Wanawake wote ndivyo mlivyo hata mkikataa. Wanaume kuweni makini katika maamuzi yenu

Wanawake wote ndivyo mlivyo hata mkikataa. Wanaume kuweni makini katika maamuzi yenu

Inahitaji tafakuri si kila mara ni sahihi kufanya hivi. Kuna mijimama mingine haijielewi bora tu kumchukua mtoto akawa chini ya himaya yako
ni kweli haujakosea ila ni vyema unapomchukua mtoto uangalie vitu viwili

1.nakuja kukaa nae(atunzwe na mkeo)

2.nimpeleke kwa bibi ake (atunzwe na mama yako)

Mwisho : maamuzi yapo mikononi mwako kama BABA.
 
Nalea mtoto wa mume wangu, ni mdogo kuliko mwanangu. Simtesi wala simnyanyasi ila namlea kwa uangalifu sana. Najua akilia kidogo tu watu watasema namtesa.

Hata wakikosea wote namchapa wangu tu kwa kisingizio kwamba yeye ni mkubwa. Wamepishana mwaka mmoja.

Huwa najisikia vibaya sababu najua siwapi malezi sawa ila naogopa kusemwa semwa kuwa namtesa.
Ila upendo wa mama kwa mtoto wake hauwezi kuhamishiwa kwa mtoto mwingine. Hatakama simchukii lakini upendo wangu kwake ni wa kawaida tu.
 
Nalea mtoto wa mume wangu, ni mdogo kuliko mwanangu. Simtesi wala simnyanyasi ila namlea kwa uangalifu sana. Najua akilia kidogo tu watu watasema namtesa.

Hata wakikosea wote namchapa wangu tu kwa kisingizio kwamba yeye ni mkubwa. Wamepishana mwaka mmoja.

Huwa najisikia vibaya sababu najua siwapi malezi sawa ila naogopa kusemwa semwa kuwa namtesa.
ila ukweli unajua "humpendi na wala humchukiii" ila unatimiza wajibu wako kama mzazi

mtoto anapokosea panapohitaji kuchapwa achapwe,panapohitaji kupongezwa apongezwe

Tofauti ya malezi yako na kwa mwanao nadhani umeshaona jinsi unavyokosea mahali flani

IF you realy n realy love him/her akikosea mchape usiangalie watu watasema nini "mlee ktk usawa"

akikua ataona jinsi unavyomchapa ndugu yake "hatopenda" atatengeneza image mbaya akilini mwake

Waleee kwa usawa kama jinsi usivyo jali watasema nini unapomchapa mwanao akikosea inabidi pia USIJALI

watasema nini utapomchapa mtoto wa mume wako.( lea wote kwa usawa)
 
Ok so huyo mtoto asikae na mwanamke mwingine kisa hatopendwa. Kwahiyo huyo mwanaume mwingine ndiyo atampenda mwanao.

Umemlipia mahari unamlisha kisha unaogopa kuileta damu yako nyumbani? Nigga die
 
100% mwanaume mwingine ana uwezo wa kumpenda mwanao kama vile ni wake

ila hamna mwanamke wa kumpenda mtoto wa mwanamke mwingine (tena aliezalishwa na mume wake)

kama wake aliyemzaa.

Uwezo huo wanao wanaume TU.
Hapo tu kwa Baba wa kufikia kumpenda mtoto wa mkewe 100% huo ni ukweli kabisa.!! Tena anaweza mpenda kuliko mwanae wa kumzaa endapo mtoto huyo akimtii.!! Na mfano hai hapo ninao kiukweli.!
 
Hapo tu kwa Baba wa kufikia kumpenda mtoto wa mkewe 100% huo ni ukweli kabisa.!! Tena anaweza mpenda kuliko mwanae wa kumzaa endapo mtoto huyo akimtii.!! Na mfano hai hapo ninao kiukweli.!

Jamani tutofautishe kupenda na kuhudumia. Hata wanawake wanawalisha, wanawavisha na kuwaogesha hao watoto kama wajibu tu. Hayo ya kumpenda kuliko mwanae wa kumzaa ni maigizo tu kama ambavyo wanawake huigiza.
 
Nalea mtoto wa mume wangu, ni mdogo kuliko mwanangu. Simtesi wala simnyanyasi ila namlea kwa uangalifu sana. Najua akilia kidogo tu watu watasema namtesa.

Hata wakikosea wote namchapa wangu tu kwa kisingizio kwamba yeye ni mkubwa. Wamepishana mwaka mmoja.

Huwa najisikia vibaya sababu najua siwapi malezi sawa ila naogopa kusemwa semwa kuwa namtesa.
Ila upendo wa mama kwa mtoto wake hauwezi kuhamishiwa kwa mtoto mwingine. Hatakama simchukii lakini upendo wangu kwake ni wa kawaida tu.

Hapa ndio patamu na hizi kesi ni nadra sana, yaani ‘mtoto wa mmeo’ ni mdogo kuliko ‘wako’ kwa maana hiyo amezaliwa nje ukiwa tayari umeshaolewa.... aisee nikupongeze sana kama nimekuelewa vema.
 
Jamani tutofautishe kupenda na kuhudumia. Hata wanawake wanawalisha, wanawavisha na kuwaogesha hao watoto kama wajibu tu. Hayo ya kumpenda kuliko mwanae wa kumzaa ni maigizo tu kama ambavyo wanawake huigiza.
lakini zuu unajua huwezi muhudumia mtu usiempenda,unajua hilo kweli?

ukiji force utafanya hizo huduma kwa muda fulani then utaacha tu.
 
Jamani tutofautishe kupenda na kuhudumia. Hata wanawake wanawalisha, wanawavisha na kuwaogesha hao watoto kama wajibu tu. Hayo ya kumpenda kuliko mwanae wa kumzaa ni maigizo tu kama ambavyo wanawake huigiza.
switihati, these ain't bare words, I am talking about 'Experience'.. A reality observation..!!
 
Mkuu wanaume mngekuwa hivyo msingekuwa mnawaponda single mothers kila siku na kusema kuwa hawafai kuolewa eti kwa sababu wana watoto, wakati huo huo wanawake wana uwezo wa kukubali kuolewa na single fathers bila kuangalia watoto.
100% mwanaume mwingine ana uwezo wa kumpenda mwanao kama vile ni wake

ila hamna mwanamke wa kumpenda mtoto wa mwanamke mwingine (tena aliezalishwa na mume wake)

kama wake aliyemzaa.

Uwezo huo wanao wanaume TU.
 
Hamna mahali popote pameandikwa mwanamke utakae zaa nae ndio unatakiwa umuoe awe mke waako wa ndoa"hakuna".

Ila pia hakuna mahali pameandikwa kwamba mwanamke utakae mzalisha usimpende wala usimpe huduma zote muhimu "hakuna"

Mwanaume unaweza kuwa ulishawahi kuwa na mtoto kwa mwanamke ambae si mkeo kwa sasa so kutokana na kujitambua kwako ukaona uendelee kutoa huduma zote za muhimu kwa mwanao kwasababu unajua fika ile ni damu yako,na hakuna mwingine wa kufanya hivyo zaidi yako.

Bahati nzuri ni kwamba mama mtoto wako (yule x) Anaolewa na mwanaume mwingine na Maisha yao kiuchumi si mazuri. Hata wewe umeona,unaamua kumwomba mama mtoto wako (yule x) umchukue mtoto ili asiteseke unamleta mwanao. Kuja kulelewa na mkeo nyumbani (makosa makubwa sana haya)

Acha nikwambie kitu,

Mkeo hatakwambia simtaki huyo mtoto (ila moyoni mwake kashakwambia)

Mkeo hatokwambia hapendi hata kumuona huyo mtoto (ila moyoni mwake jua hampendi)

Mwanaume wewe unamleta mwanao ukiamini atapata upendo kama wa kwa mama yake (unajidanganya)

Hata kama mama mtoto wako (yule x) utamuona anapitia maisha magumu kwa asilimia 200 usije thubutu mpokonya mtoto. Uje umlete kwa huyu mkeo ulie nae,Pamoja na shida atakazopitia mama mtoto wako (yule x) hatoruhusu shida zile zimpate

Mwanae na hata kama zikimpata mwanao mama yake atajua jinsi ya kumpa maneno mazuri ya kumbembeleza ajione naye yupo kawaida. Wanaume nataka tu muelewe jambo 1 hao wanawake mliowaoa (anakupenda wewe tu) usije jidanganya atampenda.

Mtu mwingine tofauti na wewe na wanae wa kuwazaa. Jitahidi uwezavyo kama una mtoto nnje na ulikua na mpango mwakani (umchukue uje uishi nae), acha maana unamleta jehanam mtoto wako mwenyewe (usijipe moyo kwa matendo yanayofanywa na mkeo ukiwepo) acha huo ujinga.

Muache mtoto wako huko huko kwa mama ake kama ni matumizi mtunze akiwa huko huko kwa mama ake. Kama unahisi unampenda sana huyo mwanao hutaki ateseke (mrudie mama yake muoe). Sasa jitie kichwa ngumu (mletee mkeo mtoto wa mwanamke mwenzie) utaona what next.

Wanawake ndivyoo hivyo walivyo, waelewe then ishi nao kwa akili mingi mingi.



View attachment 1249705
Kwahiyo mkuu unatushairi Nini ambao hatuna Watoto na hatujaoa!!

Maana ndo tunakokuja huko muda si mrefu.
 
Mkuu mbona unaongea mambo ya kufikirika tu yasiyo na uhalisia?? Hivi mfano huyo mwanaume naye wazazi wake wote walishafariki na ex wake ndiyo kaamua hivyo atafanyaje??
MTOTO SI WAKO BWANA ok iko hivi

ex wako hakai na mtoto kampeleka kwao huko kwa bibi(mama wa ex wako)

kwanza utambue wewe hujui familia ya ex wako yani (mama ake na ndugu zake huko wanaishije na wakoje)

kwa kua kashadhihirisha hawezi kaa na mtoto basi Tumia fursa hiyo kwenda kumchukua mwanao kisha mpeleke

kwa Bibi ake (mama yako wewe) kisha mtunze mwanao akiwa kwenye sehemu uliyo na uhakika nayo.

Mwanamke akikuruhusu ukamfate mwanao na unajijua umeshaoa USIKATAE mkimbilie mfate mtoto wako then

Fanya kile kile nilichokwambia hapo juuuu (mpeleke kwa bibi ake "mama ako wewe")
 
Mkuu wanaume mngekuwa hivyo msingekuwa mnawaponda single mothers kila siku na kusema kuwa hawafai kuolewa eti kwa sababu wana watoto, wakati huo huo wanawake wana uwezo wa kukubali kuolewa na single fathers bila kuangalia watoto.
tunawapondaga wao mkuuuu ila si watoto

hata siku moja hatunaga ugomvi na watoto

sisi ugomvi wetu ni kwamba single mother wanamtindo wa kupasha viporo

na wanaume walio zaa nao ndio mana tunawapiga sana vita.

ila linapokuja swala la mtoto Huwa tunakuaga wengine kabisa.
 
Mkuu mbona unaongea mambo ya kufikirika tu yasiyo na uhalisia?? Hivi mfano huyo mwanaume naye wazazi wake wote walishafariki na ex wake ndiyo kaamua hivyo atafanyaje??
mkuuu hapa tunajadili na haina maana ninachokiandika ndio kiwe sheria

mawazo yangu si sheria kwa mtu yeyote yule unahaki ya kuyakubali na kuyapinga pia

hivi vitu hatuongelei kwenye situation za wazazi kufariki,mada kama hizi tunapo discuss huwa

tuna assume wazazi wote wapo na hamna kipingamizi cha aina yeyote ile.

ingekua tunaongelea mapungufu mwingine angeweza kusema:

Mimi mbona mke wangu ni kipofu na ni kilema,atamtesaje mtoto wa mwingine?

so tunajua kuna vitu kama hivyo ulivyosema ila mara nyingi tunapo jadili mada za hivi

ondoa mawazo ya Kifo,magonjwa,ulemavu ondoa kabisa
 
Ninavyofahamu pia, watoto waliozaliwa na mama mmoja ila baba tofauti hupendana na huwa wamoja.

Ila watoto waliozaliwa baba mmoja ila mama tofauti mara nyingi hawapendani na ni ngumu kuwanganisha.

Ni kwamba mama anauwezo wa kuwanganisha watoto wake hata kama ni wa baba tofauti ila baba hawezi kuwanganisha wanae aliyewazaa na mama tofauti.

Kwa hiyo, mtoto akae na mama maana mama anaweza kuunganisha wanae.
 
Kwahiyo mkuu unatushairi Nini ambao hatuna Watoto na hatujaoa!!

Maana ndo tunakokuja huko muda si mrefu.
kuwa makini sana sana mkuuu na mwanamke unae fanya nae mapenzi na unaona kabisa HUYU

siwezi kuja kumuoa yani mwanamke unae ona hutoweza kuja muoa vaa kondom hata 5 asidake mimba asee

maana kama akidaka mimi sitokaa nikushauri umtoe na sitokushauri uoe mke mwingine.

Jisemeee moyoni (kuanzia leo ntato..mba mwanamke ambae tu anaweza kuja kuwa mke wangu)

yani we puyanga weeeeeee ila siku ikatokea bahati nzuri mdada wa watu ktk wale unaruka nao kakwambia ana mimba yako

Jisemee tu moyoni (asante baba maana huyu ndie mke wangu)
 
Back
Top Bottom