wadau wakasema Katoe , mimi daaa kitu hicho sijawahi hata kufanya , nikimuangalia binti yeye namuona she is not okay muda wote mpk wenzie wanamuliza shida nini.

Nikaa kimya tuu siku zinaenda naona tumbo hilo. Baada ya miezi kama 3 hivi ujauzito ukaanza kumsumbua sana. Mpk akaanza kunilaumu mimi. Akalazimika kwenda kwao. Kwao walimzingua sana tena sana.

Alikuwa ananipigia simu huku akinilaumu kwa siku ile.

Akalazimika kusitisha chuo. Baada ya kujifungua mimi nilikuwa nishamaliza chuo.
Mbaya zaidi akajifungua kwa operation mda wa kukaa home ndo ukazidi.

Akarudi chuo wenzie wako mwaka wa 3 yeye anaendelea na semester ya 2 mwaka wa kwanza. Mshono wa operation ulimsumbu sana.

Mimi nilisena tuu home wakanitupia maneno sana kwani wazazi wangu ni watu wa dini sana. Tukio lile lilinifanya niache kuzini kabisa.

Ila baadae nilikutana na binti mwingine. Na kumuoa .
Japo mama alinisisitiza sana muoe mama mtoto wako. Kwa sababu pale umemuaribu mtoto wa watu. Mimi wala sikujali.

Ila mzazi mwezangu yule. Tangu kamaliza chuo akipata mwanaume, akijua anamtoto jamaa anamuacha. Kila anayepata anamuacha. Baadae nikaona ngoja nimchukue mtoto nikae nae. Ili na yeye apate mtu amuoe . Ila wapi.

Mwaka juzi alipata mmoja alikubali ila alivyokuja kugundua alijifungua kwa operation akamuacha. Mara nyingine anakuwa ananilalamikia sana nimemualibia system mzima ya life yake.

Kwa sasa anaumri wa miaka 32. Rafiki zake wote tayari wameolewa ila yeye bado , mara nyingi anakuwa ni mtu wa huzuni sana , she is not happy always.

Hiki kitu mara nyingi kinaniumiza sana , maana naona kama nimemuaribia maisha binti wa watu.

Na mimi hapa home nina mtoto wa kike nafikilia na yeye akikutwa na tukio kama lile itakuwaje huwa nafikilia sana na kumuangali binti yangu huyu hapa home.

Daaa we acha .

KAMA NIMEKOSEMA UANDISHI NAOMBA RADHI.[emoji2969][emoji120][emoji120][emoji120]
Bro pole kwa majuto ila bado hujachelewa, ikiwa kama umepata moyo wa huruma wa kutafuta namna ya kumchukuwa mtoto wake ili nae apate mwenza wake ila imeshindikana fanya uwe nae wewe, maana hayo majuto hayatakwissha na lawama kwako hazitaisha.... Jiongeze mke mwingne kwa kumfurahisha mwenzio
 
Hata mimi nilisema huko juu mbona kati ya hivyo hakuna kinachozuia binti kuolewa ? Wamekazana eti wanaume wanamuacha kwa sababu ana mtoto eti mwingine alimuacha kwa sababu ya mshono !! Ni wakati wake tu haujafika , au hana bahati au mienendo tu !!
Huyu dada hajamuacha ex wake katika nafsi hata akiwa peke yake fikra zake ni ex, hawezi kupata mwnaume km bado anaishi kwenye kivuli cha ex
 
Kwani kuna kosa gani hapo? Kuto kuolewa kwa huyo mwanamke hakuhusiani na kuzalishwa. Ni matabia yake tu ya hovyo,asitafute mchawi.mbona kuna wadada kibao tu walizaa na waliolewa vizuri tu.
Huoni kosa hapo??
 
ajabu ni kwamba kuna male atasoma hichi kisa thereafter atarudia the same mistake
Kwani kuna kosa gani hapo? Kuto kuolewa kwa huyo mwanamke hakuhusiani na kuzalishwa. Ni matabia yake tu ya hovyo,asitafute mchawi.mbona kuna wadada kibao tu walizaa na waliolewa vizuri tu.
Huoni kosa hapo??
Hilo siyo kosa,
 
Kwani kuna kosa gani hapo? Kuto kuolewa kwa huyo mwanamke hakuhusiani na kuzalishwa. Ni matabia yake tu ya hovyo,asitafute mchawi.mbona kuna wadada kibao tu walizaa na waliolewa vizuri tu.

Hilo siyo kosa,
Kwa io yeye aliyefanya anajutia bure?? kwa fikra zako si ndio.
 
Sioni hasa unachojuta,hata umgemuoa mngeweza kuachana vile vile .Hiyo ndo dunia,usijifanye una huruma sana!
Nashangaa anachojutia hasa na watu wanavyomsimanga sijui ni nini kwakweli. Sibariki wala kuyakubali matendo aliyoyafanya ila wote hapo wamecheza 50 50 kuleta hiyo kadhia, sasa uje ujilaumu wewe, kwani yeye hana akili. Hakumbaka, ila binti alifanya choice, huko kushawishiwa mbona wanaume tunarubuniwa na wanawake mara nyingi kuwahudumia na kuwasomesha ila siwaoni wakijutia na mwanaume kosa utalibeba mwenyewe na hutalifanya tena kwasababu mtu unakuwa umejifunza. Hot period ndio ukae useme nilishindwa kuvumilia nyege nikaamua tu liende, sasa siutalala na kila mwanaume atakayekurubuni. Mbona tuliyofanyiwa na hao wanawake tumeshasahau na tumeshasonga mbele na siwalaumu hata ila in one way au the other walirudisha maisha ya mtu some step backwards. Aisee, wanawake jifunzeni kutake accountability of your own actions hasa kipindi hiki ambacho dunia mmeibadilisha wenyewe.
 
Na ulivyo na roho mbaya, unasubiri aolewe ili ukamvurugie mahusiano yake.
 
Back
Top Bottom