Watu dhaifu ni hatari sana, wanakuwa hatari zaidi wanapopata fursa za uongozi

Watu dhaifu ni hatari sana, wanakuwa hatari zaidi wanapopata fursa za uongozi

JERUSALEMU

JF-Expert Member
Joined
Sep 19, 2012
Posts
3,114
Reaction score
3,541
Naam, wana bodi !

Niende moja kwa moja kwenye mada. Nayo inahusu watu dhaifu. Watu dhaifu ni watu hatari sana. Wakiwa wanasiasa wanakuwa hatari zaidi. Ni waoga wa mabadiliko. Waangalie wale wote waliobeba agenda ya mitano tena. Karibu wote ni dhaifu kisiasa na kijamii. Wanaposema mitano tena wanasukumwa na ubinafsi na kuogopa kuwa akija kiongozi mwingine watabaki na ulaji wao kweli?

Ukimtazama yule Mbunge wa Makambako utagundua haya ninayosema. Kwanza yule hata darasa la Saba hajafika, anawaza kwamba hivi akija kiongozi mwingine atakubali kumwacha aendelee kugombea ubunge na elimu yake duni ilihali ndani ya chama kuna wasomi wazuri tu? Kwa hiyo dawa ni kujifanya anampenda Rais na kutaka aendelee milele. Ni udhaifu wake ndio uliomfikisha hapo.

Mwigulu Nchemba ni msomi dhaifu. Ni kiongozi dhaifu hata kuliko watu ambao hawajasoma. Amefikia hatua anauliza watu wanadai KATIBA, KATIBA ya nini wakati Magufuli anatosha? Unajua kwanini? Amejua mapungufu ya mtukufu bosi wake kwa hiyo yupo tayari kuweka pembeni elimu yake yote ilimradi anapata mkate wa kila siku na kulinda maslahi yake kisiasa. Ni mtu dhaifu siyo mtu wa principles.

Kuna yule sijui Kessy, Mbunge Wa zamani wa Nkasi. Wajumbe walimchinjia baharini baada ya kuona amebeba agenda mfu. Nkamia naye wajumbe waliona dawa inayomfaa ni kumchinjia baharini. Ametulia !

Ninachotaka kusema ni kwamba watu dhaifu popote pale ni hatari. Wanakuwa hatari zaidi wanapokuwa wanasiasa. Mara nyingi hawana aibu. Ni wajinga wa milele. Kwao wao ustawi wa Nchi siyo kitu cha maana kuliko mafanikio yao binafsi. Hawabebi agenda za Nchi. Hawaangalii ajira kwa vijana, Utawala bora, Taswira ya Nchi Duniani n.k.

Kuna mjinga moja bila aibu aliutangazia ulimwengu kuwa ati watanzania sisi tunatamani kuona Chato ina kuwa kama Singapore!!! Kweli? Watu dhaifu wakimzunguka Rais ni hatari sana. Watu dhaifu nadra sana kutumia akili, mara nyingi huenenda na alama za nyakati au huangalia upepo unavuma kuelekea wapi. Hao ni watu dhaifu.
 
Tatizo Tanzania hata hao watu makini na madhubuti wakipewa ulaji hugeuka na kuwa dhaifu. Mifano tunayo mingi tuu.

Matatizo makubwa Tanzania ni njaa na ubinafsi, Rais wa awamu hii ndio kaharibu kabisa raia wake kila mteule wa Rais ni mtu dhaifu.

Kutengeneza taasisi imara Tanzania itatuchukua miaka mingi sana yaani kila mtu anaangalia tumbo lake tuu.
 
Sasa we unafikiri mtaani kuzuri jamaa, hata mie ningecheza CD ilioko redioni kwa sasa.

Huo ushujaa ambao hautakusaidia ni bora kuuweka pembeni kwa muda ili umalize muhula wako vizuri. VX V8 kila unapoenda shughulini mwako, kodi ya nyumba, ada zinalipwa bila shida na heshima pia ambayo mtu unakuwa nayo katika wadhifa uliopewa.

Ubaya ni kwamba nyie ambao mnasakama kuwa watu ni dhaifu pia mgefanya hayo hayo ambayo wanayafanya walioko katika nafasi za kisiasa. We una hakika ungeweza kuleta ujuaji ufukuzwe kitengo na kukabidhi ofisi kwa fedhea kubwa?

Ukaanze kula msoto si utaonekana chizi 😁😁😁
 
Tatizo ni kujipendekeza kwa mtawala, wameshajua wakipita kwake huku wakijichekesha chekesha wanapewa teuzi, na kuongea pumba pia ni sifa nyingine ya ziada inayawapa teuzi toka kwa mtawala.
Hahahahah thats why kuna ule msemo, "In Rome, better act like Romans"
 
Tatizo Tanzania hata hao watu makini na madhubuti wakipewa ulaji hugeuka na kuwa dhaifu. Mifano tunayo mingi tuu...
Kwa maoni yangu ili tutengeneze taasisi imara kuna mawili, ama jeshi lichukue Nchi kwa miaka kadha watulazimishe kujenga taasisi hizo au Chama cha upinzani kichukue Nchi na kuamua kutetekeleza mahitaji ya wana Nchi .

Kwa sasa inaonekana CCM wamejisahau na taratibu wameanza kuwashirikisha polisi, Takukuru na Wafanyakazi wengine Wa serikali kuiba kura. Nusu ya wabunge Wa CCM hawakushinda uchaguzi.
 
Tatizo la watanzania tunadhani viongozi wanaweza kututengenezea taasisi imara, trust me bila sisi wananchi hakuna kiongozi atakae fanya hivyo!!!
Mkuu Watanzania kuja kuzinduka sio kizazi chetu hiki cha 1980s - 2000s labla vizazi vijavyo maana hata hao viongozi ni kizazi hiki hiki kama kina Patrobas na Silinde.
 
Njaa ndio inasumbua na security, kumbuka ukienda kinyume na itikadi za mtawala aliyepo madarakani kuna jambo flani litakupata na hutalifurahia. Mifano iko mingi mno tu!
Mkuu kwa maoni yako naona upo hatarini kufedheheshwa ili upewe pesa.
 
Kwa maoni yangu ili tutengeneze taasisi imara kuna mawili, ama jeshi lichukue Nchi kwa miaka kadha watulazimishe kujenga taasisi hizo au Chama cha upinzani kichukue Nchi na kuamua kutetekeleza mahitaji ya wana Nchi . Kwa sasa inaonekana CCM wamejisahau na taratibu wameanza kuwashirikisha polisi, Takukuru na Wafanyakazi wengine Wa serikali kuiba kura. Nusu ya wabunge Wa CCM hawakushinda uchaguzi.
Theluthi mbili ya wabunge wa sasa sio chaguo la wananchi.
 
Tatizo Tanzania hata hao watu makini na madhubuti wakipewa ulaji hugeuka na kuwa dhaifu. Mifano tunayo mingi tuu.

Matatizo makubwa Tanzania ni njaa na ubinafsi, Rais wa awamu hii ndio kaharibu kabisa raia wake kila mteule wa Rais ni mtu dhaifu.

Kutengeneza taasisi imara Tanzania itatuchukua miaka mingi sana yaani kila mtu anaangalia tumbo lake tuu.
Kiukweli inafikirisha sana, inakuwaje taifa lililokuwa limejengwa kwenye msingi wa kijamaa kuwa na watu wabinafsi na mabepari wa nafsi kuliko Hata nchi za kibepari zenyewe.
 
Mkuu kwa maoni yako naona upo hatarini kufedheheshwa ili upewe pesa.
Itategemea na wadhifa husika, kitu ambacho siwezi kubali ni kuwa choko tu 😁😁😁 ila kupewa nyadhifa za kumenya kwenye ma Vieite aah mbona sana tu...Huku 12M inaingia kila mwezi tutaimba mapambio freshi tu usishangae ndio hali ya nchi ilipofikia.
 
Kwa maoni yangu ili tutengeneze taasisi imara kuna mawili, ama jeshi lichukue Nchi kwa miaka kadha watulazimishe kujenga taasisi hizo au Chama cha upinzani kichukue Nchi na kuamua kutetekeleza mahitaji ya wana Nchi . Kwa sasa inaonekana CCM wamejisahau na taratibu wameanza kuwashirikisha polisi, Takukuru na Wafanyakazi wengine Wa serikali kuiba kura. Nusu ya wabunge Wa CCM hawakushinda uchaguzi.
Kuna jamaa yangu Mwalimu alikuwa msimamizi mkuu kwenye moja ya vituo vya kura, anasema kituoni kura zilizidi Mara mbili ya kura halali zilizo pigwa baadae ikagundulika wenzake waliingia nazo so solution ni kuacha tu mana kumbe hata wale waangalizi wa upinzani nao walikuwa CCM. NI AIBU KWELI KWA YALIYOFANYIKA.

CCM ijue waliosimamia uchaguzi ni wananchi hivyo uchafu wao unafahamika nje ndani.

Walimu,, Maaskari na Usalama watakufa na siri kubwa sana kwa yaliyofanyika 2020.
 
Back
Top Bottom