Watanzania lazima Tufahamu Rais wa nchi siyo Sawa na Rais Wa Bendi ya Mziki kiulinzi na Kiusalama

Watanzania lazima Tufahamu Rais wa nchi siyo Sawa na Rais Wa Bendi ya Mziki kiulinzi na Kiusalama

Ndugu zangu Kuna watu wanaleta ujuaji Sana hapa nchini, Kuna watu wanafikiri kila kitu ni siasa, Kuna watu wanafikiri kila kitu ni sawa na wanavyowaza, kuna watu wanamchukulia Rais Kama raia wa kawaida, kuna watu kwa upeo wao mdogo wanamlinganisha Rais na sisi, Kuna watu wanazani uzito wa Rais Ni Sawa na uzito wa Mwenyekiti wa chama kilicho kama Saccos.

Lazima Tufahamu kuwa Rais wa nchi Ni mkuu wa nchi na kiongozi wa Serikali, Ni Amiri Jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama, Akishakupigiwa kura na kuapishwa hawi Kama yule uliyekuwa unamfahamu, hajiamulii mambo Kama alivyookuwa anajiamulia kiusalama, Haendi kila sehemu aliyokuwa anaenda awali, hapiti kila eneo alikokuwa anapita awali, Hali chakula kila mgahawa alikokuwa anakula awali, hasalimiani na kila mtu Wala hasogeleani na kila mtu hata Kama alipanga msitari kumpigia kura katika uchaguzi, Wala hapandi kila gari na kupita popote pale na njia yoyote ile.

Lazima Tufahamu kuwa kila kitu kinawekwa katika utaratibu maalumu, utaratibu wa kijasusi,utaratibu wa kiusalama na kiulinzi, lazima Tufahamu kuwa usalama na ulinzi wa Rais wa nchi Ndio Jambo la muhimu kuliko kitu kingine chochote kile hapa nchini, amani na utulivu wa nchi hauwezi ukatenganishwa na usalama wa Rais na familia yake.

Rais hawezi akayumba kiafya halafu utegemee nchi isiyumbe, lazima iyumbe, itetemeke, ipepesuke, mambo lazima yatetereke na kusua sua, lazima idara zisimame kazi zake, lazima watu watege masikio juu ya Hali ya Rais, lazima mawazo ya watu yawe mahali pamoja tu, lazima kila muda iulizwe Hali ya Rais ikoje, lazima ufanisi wa kazi upungue makazini kwote na kila idara, mpaka Rais atakapo toka hadharani kulipungia mkono na kulisalimu Taifa ama kulihutubia Taifa letu ndipo mioyo ya watu itapona na kupata amani na Kuendelea na kazi kwa moyo wote.

Hivyo tusiwafundishe Wala kuwaingilia katika kazi watu waliopewa dhamani juu ya ulinzi na usalama wa Rais wetu, Tusiwachanganye Wala tusiwaone Ni wajinga, Mwenyezi Mungu alitupatia maarifa wanadamu hivyo lazima maarifa yote yatumike katika kuhakikisha Rais anakuwa salama muda wote, hiyo ni kazi yao. Ni wajibu wao wakufa na kupona kuhakikisha Rais Ni salama. Tusilete uanaharakati kwa kila Jambo.

Macho yetu lazima tujuwe Ni vipofu linapokuja suala la ulinzi na usalama wa Rais, sisi tunaona kwa macho haya ya nyama pekee, macho ya kukosoa, ambayo yanafumba hata upepo ukipita, macho yetu siyo Kama ya wale tuliyowapa dhamani ya ulinzi wa Rais wetu mpendwa, wao wanaona mbali, wanao hata tusivyoweza kuona kwa macho ya kawaida, wanaona hata kabla ya kukaa, wanaona hata mioyo yetu, wanaona hata ishara zetu, wanaona hata mifuko yetu, wanaona hata katikati yetu. Wakati sisi hata tukizibwa na mtu mrefu mbele yetu hatuwezi kusimulia kilichokuwa mbele yetu hatua chache.

Tuache ujuaji na kukosoa kila kitu, tuache uanaharakati kwa kila kitu, tuache utalaamu kwa vitu ambavyo hata darasni hatujawahi kukaa kujifunza, tuache umbilikimo wa kifikira na kimawazo, tuache werevu wakati ni vipofu wa masuala ya usalama, Tuache idara zetu za usalama zifanye kazi zake, zitekeleze wajibu wake.

Idara yetu ya ulinzi na usalama wa Rais Rai yangu kwenu ni kuwa endeleeni na majukumu yenu Wala msiyumbishwe Wala kuondolewa katika mstari wenu ,Wala kufundishwa kazi, Wala kuelekezwa na mtu wa nje kipofu wa masuala ya ulinzi na usalama, tunachohitaji Ni kuona Rais wetu ni salama kwa gharama zozote zile, tunampenda Rais wetu na tumewakabidhini ulinzi na usalama wake muutekeleze ipasavyo na kwa weledi mkubwa kwa msaada wa Mwenyezi Mungu mtoa njia maarifa.

Kazi iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

Hicho kiti mbona hakwenda nacho UK?
 
Kabisa hasa suala Hilo la ulinzi na usalama wa mh Rais wetu mpendwa mama Samia suluhu Hassani tuviachie vyombo vyetu vinavyohusika na ulinzi wa Rais

Kwahiyo hapa Tanzania ambapo mnasema aliingia madarakani kwa kura halali ndio usalama wake mdogo, ila kule UK alikopakizwa bus usalama wake ndio mkubwa?
 
Ndugu zangu Kuna watu wanaleta ujuaji Sana hapa nchini, Kuna watu wanafikiri kila kitu ni siasa, Kuna watu wanafikiri kila kitu ni sawa na wanavyowaza, kuna watu wanamchukulia Rais Kama raia wa kawaida, kuna watu kwa upeo wao mdogo wanamlinganisha Rais na sisi, Kuna watu wanazani uzito wa Rais Ni Sawa na uzito wa Mwenyekiti wa chama kilicho kama Saccos.

Lazima Tufahamu kuwa Rais wa nchi Ni mkuu wa nchi na kiongozi wa Serikali, Ni Amiri Jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama, Akishakupigiwa kura na kuapishwa hawi Kama yule uliyekuwa unamfahamu, hajiamulii mambo Kama alivyookuwa anajiamulia kiusalama, Haendi kila sehemu aliyokuwa anaenda awali, hapiti kila eneo alikokuwa anapita awali, Hali chakula kila mgahawa alikokuwa anakula awali, hasalimiani na kila mtu Wala hasogeleani na kila mtu hata Kama alipanga msitari kumpigia kura katika uchaguzi, Wala hapandi kila gari na kupita popote pale na njia yoyote ile.

Lazima Tufahamu kuwa kila kitu kinawekwa katika utaratibu maalumu, utaratibu wa kijasusi,utaratibu wa kiusalama na kiulinzi, lazima Tufahamu kuwa usalama na ulinzi wa Rais wa nchi Ndio Jambo la muhimu kuliko kitu kingine chochote kile hapa nchini, amani na utulivu wa nchi hauwezi ukatenganishwa na usalama wa Rais na familia yake.

Rais hawezi akayumba kiafya halafu utegemee nchi isiyumbe, lazima iyumbe, itetemeke, ipepesuke, mambo lazima yatetereke na kusua sua, lazima idara zisimame kazi zake, lazima watu watege masikio juu ya Hali ya Rais, lazima mawazo ya watu yawe mahali pamoja tu, lazima kila muda iulizwe Hali ya Rais ikoje, lazima ufanisi wa kazi upungue makazini kwote na kila idara, mpaka Rais atakapo toka hadharani kulipungia mkono na kulisalimu Taifa ama kulihutubia Taifa letu ndipo mioyo ya watu itapona na kupata amani na Kuendelea na kazi kwa moyo wote.

Hivyo tusiwafundishe Wala kuwaingilia katika kazi watu waliopewa dhamani juu ya ulinzi na usalama wa Rais wetu, Tusiwachanganye Wala tusiwaone Ni wajinga, Mwenyezi Mungu alitupatia maarifa wanadamu hivyo lazima maarifa yote yatumike katika kuhakikisha Rais anakuwa salama muda wote, hiyo ni kazi yao. Ni wajibu wao wakufa na kupona kuhakikisha Rais Ni salama. Tusilete uanaharakati kwa kila Jambo.

Macho yetu lazima tujuwe Ni vipofu linapokuja suala la ulinzi na usalama wa Rais, sisi tunaona kwa macho haya ya nyama pekee, macho ya kukosoa, ambayo yanafumba hata upepo ukipita, macho yetu siyo Kama ya wale tuliyowapa dhamani ya ulinzi wa Rais wetu mpendwa, wao wanaona mbali, wanao hata tusivyoweza kuona kwa macho ya kawaida, wanaona hata kabla ya kukaa, wanaona hata mioyo yetu, wanaona hata ishara zetu, wanaona hata mifuko yetu, wanaona hata katikati yetu. Wakati sisi hata tukizibwa na mtu mrefu mbele yetu hatuwezi kusimulia kilichokuwa mbele yetu hatua chache.

Tuache ujuaji na kukosoa kila kitu, tuache uanaharakati kwa kila kitu, tuache utalaamu kwa vitu ambavyo hata darasni hatujawahi kukaa kujifunza, tuache umbilikimo wa kifikira na kimawazo, tuache werevu wakati ni vipofu wa masuala ya usalama, Tuache idara zetu za usalama zifanye kazi zake, zitekeleze wajibu wake.

Idara yetu ya ulinzi na usalama wa Rais Rai yangu kwenu ni kuwa endeleeni na majukumu yenu Wala msiyumbishwe Wala kuondolewa katika mstari wenu ,Wala kufundishwa kazi, Wala kuelekezwa na mtu wa nje kipofu wa masuala ya ulinzi na usalama, tunachohitaji Ni kuona Rais wetu ni salama kwa gharama zozote zile, tunampenda Rais wetu na tumewakabidhini ulinzi na usalama wake muutekeleze ipasavyo na kwa weledi mkubwa kwa msaada wa Mwenyezi Mungu mtoa njia maarifa.

Kazi iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
Kijana pamoja uchawa wako wote huo katika awamu hii, pengine mbali na kunufaika na hizo buku 7 unazozipata, zidi kujipendekeza hata uambulie nafasi ya katibu mtendaji kata,
 
Hicho kiti mbona hakwenda nacho UK?
Tindo ndugu yangu embu acha kuniabisha kwa maswali yasiyoendana na uwezo wako wa kufikiri, Mimi nafahamu uwezo wako Ni zaidi ya hapa na huwezi ukauliza swali la namna hii
 
Kijana pamoja uchawa wako wote huo katika awamu hii, pengine mbali na kunufaika na hizo buku 7 unazozipata, zidi kujipendekeza hata uambulie nafasi ya katibu mtendaji kata,
Siandiki hapa kwa malipo ya aina yoyote Ileeeee , naandika kwa utashi wangu binafsi na msukumo unaotokana na kuridhishwa na utendaji kazi wa kutukuka wa mh Rais wetu mpendwa mama Samia suluhu Hassani , Nami nahangaika natafuta vocha Kama wewe nakuingia humu kuchangia mawazo na mtizamo wangu, Kama wewe unalipwa Ni wewe binafsi usifikiri wote tunaingia humu kwa malipo
 
Kwahiyo hapa Tanzania ambapo mnasema aliingia madarakani kwa kura halali ndio usalama wake mdogo, ila kule UK alikopakizwa bus usalama wake ndio mkubwa?
Kwani John F Kennedy hakuingia madarakani kwa kura halali? Abraham linkolin hakuingia kwa kura? Mambo ya usalama tuviachie vyombo vyetu vifanye kazi yake bila kuingiliwa na mtu yoyote yule
 
Ndugu zangu Kuna watu wanaleta ujuaji Sana hapa nchini, Kuna watu wanafikiri kila kitu ni siasa, Kuna watu wanafikiri kila kitu ni sawa na wanavyowaza, kuna watu wanamchukulia Rais Kama raia wa kawaida, kuna watu kwa upeo wao mdogo wanamlinganisha Rais na sisi, Kuna watu wanazani uzito wa Rais Ni Sawa na uzito wa Mwenyekiti wa chama kilicho kama Saccos.

Lazima Tufahamu kuwa Rais wa nchi Ni mkuu wa nchi na kiongozi wa Serikali, Ni Amiri Jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama, Akishakupigiwa kura na kuapishwa hawi Kama yule uliyekuwa unamfahamu, hajiamulii mambo Kama alivyookuwa anajiamulia kiusalama, Haendi kila sehemu aliyokuwa anaenda awali, hapiti kila eneo alikokuwa anapita awali, Hali chakula kila mgahawa alikokuwa anakula awali, hasalimiani na kila mtu Wala hasogeleani na kila mtu hata Kama alipanga msitari kumpigia kura katika uchaguzi, Wala hapandi kila gari na kupita popote pale na njia yoyote ile.

Lazima Tufahamu kuwa kila kitu kinawekwa katika utaratibu maalumu, utaratibu wa kijasusi,utaratibu wa kiusalama na kiulinzi, lazima Tufahamu kuwa usalama na ulinzi wa Rais wa nchi Ndio Jambo la muhimu kuliko kitu kingine chochote kile hapa nchini, amani na utulivu wa nchi hauwezi ukatenganishwa na usalama wa Rais na familia yake.

Rais hawezi akayumba kiafya halafu utegemee nchi isiyumbe, lazima iyumbe, itetemeke, ipepesuke, mambo lazima yatetereke na kusua sua, lazima idara zisimame kazi zake, lazima watu watege masikio juu ya Hali ya Rais, lazima mawazo ya watu yawe mahali pamoja tu, lazima kila muda iulizwe Hali ya Rais ikoje, lazima ufanisi wa kazi upungue makazini kwote na kila idara, mpaka Rais atakapo toka hadharani kulipungia mkono na kulisalimu Taifa ama kulihutubia Taifa letu ndipo mioyo ya watu itapona na kupata amani na Kuendelea na kazi kwa moyo wote.

Hivyo tusiwafundishe Wala kuwaingilia katika kazi watu waliopewa dhamani juu ya ulinzi na usalama wa Rais wetu, Tusiwachanganye Wala tusiwaone Ni wajinga, Mwenyezi Mungu alitupatia maarifa wanadamu hivyo lazima maarifa yote yatumike katika kuhakikisha Rais anakuwa salama muda wote, hiyo ni kazi yao. Ni wajibu wao wakufa na kupona kuhakikisha Rais Ni salama. Tusilete uanaharakati kwa kila Jambo.

Macho yetu lazima tujuwe Ni vipofu linapokuja suala la ulinzi na usalama wa Rais, sisi tunaona kwa macho haya ya nyama pekee, macho ya kukosoa, ambayo yanafumba hata upepo ukipita, macho yetu siyo Kama ya wale tuliyowapa dhamani ya ulinzi wa Rais wetu mpendwa, wao wanaona mbali, wanao hata tusivyoweza kuona kwa macho ya kawaida, wanaona hata kabla ya kukaa, wanaona hata mioyo yetu, wanaona hata ishara zetu, wanaona hata mifuko yetu, wanaona hata katikati yetu. Wakati sisi hata tukizibwa na mtu mrefu mbele yetu hatuwezi kusimulia kilichokuwa mbele yetu hatua chache.

Tuache ujuaji na kukosoa kila kitu, tuache uanaharakati kwa kila kitu, tuache utalaamu kwa vitu ambavyo hata darasni hatujawahi kukaa kujifunza, tuache umbilikimo wa kifikira na kimawazo, tuache werevu wakati ni vipofu wa masuala ya usalama, Tuache idara zetu za usalama zifanye kazi zake, zitekeleze wajibu wake.

Idara yetu ya ulinzi na usalama wa Rais Rai yangu kwenu ni kuwa endeleeni na majukumu yenu Wala msiyumbishwe Wala kuondolewa katika mstari wenu ,Wala kufundishwa kazi, Wala kuelekezwa na mtu wa nje kipofu wa masuala ya ulinzi na usalama, tunachohitaji Ni kuona Rais wetu ni salama kwa gharama zozote zile, tunampenda Rais wetu na tumewakabidhini ulinzi na usalama wake muutekeleze ipasavyo na kwa weledi mkubwa kwa msaada wa Mwenyezi Mungu mtoa njia maarifa.

Kazi iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
Rais asichukuliwe kama mungumtu. Anatakiwa awapende raia wake na kuongoza utatuzi wa matatizo yao. Akiwa rais ni binadamu wa kawaida kwenye hali ya kawaida. Atavaa mamlaka yake pale inapohitajka mfano kiutangaza vita, kutoa amri fulani, kuteua nk. Wananchi humpenda raisi anayewapenda na kuwatumikia na sie anayewatawala na kuwapa amri kisa ni raisi tu.
 
Rais asichukuliwe kama mungumtu. Anatakiwa awapende raia wake na kuongoza utatuzi wa matatizo yao. Akiwa rais ni binadamu wa kawaida kwenye hali ya kawaida. Atavaa mamlaka yake pale inapohitajka mfano kiutangaza vita, kutoa amri fulani, kuteua nk. Wananchi humpenda raisi anayewapenda na kuwatumikia na sie anayewatawala na kuwapa amri kisa ni raisi tu.
Rais siyo Mungu mtu lakini usalama na ulinzi wa Rais hauwezi ukawa sawa na Mimi au wewe, hiyo haiwezekani hata kidogo na haiji kuwezekana popote pale Dunianiii, Usalama na ulinzi wa Rais wetu mpendwa lazima ndio kiwe kipaombele Cha idara zetu za ulinzi na usalama popote pale anapokuwepo au atakapokuwepo Rais wetu,
 
Tindo ndugu yangu embu acha kuniabisha kwa maswali yasiyoendana na uwezo wako wa kufikiri, Mimi nafahamu uwezo wako Ni zaidi ya hapa na huwezi ukauliza swali la namna hii

Hamna kitu, kutaka umaarufu wa kijinga. Mnaingia madarakani kwa wizi wa kura, kisha mnapeleka utukufu usio na tija kwenye nyumba za ibada!
 
Kwani John F Kennedy hakuingia madarakani kwa kura halali? Abraham linkolin hakuingia kwa kura? Mambo ya usalama tuviachie vyombo vyetu vifanye kazi yake bila kuingiliwa na mtu yoyote yule

Kwahiyo akiingia kanisani na kiti chake ndio hayawezi kumkuta ya akina Kennedy? Acheni kutaka sifa za kijinga. Kwahiyo huko msikitini ataingia na jamvi lake? Utukufu wa kijinga kabisa.
 
Hamna kitu, kutaka umaarufu wa kijinga. Mnaingia madarakani kwa wizi wa kura, kisha mnapeleka utukufu usio na tija kwenye nyumba za ibada!
Serikali ya CCM ipo madarakani kihalali kabisaa Ndio maana hata Lisu aliposema muandamane kupinga matokeo wote wafuasi wake mlimgomea kuandamana maana mlijuwa matokeo Ni halali kabisaa na kwamba hakuwa na Sera Wala ajenda ambazo zingemfanya Apewe kura na watanzania.
 
Serikali ya CCM ipo madarakani kihalali kabisaa Ndio maana hata Lisu aliposema muandamane kupinga matokeo wote wafuasi wake mlimgomea kuandamana maana mlijuwa matokeo Ni halali kabisaa na kwamba hakuwa na Sera Wala ajenda ambazo zingemfanya Apewe kura na watanzania.

Watu hawakuandamana kutokana na woga wa kuuwawa, sio kwa uhalali wa matokeo. Endeleeni kuomba uoga uendelee kuwa wa kiwango hiki hiki, siku woga ukiisha ndio itakuwa mwisho wa CCM kukaa madarakani kwa shuruti.
 
Kwahiyo akiingia kanisani na kiti chake ndio hayawezi kumkuta ya akina Kennedy? Acheni kutaka sifa za kijinga. Kwahiyo huko msikitini ataingia na jamvi lake? Utukufu wa kijinga kabisa.
Vyombo vyetu vya ulinzi na usalama ndio vinajuwa uratibu wa suala Hilo la ulinzi wa Rais wetu mpendwa, kwa hiyo usianze habari za kusema huku itakuwaje au kule atabeba Nini, ndio maana Nilishasema nyie chadema Ni watu wakudandia matukio yasiyo hata wapa kitu, mkitoka hapa mnapoteana Tena maana hamnaga ajenda za kudumu,
 
Watu hawakuandamana kutokana na woga wa kuuwawa, sio kwa uhalali wa matokeo. Endeleeni kuomba uoga uendelee kuwa wa kiwango hiki hiki, siku woga ukiisha ndio itakuwa mwisho wa CCM kukaa madarakani kwa shuruti.
Sasa na wewe usiye muoga mbona hukuandamana? Halafu acheni kuwatukana watanzania kwa kusema Ni waoga baada ya kuwa wamewapuuza kutokana na kukosa kwenu muelekeo na dira ya kueleweka
 
Vyombo vyetu vya ulinzi na usalama ndio vinajuwa uratibu wa suala Hilo la ulinzi wa Rais wetu mpendwa, kwa hiyo usianze habari za kusema huku itakuwaje au kule atabeba Nini, ndio maana Nilishasema nyie chadema Ni watu wakudandia matukio yasiyo hata wapa kitu, mkitoka hapa mnapoteana Tena maana hamnaga ajenda za kudumu,

Mnafanya matukio ya kijinga kisha mnashangaa watu kuyakosoa?!
 
Sasa na wewe usiye muoga mbona hukuandamana? Halafu acheni kuwatukana watanzania kwa kusema Ni waoga baada ya kuwa wamewapuuza kutokana na kukosa kwenu muelekeo na dira ya kueleweka

Nasema hivi, hakuna watu waoga kama watanzania, lakini uoga huu utaisha tu maana tayari wameshajitambua. Sasa hivi watu wamelipuuza box la kura maana wamejua linachezewa. Iko siku mtakuta hawa waoga wako barabarani hamtaamini.
 
Hakuna tukio la kijinga Ila nyie ndio mmefanya watu wawashangae na kuwaona wababaishaji kwa kushupalia kitu Cha kawaida katika masuala ya ulinzi na usalama wa Rais wa nchi,Hii yote ni kutokana na kuwa mlishaishiwa Sera za kuwaweka masikioni na mioyoni mwao watanzania ndio maana mnajaribu kujirusha kila eneo
Mnafanya matukio ya kijinga kisha mnashangaa watu kuyakosoa?!
 
Anza wewe kwanza usiye muoga ili wengine wafuatw nyuma yako,
Nasema hivi, hakuna watu waoga kama watanzania, lakini uoga huu utaisha tu maana tayari wameshajitambua. Sasa hivi watu wamelipuuza box la kura maana wamejua linachezewa. Iko siku mtakuta hawa waoga wako barabarani hamtaamini.
 
Back
Top Bottom