Watanzania wana bidii ya maombi sana, bila dhana ya Mungu watakosa maana ya maisha kabisa

Watanzania wana bidii ya maombi sana, bila dhana ya Mungu watakosa maana ya maisha kabisa

Mungu ni neno uchwara mlilo jitungia vichwani mwenu ninyi watu wa dini na imani, Mnalo amini, lina uwezo wa kutenda yote na ndio muumbaji wa vyote.

Mungu ni dhana uchwara inayo aminiwa na nyie watu wa imani pamoja na dini kwamba ndio muumbaji, mmiliki na mwendeshaji mkuu wa ulimwengu.

Elimu ya kiroho ni nini?

Roho ni nini?

Na unathibitishaje roho ipo?

Au unaongea dhana zako uchwara zisizo na uthibitisho wowote ule..!!
Haka kafilosofia ka JF hakawezi kukuelewa,...kanajikutaga kana nondo kweli,...😁😁😂😂😂😂
 
Hapa kuna mambo matatu...., Maombi ni kama confidence booster na stress removal ; Na hapa siongelei tu Mungu huyu aliyeletwa na hawa wakuja, bali hata mizimu ya mababu na Imani za asili.....;

Mbili kwahio mtu aliyepo Dodoma au huko Kijijini hana la kufanya zaidi ya kushirikia kwa kujiridhisha yeye kwamba anasaidia (be it msaada wake kwa hao hauna nguvu ila kwake huenda unamsaidia kuondoa Stress)

Mwisho kabisa kwa wahusika wanaotakiwa kuweka mambo sawa, au wale waliopo ground itakuwa ni kukosa maarifa na kutokuwa na ufanisi badala ya kuokoa watu na kupanga mikakati kupoteza hata dakika kumi kufanya maombi...., Kwa wanaotaka maombi au kufanya maombi wakafanye Kanisani hapo ground zifanyike shughuli practical na kwa watumishi wetu (Idara husika) zijaribu kuwa proactive ili kama ni uzembe usitokee tena...
 
Hiyo ni kulingana na wewe.

Una amini kuna Mungu unayemtegemea, Halafu kwenye majanga, Huyo Mungu unaye mtegemea na kumtumainia haonekani akitoa msaada wowote.

Kama wewe sio Mpumbavu ni nini?

Ni uwendawazimu wa hali juu, Unakaa una amini kuna Mungu wa kukuokoa, Halafu yakitokea majanga, unaomba binadamu wenzako waje kukuokoa.

Kwa nini usi subiri huko chini ya kifusi, Huyo Mungu wako unayemtegemea aje aku okoe?
unapiga sana kwenye mishono,...kwani sehemu zingine huoni mkuuu?😂😂🙌🙌
 
Nimekuambia kipofu unamthibitishiaje kûna Mwezi juu ya anga?
Kama utashindwa kuthibitisha itaamaanisha Mwezi haupo?
Kuna mtu alikuuliza hapo juu unazungumzia Mungu yupi?

Dhana nzima ya kupinga uwepo wa Mungu ni mkanganyiko wa sifa alizopewa katika vitabu vya dini na uhalisia wa mambo.

Kipofu akikuambia ninaweza kuendesha BMW X5 kwa spidi ya 180km/ph utaamini au utaomba uthibitisho?
 
Kwa nini unaona tunapaswa kuamini na sio kujua mkuu?
Uko sahihi Kabisa ..

Mungu anasema Tusiamini Ila Tumjue...
Neno kuamini limekaa Kitumwa Tumwa sana ni bora neno Kumjua Mungu..

Ayubu 22:21

"Mjue sana Mungu, ili uwe na amani;

Ndivyo mema yatakavyokujia."

NA Hata Yesu aluwahi Kufundisha..

Yohana 8:32
"Tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru."
And ye shall know the truth, and the truth shall make you free.
 
Kuna mtu alikuuliza hapo juu unazungumzia Mungu yupi?

Dhana nzima ya kupinga uwepo wa Mungu ni mkanganyiko wa sifa alizopewa katika vitabu vya dini na uhalisia wa mambo.

Kipofu akikuambia ninaweza kuendesha BMW X5 kwa spidi ya 180km/ph utaamini au utaomba uthibitisho?
Dah Hii hoja Imebidi Nikaiprint kabisa 🤣🤣🤣
Naomba Niiweke na Kwenye Lamination🤣🤣
 
Katika mkasa wa jengo la Kariakoo kuanguka nimewasikia watu wengi wanaotegemea watu kutolewa au ambao waliangukiwa na jengo wakiomba na kushukuru Mungu, Allah au Yesu katika mkasa huo mkasa. Kila posti niliyosoma mtandaoni, kila clip au maongezi ya kila mtu aliyefukuliwa huwezi kuyakosa haya maneno(Maombi, Mungu, Allah, Ya Rabbi, Alhamdulillah na Yesu)

Hakika Watanzania dini imewakaa, ni viumbe wa kidini, bila dini na mungu sidhani kama wana tumaini lolote au muelekeo wowote wa maisha.
Watanzania tunampenda Mungu wa Wazungu na Waarabu lakini hatupendi.
 
Uko sahihi Kabisa ..

Mungu anasema Tusiamini Ila Tumjue...
Neno kuamini limekaa Kitumwa Tumwa sana ni bora neno Kumjua Mungu..

Ayubu 22:21

"Mjue sana Mungu, ili uwe na amani;

Ndivyo mema yatakavyokujia."

NA Hata Yesu aluwahi Kufundisha..

Yohana 8:32
"Tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru."
And ye shall know the truth, and the truth shall make you free.
Kumbe neno lenyewe linataka mtu upate kujua kwa hakika na sio kuamini tu🤔
 
Mungu yupo ndugu Hilo halina ubishi, haushangai hata taifa la wajanja zaidi marekani wanamuamini Mungu wewe ni Nani upinge,in God we trust
Mungu yupo, wapi?

Ulijuaje na unathibitishaje kwamba Mungu yupo?

Marekani kuamini Mungu yupo, sio uthibitisho wa kwamba ndio kuna Mungu kweli.

Kuamini unaweza kuamini hata uongo. Hata wamarekani wana amini kuna Dragons 🐉 watemao moto 🔥 midomoni mwao. Kwa sababu ni jambo la "kuamini" tu bila kuhitaji uthibitisho wowote ule.

Lakini tukitaka kuverify hiyo imani lazima tutake uthibitisho wa uwepo wa hao Dragons wenyewe walivyo, tuhakikishe na tuthibitishe.

Vivyo hivyo hata imani kwamba kuna Mungu, watu pamoja na wamarekani wana amini tu kuna Mungu, ila hawana na hakuna uthibitisho wowote ule wa uwepo wa huyo Mungu.

Sasa Tutahakikisha vipi na unathibitishaje kwamba kuna Mungu?

Kwa nini uhitaji kuamini Mungu yupo, Badala ya kujua kwa uhakika, ushahidi na uthibitisho kwamba Mungu yupo?
 
Nadhani Africa tuna shida, tunataja taja Mungu hovyo bila.kuwa na vitendo. Siku moja nilienda Helsinki Finland, kuna fire detector ikapiga alarm, yaani zima moto na kikosi cha uokozi kilifika ndani ya dakika 5. Watu wakaamriwa watoke na eneo likazungushiwa zile tap za tahadhari. Na hakuna mtu kusogea eneo hilo kama sio wa kikosi maalum.
Tuna kazi kubwa sana Africa
 
Back
Top Bottom