JUAN MANUEL
JF-Expert Member
- Nov 26, 2010
- 7,808
- 16,972
Huwa nasikiliza watangazaji wa, wasafi, efm, TBC, pale kuna vilaza watupu, wasafi pale kuna kitenge, zembwela, Ando, huwa hakuna cha maana, cha kiuchunguzi, ni porojo kama za, Kjiwe cha bodaboda!Ukiweka Siasa Pembeni hatuna Watangazaji levo za kuwakaribia Wakenya,na tuna kwama sana kama nchi, kama umefuatilia mahojiano ya leo jioni ya Ruto na Watangazaji wa habari utagundua kwamba tuna kosa sana Watangazaji aina ile.
Watatangazi wetu ni weupe sana hata aina ya vipindi vyao tu ni kielelezo tosha, watangazaji wanawezea Maada za kijingajinga kama za kufumaniania, maada za Ndoa, maada za Yanga na Simba na Maada za kusifu na kuabudu(Uchawa)
Watangazaji kaliba ya Mauldi Kitenge ndio tegemeo kwa nchi, angakia utangazaji wake ulivyo wa kitoto. Mtu kama Zembwela ni Mtangazaji, mtu kama Mwijaku full comedian.
Hatuna watangazaji wala Waandishi wa Habari wa kuweza hata kumuhoji mkuu wa wilaya achilia mbali Mkuu w Mkoa, kwa Raisi ndio kabisaa,ndio maana Pres confrance za hii nchi huwa huwezi sikia swali linaulizwa sana sana wanapongeza.
Kiongozi anaitisha Press anaongea ananalia anaondoka hakuna swali make hakuna mwenye uwezi wa kumuuliza swali.
Ndio maana hata Wageni wa nje wanao tembelea Tanzania huwa hawafanyi Press yoyote make hakuna mtu wa kuwauliza maswali sana watangazaji wanaweza jikuta wanaishia kumsifia kwamba amependeza, mara alinunua wapi hio saa alio vaa.
Tuna wana habari weupe sana vichwani na now day asilimia 98 wamehamia kwenye mpira wa Yanga na Simba kituo cha Radio kutwa nzima ni Maaada za Yanga na Simba.
Juzi nikamsikia, zembwela akisema, "anakula vzr Sana sasa hv kufidia maisha magumu aliyoishi akiwa mtoto"sasa nikajiiuliza kuna haja gani, ya,kusema hv kwenye national TV, haisadii chochote, ni swala binafsi Sana, halina maana yoyote kwa jamii,
Inge kuwa anasema, kutoka na na maisha magumu aliyoishi akiwa mtoto, aliamua tangu zamani, atakuwa anatoa 50% ya mshahara wake kusaidia vituo vya yatima, au anasomesha watoto kadhaa, Inge kuwa na, maana Sana, ni, taharifa kama hii ni for public consumption,
Kuna upuuzi mwingine pale efm, kipindi, cha jioni ya Leo, kuna masimulizi, ya kutunga na ujinga mwingi, nikisikia biki kipindi, huwa, nasikia kutapika,
Kuna wachambuzi wao wa mpira dada mmoja anasauti mbaya kama katuni