Wanawake mnatuchukuliaje sisi Wanaume?

Wanawake mnatuchukuliaje sisi Wanaume?

IamBrianLeeSnr

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2022
Posts
2,010
Reaction score
4,179
Habari wanajamii,

Nimeona nielekee kwenye mlengo wa madaa husika, Nimejaribu kufanya uchunguzi sana kwenye baadhi ya mazungumzo ya hawa wanawake tulionao humu ndani ya hii forum na kubaini kuwa wengi wa mabinti waliojiunga na hii forum ni sehemu ya wanawake waliopitia shida na mateso mengi sana hadi hivi sasa kuna wengine bado wamefungamana na mateso hayo hadi hivi leo.

Hivyo hii hali imewapelekea kutotambua nini haswa wanachohitaji kupatiwa katika maisha yao binafsi, Na hili limewafanya kuchanganya hali ya maisha na mahusiano kwani wengi wao wamekuwa wakitafuta wapenzi wa kuwatoa kimaisha lkn wengi wamejikuta wakiangukia pua kwa kutotambua nini haswa wanachohitaji kwenye mahusiano yao, Ingawa sijajumuisha wote humu ila ni baadhi yao wamekua na mihemko ya ajabu sana pale linapokuja suala la mahusiano.

Wengi wao wanafikiria mahusiano ni lazima kuwa na mtu mwenye hela nyingi ndio mwanzo mzuri wa wao kufanikiwa lkn wamejikuta wanakutana na hali ya ndivyo sivyo na kuambulia mateso mengi sana katika maisha yao.

Qn: HIVI NI NINI HASWA WANAWAKE MNAHITAJI MAISHANI KWENU MFANYIWE ILI MTULIE KAMA WATOTO NA NDIVYO MNAPENDEZWA KUWA NA HALI HIYO!

Cc: Clepatina , cocastic , Cute Wife , Shunie , Amehlo , Darlin , Ms eyes , Mrs Thabo Bester , charrote & all who ain’t in a list but we do love to show our respects.

Best Regards

All JamiiForums members
 
Nimejaribu kufanya uchunguzi sana kwenye baadhi ya mazungumzo ya hawa wanawake tulionao humu ndani ya hii forum
Huu muda unatoa wapi mkuu?? Unaweza kuta asilimia 50 ya uliowachunguza sio wanawake halisi bali ni wanaume. Usichukulie siriaz sana maisha ya mtandaoni inaweza ikakugharimu hata furaha yako
 
Habari wanajamii...

Nimeona nielekee kwenye mlengo wa madaa husika, Nimejaribu kufanya uchunguzi sana kwenye baadhi ya mazungumzo ya hawa wanawake tulionao humu ndani ya hii forum na kubaini kuwa wengi wa mabinti waliojiunga na
Wanakuchukulia kama mtu uliyejiunga na mitandao kupunguza stress
 
Huu muda unatoa wapi mkuu?? Unaweza kuta asilimia 50 ya uliowachunguza sio wanawake halisi bali ni wanaume. Usichukulie siriaz sana maisha ya mtandaoni inaweza ikakugharimu hata furaha yako
Sipo serious in that way! Ila kati ya I niliopitia sehemu ya maongezi yao ni wenye maumivu sana...
 
Back
Top Bottom