Wanawake wenzangu mnazoeaje maumivu haya ya tumbo?

Wanawake wenzangu mnazoeaje maumivu haya ya tumbo?

Status
Not open for further replies.
Pole kipenzi ila jitahidi uonane na daktari wa wanawake.
Maradhi mengi ya wanawake ya uzazi huwa dalili zao kuu ni maumivu makali wakati wa MP. Ni kawaida kusikia maumivu ila hayapaswi kuwa namna hiyo.

Get well soon
Asante ciccy,, naufanyia kazi ushauri wako
 
Mi sijawahi umwa kiukweli ila nilichobahatika ni tarehe kugonga mulemule....ivo huwa najua kuwa kesho naingia period na haikosei....lasivyo bila tarehe kutokuyumbayumba ningekuwa naaibika kwa kuingia period bila kujua.

Pole sana cute...
Ndio uwanawake huo
Hongera dada, mie kwanza sijawahi kuelewa tarehe maana naona zinanivuruga tu, hazieleweki
 
Kwa maelezo yako hizo zinaweza kuwa dalili za tatizo linaloitwa secondary Dysmenorrhea. Haya ni maumivu makali na muda mwingine huweza kudumu kwa kipindi kirefu zaidi ya kipindi cha hedhi na yanatokea wakati wa hedhi. Baadhi ya wanawake hufikia hatua ya kulazwa hospitali hadi muda wa hedhi utakapoisha.

Wanawake wengi wenye maumbo yanayowavutia wanaume mara nyingi huwa na tatizo hili (utafiti wangu) na isitoshe nawe una umbo la namna hii[emoji23]

Sababu kuu ya tatizo hili inakisiwa kuwa ni ulemavu wa kiungo katika mfumo wa uzazi (disorder in the reproductive organs). Ninaweza kukubaliana na makisio haya kwa sababu wanawake wengi, kama siyo wote, waathirika wa hali hii, huwa wanayo shida ya kupata watoto.

Hivyo, ninakushauri. Tafadhali, kutana na daktari bingwa wa magonjwa ya kinanama kwa ushauri zaidi wa kitabibu. Achana na bush doctors la, sivyo, utakuja kujuta baadaye.

POLE SANA.
Mkuu wewe ni Dr? Nina shida ya kupata maumivu makali sana wakati wa hedhi
 
Niliwahi kuskia uzile wa kuchemsha ni mzuri kwa tumbo la P. Ila pia tumia panadol special za P zile kubwa unawekaga kwenye maji zinachemka kama dawa za gesi. Sijui sasa kama TZ zipo zile. Hivi juzijuzi nilimskia mtu anasema toothpaste za forever living pia nzuri unaweka kdg kwenye maji unachanganya then unakunywa. Jarib ivo na Mungu Atakusaidia, pole sn
Asante sana kipenzi
 
Pole sana,

Wenzio tunagonga 15yrs, na hilo tumbo, vikibana sana sijizuii nalia . nishatumia dawa zote lkn wapi,


Na nikiwa hivyo haifichiki kama pembe la ng'ombe.
Yani sijui mwisho wake lini haaa😭😭😭
 
Acha kulalamika wewe hiyo ni hali ya kawaida kabisa. The more unaiona hali ya ajabu na ndivyo itazidi kukufanya ujione mgonjwa.

Miaka ya nyuma bibi na mama zetu hata tulikuwa hatujui kuwa wanapitia hali hizi ila walijikaza na kuyapotezea hadi miili yao ika adopt na ikawa ni kitu cha kawaida sana kwao kiasi kwamba ukilalamika wanawake wenzako wanakushangaa na wanaweza kukucheka.

Ila mabinti wa miaka hii changamoto kweli eneo hilo, mnadeka utadhani hizo hali ni za kubambikiwa au mlipewa kama adhabu kumbe ni maumbile tu. Jifunzeni kukubaliana na asili yenu utaona hata mwili una anza kuadopt na hautakuwa unakuwa sensitive na hiyo hali.

Najua mtamind ila huo ndio ukweli.
Mkuu umefufuka tena[emoji23]
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom