Watanzania tuelezwe ni wapi alipo Rais wetu Mpendwa John Magufuli, ni haki yetu kujua

Watanzania tuelezwe ni wapi alipo Rais wetu Mpendwa John Magufuli, ni haki yetu kujua

Status
Not open for further replies.
Watu wa nchi hii wajinga sana. Sijui kwanini nimezaliwa nchi hii. Akionekana kila siku mnasema rais anapenda media. Mnapiga sana kelele kusema hata jambo dogo rais anapenda attension media kibao. Leo hajaonekana siku mbili tu mnapiga kelele sijui haonekani mlienda ikulu mkamkosa? Au mnataka tena aonekane kwenye media
Ujinga wa watu wa nchi hii ni kweli japo panaweza pasiwe na takwimu au tafiti iliyofanyika.
Lakini kuita watu wajinga halafu kwenye post hiyo hiyo ukaonyesha ufinyu wa ku reason ni ujinga wa namna yake pia.
Hoja ya mtoa mada si Rais aonekane kwenye media kila siku, kwa hiyo hoja unayotumia si relevant kwa mjadala huu.
 
Kusini ni mabingwa sana kwa kusoma kitabu na kuchanganya na mengine, sasa sijui kijana wao wa kimakonde aliwaitisha wazee kikao wakati wa ziara?!
 
Hivi kikwete na walivokuwa wanaumwa watu walishangilia hivihivi? Kama hawakushangilia basi kuna tatizo.
Unawajua wabongo wewe?? Hebu wasome hapa kipindi jk kaanguka jukwaani hadi mods wakaamua kuufunga uzi!
 
Ni kweli taarifa zinazoenea mitandaoni zinaleta taharuki tuna haki ya kujulishwa alipo rais wetu kipenzi wakiacha ziendelee hivi hivi wananchi wataamini uzushi huu kuwa ni kweli.
Heshima kwenu wakuu,

Kuna habari zinasambaa kwamba Rais wa Tanzania John Magufuli anaumwa wengine wanasema amekatiza Ziara huko Kusini ili kushughulikia Masuala mengine ya Kitaifa. Hili sina tatizo nalo.

Kinachoniumiza na kunitatiza ni kuona Taasisi ya Rais akiwemo Msemaji Mkuu wa Ikulu na Msemaji wa Serikali kutokanusha au kuweka sawa habari hizi zinazosambaa na kuacha watu waendelee kumsema vibaya Rais wetu. Ukiacha uongo ukaendelea kuongelewa unageuka kuwa kweli.

Rais sio mali ya Ikulu bali ni mali ya Watanzania wote wa vyama vyote, dini zote, rangi zote na Makabila yote.

Msemaji wa Ikulu, Gerson Msigwa huwa ni mwepesi kukanusha na kutupa update za Rais. Ajitafakari kwa hili kama vipi ajiuzulu tu. Kazi imemshinda ya kuwatumikia Watanzania.

Tunapata wakati mgumu kuelewa.

Kama anaumwa sio jambo la kushtua pia kwani maradhi kwa binadamu ni kawaida, kama anaumwa ni haki wananchi wake wakajulishwa na maendeleo yake yakaelezwa kwa uwazi.

Tumefanya hivyo kwa Baba wa Taifa Nyerere, Askofu Mkuu Mwandamizi Yuda Thadeus Ruwa'ichi, Benjamin Mkapa, Kikwete alipoumwa Tezi dume akiwa Rais na wengine wengi.




Kama yu mzima wa afya tujulishwe ili roho zetu zitulie.

Ni haki yetu kujua Rais alipo na maendeleo yake sababu anaishi kwa kodi zetu na tulimchagua wenyewe ndio maana Televisheni ya Yaifa inamuonesha popote aendapo bure ili wananchi wajue anachofanya Rais wao.

Hata kama kapumzika Ikulu, hakuna sababu ya kuzua taharuki.

Tunajua Rais wetu anapenda mpira hasa timu ya Taifa, Jana timu yetu imeshinda na kufuzu Michuano ya CHAN, hatujaona anapongeza na kushangilia kama kawaida yake.

Hata Msemaji wa Ikulu hajatuma picha akiangalia mpira wa watoto wake kama kawaida yao.

Tunamtaka Rais wetu.

Asanteni sana

TUJIKUMBUSHE;

"Taifa Stars wameipa heshima nchi yetu. Leo nimeona mpira, sio ule wa siku za nyuma."- Rais Dkt Magufuli akifurahia Tanzania kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika #AFCON2019
View attachment 1238150
 
Kuna wahuni na baadhi ya wanasiasa tuliowaheshimu wameonesha kushangilia tetesi hizo! Tabia za kichawi kabisa hata kama huwangi usiku.

Rais wetu ametenda mambo makubwa na yenye manufaa kuliko madhaifu mnayomhukumu nayo na kumtakia mabaya.

Serikali itoe taarifa rasmi badala ya kuacha redio za mbao ziendelee kulisha jamii chuki na tabia mbaya kabisa kuombeana mabaya kwa matamanio binafsi.

Ukweli haupiganiwi bali unajipigania.
Mambo makubwa unayosema unayaona kwa kutumia darubini gani? Mbona sisi wengine hatuyaoni??
Unadhani kumpiga tundu lisasi 38 ni jambo dogo??
 
Mungu hashindwi!
FB_IMG_1569386949512.jpeg
 
Huku sio Nigeria mzee baba..Nigeria kuna separation kubwa baina ya raia ndani ya nchi sio wamoja wale na kuna watu hawamtambui Buhari kama ni raisi wao..ila sisi tumejengwa kwa misingi ya umoja na mshikamano bila kujali tofauti zetu za kidini na kikabila tuna haki ya kujua alipo raia namba moja ambaye bila yeye hakuna sisi maana tunamtegemea alisongeshe gurudumu
Na aliyebomoa umoja tumuiteje?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom