Watanzania tuchutame, Uchaguzi Mkuu nchini Kenya umetuacha uchi

Watanzania tuchutame, Uchaguzi Mkuu nchini Kenya umetuacha uchi

Magufuli as an individual + enforcers wake walikusudia kupata faida gani kwa kuua vyama vya upinzani nchini ?

Sometimes people can be so silly. So facking silly.
Magufuli ametusaidia kutuonesha kwamba nchi hii Ina mifumo dhaifu sana. Kikwete na watangulizi wake walitudanganya kuwa tuna demokrasia nzuri lahasha hatuna kabisa kitu kama hicho. Hivi CCM imefanya mambo mazuri saaaana hapa Tz kiasi kwamba iendelee kushika madaraka? Siamini katika hilo nchi nyingi Afrika hata duniani kwa ujumla wameshabadili vyama kushika madaraka mara nyingi sana kwanini Tz? Kuna kitu hakipo saaa kabisa hasa mifumo yetu ya namna ya kupata Viongozi.
 
Tuseme ukweli tu kuwa majirani zetu hawa wametupiga gap kubwa sana, Sahivi wameanza kuhesabu kura kila kituo nchi mzima na zoezi la kuhesabu linafanyika kwa uwazi kabisa na makamera yakimulika na kila kitu kinachoendelea kuonyeshwa live kabisa hatua kwa hatua... Ile habari ya mawakala wa upinzani kufukuzwa kwa mtutu wa bunduki kisha kura feki kuingizwa kwa mabegi meusi huwezi kuyaona kwa wenzetu..
Wamepiga hatua kubwa sana yaani ni jambo la kuigwa sana hili. Hapa Tz tumejawa na mambo ya kihunihuni tu Kikwete ni bora asingeenda Kenya. Kuna yule jamaa nadhani anaitwa Mahera alikuwa kwenye Tume ya Uchaguzi uliopita ajifunze kule kenya.
 
Kuna yule jamaa nadhani anaitwa Mahera alikuwa kwenye Tume ya Uchaguzi uliopita ajifunze kule kenya.
Kuna watu wana uwezo wa kujifunza lakini pia wapo wasio na uwezo kabisa wa kujifunza na watu hao ndio CCM inawapenda.

They cannot learn and if learning was thrust down their throats they would only end up suffocating...they cannot swallow!

Watu aina hii CCM inawapenda sana kwani ndio mtaji wao...ujinga ni mtaji mkubwa wa CCM na ukichanganywa na unafiki, CCM baba lao!
 
Kenya walianza kubadili katiba, Bongo hamtaki kabisa mambo ya katiba ili muendelee na hila zenu. CCM wanajua wanachokiogopa na sio uchaguzi mfumo mzima wa kufanya siasa ni wa kiwaki hapa bongo
Mijitu inakwambia katiba mpya haiko kwenye ilani yetu!!!kwaiyo ni mpaka watakapojiskia wao kitu ambacho hakitatokea
 
Kenya mpaka wamefikia hapo walichapana na damu ikamwagika, naomba sisi tusipitie njia kama hiyo ila kuna mijitu inatulazimisha kufika uko kwa wizi wao wa kura
Ni bahati mbaya lakini wakati mwingine kwenye maisha hauwezi kupata heshima unayostahili mpaka ukiwashe.
 
Hivi hili dude bado lipo...bado linalipwa kodi zetu. Dah, Watanzania wakati mwingine tuwe tunaona hata aibu! Kama ni kweli kodi zetu bado zinatafunwa na watu kama hawa basi ni halali kabisa kwetu kuendelea kutawaliwa na CCM!

Tunakubalije ujinga kama huu? Tunakubalije pesa zetu kuchezewa hovyo namna hii? Tunakubalije kuendelea kulifumbia macho genge ambalo pamoja na kutokuwa na sifa wala uwezo linang'ang'ania uongozi ndani ya taifa letu?

Watanzania tuna tatizo, tuna tatizo kubwa sana. Kibaya zaidi ni uhaba wa wenye weledi, sifa na uwezo wa kutambua na kukiri ukweli huo. Wengi ni wanafiki wanachapa tu usingizi wala hawana habari dunia inakoelekea au tuko karne gani.

Hakuna laana kama kutojua kwamba hujui. Katika dunia ya sasa ya sayansi na tekonolojia, vituko kama tunavyoshuhudia katika zoezi la kuhesabu kura ni aibu tupu. Cha kustaabisha na kushangaza unakuta anayesimamia eti ni msomi mbobezi!
Hapa kwetu, takataka za aina hiyo ndio zimejaa mahakamani, bungeni, vyombo vya dola na madarakani.
 


Sina la kusema, nimepigwa butwaa. Najiuliza kama ule nilioushuhudia nchini Tanzania mwaka 2020 ulikuwa ni uchaguzi kweli.

Tukubali tusikubali, huu uchaguzi nchini Kenya umetuvua nguo na kutuacha uchi wa mnyama na kama bado tunazo tuchutame.

Nafuatilia matokeo yanavyotiririka kwenye TV na kushuhudiwa na Dunia nzima, bila kusubiri ruhusa.

Eti siri katika kuhesabu kura, really? Kura zikishapigwa kuna siri gani tena? Si ni kutangaza tu matokeo? Huu ujinga aliuanzisha nani hapa Tanzania?

Salaam zetu kutoka Twitter

View attachment 2320157
Kwa kweli tumevuliwa nguo...

Subiri matokeo
Hadi leo siku ya tatu bado wanajumlisha tu
 
Hapa kwetu, takataka za aina hiyo ndio zimejaa madarakani, bungeni, vyombo vya dola na madarakani.
Kwa maneno yao wenyewe wengi wao wanakiri kuokotwa tu majalalani. Nobody, I repeat, hakuna mtu mwenye akili timamu anaweza kuunga mkono hiki chama chakavu kisicho na malengo wala vision ila kwa ulafi tu,
 
\

Ni jambo la kustaajabisha sana kwamba wapo baadhi ya Watanzania wanakesha wakiomba na kutamani machafuko yatokee Kenya.

Kinachawafanya wawe na fikra hizo za kishenzi ni ili wapate nafasi ya kuhalalisha chaguzi zetu ambazo huandamwa na uchafuzi na udanganyifu.

Vyombo vyetu vya dola na hasa polisi vimekuwa mstari wa mbele kuwalinda wezi wa kura na kuwa chanzo cha vurugu kwenye vituo vya kupigia kura
1660211726979.jpeg
 
Subiri matokeo
Hadi leo siku ya tatu bado wanajumlisha tu
Ndio nyie hao tunaowasema, hebu angalia hii procedure ambayo kwa hapa kwetu ingekuwa kama kwenda sayari ya Pluto na kurudi...
1660211981187.png

Na hii ni safari ya kwanza wanaitumia...teknolojia hii...

Kwa hapa kwetu tumeunda taasisi ya teknolojia ambayo kazi zake ni kufuatilia wakosoaji wa serikali wanaandika nini mitandaoni na kuwatoza fedha maradufu watumiaji wa mitandao wanaotafuta tu namna ya kujiajiri katika ulimwengu huu wa utandawazi unaoenda kasi.

Tunapenda mno vya bure. Tunavuna kwenye mashamba ya wenzetu. Tumeletewa bure mitandao kurahisisha mawasiliano, sisi tuna watu wameajiriwa wakilipwa mamilioni eti kupanga bei katika kutumia mitandao hiyo. Je kama Watanzania tuliwekeza nini katika mitandao hii hadi tuvune?

Afrika Mashariki tulikuwa wa kwanza kupewa, na si kupigania uhuru kama wenzetu, lakini tutakuwa wa mwisho kutetea na kulinda uhuru wa watu wetu....shame, shame, shame!
 
Ndio nyie hao tunaowasema, hebu angalia hii procedure ambayo kwa hapa kwetu ingekuwa kama kwenda sayari ya Pluto na kurudi...
View attachment 2320886
Na hii ni safari ya kwanza wanaitumia...teknolojia hii...

Kwa hapa kwetu tumeunda taasisi ya teknolojia ambayo kazi zake ni kufuatilia wakosoaji wa serikali wanaandika nini mitandaoni na kuwatoza fedha maradufu watumiaji wa mitandao wanaotafuta tu namna ya kujiajiri katika ulimwengu huu wa utandawazi unaoenda kasi.

Tunapenda mno vya bure. Tunavuna kwenye mashamba ya wenzetu. Tumeletewa bure mitandao kurahisisha mawasiliano, sisi tuna watu wameajiriwa wakilipwa mamilioni eti kupanga bei katika kutumia mitandao hiyo. Je kama Watanzania tuliwekeza nini katika mitandao hii hadi tuvune?

Afrika Mashariki tulikuwa wa kwanza kupewa, na si kupigania uhuru kama wenzetu, lakini tutakuwa wa mwisho kutetea na kulinda uhuru wa watu wetu....shame, shame, shame!
Amen
 
\

Ni jambo la kustaajabisha sana kwamba wapo baadhi ya Watanzania wanakesha wakiomba na kutamani machafuko yatokee Kenya.

Kinachawafanya wawe na fikra hizo za kishenzi ni ili wapate nafasi ya kuhalalisha chaguzi zetu ambazo huandamwa na uchafuzi na udanganyifu.

Vyombo vyetu vya dola na hasa polisi vimekuwa mstari wa mbele kuwalinda wezi wa kura na kuwa chanzo cha vurugu kwenye vituo vya kupigia kura
Inasikitisha sana
 
Hatuchukulii kila mchango kwa umuhimu huo bro, ukiuliza swali kama halijajibiwa ni jambo la kawaida kabisa maana sio mtihani. Fahamu humu ni mitandaoni, sio kwenye chumba cha mtihani useme kwamba kila swali lina marks kadhaa.
EeeenHeeeee!

Naona hii "mitihani" ilikuachia alama ya kudumu!

Basi sawa, mkuu 'Tindo'.
 
Back
Top Bottom