Watanzania hawana imani na Waziri wa Nishati January Makamba, anapaswa kuachia ngazi, asipoachia Rais amuondoe

Watanzania hawana imani na Waziri wa Nishati January Makamba, anapaswa kuachia ngazi, asipoachia Rais amuondoe

Ikimpendeza Rais amhamishie Januari Wizara mambo ya nje patamfaa zaidi kwa kuzingatia uzoefu alonao wa miaka mingi juu ya mambo yale.

Hapo Tanesco ishakuwa nongwa na kwa kuzingatia mikingamo ya yule alotolewa na wale mahasimu pamoja na mahasidi na hivi na vile.

Ikimpendeza Rais afanye marekebisho madogo ya baraza la mawaziri kwa kufanya minor recategorization.

I prophecies it to be done [emoji123] in Jesus Name.
 
Hivi watu hawaoni ya kuwa January na uongozi mpya wa Wizara ya Nishati pamoja na TANESCO wapo katika nafasi walizo kuwanazo kwa muda mfupi uliopita! Katika kipindi kama hicho ni lazima tuwe wavumilivu na wapewe muda ili kuweka mambo sawa...
Wewe unapewa gari inatembea kisha unaihalibu kisha unaomba upewe muda hiyo inaleta maana kweli?

Kama hajui chochote si ajiuzuru tu kuliko kurudisha watu nyuma.

Kwa hiyo tanesco ni sehemu ya kupeleka watu wajifunze utendaji wakati watu wanaumia?
 
Kila kona manug'uniko ya watanzania ni juu ya dalili za wizara nyeti ya nishati na umeme kuwa na waziri ambae watu hawana imani nae. Tangu ateuliwe kuwa waziri basi taifa limekuwa na mauzauza tu juu ya upatikanaji wa umeme na hata uongozi na uendeshaji wa Tanesco...
Acha wivu wewe, hebu tueleza baya alilolifanya na lenye ushahidi mpaka sasa. Wewe sema humpendi tu. Yaani unamu evaluate mtu kwa mwezi mmoja au miwili kisha unakuja na generalization eti hafai, serious? Hii si haki. Bila shaka ulitaka wale unaowashabikia ndio wateuliwe. Vumilia tu maumivu ndugu.
 
Watu wengi wasichokijua kama hufai hautafaa kwa kumchafua mwingine na kutaka kumfanya aonekane haifai.

Dhahabu itabaki kuwa ni dhahabu ile ile hata ikipakazwa matope [emoji108]

Salamu ziwafikie mahasidi na mahasimu wote na chawa wao popote walipo!
 
kuongoza tanzania ni shughuli kweli sasa ubaya wa huyu waziri ni upi mnataka alete mvua mabwawa yajae au
Acha tu. Wanachuki naye binafsi. Walitaka wateuliwe wale wanaowashabikia wao. Naanza kuamini kuwa kuna kundi limemwagwa humu kumchafua tu. Wanatetea maslahi ya kundi lao bila shaka.
 
Wewebunapewa gari inatembea kisha unaihalibu kisha unaomba upewe muda hiyo inaleta maana kweli?
Kama hajui chochote si ajiuzuru tu kuliko kurudisha watu nyuma.
Kwa hiyo tanesco ni sehemu ya kupeleka watu wajifunze utendaji wakati watu wanaumia?
Wewe ni mmoja wa lile kundi lililomwagwa humu kumchafua tu na si vinginevyo. Ukiulizwa kafanya lipi baya utaumauma midomo tu.
 
Sasa niwaulize swali:

Kwa hiyo Rais akiamua kumrudisha yule Ngosha leo umeme hautakatika katika tena kwa wakati huu ambapo kina cha maji kimepungua sana kwa wakati huu?

Kwa hiyo hali inayojitokeza angekuwepo ngosha umeme usingekatika?

Tatizo laweza kuwa ni mfumo mzima wa kitaasisi kutoka juu na la kihistoria na wala sio mtu binafsi.
 
Ww unaishi Tanzania ya uhamishoni? Au Tanzania ya vijijini kusiko na nishati ya umeme? Kumtetea Makamba eti ipo siku atafanya vizuri ni sawa na mashabiki wa Arsenal kuamini ipo siku tutamfunga Man United
Wewe ni kundi maslahi tu. Sioni baya kwa waziri mpaka sasa.
 
Kila kona manug'uniko ya watanzania ni juu ya dalili za wizara nyeti ya nishati na umeme kuwa na waziri ambae watu hawana imani nae. Tangu ateuliwe kuwa waziri basi taifa limekuwa na mauzauza tu juu ya upatikanaji wa umeme na hata uongozi na uendeshaji wa Tanesco...
Sukuma Gang kazini.
 
Ki ujumla Kama wewe ni kijana hafu bado unashabikia ccm na sadiki kusema wewe ni crazy
Kijana mwenye akili atashabikia uwepo wa wagombea binafsi na siyo vyama tu. Ikibidi tuwe na democratic system ya Switzerland kabisa ipo inclusive kuliko zote duniani.
 
Kila kona manug'uniko ya watanzania ni juu ya dalili za wizara nyeti ya nishati na umeme kuwa na waziri ambae watu hawana imani nae. Tangu ateuliwe kuwa waziri basi taifa limekuwa na mauzauza tu juu ya upatikanaji wa umeme na hata uongozi na uendeshaji wa Tanesco...
Eti kila kona. Yaani kundi lenu lenye maslahi binafsi lililomwagwa humu ndio manung'uniko kila kona?
 
Eti kila kona. Yaani kundi lenu lenye maslahi binafsi lililomwagwa humu ndio manung'uniko kila kona?
Watu wengi hawataki umeme wa mgao, walete umeme na nobody will give a f**k hata akiwa waziri miaka 20.
 
Kila kona manug'uniko ya watanzania ni juu ya dalili za wizara nyeti ya nishati na umeme kuwa na waziri ambae watu hawana imani nae. Tangu ateuliwe kuwa waziri basi taifa limekuwa na mauzauza tu juu ya upatikanaji wa umeme na hata uongozi na uendeshaji wa Tanesco...
Tatizo sio makamba tatizo ni ccm tuiondoe kwanguvu ya umma
 
Watu wamejaa husuda kali mpaka inawala kwenye mifupa yao ! [emoji3][emoji3]

Hali hiyo mkiiendekeza ikawala kwa muda mrefu inaweza pelekea mkaumwa magonjwa sugu .

Hiyo ni kwa mujibu wa Maandiko Matakatifu.

Chuki na husuda hula hadi mifupa ya mwenye kuibeba zidi ya mtu mwingine.

Na unafahamu umuhimu wa kazi za mifupa mwilini ni pamoja na kuratibu utendajikazi wa mifumo yote ya mwili, kutengeneza damu , kutembea, nerveus n.k

Jifunzeni namna ya kuyapokea mabadiliko na kuya support.
 
Watu wengi hawataki umeme wa mgao, walete umeme na nobody will give a f**k hata akiwa waziri miaka 20.
Umeme uta stabilize tu. Mpeni haki yake ya benefit of doubt mpaka baada ya muda fulani. Tumepitia kipindi cha ukame hadi maji ya kunywa yakawa shida, sembuse yakuzalisha umeme?Tatizo mmeanza kumlaumu kuanzia day one alipoteuliwa. Sasa hii inaonesha kuna chuki binafsi.
 
Hamna cha sukuma gang wala upumbavu huo tunataka umeme siyo maneno mengi toka kwa mfungwa mtarajiwa.


Kwani amefanya makosa gani?

Dua la kuku hilo huwa halimpati mwewe!

Mnaongozwa na mihemko yenye kusukumwa na chuki na husuda tu!

Nimewauliza swali Kwa hiyo akirudishwa leo huyo Ngosha wenu kina cha maji kule kwenye mabwawa ya umeme kitajaa na umeme hautakatwakatwa tena?

Je Ngosha anaoweza kufanya huo muujiza?

Ningekuwa Karibu na Rais ningemshauri amrudishe huyo Ngosha wenu kwa wakati ule hata mvua bado hazijanyesha na kina cha maji kuongezeka kidogo halafu tuone Je mgawo wa umeme utakoma?
 
CCM ni walewale, aondoke makamba aje mwingine business as usual.
 
Back
Top Bottom