Wasioamini juu ya uwepo wa Mungu wanasemaje kuhusu mchawi aliyedondoshwa na nguvu za Mungu?

Wasioamini juu ya uwepo wa Mungu wanasemaje kuhusu mchawi aliyedondoshwa na nguvu za Mungu?

Matukio ya kupika kama hayo yapo mengi sana, sema kama ndo umeshika smartphone miaka ya karibuni kiasi cha kuamini video za YouTube siwezi kukulaumu.
Hakuna uthibitisho wowote wa kuaminika kuwa kuna Mungu au Shetani, na hautakuja kuwepo kwa sababu hawapo.
 
Matukio ya kupika kama hayo yapo mengi sana, sema kama ndo umeshika smartphone miaka ya karibuni kiasi cha kuamini video za YouTube siwezi kukulaumu.
Hakuna uthibitisho wowote wa kuaminika kuwa kuna Mungu au Shetani, na hautakuja kuwepo kwa sababu hawapo.
1. Video umeiona!
2. Majirani wamesema walimzika "victim" 2020
3. Ndugu wamethibitisha kuwa ndugu yao alikufa kwa ajali ya gari 2020
4. Mkuu wa wilaya kakiri kuwa huyo "victim" alichukuluwa msukule. Kumbuka na yeye alikuwa haamini mpaka aliposhuhudia kwa macho yake.

Tuambie! Tukuamini wewe au Mkuu wa wilaya?
 
1. Video umeiona!
2. Majirani wamesema walimzika "victim" 2020
3. Ndugu wamethibitisha kuwa ndugu yao alikufa kwa ajali ya gari 2020
4. Mkuu wa wilaya kakiri kuwa huyo "victim" alichukuluwa msukule. Kumbuka na yeye alikuwa haamini mpaka aliposhuhudia kwa macho yake.

Tuambie! Tukuamini wewe au Mkuu wa wilaya?
Ujuha unaanzia kwenye imani tu bila udhibitisho ulio jijenga kwenye mawanda yake.
 
Matukio ya kupika kama hayo yapo mengi sana, sema kama ndo umeshika smartphone miaka ya karibuni kiasi cha kuamini video za YouTube siwezi kukulaumu.
Hakuna uthibitisho wowote wa kuaminika kuwa kuna Mungu au Shetani, na hautakuja kuwepo kwa sababu hawapo.
Baada ya wazungu kugundua ndege nakueleza jinsi inavyofanya kazi ,watu wameona ni kawaida tu sio miujiza tena ,ila hizi blabla zisizo ata na faida kwenye jamii wanaona ni nguvu za mungu ama za shetani.
 
Baada ya wazungu kugundua ndege nakueleza jinsi inavyofanya kazi ,watu wameona ni kawaida tu sio miujiza tena ,ila hizi blabla zisizo ata na faida kwenye jamii wanaona ni nguvu za mungu ama za shetani.
Nini kilimpata huyu mwanamke.
 

Attachments

  • ALIYEFARIKI_2020_AONEKANA_2024,_WANANCHI_WAFURIKA_KUMUONA,_NDUGU_ZAKE_WASIMULIA__ALIGONGWA_NA_...mp4
    18.8 MB
Tupe mawazo yako kuhusiana na hili tukio

As always hizi habari zinatamalaki kwenye jamii za watu wajinga na maskini. Habari kama hii huwezi kuisikia Dar let alone Ulaya/Amerika. Hizi habari zinaripotiwa na media za hovyo zisizojali integrity ya fani yao. Habari kama hii BBC au al Jazeera hawawezi kuripoti hata kwa bahati mbaya wanajua wasomaji wao wengi ni watu wenye akili timamu.

Kuna mtu alisema kajifungua Jiwe unajua iliishia wapi? Hizi habari za kijinga za mtu kufufuka zinatokea kila wk ila hazina uthibitisho hata siku Moja na zote hupotea kama upepo. Nchi isiyo na technology hata ya kuunda toilet paper leo ifufue mtu? you must be dumb as a brick to believe this.
 
Mwaka 2007 Singida, tukiwa tumelala kwenye chumba kimoja(tulikuwa kwenye kambi ya kidini) lakini tulikuwa bado yupo macho, na mlango ukiwa umefungwa, mtu aliingia ndani bila mlango kufunguliwa, na karibia wote tuliokuwemo humo mimi nikiwemo tulimwona. Akijaribu kudogelea tulipokuwa tumelala, lakini mmoja wetu aliposema,"katika Jina la Yesu", alitoweka.

Mungu yupo, na uchawi upo, lakini nguvu ya Mungu ni kuu kuliko nguvu zingine zote.

Najua unajua hilo hata kama utaigiza kuwa hujui.
Maigizo hayo, bado hawajakuamini ipo siku na wewe watakupa kisehemu cha kuigiza
 
Walitaka "kumshughulikia" Mchungaji aliyekuwa akikwamisha kazi zao, lakini wakaishia kukutana na nguvu za Mungu na hatimaye kiongozi wao kudondoka na ungo.

"Atheist" atalichukuliaje tukio hilo?

Mungu Yupo, na watu wanaomwamini si wa kuchezewa na wachawi.

Video hiyo hapo.
View attachment 2851247View attachment 2851248

Sheria inasemaje kuhusiana na masuala ya kichawi? Mtu anapokamatwa kwa tuhuma za kichawi hufanyweje? Itasaidia akipelekwa kituo cha Polisi?
View attachment 2851268
Mara nyingi wakipelekwa police huishia kuachiwa huru na kama italazimika kwenda mahakamani basi kisa litakuwa tress passing ama usumbufu kwa wengine

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Afya ya akili ukiielewa kwa mapna utanielewa , pia kutojishughulisha na kuwa bize ndio kuna zalisha majuha .
Na wewe ukikubali kuyaweka wazi unayoyajua kuhusu ulimwengu wa roho, wengi wataduwaa! Naamini unayajua mengi ila tu umechagua kusimamia unachosimamia.
 
Hizo ni drama tu wala sio mara ya kwanza kutokea hapa Tanzania.

Njaa hua zinasababisha watu kufanya mambo ya ajabu. Hapo huyo kapewa hela na mganga ili kumtaftia soko la wateja.

Achana na hadithi zisizo na kichwa wala miguu hakuna cha mungu wala shetani.
kuna tukio lilitokea la mama kujifungua mtoto halafu baada ya kushuka kutoka kwenye bajaji yule mtoto aliyekuwa amemkumbata likawa jiwe.

Nilibishana sana na watu nikawaambia hili game linachezwa, na kweli baada ya siku iloonekana yule mama na shangazi mtu kuna michezo michafu walitaka kufanya.

Huyo mchungaji hapa anafanyiwa promotion ya hatari, sioni chochote zaidi ya maneno tu wanayoongea.

Labda mtoa mada aseme yeye huo uchawi upo wapi hapo?
 
We
Alifikaje juu ya paa la nyumba ya Mchungaji?

Vipi huyo "aliyeyeyukia" mkononi mwa nduguye Mchungaji?
wewe huyo aliyeyuka umemuona?

Kwani huyo mchungaji kama alimpandisha na ngazi utajuaje?

Kwanini uweke conclusion kwamba hilo ni jambo la kichawi?

Tuletee tukio ambalo haliwezi kuelezeka na si maneno yake huyo bibi!

Hata macho yanaonyesha anachoongea ni script na mchungaji kafanya chaguzi nzuri sana kwa muonekano wa huyo bibi.

Hii promotion ni nzuri sana.
 
kuna tukio lilitokea la mama kujifungua mtoto halafu baada ya kushuka kutoka kwenye bajaji yule mtoto aliyekuwa amemkumbata likawa jiwe.

Nilibishana sana na watu nikawaambia hili game linachezwa, na kweli baada ya siku iloonekana yule mama na shangazi mtu kuna michezo michafu walitaka kufanya.

Huyo mchungaji hapa anafanyiwa promotion ya hatari, sioni chochote zaidi ya maneno tu wanayoongea.

Labda mtoa mada aseme yeye huo uchawi upo wapi hapo?
Umewasikia hawa?
 

Attachments

  • ALIYEFARIKI_2020_na_KUONEKANA_2024_AZUNGUMZA_KWA_MARA_YA_KWANZA_-AULIZWA_HUYU_NANI_ASEMA_WAZIR...mp4
    20.1 MB
  • WASIMULIA_NDUGU_YAO_ALIYEFARIKI_2020_NA_KUONEKANA_HAI_2024,__TULIMZIKA,_ALIGONGWA_NA_GARI_(240p).mp4
    14.2 MB
  • ALIYEFARIKI_2020_AONEKANA_2024,_WANANCHI_WAFURIKA_KUMUONA,_NDUGU_ZAKE_WASIMULIA__ALIGONGWA_NA_...mp4
    18.8 MB
Toka nishuhudie laivu wanangu kwa TV kwenye haya makanisa ya kitume na kinabii wakiingiza walemavu, imani imeingia ukakasi sana na makanisa haya. Mtafute Mungu kwa nia haya makanisa yana mambo mengi sana na wengi wapo kibiashara japo sio wote.
 
Ni vigumu kuthibitisha ukweli wa taarifa maana haya yanatokea kila siku tu. Mwaka juzi kuna moja ilitokea mbeta eti kanaswa juu ya bati la mchungaji. Kumbe mwanamke katoka Mwanza kalipwa ila hakujua kuwa ile habari itasambaa sana kwa sababu ya mtandao ikasambaa hadi watoto na mmewe wakaiona na wao hawakuwa na taarifa kuwa maza yuko mbeya walidhani yuko kwenye sijuo semina.
Mama akaona hapa maji yamezidi unga ikabidi aseme ukweli kuwa alilipwa ionekane kanasa juu ya paa la mchungaji.
Haya maigizo si kwa wachungaji tu, umesahau tukio la kiroba kunasa kichwani kimara eti jamaa kaweka dawa toka kwa mganga ukiiba mzigo haushuki. Kumbe usanii tu wa kumfanya mganga avute watu na kweli taarifa ikasambaa watu wakaamini hadi polisi walipoingilia.
Nilitaka kusema hili ila umemaliza kila kitu mkuu!
 
Mkuu, unataka kutuaminisha kuwa Polisi, diwani, na mkuu wa wilaya nao ni waigizaji?
Mkuu,
Polisi walikuwepo kipindi binti anafariki? Na kwenye maziko yake?

Mkuu wa wilaya alijuaje binti huyo kafariki na kuzikwa?

Kuna autopsy yoyote iliyofanyika? Zipo wapi document za kitabibu?
 
Back
Top Bottom