Wapenda haki hatutompa Kura Diamond Platnum kama tulivyokubaliana

Mkuu GT nifanyie wepesi kwakunipa Linki ya hule uzi wako bora kuhusu SIRi.

Natanguliza Shukrani zangu za dhati kabisa
 
Naunga mkono hoja ,hawezi kushinda Domondi huko BET,awaambie kina pole pole wampigie kura.
Mbona nasikia hii hakuna kupiga Kura watu Kama sie? Kura inapigwa na wahusika huko huko bet.
Sijaona hata maelekezo ya jinsi ya kupiga Kura au nakosea? Nieleweshe
 
Etii wapenda haki, my foot
Unayofanya we ndo mtenda haki au?
Kila mtu afanye yake, mi nampigia ashinde asishinde fresh tuu kwan Nini!

Acha chuki binafsi
Tunapigaje Kura?
 
Wanawake gani waliodhalilishwa? Hawa waliojipeleka wenyewe na hawakubakwa?
Diamond peleke Moto mzee baba na akijileta mwingine mpelekee Moto na usisahau kumzalisha
 
Bahati nzuri jamiiforums haitumiwi Sana na vilaza wengi, ingekuwa ndio watoa tuzo huyo Mondi angeangukia pua

Lakini wapiga kura wangekuwa whatsup,fb na insta angeshinda mapema Sana maana hiyo ndio mitandao ya mburura wengi wasiopenda kufikiri
 
Kweli mkuu lakini linajuaa
 
Bahati nzuri jamiiforums haitumiwi Sana na vilaza wengi, ingekuwa ndio watoa tuzo huyo Mondi angeangukia pua

Lakini wapiga kura wangekuwa whatsup,fb na insta angeshinda mapema Sana maana hiyo ndio mitandao ya mburura wengi wasiopenda kufikiri
Mbona jamiiforums inaelekea huko kwenye kuwa kama FB na Instar, kama members wa JF wanashughulishwa na Diamond unadhani ni kipi unategemea?
 
Amna kitu hapa. Yani unampangia mtu aimbe nini!! Aimbe tu hata kama hakina soko ili amridhishe ROBERT HERIEL .

Wasikilize unaowapenda mkuu kina roma,ney, sugu, prof jay na kama hao ambao sote tunajua ni wanaharakati. Tangu lini mbana pua bongo hii akawa mwanaharati, mnamuonea tu kijana wa watu.

Acha nikampe kura yangu apeperushe bendera ya nchi yetu pendwa. Ushindi wake ni wangu na wako ROBERT HERIEL
 
Kwa kauli hizi za Mbowe uchaguzi haukuwa wa uhuru Na haki.
Magufuli kafarika kabadili kauli anasema Chadem hawakuwa na wagombea sahihi wenye ushawishi kwa jamii.
Tuelewe nini.
Hizo tuzo za wenyewe wanampa wanayemtaka kula yako haiwezi kubadili matokeo.
CHADEM mnajiingiza kwenye mtego wenyewe akishinda kwenye hizo tuzo inamaana Chadem hawana ushawishi kwa Wananchi

watu wamepandisha idadi ya wapiga kura kwenye uchaguzi wa America washindwe kwenye tuzo za msanii
 

Huna ujualo,

Usifikiri kila mtu ni mpuuzi.

Kama hujui maana ya Msanii mkubwa Bora ungekata kimya au ungemuuliza hata mtoto uliyemzaa akuelezee maana Baba ni hamnazo
 

Mtu hapangiwi chakufanya Ila nafasi yake kwenye jamii ndio inampangia cha kufanya.

Diamond anaweza asiwe na interest ya kupigania haki lakini nafasi aliyonayo inamlazimu kufanya hivyo.

Kama hujui mambo madogo Kama haya naomba nikuache Kwanza,

Ukamuulize mtoto uliyemzaa huenda akakuzidi upeo katika hili
 
Sio lazima kupigania iyo unayoiita haki, unamshambulia kisa alikua mlengo tofauti na wewe. Ukionacho wewe sicho akionacho yeye, tatizo kubwa la upinzani ni hili mtu asiyewaunga mkono ni adui kwao.

What if kama yeye aliona yupo upande wa haki, ndio maana nasema wewe unampangia cha kufanya, una uhakika iyo jamii yote ilitaka hivyo unavotaka wewe afanye.
Tafakari mkuu, halafu jaribu kukubali mawazo ya wengine sio kujiona wewe ni bora sana, utakosa vingi.
 

Wewe ndio ujitafakari.

Nimeshakuambia Personal mtu sio lazima kuwa na interest ya Jambo Fulani

Lakini Nafasi uliyonayo ndani ya jamii inaweza kukulazimisha kuwa na interest ya Jambo usilotaka personal.

Wapi huelewi Budah!

Au ndio upeo mdogo??
 
Wewe ndio ujitafakari.

Nimeshakuambia Personal mtu sio lazima kuwa na interest ya Jambo Fulani

Lakini Nafasi uliyonayo ndani ya jamii inaweza kukulazimisha kuwa na interest ya Jambo usilotaka personal.

Wapi huelewi Budah!

Au ndio upeo mdogo??
Tatizo lako unataka apinge upingacho wewe na asifie utakacho. Diamond kachagua upande wa kisiasa. Au labda ndgu ni jamii gani unayozungumzia.Mpaka awe mpinzani ndo mjue anaipigania jamii.
Tatizo umekalili kua kuipinga serikali basi ndo uko karibu na jamii.
Wapi huelewi Budah!

Au ndio upeo mdogo??
.
Mkuu punguza ego, ego ni ya watu wenye uelewa wa chini wanaojaribu kujikweza waonekana wanajua vitu vingi wakati sivyo. Unapopinga au kutoa hoja nakushauri achana na hayi maneno kwa wajuvi watakuona huna kitu kichwani.
 
Wewe ndio ujitafakari.

Nimeshakuambia Personal mtu sio lazima kuwa na interest ya Jambo Fulani

Lakini Nafasi uliyonayo ndani ya jamii inaweza kukulazimisha kuwa na interest ya Jambo usilotaka personal.

Wapi huelewi Budah!

Au ndio upeo mdogo??
Wewe Jamaa uko njema Sana,sasa Maanza kukufatilia
 

Unajua maana ya Nafasi kubwa ndani ya jamii?

Unajua nafasi ya Public Figure ndani ya jamii??

Nakupa mfano maana naona upeo wako upo chini.

Mama Samia ni Muislam kindaki ndaki, na hauamini Ukristo kabisa.
Na kamwe hatakubali kuingia Kanisani kusali.

Lakini Nafasi yake ya Ukuu WA nchi unamlazimu kuingia mpaka Kanisani ikiwezekana kuimba mpaka Mapambio.

Bado hujaelewa logic ya Nafasi kubwa ndani ya jamii aliyonayo mtu na personal interest zake ni mambo mawili tofauti?

DIamond hatumkatazi kuwa CCM au kuwa CHADEMA au kutokuwa na chama, lakini linapokuja suala la kutetea jamii yake kulingana na nafasi yake Hana budi kujionyesha Kama anatambua wajibu wake Kwa nafasi aliyopo.

Sasa wewe Kama huelewi Jambo dogo Kama hili sijui nikuweke kundi gani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…