Watendaji Wizara ya Fedha wasimamishwa kazi kwa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha

Halafu naye anasema ana PhD ya Uchumi kama Mwendazake aliyekuwa anadai ana PhD ya Chemistry.

Kwa kweli utoaji PhD wa UDSM unatia mashaka makubwa sana ukiangalia hawa watunikiwa wawili Magufuli na Mwigulu
Unaandika utopolo Dkt Mwigulu amekaa muda gan paleee???this is utter nonsense unayoongea
 
Khaaaa....🤣🤣

Maneno yanakutoka tu.....

Ingekuwa kuachia NGAZI ni jambo rahisi kihivyo basi hakuna KIONGOZI NA BOSI yeyote angesalia UONGOZINI kila "rafu" zinapochezwa CHINI YAKE....kwani ni NYINGI....ziko hadi katika MAKUSANYO YA NYUMBA ZA IBADA......

#KaziIendelee
 
Kuna nini,? fungukeni, kama kuna upigaji sehemu tujuzeni tupige kelele wote mpaka kieleweke acheni mafumbo na kuzunguka aitasaidia.
Umeuliza nami kabla sijauliza, mara paap, ndi-ndi! msg ya Whatsapp imeingia na hotuba ya majaliwa; P.M.
Sikiliza hiyo:
View attachment 1800330
Your browser is not able to display this video.
 
Halafu naye anasema ana PhD ya Uchumi kama Mwendazake aliyekuwa anadai ana PhD ya Chemistry.

Kwa kweli utoaji PhD wa UDSM unatia mashaka makubwa sana ukiangalia hawa watunikiwa wawili Magufuli na Mwigulu
Nini kimetokea
 
Waziri Mkuu ameshalishughulikia kwa kuona TATIZO LILIKO...

PM hakusita kuiagiza TAKUKURU ifanyie kazi jambo hilo....

Leo kumtuhumu WAZIRI ambaye hata ROBO MWAKA hana ni KUMUONEA TU .....

NI KUMUONEA TU....

NI SIASA KOKO TU ....

#KaziIendelee
 
Hivi, ni mfumo upi wa kuhakikisha pesa ya umma haicheziwi??

Mbona Kila utawala unachemka??
 
Kama waziri mkuu Kassim Majaliwa alikuwa hajui huu utaratibu basi inabidi ajitafakari sana. Huu ni utaratibu wa kawaida kabisa kwa watumishi wa serikali kulipana posho kwa kazi nyingi za ofisini kama kuandika taarifa za mwezi na mwaka, kuandika hotuba za bajeti, kuandika taarifa mbalimbali za utendaji kazi zao nk.

Hakuna kazi serikali inayofanywa bila posho na hii imesababisha ugumu kwa viongozi katika kuwasimamia watumishi walio chini yao kama hakuna fedha. Bila posho kazi itafanyika kwa mbinde sana au huyo boss atoe ahadi ya posho pindi fedha itakapopatikana, na ahadi yenyewe iambatane na kuandikwa kwa vocha.

Kwa hiyo hii hatua anayotaka kuichukua waziri mkuu haitafanikiwa kwani posho hizi zilikwisha halalishwa wizara zote na watumishi wanajua kuwa ni haki yao. Vinginevyo asubiri mgomo baridi na ufanisi hafifu kutoka kwa watumishi.
 
Wala nafikiri msihangaike sana, kama matumizi ya pesa yamesemwa kuwa yalikuwa ni ya'shughuli na kazi maalumu'..... kazi iendelee.
 
Ndugu yangu Mwigulu alitokea kuwatungia watu kesi ya aibu ya "UGAIDI". Mahakama Kuu Kanda ya Tabora ikamtimua kwa kumwambia atafute shitaka lingine, kwani hapakuwa na Ugaidi Tanzania. Huyu si mtu mwema hata kidogo
 
Msimkorofishe rais acheni afanye kazi
Mnataka kesho na kesho kutwa mambo kama hayo yafanywe chinichini hapa waziri mkuu ale fungu na yeye mambo yaishie hukohuko we utajulia wapi?

ikiwa Madudu yanaanikwa mnakimbilia kumlaumu rais kwa lipi sasa
Waziri mkuu ni mteule wa rais mbona hamumsifu rais kwa kufanya kazi nzuri ya kumteua waziri mkuu ambaye ni mtendaji mzuri aliyeona hii changamoto na kuifanyia kazi?
Mwigulu mwenye wizara yake ni mteule wa rais pia kafanya Madudu yameanikwa sasa ni kazi ya rais kuangalia afanye nini juu ya huyu mtu ili mambo yaende sawa na hii ndiyo kujenga nchi
Kama wewe ndiyo rais utafanya nini ili kuweka mambo sawa Magufuli alizuia watu kusema leo watu wanasema ndiyo tunajua haya yote cha muhimu mama afanye maamuzi yasiyo na kigugumizi jela zipo
 
Hii maana yake kuna watu wana akili ambazo wengine hawana. Wana uwezo wa kiutumishi ambao hauna mfano kwa wengine.
Hii ni dhana tu ambayo ukweli ni tofauti. Wapo watu wengi na wenye uwezo, lakini kwa sababu hawajapewa nafasi ndiyo maana bila kujua wanapigiwa debe walewale.

Huwezi kujua uimara na udhaifu wa mtu kabla hajapewa nafasi kujaribu.
 
Licha ya kuwa naye atakuwa kwenye nafas ya kujieleza ili tujue ni vipi amekuwa nyuma ya tukio,lakini naunga nawe mtoa post. Mh.Waziri hili limekuchafua vibaya....Kiungwana achia ngazi pengine tutakuelewa!!!
 
Kuna muda itabidi tuingie barabarani kudai haki kwa lazima.
Nchi unaambiwa hatuna hela ya kuongeza mishshara lakini kila kona mbwa wanapiga dili.
Kwa taarifa ya Wazir Mkuu leo unawaza kwanini tusingefanya kama Kibwetele tu, yaani unamuambia Wazir Mkuu na hao waandishi tokeni nje halafu piga kibiriti tutakutana jehanamu.
 
kwani Mwigulu ndio kawatuma waibe Fedha za umma, inaonekana hao ndio tabia yao hiyo ya kupiga fedha za walipa kodi.
 
Waziri wa Fedha Mhe Dkt Mwigulu Nchemba mpaka muda huu yupo kazini wakati wizara yake imechafuka kiasi hiki. Yaani mpaka Waziri mkuu anagundua uchafu huu waziri ulikua umelala wapi?

Majina yanayowatukuza ndiyo chanzo cha uzembe na majivuno kazini na kuacha mambo ya msingi, nakumbuka aliwahi kusema ana the highest GPA na yuko smart upstairs kumbe hamna kitu
 
Wachunguzi nao watajilipa mamilioni kama posho ya kazi maalum. Bado dipipi, hakimu na wajanja wengine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…