jiwe angavu
JF-Expert Member
- Aug 28, 2015
- 20,419
- 39,217
Peno....
Wakili Rugemaliza Nshala mtazame anatoka kundi lipi utamwelewa.
Hapo ndipo kwa kuanzia.
Utaelewa pia kwa nini ameweza kutoa maneno hayo.
Anamtetea Prof. Shivji.
Ningekuwa na uwezo ningemwambia kabla ya kumweleza Prof. Shivji kama "mtetezi" wa haki asome historia ya Mussa Kwikima.
Mussa Kwikima alisimama kutetea haki mwaka wa 1968 akiwa Jaji kijana sana.
Akimaliza kumsoma Mussa Kwikima atueleze Kwikima alikuwa anatetea nini na Shivji anatetea nini na kwa nini Kwikima alipigwa vita hadi akaondaka serikalini.
Atueleze vipi Prof. Shivji amedumu hadi kastaafu kwa khiyari yake mwenyewe.
Kuna mengi tunayajua lakini tuko kimya kwa nini mishipa ya shingo imewasimama kuhusu Waarabu.
Nyimbo hii ni maarufu kwetu na wala haikuanza kusikika leo.
Tuko kimya kwa staha na heshima ya viongozi wengi waliopita kwani nchi itanufaika nini kwa kusambaza maneno?
Ushahidi wa maneno yao uko wazi kabisa.
Sisi si kama Wakili Nshala na mfano wa Wakili Nshala.
Tumefunzwa adabu kwetu na tunajua ustaarabu wa kueleza jambo.
Hatutokwi na maneno.
Muhimu ni kuwa akina Nshala wajue kuna kundi kubwa la watu liko kimya na wakati utakapofika litasimama kuzungumza ukweli.
Wakati upi we mnafiki,na kipi kinakuzuia kusema sasa.