Watendaji Wizara ya Fedha wasimamishwa kazi kwa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha

Watendaji Wizara ya Fedha wasimamishwa kazi kwa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi Mkaguzi Mkuu, Mkaguzi Msaidizi na baadhi ya Watendaji wa Wizara ya Fedha. Amefanya hivyo ili kupisha Uchunguzi wa tuhuma za matumizi mabaya ya Fedha za Umma.

Ametoa agizo kwa Mkurugenzi wa TAKUKURU, ACP Salum Hamdun kufanya uchunguzi. Tuhuma mojawapo inayokabili ni malipo ya Milioni 251 yaliyofanyika Machi 31, 2021 yakielezwa kuwa ni malipo maalum bila kutaja kazi na waliohusika.

======

Waziri mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi mkaguzi mkuu, mkaguzi msaidizi na baadhi ya watendaji wa Wizara ya Fedha na Mipango kupisha uchunguzi wa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha za umma zinazowakabili.

Taarifa kutoka ofisi ya waziri mkuu iliyotolewa leo Mei 28, 2021 inaeleza kuwa katika kikao kazi na waziri wa fedha na mipango, katibu mkuu, manaibu katibu wakuu na watendaji waandamizi wa wizara hiyo mkoani Dodoma jana, Majaliwa amemuagiza mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (Takukuru), Salum Hamdun kufanya uchunguzi kuhusu tuhuma hizo na ikithibitika si za kweli wahusika warejeshwe kazini.

Majaliwa amezitaja tuhuma hizo kuwa ni malipo yaliyofanyika Machi 31, 2021 kupitia vocha 30 ya Sh251 milioni yakielezwa kuwa ni malipo maalum bila kutaja kazi maalum ni nini na nani aliifanya.

Amebainisha kuwa siku hiyo hiyo pia zililipwa Sh198.8 milioni kwa madai kuwa ni posho ya honoraria.

Mtendaji mkuu huyo wa Serikali amesema Aprili 8, 2021 watumishi 27 wa wizara hiyo walilipwa Sh44.5 milioni za posho ya kazi maalum ya wiki nne na Aprili 13, 2021 zililipwa Sh155.2 milioni kwa watumishi 68 ikiwa ni posho ya kazi maalum ya wiki tatu.

Pia Aprili 30, 2021 zililipwa Sh43.9 milioni kwa ajili ya kuandaa mpango wa kuhifadhi mazingira na siku hiyohiyo zililipwa Sh14.4 milioni kwa ajili ya siku ya wanawake.

Inaeleza kuwa fedha nyingine Sh43 milioni zililipwa siku hiyo na kufanya jumla ya malipo yaliyolipwa siku hiyo kuwa Sh101.8.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa Meimosi, 2021 zililipwa Sh184.1 milioni na mchana wa siku hiyo zikalipwa Sh264 milioni zikiwa ni malipo ya kazi maalum.

"Sisi tulikuwa Mwanza tunasherehekea siku ya wafanyakazi duniani nyinyi hapa ndani mnalipana posho,” amesema Majaliwa.

Inabainisha kuwa Mei 3, 2021 zililipwa Sh146.5 milioni kwa watumishi 125 zikiwa ni malipo ya kuandaa mpango kazi wa manunuzi kazi ambayo ni sehemu ya majukumu yao ya kila siku na siku hiyohiyo zililipwa Sh171.2 milioni kwa ajili ya kuandaa nyaraka za Bunge.

Taarifa hiyo imemnukuu Majaliwa akisema Sh155 milioni zililipwa kwa baadhi ya watumishi zikiwa ni posho yakuandaa miongozo wakazi.

"Yaani hii kazi ya ukaguzi inalipwa kwenye maeneo manne, huu ni utaratibu wa wapi? Mnazidi kutupunguzia imani, na sijaongelea eneo la kuhamisha mafungu na utaratibu kuhamisha fedha kisha mnakwenda kuzichukua huko mlikozihamishia,” amesisitiza Majaliwa.

Amewataka watendaji wa wizara hiyo kujenga uaminifu kwa wanaokusanya mapato kwa kufanya kazi kwa uaminifu na kuwatahadharisha kuwa watakaoendekea kucheza na fedha za umma hatua kali zitachukuliwa dhidi yao huku akiwapongeza wafanyakazi wenye weledi.

Chanzo: Mwananchi
Kwakweli ndiyo maana watu wamepoteza imani na serikali, wamepoteza morali ya kazi wamepoteza hata nia ya kuendelea kulipa kodi kumbe kuna genge la watu wanajinufaisha na fedha za umma
 
Kodi inakusanywa kutoka kwa WALALAHOI halafu hela inalambwa tu......

Vyema UCHUNGUZI uje na majibu kuwa si kweli na waendelee na majukumu yao!!

#KaziInaendelea
 
Hii habari haijakaa sawa.

Taratibu za fedha zina mtu aliyeomba hiyo fedha, wapo walioidhinisha hayo malipo, ndo na mkaguzi ni mmojawapo, yupo aliyelipwa, aliyetumia nk.

Na kila kitu kipo kwenye mfumo wa fedha.

Mtu muhimu ni aliyeinitiate hayo malipo. Faili la malipo lipo online.
Mkuu usemacho ni kweli ila hapo chini kumeongezwa neno "na baadhi ya watendaji ....".
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi Mkaguzi Mkuu, Mkaguzi Msaidizi na baadhi ya Watendaji wa Wizara ya Fedha. Amefanya hivyo ili kupisha Uchunguzi wa tuhuma za matumizi mabaya ya Fedha za Umma.

Ametoa agizo kwa Mkurugenzi wa TAKUKURU, ACP Salum Hamdun kufanya uchunguzi. Tuhuma mojawapo inayokabili ni malipo ya Milioni 251 yaliyofanyika Machi 31, 2021 yakielezwa kuwa ni malipo maalum bila kutaja kazi na waliohusika.

======

Waziri mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi mkaguzi mkuu, mkaguzi msaidizi na baadhi ya watendaji wa Wizara ya Fedha na Mipango kupisha uchunguzi wa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha za umma zinazowakabili.

Taarifa kutoka ofisi ya waziri mkuu iliyotolewa leo Mei 28, 2021 inaeleza kuwa katika kikao kazi na waziri wa fedha na mipango, katibu mkuu, manaibu katibu wakuu na watendaji waandamizi wa wizara hiyo mkoani Dodoma jana, Majaliwa amemuagiza mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa (Takukuru), Salum Hamdun kufanya uchunguzi kuhusu tuhuma hizo na ikithibitika si za kweli wahusika warejeshwe kazini.

Majaliwa amezitaja tuhuma hizo kuwa ni malipo yaliyofanyika Machi 31, 2021 kupitia vocha 30 ya Sh251 milioni yakielezwa kuwa ni malipo maalum bila kutaja kazi maalum ni nini na nani aliifanya.

Amebainisha kuwa siku hiyo hiyo pia zililipwa Sh198.8 milioni kwa madai kuwa ni posho ya honoraria.

Mtendaji mkuu huyo wa Serikali amesema Aprili 8, 2021 watumishi 27 wa wizara hiyo walilipwa Sh44.5 milioni za posho ya kazi maalum ya wiki nne na Aprili 13, 2021 zililipwa Sh155.2 milioni kwa watumishi 68 ikiwa ni posho ya kazi maalum ya wiki tatu.

Pia Aprili 30, 2021 zililipwa Sh43.9 milioni kwa ajili ya kuandaa mpango wa kuhifadhi mazingira na siku hiyohiyo zililipwa Sh14.4 milioni kwa ajili ya siku ya wanawake.

Inaeleza kuwa fedha nyingine Sh43 milioni zililipwa siku hiyo na kufanya jumla ya malipo yaliyolipwa siku hiyo kuwa Sh101.8.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa Meimosi, 2021 zililipwa Sh184.1 milioni na mchana wa siku hiyo zikalipwa Sh264 milioni zikiwa ni malipo ya kazi maalum.

"Sisi tulikuwa Mwanza tunasherehekea siku ya wafanyakazi duniani nyinyi hapa ndani mnalipana posho,” amesema Majaliwa.

Inabainisha kuwa Mei 3, 2021 zililipwa Sh146.5 milioni kwa watumishi 125 zikiwa ni malipo ya kuandaa mpango kazi wa manunuzi kazi ambayo ni sehemu ya majukumu yao ya kila siku na siku hiyohiyo zililipwa Sh171.2 milioni kwa ajili ya kuandaa nyaraka za Bunge.

Taarifa hiyo imemnukuu Majaliwa akisema Sh155 milioni zililipwa kwa baadhi ya watumishi zikiwa ni posho yakuandaa miongozo wakazi.

"Yaani hii kazi ya ukaguzi inalipwa kwenye maeneo manne, huu ni utaratibu wa wapi? Mnazidi kutupunguzia imani, na sijaongelea eneo la kuhamisha mafungu na utaratibu kuhamisha fedha kisha mnakwenda kuzichukua huko mlikozihamishia,” amesisitiza Majaliwa.

Amewataka watendaji wa wizara hiyo kujenga uaminifu kwa wanaokusanya mapato kwa kufanya kazi kwa uaminifu na kuwatahadharisha kuwa watakaoendekea kucheza na fedha za umma hatua kali zitachukuliwa dhidi yao huku akiwapongeza wafanyakazi wenye weledi.

Chanzo: Mwananchi
Wazee wetu WASTAAFU Wanateseka kusogeza Mafao yao Wengine Wanajilipa Pesa
 
Hayo ndiyo matokeo ya kumhamisha katibu mkuu wa fedha, Bw. Dotto, aliyekuwa ameidhibiti vizuri wizara hiyo. Katibu mkuu wa sasa ndiye anatakiwa kutumbuliwa. Hizo pesa hazingeweza kuwa zinachotwa ovyo ovyo bila idhini yake.
 
Hii habari haijakaa sawa.

Taratibu za fedha zina mtu aliyeomba hiyo fedha, wapo walioidhinisha hayo malipo, ndo na mkaguzi ni mmojawapo, yupo aliyelipwa, aliyetumia nk.

Na kila kitu kipo kwenye mfumo wa fedha.

Mtu muhimu ni aliyeinitiate hayo malipo. Faili la malipo lipo online.
Matumizi yale yalikuwa ya nini? Online payment yes...nani aliruhu na kwanini?
 
Kwakweli ndiyo maana watu wamepoteza imani na serikali, wamepoteza morali ya kazi wamepoteza hata nia ya kuendelea kulipa kodi kumbe kuna genge la watu wanajinufaisha na fedha za umma
Watetezi wao wapo hapa JF, angalia uzi unavyochangiwa....ama kweli JPM uliondolea wakati taifa bado linakuhitaji Sana, nasikia makusanyo huko TRA ni kichefuchefu....
Dawa hospital mtaniambia kufika julai hali itakuwaje.
SSH apewe mikumi!
 
Huu ni upuuzi tu, unless mwandishi kakosea. Sina hakika kama ni kazi ya Mkaguzi Mkuu kufanya kazi ya Pre-Audit. My understanding pre-audit inafanyika kabla malipo hayajafanyika.

Hii ni kazi ya Mweka Hazina/ Accountant. Lingekuwa ni tukio la mwaka uliopita ambao tayari Mkaguzi ameufanyia kazi, basi ningemuelewa Majaliwa.

Napataga shida kumuelewa huyu bwana.
Kwa kweli haijakaa sawa. Accounting Officer aka Afisa Masululi (mwenye vote) ni katibu mkuu wa wizara hiyo ambaye pia anaitwa Mlipaji Mkuu. Pesa ye yote haiwezi kulipwa bila idhini ya Afisa masululi. Mkaguzi mkuu wa ndani si mlipaji na wala hawezi kumzuia afisa masululi kufanya malipo. Kazi yake ni kushauri tu na ushauri wake si lazima ufuatwe.

Hivyo wakuwajibishwa na ubadhirifu huo ni katibu mkuu pamoja na mhasibu mkuu wake. Mkaguzi mkuu wa ndani yeye ni shahidi wa ubadhirifu huo. Of course mwenye mamlaka ya kumwajibisha katibu mkuu si waziri mkuu bali ni rais wa JMT. Waziri mkuu saizi yake ni Mhasibu mkuu - huyu ndiye angaliondoka naye na kumuachia rais kushughulika na katibu mkuu wake. Hao watendaji wengine wadogo wadogo ni kuwaonea tu maana wao wanatekeleza kilichoidhinishwa na hao mabosi wao ie katibu mkuu na mhasibu mkuu.

Ni vizuri sasa Mama akapunguza muda wa kukaa DSM akifanya diplomasia na kukaa zaidi Dom akifanya uendeshaji (executive duties) wa serikali.
 
Na wewe hueleweki...

Hawa uliowataja "wanapakua...." au "walipakua fedha ya umma?"

Hebu rekebisha "wakati" hapo. Kwamba, msomaji aelewe iwapo unaongelea wakati huu wa sasa au uliopita...

Kwa sababu as far as it concerned, hawa uliowataja karibu wote hawapo serikalini...
Kosa la jinai lina mwisho?
 
Hivi JPM alikutenda nini? Kila siku ni kumpalamikia kama msimbe
Utawala wake wa hovyo umenisababishia majanga mengi sana, mojawapo kuondoka Tz bila hata ya kupenda, hali iliyosababisha mambo yangu mengi kusimama huko nyumbani.
 
Back
Top Bottom