Wasomi jifunzeni kwa dada Mwasu, dereva wa bajaji msomi mwenye shahada mbili

Wasomi jifunzeni kwa dada Mwasu, dereva wa bajaji msomi mwenye shahada mbili

Ni Jukumu la lazima kwa serikali kuajiri watu wake au kuwasaidia wajiajiri. Na wanalipwa pesa za walipa kodi kwa sababu hiyo.

Kama wameshindwa kufanya hilo, wap8she wawaachie wanaoweza.

Huwezi kumlipa mtu alime barabara upite, pesa anakula kila siku halafu anakwambia tatizo lako boss hutaki kujiongeza kulima tu mwenyewe upite.

Na wakati huo huo, hataki kuachia hiyo tenda ya kutengeneza barabara.

Wanachokifanya watawala ni kutafuta namna ya kukwepa wajibu wao ili watafune kodi za walalahoi bila kufanya kazi wala kupigiwa kelele.
Siasa hizi,kwa hiyo wakiingia wengine tatizo la ajira linaisha hapo hapo ?
 
Tunasubiri sasa amiliki kiwanda cha bajaji,

Manake kuna motivesheni spika hapa anasema alianza kula yai la kuku moja la kukaanga sasa hivi ana miliki kuku wa mayai 10,000
 
Utopolo mtupu.
Hivi unajua kuwa kuna kazi zingine za serikali matangazo yake huishia ofisini ndani kwa mkuu wa mkoa, mkuu wa Wilaya na ndani ofisi ya mkuu wa kitengo mkoa au wilaya?
Na ifahamike wengine huajiriwa na hawakai ofisini.
Kuna mama muuza mihogo barabarani VETA dar , yule mama ile kazi ya kuzurura juani haitegemei, yupo pale kwa mission.
Kama hadi wengine hujifanya machizi ili wapate info mtaani unakuja kushangaa huyo dada na shahada zake 2 kudrive bajaji?
Unamjua mmiliki wa hiyo baiaji?.
Kabla hamjaja juu kuhusu habari za mtu yeyote tafuteni nature yake mtajua ukweli.
Mkuu mi naona kashindwa tu kutumia elimu yake...
Angekuwa na hiyo kazi unayomdhania asingetafuta kujulikana kupitia magazeti vinginevyo uniambie anatumika na serikali kupiga propaganda ili vijana wa wasio na ajira wajione Kuna mahali hawajafanya wajibu wao...
Pia mkuu kutumia elimu kuibadilisha kuwa kitu halisi si skills kidogo zinahitajika ni maarifa ya Hali ya juu Sana na wanayoyafikia ni watu wabunifu na wenye akili si kila mtu
 
View attachment 1660402


Nancy Lema ni msomi wa Elimu ya Masters ya Project Management Chuo cha SAINT MARY’S UNIVERSITY OF MINNESOTA Nchini Marekani na ameishi Marekani kwa miaka 10, mwaka 2015 aliamua kurudi rasmi Tanzania na kwenda kwao Mwanza na kuanza kutafuta kazi kwenye Makampuni bila mafanikio ndipo akaja na wazo la kuuza chakula aina ya makande kwenye ofisi Mwanza.

“Nilijua nimemaliza Masters yangu nakuja Tanzania kutafuta Kazi haitakuwa ngumu lakini kila sehemu niki-apply naambiwa subiri kwanza ilinifanya nifikirie nini cha kufanya” Nancy Lema

” Wazazi wangu hawakukubliana na mimi nianze kupika wakati wamenisomesha walitegemea niwe Meneja Kampuni flani na elimu kubwa, Ila kwa sasa ndio Wateja wangu wakubwa” Nancy Lema


Dada huyu msomi naye gumzo kwa kutafuta pesa bila kujali elimu kwani anaelewa nini maana ya neno moshi kwa wachaga !
Huyu kwao wanahela bhana hapa kaamua tu kutangaza biashara yake
 
Kuwa na masters si ishu kubwa. Ulicho nacho kichwani baada ya masomo ndio habari kamili.
Sasa huyu dada na masters alikuwa analipwa chini ya laki 4 na institution gani hiyo?
Pengine hiyo masters yake ni cheti tu ila yuko empty!
Some people are not meant for greatness, the universe serves what's best for the kind of person you are.
Aisee umeongea kweli Kuna watu wanajigamba tu na vielimu vyao lakini nje ya hicho Cheti hana chochote cha maana.
 
Tunasubiri sasa amiliki kiwanda cha bajaji,

Manake kuna motivesheni spika hapa anasema alianza kula yai la kuku moja la kukaanga sasa hivi ana miliki kuku wa mayai 10,000
Bakhresa alianza kuuza urojo saivi ana maviwanda

Hapo je[emoji1787][emoji1787]
 
Bakhresa alianza kuuza urojo saivi ana maviwanda

Hapo je[emoji1787][emoji1787]
Yule mzee hajaenda shule kihistoria so kastruggle kwelikweli miaka yote Hadi kawa bilionea,ila huyu bi mdada kapoteza muda class halafu anakuja kutamba eti ana masters anaendesha bajaji,angeishia la 7 na kuanza kuendesha bajaji then akaja mitandaoni na kusema niliishia la 7 nikajiajiri kuendesha bajaji na sasa nina miliki bajaji 10 ange-motivate vijana na wasomi wengine ,ila huyu dada ni kama anatumika kipropaganda na kuishusha hadhi elimu yetu
 
The last standing man@Mshana Jr kuna ramli +-++ uteuzi unakuja unakatika kilinge kinapungukiwa kasi kuni zipo nyingi mbichi zinahitaji joto kali kutoa moto wa kutosha kusogeza usukani
 
Yule mzee hajaenda shule kihistoria so kastruggle kwelikweli miaka yote Hadi kawa bilionea,ila huyu bi mdada kapoteza muda class halafu anakuja kutamba eti ana masters anaendesha bajaji,angeishia la 7 na kuanza kuendesha bajaji then akaja mitandaoni na kusema niliishia la 7 nikajiajiri kuendesha bajaji na sasa nina miliki bajaji 10 ange-motivate vijana na wasomi wengine ,ila huyu dada ni kama anatumika kipropaganda na kuishusha hadhi elimu yetu
UMEONGEA hoja ya msingi sana ..hiyo ni propaganda iliyo be calculated ...maana naona habari yenyewe ipo front page za magazeti.
 
Back
Top Bottom