Wanawake wenye miaka 35+ wanachukuliaje hali ya kuwa "single"?

Wanawake wenye miaka 35+ wanachukuliaje hali ya kuwa "single"?

Hakuwa na miaka 40 masimulizi sahihi yanasema alikuwa na miaka 28. Yaani alimzidi miaka 3 tu
Shukran sana Brother. Allah akulipe kheri nyingi.

Na kwa kujazia tu ni kuwa riwaya iliyokuja kusema kuwa Bibi Khadija (Radhiya Allahu 'Anha) aliolewa na Mtume (Swalla Allahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam) wakati yeye Bibi Khadija akiwa na miaka 40 ni riwaya dhaifu sababu imesimuliwa kutoka kwa Ibn al-Waaqidi ambaye ni dhaifu. Na Ibn Is-haaq ambaye ni Thiqah (Reliable) amesimulia/amepokea kuwa Bibi Khadijah aliolewa akiwa na umri wa miaka 28.

Ibn al-Waaqidi ni dhaifu na anajulikana kwa hilo. Baadhi ya Wanachuoni wamezikubali Riwaya zake za Seerah na Maghazi, hata hivyo huko nako katika Riwaya zake za Seerah na Maghazi alikosolewa. Hata hivyo Wanachuoni walikuwa ni Mutasaahil (wamelegeza masharti) katika kuzikubali Hadith Dhaifu kuhusu Seerah na Maghazi.

Ibn Is-haaq ni thiqah (Reliable) zaidi. Na ndie aliye narrate kuwa Bibi Khadijah aliolewa akiwa na miaka 28. Na Bi Khadija kumzalia Mtume watoto sita (6) kunaipa nguvu zaidi Riwaya ya Ibn Is-haaq ya kuwa Bi Khadija aliolewa akiwa na miaka 28 kuliko Riwaya ya kuwa aliolewa akiwa na miaka 40, sababu kuzaa watoto sita baada ya miaka 40 kwa mwanamke sio kitu cha kawaida.

Ila ndio hivyo hadith ya al-Waaqidi ndio imekuwa mashuhuri zaidi kwa Waislam wengi wa kawaida.

Ilmu za Hadeeth ni tamu mno.

Utanirekebisha kama kuna sehemu nimekosea.

Na Allah anajua zaidi.
 
Ilmu za Hadeeth ni tamu mno.

Utanirekebisha kama kuna sehemu nimekosea.

Na Allah anajua zaidi.
Umepita mule mule.

Elimu ya Hadithi ni dume hawaipendi ila Wanaume. Ukitaka kuona miujiza ya elimu soma elimu hii adhwimu ya Hadithi.

Nimerudi tena shule.
 
Hawa jamaa mmoja ni mchina na Mwingine mkorea.
mmoja ni Mrusi mwingine ni Myukrein.
Mmoja ni Mfia dini na mwingine ni Mkana Mungu.

ila Makirita acha ubishi na kubaliana na ukweli
Naona ulipotea, vipi uliishiwa nguvu umerudi?! Ushakunywa maji? Mxiewww
 
Back
Top Bottom