Watu dhaifu ni hatari sana, wanakuwa hatari zaidi wanapopata fursa za uongozi

Watu dhaifu ni hatari sana, wanakuwa hatari zaidi wanapopata fursa za uongozi

Anaesema Mwalimu kufundisha masomo matano nae ni dhaifu au Mwalimu ndiyo atakuwa dhaifu kwa kutengeneza elimu dhaifu, kwa kifupi udhaifu ni ugonjwa wa mTz,
 
Tusilolijua ni kwamba, kutafuta madhaifu ya watu ni njia nzuri ya kuimarisha udhaifu wako.
 
Naam, wana bodi !

Niende moja kwa moja kwenye mada. Nayo inahusu watu dhaifu. Watu dhaifu ni watu hatari sana. Wakiwa wanasiasa wanakuwa hatari zaidi. Ni waoga wa mabadiliko. Waangalie wale wote waliobeba agenda ya mitano tena. Karibu wote ni dhaifu kisiasa na kijamii. Wanaposema mitano tena wanasukumwa na ubinafsi na kuogopa kuwa akija kiongozi mwingine watabaki na ulaji wao kweli??

Ukimtazama yule Mbunge wa Makambako utagundua haya ninayosema. Kwanza yule hata darasa la Saba hajafika, anawaza kwamba hivi akija kiongozi mwingine atakubali kumwacha aendelee kugombea ubunge na elimu yake duni ilihali ndani ya chama kuna wasomi wazuri tu? Kwa hiyo dawa ni kujifanya anampenda Rais na kutaka aendelee milele. Ni udhaifu wake ndio uliomfikisha hapo.

Mwigulu Nchemba ni msomi dhaifu. Ni kiongozi dhaifu hata kuliko watu ambao hawajasoma. Amefikia hatua anauliza watu wanadai KATIBA, KATIBA ya nini wakati Maguli anatosha? Unajua kwanini? Amejua mapungufu ya mtukufu bosi wake kwa hiyo yupo tayari kuweka pembeni elimu yake yote ilimradi anapata mkate wa kila siku na kulinda maslahi yake kisiasa. Ni mtu dhaifu siyo mtu wa principles.

Kuna yule sijui Kessy, Mbunge Wa zamani wa Nkasi. Wajumbe walimchinjia baharini baada ya kuona amebeba agenda mfu. Nkamia naye wajumbe waliona dawa inayomfaa ni kumchinjia baharini. Ametulia !

Ninachotaka kusema ni kwamba watu dhaifu popote pale ni hatari. Wanakuwa hatari zaidi wanapokuwa wanasiasa. Mara nyingi hawana aibu. Ni wajinga wa milele. Kwao wao ustawi wa Nchi siyo kitu cha maana kuliko mafanikio yao binafsi. Hawabebi agenda za Nchi. Hawaangalii ajira kwa vijana, Utawala bora, Taswira ya Nchi Duniani n.k.

Kuna mjinga moja bila aibu aliutangazia ulimwengu kuwa ati watanzania sisi tunatamani kuona Chato ina kuwa kama Singapore!!! Kweli? Watu dhaifu wakimzunguka Rais ni hatari sana. Watu dhaifu nadra sana kutumia akili, mara nyingi huenenda na alama za nyakati au huangalia upepo unavuma kuelekea wapi. Hao ni watu dhaifu.
Nyerere alisha sema maadui wa hii nchi ni:
1. Ujinga
2. Maradhi
3. Umaskini
Huyu namba 3 ndo hatari yani analeta udhaifu kila kona. Ndomana kila anae pewa nafasi kutumikia hii nchi lazima awe mdhaifu na mlafi mana ukizingatia viongozi wengi wametoka familia maskini wanatamani kupata hata stare kidogo huku wanasahau kwamba wanakula pesa za wananchi na wanatakiwa kutumikia hii nchi.
 
Hofu akiingia mwingine watakufa njaa.Hawana maarifa ya kuishi nje ya kupewa
 

Attachments

  • FB_IMG_1612431534245.jpg
    FB_IMG_1612431534245.jpg
    36.6 KB · Views: 1
Nyerere alisha sema maadui wa hii nchi ni:
1. Ujinga
2. Maradhi
3. Umaskini
Huyu namba 3 ndo hatari yani analeta udhaifu kila kona. Ndomana kila anae pewa nafasi kutumikia hii nchi lazima awe mdhaifu na mlafi mana ukizingatia viongozi wengi wametoka familia maskini wanatamani kupata hata stare kidogo huku wanasahau kwamba wanakula pesa za wananchi na wanatakiwa kutumikia hii nchi.
Thus huyu Bwana alikuja na falsafa ya kuwafanya watz wawe masikin Ili awatawale kwa kuwasomesha namba Ili KILA mwenye njaa aikimbie kwa kumuabudu ndo tunapata watu sampuli hizi takataka tumbo.
 
Bora kuwa mkweli tu, awamu hii ya jiwe kama huna maghorofa kariakoo hio biashara ya kukupa 30M kila mwezi bila stress za ajabu ni biashara ipi?

Kama ipi unadhani huoa mtaji wake utakuwa bei gani?
Lá a yani wewe uko muwazi kama jirani yangu. Tulikuwa tukimzungumzia kubadilika ki mtazamo Mr slow slow, tukagundua ni haki yake.

Night out allowance na travelling allowance, night moja ni 1.3 M akisafiti siku 20 kwa mwezi, kuongezea na allowances zote , na mkoba wa entertainment allowance 10M. Jumla 37 M, lazima kelele ziwe nyingi tuu.

Miaka kumi tayari kutengeneza maisha na heshima tele nyumbani. Sisi wa kuzomea tuendelee tuu hawezi kujali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo ni kujipendekeza kwa mtawala, wameshajua wakipita kwake huku wakijichekesha chekesha wanapewa teuzi, na kuongea pumba pia ni sifa nyingine ya ziada inayawapa teuzi toka kwa mtawala.
Ukisujudia nami nitakupa milki na fahari zote za duniani we anguka tu na usujudu.76% ya teuzi zimelenga mlemle
 
Tatizo Tanzania hata hao watu makini na madhubuti wakipewa ulaji hugeuka na kuwa dhaifu. Mifano tunayo mingi tuu.

Matatizo makubwa Tanzania ni njaa na ubinafsi, Rais wa awamu hii ndio kaharibu kabisa raia wake kila mteule wa Rais ni mtu dhaifu.

Kutengeneza taasisi imara Tanzania itatuchukua miaka mingi sana yaani kila mtu anaangalia tumbo lake tuu.
Mkuu hiyo avatar inakusaliti
 
Lá a yani wewe uko muwazi kama jirani yangu. Tulikuwa tukimzungumzia kubadilika ki mtazamo Mr slow slow, tukagundua ni haki yake.

Night out allowance na travelling allowance, night moja ni 1.3 M akisafiti siku 20 kwa mwezi, kuongezea na allowances zote , na mkoba wa entertainment allowance 10M. Jumla 37 M, lazima kelele ziwe nyingi tuu.

Miaka kumi tayari kutengeneza maisha na heshima tele nyumbani. Sisi wa kuzomea tuendelee tuu hawezi kujali.

Sent using Jamii Forums mobile app
Baba acha tu, yani hamna namna ni kujiunga na Praise and worship team tu 😁😁😁 kulinda maslahi ya ugali wako. Camera zikikutembelea wewe ni kumwaga u spoon tu kwa mzee wa Chattle!

Ikibidi unakandamizia mi naona aongezewe mitano ya nyongeza mambo ni mengi ya kukamilisha. Bado tunamhitaji kiongozi imara kama huyu!
 
Kwangu mimi ni bora iwe hivyo kuliko hapa tulipo fika. Kura za wana Nchi haziheshimiwi hata kidogo. Nusu ya wabunge waliopo Bungeni hivi sasa hawakuchaguliwa na wapiga kura. Ni bora jeshi lichukue Nchi ili tujipange kuheshimu KATIBA na matakwa ya wana Nchi.
Jeshi lipi hili linalobangulishwa korosho,mabosi zao ndio wanufaika wakubwa we hata ufe kwa njaa maadamu wao hushiba,hulka ya mwafrika aangalii Jamii bali tumbo lake.
Afrika udikteta sio tatizo tatizo ni wanufaika walionyuma ya dikteta je akiingia mwingine watakula wapi? Ingekuwa si wanufaika kitambo Sana ndoto yako ingeshatimia,shida akiingia mwingine wataishije?
 
Baba acha tu, yani hamna namna ni kujiunga na Praise and worship team tu 😁😁😁 kulinda maslahi ya ugali wako. Camera zikikutembelea wewe ni kumwaga u spoon tu kwa mzee wa Chattle!

Ikibidi unakandamizia mi naona aongezewe mitano ya nyongeza mambo ni mengi ya kukamilisha. Bado tunamhitaji kiongozi imara kama huyu!
Flashback tumeshuhudia watendaji Kama mahakimu,mapolisi,ma DC,rc wakiwatendea wapinzani ukatili Mkubwa sana na wakalipwa teuzi mifano hii hai mingi.Falsafa za kikomunisti wafanye watu wawe masikini ili uwatawale.Ili uepuke njaa ni kuomba camera zikutembelee mifano hai ni mingi.
 
Sasa we unafikiri mtaani kuzuri jamaa, hata mie ningecheza CD ilioko redioni kwa sasa.

Huo ushujaa ambao hautakusaidia ni bora kuuweka pembeni kwa muda ili umalize muhula wako vizuri. VX V8 kila unapoenda shughulini mwako, kodi ya nyumba, ada zinalipwa bila shida na heshima pia ambayo mtu unakuwa nayo katika wadhifa uliopewa.

Ubaya ni kwamba nyie ambao mnasakama kuwa watu ni dhaifu pia mgefanya hayo hayo ambayo wanayafanya walioko katika nafasi za kisiasa. We una hakika ungeweza kuleta ujuaji ufukuzwe kitengo na kukabidhi ofisi kwa fedhea kubwa?

Ukaanze kula msoto si utaonekana chizi 😁😁😁
Wafanye wawe masikini ili uwatawale principal
 
Let them poor to rude them hii ni falsafa ya kikomunisti KILA asiye na chapa na kugoma kuisujudia Sanamu ni lzm atashughulikiwa,
 
Unataka wanajeshi waingie utafikiri wata compromise na matakwa ya raia, kiongozi wa kijeshi ataongoza nchi kama taasisi ya jeshi, yaani ni amri mbele. Halafu inaweza kuleta instability ya muda mrefu, mfano kupinduana kwa hapa na pale.....kule Nigeria hawajawahi kuondoka kwenye nafasi za juu za uongozi wa nchi na hata yanayoendelea kule Myannmar kila mtu anajua...
Wanajeshi wao ni wanufaika sawa na sanga, nkamia, Kessy,pinda,katambi,musiba, mwigulu,masanja,lugola hofu akiingia mwingine wataishije?
 
Jamani mbona mnamuhandama mwigulu aka Lameck Madelu jamaa siku hizi anajiuna mjanja huku alikuwa bonge la mshamba.
Alikuwa mshamba au ni mshamba mpaka leo ila anajiona tu ni mjanja?
 
Back
Top Bottom