WARAKA: Maaskofu Katoliki waonya uminywaji wa demokrasia na uhuru wa vyombo vya habari nchini

WARAKA: Maaskofu Katoliki waonya uminywaji wa demokrasia na uhuru wa vyombo vya habari nchini

Zitasikika sauti zikisema "Wametumwa" au "Wanatumiwa" etc. tumsubiri "Comical Ali" atakuja kukanusha yaliyomo kwenye waraka huo. Nina hamu pia kumsikia ule Profesa wa sheria na katiba labda atalipa lecture kanisa kuhusu hali ya demokrasia nchini.
 
Page 12
"Kikatiba, nchi yetu inafuata mfumo wa demokrasia ya vyama vingi. Katiba na Sheria mbalimbali zimeainisha utaratibu wa kazi na shughuli za vylma vya siasa. Ili kuhakikisha hvamba ka'"'ina shughuli z vyamavya siasa zinakuwa endelevu, vyama vyenye kukidhi vlgezo hupewa ruzuku kupitia Bajeti ya Serikali inayopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania. Hata hivyo, shughuli za, sirsa bado zinaendelea kuzuiwa kwa kutumia vyombo vya dola. Maana yake ni kwamba shughuli za kiuenezi za vyama vya siasa, kama vile mikutano ya hadhara, maandamano, makongamano, mijadala na hata mikutano ya ndani, ambayo ni haki ya kila rua, zimekoma mpaka uchaguzi mwingine. Kisheria, huu ni uvunjifu wa Katiba na Sheria za nchi.

Vile vile baadhi ya vyombo vya habari vimefungiwa au kusimamishwa kwa muda, na hivyo kupunguza uwigo wa uhuru wa wananchi wa kupata habari, maoni na wa kujieleza. Kufungiwa huku kwa vyombo vya habari kumeenda sambaba na kuminya uhuru wa mahakama na bunge kwa njia ya kuminya haki wabunge na kutowapa nafasi ya mikutano ya hadhara kama haki yao ya msingi ya Kikatiba.

Katika mazingira haya ni rahisi kwa jamii kufarakana na hata kujenga chuki kiasi cha kuhatarisha amani, usalama na hadhi ya uhai wa binadamu. Kumekuwapo pia hali ya vurugu katika chaguzi mbalimbali. Chaguzi hizi zinaacha nyuma uchungu, hasira, tamaa ya kulipa kisasi na hata kususia chaguzi nyingine. Hali hii ni hatari kwa mustakabali wa Taifa letu. Tukiiachia hali hii izoeleke tushishangae huko mbeleni kujikuta katika mifarakano mikubwa zaidi itakayobomoa misingi ya amani na umoja wa kitaifa."
Nilikuwa nimekata tamaa hata kuhudhuria ibada baada ya ku note baraza la maaskofu wapo kimya, nikajua wameamua ku mute kwakuwa Mkatoliki mwenzao yupo ikulu.

Kwa huu waraka kwakweli imenibariki, jumapili ijayo ntakuwa wa kwanza kuingia ibadani na fungu langu la kumi juu.

Asante baraza la maaskofu asante kanisa katoliki.

Ila hapo namchungulia mnafiki moja atakavyojikana mwenyewe hahaha.... Pengo Mungu anakuona ujue
 
Nilikuwa nimekata tamaa hata kuhudhuria ibada baada ya ku note baraza la maaskofu wapo kimya, nikajua wameamua ku mute kwakuwa Mkatoliki mwenzao yupo ikulu.

Kwa huu waraka kwakweli imenibariki, jumapili ijayo ntakuwa wa kwanza kuingia ibadani na fungu langu la kumi juu.

Asante baraza la maaskofu asante kanisa katoliki.

Ila hapo namchungulia mnafiki moja atakavyojikana mwenyewe hahaha.... Pengo Mungu anakuona ujue
mkuu Mungi si wewe Mwenyewe Hata sisi wana habari tulikuwa tumekata tamaa
 
Ni waraka wa kwaresima 2018 tuusome una mafundisho makubwa kwa maisha ya kila mmoja wetu, Mimi nimeumaliza na nitaurudia tena na tena kujifunza "neno la mababa" tusiushushe kwa kujadili point moja tu, na kimsingi hatupaswi hata kujadili bali kuishi yale tuliyoaswa kutenda wakati huu wa "Neema".

Kwaresima ni " kuishi moyoni" sio "kuishi mitandaoni"

Nawatakieni kwaresima njema, tukutane baada ya siku 40, kwaherini.
 
Je wanalipa kodi? TRA wana kazi ya kufanya hapa.
 
Ni upuuzi uliopindukia kutenga siasa na imani/Dini za watu. Siasa zikivurugukika, amani hakuna na kuabudu hakuna! Tusidanganyike-Hongera Askofu Kakobe, hongera kanisa Katoriki. TANZANIA ni yetu sote.
Nini ni msimamo wa BAKWATA katka hili?
Je Askofu Pengo anaunga mkono tamko la maaskofu wenzake?
 
Nimeupenda sana maana umeeleza ukweli na hauna hata tone la unafki.

Nanukuu baadhi ya mistari UK 11 ambayo imegonga mulemule..
"Maana yake ni kwamba shughuli za vyama vya siasa kama vile mikutano ya ndani ambayo ni haki ya kila raia zimekoma mpaka uchaguzi mwingine. Kisheria huu ni uvunjifu mkubwa wa katiba na sheria za nchi.

Vilevile baadhi ya vyombo vya habari vimefungiwa au kusimamishwa kwa muda, na hivyo kupunguza wigo wa uhuru wa wananchi wa kupata habari maoni na kujieleza.

Kufungiwa huku kwa vyombo vya habari kumeenda sambamba na kuminywa kwa uhuru wa mahakama na bunge kwa njia ya kuminya haki za wabunge na kutowapa nafasi ya mikutano ya hadhara kama haki yao ya msingi kikatiba"

Mwisho wa kunukuu
 
Back
Top Bottom