Wasabato mnadai Kanisa Katoliki ni alama ya mpinga kristo lakini bado mnaamini Biblia waliyoindaa Karne 16 zilizopita?!

Mkuu,

Maandiko yapi hasa yalikusanywa na wa protestants?
Maandiko au Vitabu gani vilikusanywa na Ethiopia orthodox?
 
Asante kwa kuniongezea elimu mkuu.
My bad_i draw my comment back.
Catholic ndiyo Kanisa kongwe kuliko yote. Catholic church iligawanyika baadaye na kuunda Roman Catholic na Orthodox Catholic

Hoja yangu inasalia bao kuwa catholic anakuwaje mpinga kristo wakati Biblia kama kitabu ni yeye aliyeamua Idadi na aina ya Vitabu husika kuwemo kwenye Biblia?
 
Unasema wakatoliki walichukua maandiko na kuyaunganisha? Je waliyachukua kutoka wapi? Kwa vigezo vipi? Unaweza nitajia Idadi ya hayo maandiko ambayo kimsingi ndiyo Vitabu?
 
Hivyo vitabu 27 vya Agano jipya Wasabato walivitoa wapi?
 
Hua najiuliza maswali nakosa majibu,hivi inakuwaje Mwafrika anaacha imani yake ya asili anakumbatia imani nyingine tena anaitetea kabisa kuwa eti ndio imani ya kweli huku ile yake akisema sio ya kweli-ili hali zote ni imani.

Aliye tuloga Waafrika alituweza.
 
Unasema wakatoliki walichukua maandiko na kuyaunganisha? Je waliyachukua kutoka wapi? Kwa vigezo vipi? Unaweza nitajia Idadi ya hayo maandiko ambayo kimsingi ndiyo Vitabu?
Kwa ufupi;

Imani kongwe hapo mashariki ya kati ni "Uyahudi".

Hivyo basi baadhi ya vitabu walichukua toka kwenye "Uyahudi" hususani vitabu vya agano la kale.

Maandiko mengine walichukua kutoka kwenye kumbukumbuka za kale za kiyahudi ambazo ziliandikwa miaka kadhaa huko nyuma.

Mfano Yesu aliletewa gombo (chuo cha Nabii Isaya) ili alisome, hicho ni kitabu kipo miaka mingi kabla ya Ukristo. Pia hata alipojaribiwa na Shetani alisema imeandikwa (akimaanisha vitabu vilivyokuwa vinatumika kwa ajili ya mafundisho ya imani ).

Chanzo kikuu cha biblia za imani zote ni marejeo ya maandiko ya kale yaliyoandikwa kwenye mbao, mawe au gombo pamoja na maandiko yaliyoandikwa baada ya Yesu.

Hivyo basi kila imani ilichukua huko maandiko yake kulingana walivyoona inawafaa, wengine walichukua vitabu 83, wengine 72, wengine 66, wengine 24 n.k.

Wayahudi wao wanatumia TALMUD ambayo ina mkusanyiko wa vitabu vya agano la kale.

Mpaka sasa kuna mkusanyiko wa marejeo mengi ya kale yaliyoandikwa kwenye mbao, mawe au gombo yanayozungumzia habari za kale juu ya Imani ya Mungu hususani Uyahudi ambao ndio mama wa Imani zote za mashariki ya kati ambayo hajaingizwa kwenye hizi imani zilizopo.

Hivyo basi, Ethiopian Orthodox wao walichukua maandiko toka kwenye vitabu vya kale vilivyokuwepo kabla ya Yesu na Warumi, kisha wakachukua vingine vilivyoandikwa baada ya Yesu (Injili, nyaraka na ufunuo) wakaunganisha wakaja na biblia yao yenye vitabu 83.

Kwenye Orthodox bible wanatumia jina halisi la Muumba wa vyote ambalo anaitwa ELOHIM badala ya MUNGU.
Kumbuka Mungu ni cheo sio jina, hivyo kwa mfano utakuta wanasema " Hapo mwanzo Elohim aliumba mbingu na nchi .....", na siyo Mungu aliumba mbingu na nchi.

Kwa uchache umepata chanzo kikuu cha maandiko yote yanayotumiwa kama marejeo ktk hizi imani tukianza na Uyadi kisha ikafuata Orthodox, ikaja Romans, ikaja Protestant ndo wakaja Wasabato.
 
Hivyo 63 vimeandaliwa na nani?
39 vya Wayahudi viivyoko kwenye Jewish Bible.Biblia ya kale kuliko Biblia Zote hivyo havikukusanywa na Roman uongo wa Hali juu . Biblia hiyo ipo Toka enzi za kale Kabla ya Ukristo na ipo Hadi Leo waweza I download Playstore vya agano jipya havikuwa shida kuvipata Sababu kanisa la kwanza lilikuwa likivitumia mfano nyaraka za Paulo zilipatikana kwenye makanisa alikokuwa kayaandikia na vitabu vya Injili vilikuwa vinatumika na hayo makanisa

Hakuna ubishi wowote kati ya makanisa yote na ukatoliki kwenye vitabu vya agano jipya Sababu Kila dhehebu waliweza kuvipata

Kivumbi Kiko agano la kale ambapo kanisa katoliki liliamua lichukue vile vitabu 39 vya Jewish Bible kama vilivyo likaongeza vitabu vingine juu ya Jewish Bible wakaongeza vitabu sita vipya kama tobiti,Judith,makabayo wa kwanza na wa pili ,Sira nk jumla saba hivyo kufanya agano la kale la Biblia ya katoliki viwe badala ya kuwa 39 ukiongeza saba walivyoongeza vinakuwa vitabu 46 vya agano la kale ukijumlisha na vya agano jipya 27 vinakuwa 73
 
Mkuu jiongeze vitabu vya agano la kale Roman Catholic kavikuta

Na kanisa la kwanza halikuanzia Roma umelishwa matango pori

Kanisa la kwanza lilianzia Uyahudi Yesu alikozaliwa,kuhubiri,kufa na kusulubiwa.Na lilianza pale kasome kitabu Cha matendo ya mitume walikuwa wakisali wakikusanyika nyumba Kwa nyumba ukatoliki ulikuja baadaye sana Toka Ukristo ulipoanza kule uyahudi na Korintho Kasome kitabu Cha matendo ya mitume

Au kaangalie nyaraka za Paulo Kwa makanisa ya Kikiristo mbali mbali aliyaandikia hayo makanisa Kabla huo.ukatoliki haujaanza
 
Bado hatujapata majibu ya hoja yako,watu wanaruka ruka tu😁
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…