Wanavyofanya Musukuma na Polepole ni ushahidi wa ukomavu wa Rais Samia kisiasa

Mkuu CCM iina demokrasia ya kutosha. Ingekuwa ni huko kwa wachaga tena unaepinga siyo mchana cha moto ungekiona.
 
Siku tukifanya mambo yetu bila hila za uchaguzi kwenye bongo zetu, tutaanza kupiga hatua
Saa hizi tupo pale pale tunapiga mguu sawa ,mguu pande
 
Tunaomba hao vijana washughulikiwe Ova
 
Chanjo 1m, Watanzania 60m,zimegoma kuisha mpaka zimeshaexpire tu,imebidi walete za mchina nazo doro tu.
Hiii ndo TZ ya JPM,ukijitenga naye utaangukia pua.
Endelea kujidanganya, J&J zilishaisha zamani sanaa
 
[emoji123][emoji123][emoji106][emoji106]
 
Polepole na Msukuma wake zaidi ya makelele na propaganda za kujijenga wao binafsi kwa maslahi yao hawana uchungu na Tanzania au watanzania.
Zaidi ya yote hao ni vikaragosi watiifu wa ccm
 
Watu wasiojua mambo wanadhani mtu unaweza tu kuwa Rais wa nchi.

Wanadanganyana eti ni haki yako kuchagua na kuchaguliwa.
Uhodari uko kwenye kupanga safi yako ndani na nje ya chama. Kwa katiba yetu hii kushindwa ni ujinga wako.
 
Mkuu wapo watatu wanaomkwamisha Rais, ongezea na Mzee Gwajiboy . Yes inasemekana wamechanja kimya kimya tena ile Johnson and Johnson vaccine wakaiwahi kabla haijaisha sababu yenyewe unachanja mara moja tu.
Bila kuchanja utakwendaje kuhubiri nje ya Nchi na unasema una wafuasi wa ufufuo na uzima Dunia nzima? Wajinga ndio waliwao.
 
Labda kwenye nchi ya kusadikika ambako,Bei ya sabuni,mafuta ya kula,mabando,bati,simenti zimeshuka Bei.
Bila kusahau machinga ambao wamegeuka mtaji wa kusaka vyeo zaidi.

Tofauti na hapo nafikiri ulibebwa na jini lililojigeuza bodaboda.
Bei zimepanda dunia nzima kwasababu ya covid-19. Usidanganywe na mtu, Tanzania sio kisiwa. Bei ya mafuta ya petroleum imepanda duniani kote. Hivi hata kupanda kwa bei za bidhaa nayo unambebesha Samia? Shame upon you.

Mtashindana lakini hamtashinda, Katiba yetu hii ni turufu kwa kila kitu.
 
Vitu vyote vinapanda ila mahindi na korosho havipandi.
mbolea ime-double bei nayo imepanda kwenye soko la dunia?
 
Kuna wakati niliwahi kulazimika kuishi Marekani, nilitamani kurudi Tanzania haraka. Hakuna mtu mwenye akili timamu atakaependa kuishi Marekani kuliko Tanzania. Walioishi Marekani wataniunga mkono. Wengi wanapenda waende kule kwa muda TU kwa jambo maalumu Kisha waondoke warudi. Kuna wakati pia nilikaa Nairobi kwa miezi kadhaa, nilitamani nirudi haraka dsm.
 
Vitu vyote vinapanda ila mahindi na korosho havipandi.
mbolea ime-double bei nayo imepanda kwenye soko la dunia?
Hebu tuambie, mbolea inatengenezwa kwa kutumia nini? Je, mbolea inatengenezwa kwa material gani yanayotoka waapi?
 
Ndo uwezo wako wa ufahamu umeishia hapo?
Kwani Corona imeingia mwaka huu?
Au hujui nchi iliingia uchumi wa Kati wakati Corona ikiwa imepamba Moto dunia ikiwa imejifungia kwa mwaka mzima?
Au tozo la luku ni Bei ya umeme kupanda duniani?🀣🀣🀣🀣
 
.Hebu tuambie, mbolea inatengenezwa kwa kutumia nini? Je, mbolea inatengenezwa kwa material gani yanayotoka waapi?
Kwa hiyo corona imekula hayo material au unamaanisha nin?
Mafuta ya petrol watu wa tunduma wanayoyafuata zambia yenyewe wameyachimba wao?
Kubalini mama kuwa amefeli japo mnalipwa mteteeni ili msikose ajira zenu.
 

"Polepole na Musukuma ni watu wanaopingana na Rais Mama Samia kwenye kila kitu."

😁😁

"Walipinga chanjo weeeeee lakini mwishowe nadhani na wawo walichanja kimyakimya."

😁😁

Hiiiiii bagosha!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…