Chaliifrancisco
JF-Expert Member
- Jan 17, 2015
- 26,021
- 79,710
Hatutaki mchele, kama vipi watuletee magimbi na mihogo tupikie iftar.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
I didn't expect this kind of comment from you,man!Achani wakatae, tena wanakataa kwa hoja. Wakristo kama mliletewa miujiza ya kitapeli na ushoga mnapokea itakuwa mchele?
Wazee wa bit, watalishwa na hamna kitu watafanya.Sakata la mchele wenye virutubisho kutoka Marekani limeendelea kuchukua sura mpya baada ya waislamu kuukataa bila kumumunya maneno. Wakiongea kupitia redio ya kiislamu ya Imaan FM inayounguruma kutokea mkoa wa Morogoro, wamesema hawautaki mchele huo na wametoa tahadhari kwa mtu yeyote atakayewalisha watoto wao. Wamesema chakula wanacho cha kutosha hapa nchini na kushauri waletewe vitu wasivyokuwa navyo kama vile ndege, magari na ambulance.
Ili kuonyesha kuwa hawatanii katika hili, hata watangazaji waliokuwa wakiendesha kipindi walionekana kushabikia kitendo hicho. Mtu yeyote aliyepiga simu kwenye kipindi akionyesha kwenda kinyume na msimamo wao, walimkatia simu mara moja. Hebu wasikilize wewe mwenyewe kupitia klipu hiyo hapo chini.
MAONI YANGU
Huu mchele sasa naona umeanza kutugawa kiitikadi. Wakristo nao wakitoka hadharani na kuweka msimamo wao, hapatatosha. Ifike mahali ubaguzi wa kijinga kama huu ukemewe kwani unaweza kuligawa taifa na kuhatarisha umoja na mshikamano tulio nao hapa nchini. Tusiruhusu kikundi kidogo cha watu kitugawe kwa sababu yoyote ile.
Nawasilisha.
Huko Gaza watu wanakula hiyo misaada na ndio wanaijua dini vizuri kuliko hao Walalamishi !Sakata la mchele wenye virutubisho kutoka Marekani limeendelea kuchukua sura mpya baada ya waislamu kuukataa bila kumumunya maneno. Wakiongea kupitia redio ya kiislamu ya Imaan FM inayounguruma kutokea mkoa wa Morogoro, wamesema hawautaki mchele huo na wametoa tahadhari kwa mtu yeyote atakayewalisha watoto wao. Wamesema chakula wanacho cha kutosha hapa nchini na kushauri waletewe vitu wasivyokuwa navyo kama vile ndege, magari na ambulance.
Ili kuonyesha kuwa hawatanii katika hili, hata watangazaji waliokuwa wakiendesha kipindi walionekana kushabikia kitendo hicho. Mtu yeyote aliyepiga simu kwenye kipindi akionyesha kwenda kinyume na msimamo wao, walimkatia simu mara moja. Hebu wasikilize wewe mwenyewe kupitia klipu hiyo hapo chini.
MAONI YANGU
Huu mchele sasa naona umeanza kutugawa kiitikadi. Wakristo nao wakitoka hadharani na kuweka msimamo wao, hapatatosha. Ifike mahali ubaguzi wa kijinga kama huu ukemewe kwani unaweza kuligawa taifa na kuhatarisha umoja na mshikamano tulio nao hapa nchini. Tusiruhusu kikundi kidogo cha watu kitugawe kwa sababu yoyote ile.
Nawasilisha.
Iko vile bandugu. !Mbwembwe tu maana waagiza mchele na wao dini moja
au TendeWaislamu hoyeee. Waletewe msaada wa vitu wasivyokua navyo kama ndege , magari n.k . Hii nimeipenda sanaa.
Hata nyama toka arabuni kwa wenzao wanabugiaMbona tende na heluwa hawakatai?
Mbona hawajazisema Tende?Waislamu hoyeee. Waletewe msaada wa vitu wasivyokua navyo kama ndege , magari n.k . Hii nimeipenda sanaa.
Vyakula vigawiwe wanaotaka kula watakula na wasiotaka kula na wasile !Hiyo redio ni ya kipuuzi kuwahi kutokea nchini. Hata hao watangazaji wao ni wapuuzi na wakiukaji wa miiko ya utangazaji. Hao waislam ni kina nani duniani/nchini mpaka watoe ole? Ni wapuuzi, wana uhakika gani kama huo mchele ni mbaya? Basi kama ni hivyo watoto wao wasile, watakula wengine na wasilalamike kubaguliwa, shame on them
Huo mchele waulete huku mikoani tuuchukue, huku haturembi.R.I.P Magufuli
Sasa tunaletewa vitu vya kijinga badala ya kuletewa vitu vya maendeleo kwa nchi yetu.
Ni wamarekani hawahawa kwa kumtumia mamluki Tundu Lisu wanayemsomeshea watoto wake walipinga ujenzi wa bwawa la umeme alafu wanajifanya wanatupenda sana kutuletea mchele!!
Huu msaada wa mchele umeombwa.Misaada haijaombwa wanaleta tu bila kuombwa ndo waislamu wakasema basi walete ndege na magari na ambulance bila kuombwa hivyo hivyo.
Iko vile. !Hawana jipya wataongea na kula watakula
Nani kaombaHuu msaada wa mchele umeombwa.
Usipotoshe.