Watanzania acheni roho mbaya kuhusu Zuchu na mziki wake, embu mwambieni ukweli

Watanzania acheni roho mbaya kuhusu Zuchu na mziki wake, embu mwambieni ukweli

Zuchu anajua sana kubadilikana na kujua soko linataka nini. Ndio maana nyimbo za Zuchu zinaimbwa kuanzia na watu wazima hadi watoto

Ukimsikiliza Zuchu aliyeimba "nisamehe" na aliyeimba "raha" tofauti kabisa

Ukimsikiliza Zuchu aliyeimba "nyumba ndogo" na aliyeimba "wana" au "sukari" ni tofauti

Huyu demu anajua sana, msikilize Zuchu kwenye "jaro" au "love"

Ni dhambi kumfananisha Zuchu na Nandy
 
Mkuu ingekua kuchuja sauti ni rahisi na inatoka vizuri kama ya zuchu basi wasanii wengi wangekua wazuri.

Gigy money anaimba, kwa nn hatoki na melodies nzuri kama zuchu?
Live performance inategemea umemuona ngapi. Ni ngumu kufanya vizuri show zote. Hata Messi sio kila mechi anacheza vizuri
Pamoja na kusema zuchu umeona hana sauti nzuri live lakini bado ana uwezo mkubwa wa ku-engage na crowd na moja ya kitu muhimu kwenye live performance

Ruby wanasema ana sauti nzuri sijui ana sauti natural, lakini akiwa live hana uwezo wa ku-engage na crowd mwisho anakua anajiimbia mwenyewe na show yote inaonekana mbaya
Niki kama nikki
 
Zuchu yupo talented, mzuri wa kuandika lyrics "kama tunavyoambiwa na WCB", ana best team nyuma yake lakini katokea kwenye tumbo la malkia khadija Kopa hivyo, kufikia level aliyofika kwenye bongo flavs sidhani kama kuna mtu kashangaa sana

Yote kwa yote, Shaa na Vanessa walikuwa ni bilingual artists yaani wanaimba nyimbo kwa kiingereza na kiswahili, hata nyimbo zao ziliegemea kwa soko la nje, kitu ambacho Zuchu haendani nacho maana anaimba nyimbo za kubamba Afrika mashariki, kwa hiyo Zuchu anaendeleza pale alipoishia Ray C, lady jaydee, Mwasiti, Linah etc

Ila aliyechukua mikoba ya Shaa na Vanessa bila kupepesa macho ni Abby Chams

Tofauti ya Abby na Zuchu ni moja, Aby anasimamiwa na Seven mosha, mtu anaelijua soko la nje, ila Zuchu anasimamiwa na WCB ambayo sidhani kama imetoa international act mwingine zaidi ya Diamond, mind you wakati Diamond anaanzisha WCB, alikuwa kashapenya Africa

So, nasubiri kuona Zuchu watamuuzaje maana kwenye biashara, hakuna linaloshindikana
 
Ni dhambi kubwa sana kumfananisha zuchu na hao wasanii wakawaida sana ambao vipaji vyao bado ni vidogo haviendi bila boost ya kuazima mistaria na nyimbo za kutungiwa, Zuchu ndie msanii wa kwanza wa kike kuwa na views wengi kila digital platforms, anawazid mpaka hao wasanii wenu wa kiume mnaowajaza sifa za kijinga
 

Attachments

  • Screenshot_20240207_003554_YouTube.jpg
    Screenshot_20240207_003554_YouTube.jpg
    157.8 KB · Views: 7
  • Screenshot_20240207_003736_YouTube.jpg
    Screenshot_20240207_003736_YouTube.jpg
    238.5 KB · Views: 10
Huyu nandy ambaye tangu aanze kuimba hajawai hata kufikisha viewers milion20 ndie mumshindanishe na Zuchu ambaye kwa nyimbo moja tu ya sukar anazaid ya viewers milion 90[emoji3], yaani nyimbo moja tu ya zuchu sawa na nyimbo zote za nandy+billnas na alikiba kama kifungashio, tukubali ukwel ambao ni mchungu, tuwapende wasanii wetu wanaojituma na ndipo hata mafanikio ya muziki wetu tutapata, tuache chuki kwa wasanii wenye uwezo, tuache kuwapambanisha na hao wanaodunduliza mnaowajaza sifa za kitoto
 

Attachments

  • Screenshot_20240207_003831_YouTube.jpg
    Screenshot_20240207_003831_YouTube.jpg
    262.9 KB · Views: 8
  • Screenshot_20240207_003804_YouTube.jpg
    Screenshot_20240207_003804_YouTube.jpg
    200 KB · Views: 9
Zuchu anajua sana kubadilikana na kujua soko linataka nini. Ndio maana nyimbo za Zuchu zinaimbwa kuanzia na watu wazima hadi watoto

Ukimsikiliza Zuchu aliyeimba "nisamehe" na aliyeimba "raha" tofauti kabisa

Ukimsikiliza Zuchu aliyeimba "nyumba ndogo" na aliyeimba "wana" au "sukari" ni tofauti

Huyu demu anajua sana, msikilize Zuchu kwenye "jaro" au "love"

Ni dhambi kumfananisha Zuchu na Nandy
Zuchu na Nandy wote ni sawa tu, sijaona huo utofauti zaidi ya nandy kuimba sauti flani ambayo ni generic kwa wasanii wengi waliotokea THT, huku Zuchu akiimbia mahadhi ya Pwani zaidi

Ingawa siwezi pinga, Zuchu ni hardworking sana na huu ni muda wake, maana ukiachilia promo, consistence yake toka ametambulishwa ni 🔥🔥🔥

Nandy pia anajitahidi maana nae anatoa hits day by day kwa hiyo, wote ni washindi kwa njia zao. Ila kuhusu kutufikisha international, siwezi jua kesho itakuja na nini ila tukiwapima kama bidhaa KWA SASA, bado wanacheza East Africa na Congo
 
Dooh kwahiyo unabisha kwamba wasanii hawachujiwi sauti, wakati baadhi ya wasanii wenyewe pamoja na maproducer wanakiri hilo, msanii kuwa na sauti ni jambo moja na kuwa na mafanikio ni jambo lingine mkuu

Hadi nimesema hivyo basi ujue nishaangalia shows nyingi za Zuchu hadi ile ya US ambayo alikuta watu wachache, akaanza kuimba huku analia ndio kabisa akazidi kuharibu, kwa kifupi yule hamfikii Nandy wala Ruby

Mkuu we zunguruka tu umsifie kwenye mambo mengine ila kwenye sauti uongo, wasanii wengi ni wabana pua tu mpaka wanakera ila ni vile wanatumia ujanja ujanja, wanaimba content ambazo wabongo wengi na akili zetu fupi ndio tunazipenda hivyo hatuzingatii vocals
Mlishaambiwa sauti haina maana ndiomaana burna boy&davido wanawakimbiza wasanii wenu hapo nigeria na africa nzima mnaowaona wana saut za kikike[emoji3], issue ni talent ya kujua nn mashabiki wanataka kwa muda gani, na kujua kwenda na wakati, music ni biashara
 
Huyu nandy ambaye tangu aanze kuimba hajawai hata kufikisha viewers milion20 ndie mumshindanishe na Zuchu ambaye kwa nyimbo moja tu ya sukar anazaid ya viewers milion 90[emoji3], yaani nyimbo moja tu ya zuchu sawa na nyimbo zote za nandy+billnas na alikiba kama kifungashio, tukubali ukwel ambao ni mchungu, tuwapende wasanii wetu wanaojituma na ndipo hata mafanikio ya muziki wetu tutapata, tuache chuki kwa wasanii wenye uwezo, tuache kuwapambanisha na hao wanaodunduliza mnaowajaza sifa za kitoto

Nandy amemuacha Zuchu almost miaka mitano kwenye muziki, hizo ni zama tofauti katika muziki.

Nandy ameingia na kufikia prime yake kipindi bado traditional media ina nguvu huku digital platforms ndio inaanza kueleweka

Zuchu kaingia kipindi ambacho digital platforms zina nguvu sana na hata WCB ishakuwa successful label huku ikitawala mitandao. Leo Zuchu akitoa wimbo, WCB nzima na machawa wote wataipigia promo, hivyo kupata numbers zaidi mtandaoni ni kawaida ila vipi kuhusu Nandy ?.

By the way, sitetei mtu ila ukiona mwanamuziki especially wa kike kama Nandy ameweza kusimama hadi anakaribia miaka kumi kwenye game bila kushuka. Muheshimu sana
 
Ila aliyechukua mikoba ya Shaa na Vanessa bila kupepesa macho ni Abby Chams

Tofauti ya Abby na Zuchu ni moja, Aby anasimamiwa na Seven mosha, mtu anaelijua soko la nje,
Mpaka sasa kati ya Abby na Zuchu nani anajulikana zaidi kwenye soko la nje?
 
Back
Top Bottom