Watu siku hizi Tanzania wanakufa wakiwa na sura za kung'aa, mashavu yamejaa, miili iliyonona, umri pungufu ya miaka 50; Hii sio trend ya kawaida

Watu siku hizi Tanzania wanakufa wakiwa na sura za kung'aa, mashavu yamejaa, miili iliyonona, umri pungufu ya miaka 50; Hii sio trend ya kawaida

Dawa za ARV zitaangamiza wengi, unaona mdada ni mrembo au mkaka na ana afya nzuri kumbe kaunganishwa kwenye gridi ya umeme. Ukigusa umeenda na maji
Hilo sio kweli, tatizo kubwa ni magonjwa yasiyoambukiza ndio yanaotuua vibaya kutokana na life style na vyakula ambayo ni adui wa miili yetu
ZAmani watu tulikuwa tunatembea kila siku, ila siki hizi kila mtu ana gari , kama hana atatumia boda na daladala huyo maana yake ni anajaza sumu mwilini ,hicho chakula unachokula kinageuka sukari na kuweka sumu na mafuta mwilini
Utakufa kwa sukari, cancer, figo au pressure hilo tatizo ni kubwa kuliko unavyodhania ,utadondoka na kufa huku ukiwa na afya yako
 
ARV ni kama methali....
Uzuri wa mkakasi ndani kipande Cha mti! 🥴
Enzi hizo kuna wimbo fulani niliwahi kuusikia, “Uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti”

Walikuwa wakiaminishwa na kupatiwa tahadhari kuwa urembo wa mwanamke unaweza usiakisi yaliyomo ndani.

🎶🎶
Uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti,
Matiti ya kuchongoka,
Kiuno cha mdundiko,
Waliopaka wanja, na rangi kwenye kucha,
Hao tuwaepuke, wamejaa UKIMWI.
 
Kweli aisee mwezi wa 12 tulizika mtoto wa mjomba mdada(35yrs) yaani huyu alidondoka tu akafariki hapohapo, mwezi huohuo tena kabla ya x-mass kuna janja (22yrs) mgomba wa jirani yeye alivyolala ndio hakuamka tena asubuhi anaamshwa kimya hadi tukavunja mlango kumbe tayari wa juzi.

Yaani sasahivi kidogo wazee ndio tunawauguza ila range ya (20-40yrs) wanakufa ghafla sana.
 
Kweli aisee mwezi wa 12 tulizika mtoto wa mjomba mdada(35yrs) yaani huyu alidondoka tu akafariki hapohapo, mwezi huohuo tena kabla ya x-mass kuna janja (22yrs) mgomba wa jirani yeye alivyolala ndio hakuamka tena asubuhi anaamshwa kimya hadi tukavunja mlango kumbe tayari wa juzi.

Yaani sasahivi kidogo wazee ndio tunawauguza ila range ya (20-40yrs) wanakufa ghafla sana.
Inaogopesha aisee
 
Zamani kidogo kama miaka 15 nyuma ukisikia msiba mara nyingi unakuta ni mtu pamoja na kuwa mzee wa walau zaidi ya miaka 65 ila utakuta hata ukimuangalia utaambiwa kabisa bwana huyu alikuwa mgonjwa wa ugonjwa ABCDE na hata ukimuangalia marehemu unakuta kweli kachokaa, yaani magonjwa yamempiga kweli kweli.

Sasa aisee hii miaka ya karibuni, tena karibuni zaidi, kumekuwa na trend ya vifo vingi vya watu tena wengi wao ni pungufu ya miaka 50, na ukiwaangalia unaweza kuona mtu kapost status wiki iliyopita whatsapp, meaning hakuwa kwenye hali ya ugonjwa wa kumweka kitandani. Maana yake ni vifo vya ghafla bin vuu.

Kingine pia, wanaokufa yaani hata kwa watu waliokutana nao na hata picha zao yaani hawaonekani kuwa na shida, miili imenona, mashavu yapo na nyuso zenye tabasamu.

Najua humu ni great thinkers kwamba mna uwezo wa kuangalia mambo beyond awareness.

Hii inaweza kuwa ina maana kwamba rika la kati ya miaka 30 mpaka 55 hapa Tanzania kuna wagonjwa wengi ambao ndani ya miaka 5 kutoka sasa tunaweza kuwapoteza kwa ghafula zaidi ya asilimia 30? Kama ikitokea, si itakuwa na athari kwenye labor force na economic growth? Na je family sustainability ya Tanzania itakuwa kwenye hali gani ikiwa umri wa wababa na wamama wa familia wanaangamia kwa wingi?

Aisee watu wanakufa kwa speed ya mwanga, wakitabasamu usoni, je huu ni mwanzo wa mwenendo mpya wa watu kufariki?
Si kweli. Kwani wote wanaokufa wanang'ara sura kama unavyosema? Nenda vijijini uone wanaokufa katika umri huo mwanangu.
 
Sote njia yetu Moja ila kiukweli ukimwi ni tisho ambalo linachukuliwa poa. Aisee watu wameathirika bana sio mchezo🤔
 
Hakuna mchawi zaidi ya life style. kuna mwili ulionona si dalili ya afya njema bali ni afya mbovu na muda wowote unaweza kupoteza maisha..Mwaka 2019 nilikuwa na mwili ulionona kila mtu alikiwa ananiambia nina afya njema na maisha mazuri lakini siku moja nikawa sijisiki vizuri kufika hospital dk akanimbia nina hitaji matibabu haraka coz sukari na pressure vilikuwa juu sana na ngachelewa ndio ile inakupiga heart attack..nikaanza dawa na mazoezi mengi within 2 weeks nkapona kila kitu ..now ni miaka mitano imepita nko na mwili mzuri na sina hyo magonjwa na life style yangu ni mazoezi na kungalia sana ulaji
Sahihi, waswahili wanafikiri mashavu kunona sana na kitambi ni afya nzuri wakati ni kinyume chake.
 
Zamani kidogo kama miaka 15 nyuma ukisikia msiba mara nyingi unakuta ni mtu pamoja na kuwa mzee wa walau zaidi ya miaka 65 ila utakuta hata ukimuangalia utaambiwa kabisa bwana huyu alikuwa mgonjwa wa ugonjwa ABCDE na hata ukimuangalia marehemu unakuta kweli kachokaa, yaani magonjwa yamempiga kweli kweli.

Sasa aisee hii miaka ya karibuni, tena karibuni zaidi, kumekuwa na trend ya vifo vingi vya watu tena wengi wao ni pungufu ya miaka 50, na ukiwaangalia unaweza kuona mtu kapost status wiki iliyopita whatsapp, meaning hakuwa kwenye hali ya ugonjwa wa kumweka kitandani. Maana yake ni vifo vya ghafla bin vuu.

Kingine pia, wanaokufa yaani hata kwa watu waliokutana nao na hata picha zao yaani hawaonekani kuwa na shida, miili imenona, mashavu yapo na nyuso zenye tabasamu.

Najua humu ni great thinkers kwamba mna uwezo wa kuangalia mambo beyond awareness.

Hii inaweza kuwa ina maana kwamba rika la kati ya miaka 30 mpaka 55 hapa Tanzania kuna wagonjwa wengi ambao ndani ya miaka 5 kutoka sasa tunaweza kuwapoteza kwa ghafula zaidi ya asilimia 30? Kama ikitokea, si itakuwa na athari kwenye labor force na economic growth? Na je family sustainability ya Tanzania itakuwa kwenye hali gani ikiwa umri wa wababa na wamama wa familia wanaangamia kwa wingi?

Aisee watu wanakufa kwa speed ya mwanga, wakitabasamu usoni, je huu ni mwanzo wa mwenendo mpya wa watu kufariki?
Pombe Kali na ma chorestrlo
Kiufupi ni pressure na sukari
 
Oya vijana ukimwi upo, Kuna siku nili kuwa hospital ila Kuli kuwa na ka semina.

Vijana tukawa tuna ambiwa tupime ukimwi, kwakuwa najuana na dokta fulani aka nikomalie nipime.

wakati wa majibu, aisee pisi zaidi ya 3 zili toka zina Lia. Mmoja ali zimia kudadadeki.
Fiksi hii
 
Pombe Kali energy...sukari na wanga inanenepesha sana na kuua watu sana plus spirts za pombe...unakunywa heness unajifanya unazo kumbe imetengenezwa hapo mabibo...bado Kuna majoboz mabrand kibao usalama upo wapi plus mafegi kilanaina ....
 
📌DALII KIMOKO! NI MWENDO WA KIMYAKIMYA.

📌MBAAZI HIZO LAZIMA UNONO.

📌UNAKULA MBAAZI ALAFU BADO UNABWIA MAPOMBE, HUPUMZISHI MWILI,HULI MLO KAMILI,HUACHI NGONO ZEMBE LAZIMA USEPE MAPEMA!!!

📌HAKUNA MAAJABU TAKWIMU ZINAONYESHA GITAA LA DALI KIMOKO LIKO🔥🔥🔥

📌AJALI ZA BARABARANI ZIMEONGEZEKA. HILI NALO LINAFUKUZIANA NA DALI KIMOKO!

📌LIFESTYLE ( PRESSURE NA KISUKARI) HII INASHIKA NAMBA TATU.

#TII SHERIA BILA SHURUTI!!!
 
Ukiangalia mtaani kwako tu utaona wazee sio wengi basi vijana tujue ya kwamba wengi wetu tunakufa hpa katika ujana

Wazee kwa vijana tufanye yale yampendezayo Muumba na tuwe mbali na makatazo yake

Kifo hakina umri wala saa
Huenda wapo members wengi humu jukwaani washafarikk ila hakuna wa kuthibitisha hilo kama hamjuani
 
Back
Top Bottom