Watatu walioteuliwa Ukuu wa Wilaya, akiwemo Japheth Maganga wadaiwa kukataa uteuzi

Nafasi za m-Dc na ma-Ded ni vema waulizwe kabla ya kuteuliwa na Mamlaka ya uteuzi au Serikali itangaze nafasi hizo, ili watu wenye sifa na mahaba ya kufanya kazi hizo watume maombi(Expression of interest to serve as DC or DED) .
Baada ya hapo wizara ya Utumishi wa Umma ichambue maombi hayo na kuandaa orodha ndogo ya wanaokidhi vigezo(Shortlist).
Majina ya Shortlisted applicants yafanyiwe vetting na Mamlaka husika na kuhifadhiwa kwenye Kanzi data ya Serikali kusubiri uteuzi,pindi nafasi zinapotokea.

Faida ya utaratibu huu:
- Mhusika ameonyesha dhamira ya kuhudumu kwenye kazi hiyo.
-Mhusika anakuwa anafanyiwa vetting kujua uadilifu wake na haiba yake kwa jamii
-Mtindo wa kuteuana kiushikaji utapungua Kama siyo kutokomezwa.
-Haya masuala ya kukataa uteuzi yatakwisha.

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Una pointi lakini chini ya CCM hilo halitawezekana.

Udc na uded ndio uhai wa ccm.
 
Kumbuka huyo ni mwalimu. mpwayungu village anawajua vizuri mimi mwenyewe nimeshangaa anakataa offer ambayo ni sawa na pardon.

Angekaa hapo kama ni msafi ila kwa tuhuma zile ngoja tuone labda anajiamini hana hatia
Hata kama hana hatia bado serikali ina mbinu nyingi za kumsumbua... kwa mfano serikali inaweza kumfungulia kesi ya uhujumu halafu upande wa serikali wakaweka mashahidi 60 na katika hao 60 utakuta mwaka mzima wamesikilizwa watatu tu. Hadi siku unakuja kutoka kwa DPP kusema hana nia ya kuendelea na kesi tayari huku nje ushapoteza ramani. Angekubali uteuzi ili kupisha matatizo yanayoepukika.
 
Hio ndio tunaitaga ulafi. Mtu kashapiga sana hela ila bado anataka akomae kwa kukaidi amri ya mkuu wa majeshi.
 
Nonsense, unadhani watu wote wana njaa kama zako.
 
Kiongozi wa cwt taifa anaishi mahali anapotaka kuishi, mkuu wa wilaya anapaswa kuishi mahali alipopangiwa (ndani ya wilaya)
Anakuwa chini ya aliyemteua.
Viongozi wa cwt wao ndio wenye mamlaka....kwa kifupi tofauti ni kubwa japo vyote ni vyeo
 
Kwaiyo tubadilishe walaji wa pesa ya umma? 😂
 
Huwezi kataa, nakufahamu vema.
Unaujua mshahara wa DC ni shilingi ngapi?.
Una mtu wako yoyote TRA?, muombe akuangalizie kampuni yenye Tin.No. 141-848-089, uangalie inalipa kodi kiasi gani anually halafu gawanya kwa mshahara wa DC uangalie nawalipa mishahara ma DC wangapi wa Mama Samia!. Halafu mtu kama huyo autake u DC for what?!.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…