Wasomi jifunzeni kwa dada Mwasu, dereva wa bajaji msomi mwenye shahada mbili

Wasomi jifunzeni kwa dada Mwasu, dereva wa bajaji msomi mwenye shahada mbili

View attachment 1660302

Tofauti na mawazo ya wengi kuwa ukisoma hadi chuo kikuu lazima uajiriwe, Mwasu Mavere ameonyesha upande mwingine wa shilingi, kwamba unaweza kujiajiri na kufanikiwa zaidi. Licha ya kuwa na shahada ya uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), yeye ameamua kuwa dereva wa pikipiki ya miguu mitatu (bajaji) akisafirisha abiria katikati ya makao makuu ya nchi, Dodoma.

Dada Mwasu anasema wasomi wengi wanatembea na bahasha miaka hadi mitatu bila kupata kazi, kumbe wangeuza hata karanga zingewaingizia kipato badala ya kuzunguka na vyeti. Hata hivyo, anasema mfanyabiashara msomi ni tofauti na asiyesoma, kwa kuwa ile elimu aliyonayo msomi anaitumia kufanya vizuri kwenye biashara zake. “Kuna wasomi wengi wanaendesha bajaji na bodaboda na wapo wengine wengi mtaani wanatafuta kazi, hawajajua kuwa kuna kazi ya kuendesha bajaji na kujipatia fedha kama walioajiriwa, hivyo niwatake waache kuchagua kazi,” alisema Mwasu alipozungumza na Mwananchi.

Mwasu alianza shughuli za usafirishaji abiria Desemba 2018 katika eneo la eneo la Royal Village, Dodoma lakini baada ya muda alihamia katikati ya mji ili kupata abiria wa pande zote. Anasema wasomi wengi wanatembea na bahasha miaka hadi mitatu bila kupata kazi, kumbe wangeuza hata karanga zingewaingizia kipato badala ya kuzunguka na vyeti.

Hata hivyo, anasema mfanyabiashara msomi ni tofauti na asiyesoma, kwa kuwa ile elimu aliyonayo msomi anaitumia kufanya vizuri kwenye biashara zake. “Kuna wasomi wengi wanaendesha bajaji na bodaboda na wapo wengine wengi mtaani wanatafuta kazi, hawajajua kuwa kuna kazi ya kuendesha bajaji na kujipatia fedha kama walioajiriwa, hivyo niwatake waache kuchagua kazi,” alisema Mwasu alipozungumza na Mwananchi.

Mwasu alianza shughuli za usafirishaji abiria Desemba 2018 katika eneo la eneo la Royal Village, Dodoma lakini baada ya muda alihamia katikati ya mji ili kupata abiria wa pande zote. “Elimu yangu ni masters, lakini mshahara mdogo niliokuwa nalipwa ndio uliosababisha nikaamua kuacha kazi na kujishughulisha na biashara mbalimbali ikiwemo kuuza nguo na hatimaye nikaanza kuendesha bajaji,” anasema.

Mwasu, mama wa watoto wawili anasema mshahara aliokuwa analipwa ambao haukukidhi mahitaji yake wala kuendana na kiwango chake cha elimu, ulisababisha akaichukia ajira akaamua kujiajiri mwenyewe.Alisema mwaka 2009 alihitimu shahada ya sociology and political science nchini Kenya na baada ya hapo alirudi nchini na kufanya kazi katika NGOs mbalimbali.

Ilifopika mwaka 2011 aliamua kujiendeleza katika Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) huku akiendelea kufanya kazi. Alihitimu mwaka 2013 shahada ya uzamili katika utawa (Masters of public adminstration). Alisema wakati anafanya kazi kwenye shirika lisilo la kiserikali la Afnet alikuwa programme officer na field officer baada ya muda akahamia katika shirika jingine la Ngonedo ambapo alikuwa monitoring and evaluation officer (ufuatiliaji na tathmini).

Mwasu alisema katika kipindi alichofanya kazi hakuwa na mshahara uliokuwa unazidi Sh390,000 kwa mwezi, ambao amesema haukuwa unakidhi mahitaji yake. Alisema kipindi hicho anafanya kazi alikuwa na mtoto mdogo, hivyo kutokana na mahitaji yake kuwa mengi na mshahara mdogo alipomaliza shahada ya uzamili aliamua kuacha kazi na kuanzisha biashara mbalimbali ikiwemo kuuza nguo. “Hela hiyo haikuwa inakidhi mahitaji yangu, mwisho wa siku nikaona ili nisiingie kwenye vishawishi vya kuiba fedha ofisini ili kukidhi mahitaji, bora niache kazi, niliona ni bora kujiajiri mwenyewe kuliko kuajiriwa kwani nilichokuwa ninalipwa hakilingani na elimu yangu.

“Wakati huo nafanya kazi, nilikuwa nakusanya hela kidogo kidogo na kuna siku nilienda field, pesa niliyolipwa na zile akiba zangu nikaamua kuanzisha biashara kwa mtaji wa Sh400,000. Nilikwenda Kariakoo (Dar es Salaam na kuchukua mzigo wa nguo na kuja kuuza Dodoma.” Alisema Mwasu, biashara yake ilikuwa vizuri na alikuwa anaingiza fedha kuliko zile alizokuwa analipwa wakati ameajiriwa.

Biashara hiyo aliifanya kwa muda mrefu hadi akawa anasafiri kwenda China pamoja na wafanyabiashara wengine kuchukua mzingo wa nguo na kuuza nchini. “Katika biashara kuna kuinuka, lakini pia unaweza kushuka. Biashara yangu ilikuja kuwa mbovu nikawa napata hasara, si kila siku ni kupata faida, hasara kwa mfanyabiashara haikwepeki nawakati huo tayari nilikuwa nishapata mtoto wa pili. “Licha ya hasara hiyo, sikukata tamaa badala yake nikaamua kubadilisha kazi ya kufanya. Niliamua kuachana na biashara kabisa na kuwa dereva bajaj,” alisema.

Endelea kufahamu Kilichomfanya aendeshe bajaji na Manufaa yake pamoja na Changamoto aipatayo kupitia link >>> Mwasu, dereva wa bajaj mwenye shahada mbili

View attachment 1660415
Wengine wako kazini hao mkuu
 
Hizi kasumba ndo zinashusha hadhi ya elimu.

Halafu chunguza Mara nyingi Hawa wasio na sifa za kuajiriwa, kwa kukosa vigezo ndo wanakimbilia kuinajisi Elimu. Unakuta mtu kweli kamaliza chuo na Ana degree Sawa, lakn Sasa ufaulu wake (GPA) alipata ndo unamkwamisha kupata Ajira, matokeo yake ndo anakimbilia huku na kujinadi kuwa yeye kasoma lakini amejiajiri, kumbe ukweli anaujua mwenyewe.

Mwisho wa siku usishangae mwanao akakwambia sitaki kusoma, naomba uninunulie Boxer nipige kazi. Je wewe kama mzazi mwenye malengo utakubali?.

We unafikiri mzazi wake aliemsomesha elimu ya Awali angejua kama anakuja kuendesha Bajaji angekubali kulipia Ada yote hiyo hadi kufika kuendesha Bajaji. HIYO SIO SIFA. Angalau angekuwa mwanaume.

Kwanza si kazi ya kujivunia maana Ana Risk, maana ni mtoto wa kike anashawishi kuibiwa Bajaji au kubakwa, Na pia anytym anaweza kupata ajali, akatekwa au kuvamiwa na wahalifu. halafu Hao watoto Wataangaliwa na nani, na yeye ndo mama.

Sio kila jambo la kuunga mkono, mengine ni ya kushauri au ikiwezekana kupinga kabisa. Anapaswa ajitafakari, kwanza yeye anaona sifa kupata publicity huyo kwenye magaazeti, kumbe ndo amewapa watu fursa ya kumtafuta, maana hata walikua hawamjui.

Ni kheri hata angeenda kuuza chakula, matunda au juice. Lah, kama Anapenda mambo ya usafirishaji ni kheri angekuwa Dereva wa maroli au konda wa maBus ya mikoani, Risk yake sio kubwa kama hiyo kazi.

We Ngoja tutakuja kuskia mwisho wa hiyo kazi yake kama utakuwa wa kheri .
 
Hizi kasumba ndo zinashusha hadhi ya elimu.

Halafu chunguza Mara nyingi Hawa wasio na sifa za kuajiriwa, kwa kukosa vigezo ndo wanakimbilia kuinajisi Elimu. Unakuta mtu kweli kamaliza chuo na Ana degree Sawa, lakn Sasa ufaulu wake (GPA) alipata ndo unamkwamisha kupata Ajira, matokeo yake ndo anakimbilia huku na kujinadi kuwa yeye kasoma lakini amejiajiri, kumbe ukweli anaujua mwenyewe.

Mwisho wa siku usishangae mwanao akakwambia sitaki kusoma, naomba uninunulie Boxer nipige kazi. Je wewe kama mzazi mwenye malengo utakubali?.

We unafikiri mzazi wake aliemsomesha elimu ya Awali angejua kama anakuja kuendesha Bajaji angekubali kulipia Ada yote hiyo hadi kufika kuendesha Bajaji. HIYO SIO SIFA. Angalau angekuwa mwanaume.

Kwanza si kazi ya kujivunia maana Ana Risk, maana ni mtoto wa kike anashawishi kuibiwa Bajaji au kubakwa, Na pia anytym anaweza kupata ajali, akatekwa au kuvamiwa na wahalifu. halafu Hao watoto Wataangaliwa na nani, na yeye ndo mama.

Sio kila jambo la kuunga mkono, mengine ni ya kushauri au ikiwezekana kupinga kabisa. Anapaswa ajitafakari, kwanza yeye anaona sifa kupata publicity huyo kwenye magaazeti, kumbe ndo amewapa watu fursa ya kumtafuta, maana hata walikua hawamjui.

Ni kheri hata angeenda kuuza chakula, matunda au juice. Lah, kama Anapenda mambo ya usafirishaji ni kheri angekuwa Dereva wa maroli au konda wa maBus ya mikoani, Risk yake sio kubwa kama hiyo kazi.

We Ngoja tutakuja kuskia mwisho wa hiyo kazi yake kama utakuwa wa kheri .

Ngoja wengine wapitie maoni yako !
CC:
The Happiness
madam cute
Lady nancy
my girl
Aunt Cash
BAK
Numbisa
 
Kaonesha ujasiri ,hajachagua kazi.......kuliko kusubiri ajira miaka nenda rudi ,bora kajishikiza hapo.

Ushauri:hio biashara sio ya kudumu ,akiweza ajitanue na sehemu zingine ili asije kwama.....pia ana uzoefu kama monitoring officer ,aendelee kuomba position kwenye NGO tofauti anawezavpata position ambayo itamlipa zaidi ya hapo.
sasa ajira atakayoomba ni ya kudumu...biashara ina kitu kinachoitwa exist strategy kila unapoingia...na hii ni rahisi sana...ukipata fungu flani unaiuza biashara unafanya nyingine ni vigumu kudumu na wateja miaka mitano...watu wanakuwa wanabadili marafiki na life style wengine wanatajirika wananunua vyombo vyao....simshaurikutafuta kazi ya kuajiriwa asonge mbele...
 
Kujiajiri ni kama walivyofanya kina Mendes wa KopaGas, Wasafi media, Maxence Meli wa JF.

Ni kampuni sustainable, ambazo unaweza kujua kabisa zitaajiri watu, kukuza kipato na kuvutia uwekezaji hata ni kupitia DSE.

Sasa yeye buashara ya Bajaj, akilala na yenyewe inalala
Makjuisi je
 
Kujiajiri ni kama walivyofanya kina Mendes wa KopaGas, Wasafi media, Maxence Meli wa JF.

Ni kampuni sustainable, ambazo unaweza kujua kabisa zitaajiri watu, kukuza kipato na kuvutia uwekezaji hata ni kupitia DSE.

Sasa yeye buashara ya Bajaj, akilala na yenyewe inalala
Hata mbuyu ulianza kama mchicha. Hata hivyo, viwango/aina ya kuiajiri haviwezi kufanana. Wengine wanajiajiri pakubwa wengine padogo. Jambo la muhimu anapata kipato ambacho hakitokani na mshahara.
 
Utopolo mtupu.
Hivi unajua kuwa kuna kazi zingine za serikali matangazo yake huishia ofisini ndani kwa mkuu wa mkoa, mkuu wa Wilaya na ndani ofisi ya mkuu wa kitengo mkoa au wilaya?
Na ifahamike wengine huajiriwa na hawakai ofisini.
Kuna mama muuza mihogo barabarani VETA dar , yule mama ile kazi ya kuzurura juani haitegemei, yupo pale kwa mission.
Kama hadi wengine hujifanya machizi ili wapate info mtaani unakuja kushangaa huyo dada na shahada zake 2 kudrive bajaji?
Unamjua mmiliki wa hiyo baiaji?.
Kabla hamjaja juu kuhusu habari za mtu yeyote tafuteni nature yake mtajua ukweli.
 
Usitake kuhalalisha mambo ya hovyo bwn! Unataka kunambia huyo angejua kama ataishia kuwa dereva wa bajaji angejihangaisha kuzitafuta hizo degree 2? Kama hatuwezi kuajiri watu wetu kwa nafasi zinazoendana na elimu zao, kwa nini kuwaingiza kwenye gharama na upotevu wa muda kuwapa hiyo elimu kubwa?

Tukubali tu kuwa tumeshafeli!!!!
Angeenda veta
 
Utopolo mtupu.
Hivi unajua kuwa kuna kazi zingine za serikali matangazo yake huishia ofisini ndani kwa mkuu wa mkoa, mkuu wa Wilaya na ndani ofisi ya mkuu wa kitengo mkoa au wilaya?
Na ifahamike wengine huajiriwa na hawakai ofisini.
Kuna mama muuza mihogo barabarani VETA dar , yule mama ile kazi ya kuzurura juani haitegemei, yupo pale kwa mission.
Kama hadi wengine hujifanya machizi ili wapate info mtaani unakuja kushangaa huyo dada na shahada zake 2 kudrive bajaji?
Unamjua mmiliki wa hiyo baiaji?.
Kabla hamjaja juu kuhusu habari za mtu yeyote tafuteni nature yake mtajua ukweli.
Umenasa kwenye propaganda za ujamaa enzi zile kwamba, kila watu 10 basi mmoja au wawili kutoka kitengo. Kwenye maelezo yake amepata Bajaji kwa mkopo wa CRDB kama ilivyo makampuni yanayokopesha na unalipa kwa wiki au mwezi na chombo kinakuwa chako.
 
Tungekuwa tunajua future zetu wengi tusingehangaika na Chuo Kikuu. Usomee uhandisi hadi upate degree halafu uiweke pembeni uanze kilimo cha matikiti?? 5 good years wasted!!! Bora mtu ungejua mapemaaaaa na kuanza mara tu baada ya kumaliza form 6
 
Tungekuwa tunajua future zetu wengi tusingehangaika na Chuo Kikuu. Usomee uhandisi hadi upate degree halafu uiweke pembeni uanze kuliko cha matikiti?? 5 good years wasted!!! Bora mtu ungejua mapemaaaaa na kuanza mara tu baada ya kumaliza form 6

Sio mzigo kwa mtu tuu.. serikali nayo inapoteza kumsomesha mtu asiwe productive baadae.... hela iliyotumika kumsomesha mtu huyu ingetumika eneo lingine labda ingekua na faida maradufu, we all lose, sisi na serikali pia.... tatizo tukiwashauri humu wanajifanya hawaoni.
 
Kuwa na masters si ishu kubwa. Ulicho nacho kichwani baada ya masomo ndio habari kamili.
Sasa huyu dada na masters alikuwa analipwa chini ya laki 4 na institution gani hiyo?
Pengine hiyo masters yake ni cheti tu ila yuko empty!
Some people are not meant for greatness, the universe serves what's best for the kind of person you are.
 
Back
Top Bottom