Watu wa Musoma tukumbushane stori za Musoma kuanzia 2000-2010

Watu wa Musoma tukumbushane stori za Musoma kuanzia 2000-2010

Mara ya mwisho kuonana nae ilikua ni Kitunda (Dar), alikua analima bustani ya mchicha. Nadhani ilikua 2016_ wakati huo Jack Pongo kaokoka hahaa. Hakuna marefu yasiyo na ncha!
Duchu alikua ananionea sana aisee kwa kisingizio cha baba angu kumwonea sana kipindi anasoma (baba angu alikua ni mwalimu mwisenge primary ) sasa kuna cku alinifukuza kutokea bwalo la police mpk makoko darajani ndo akanishika na kunichana na kiwembe mbavuni enzi hizo niko darasa la saba cku sita isahau asee ila baadae tulikuja kuwa marafiki wakubwa tu mpk alivyoingia jamaica mokers rasmi.
 
Huwa nikikaa na watu wa Arusha alafu wakaanza kuongelea ubabe wa huko kwao, huwa naishia kucheka tu. Musoma ilikua ni vita kamili.

Anyway, ulikua unateseka ukiwa maeneo gani hahaa?
Ni wachumba tu bado maana, kuhusu kundi kwa kundi kuuliana mtu ni swala la kawaida kabisa aisee ilikuwa noma, nimeweka sime mno kwenye modo au pemben ya mguu, aisee mpaka now nina harama ya mwana haramu mmoja ila nilichomtenda hatosahau nafikiri kila sehemu akifika anailizwa ulikuwaje...!?
 
Sehemu yenye vijana washamba na magrup yao ya kishamba kishamba .aani hawa vijana wa musoma wao wanaona mabifu ndiyo ujanja machoko sana
 
Mass town mwaka 2005 yalianzishwa makundi ya vijana kwa ajili ya kampeni za siasa vijana wapige kura kuanzia miaka 18 mpaka 30 muasisi akiwa mgombea ubunge ccm. Baada ya kampeni kuisha tu hilo kundi la WEST LAWAMA likageuka na kua kundi la wahuni wavuta bangi vibaka na waanzisha fujo musoma.mjini.ilipofika mwaka 2007 yaliibuka makundi ya vijana mengi sana karibia kila kata inakundi lake la kufanyiana fujo na makundi ya mitaa mingine:

1. USWAZI kata ya kamyonge mpaka mkendo, iringo
2. MBIO ZA VIJITI kata ya nyakoto na kigera
3. MDOMO WA FURU kata ya nyamatare
4. WABEPARI kata ya mwisenge

Ilifika kipindi wakawa musoma nzima wanafunzi wengi wako kwenye makundi ya uhuni. Siku za sikukuu hasahasa complex na tembo beach lazima mzike uzimwe mapema kisa fujo za haya makundi hasimu MBIO NA USWAZI . Tulishudia mapanga live kama picha za wahindi. Ilifika kipindi wakawa wanafungiana maeneo ya kutembea kama vile nyasho ikotokea umekutana nao we kimbua tu utapigwa lugoe.

Kuna vijana walikua maarufu sana enzi hizo kwa ubabe na uhuni kama vile Kasinia na wengine wengi nishawasahau.
Daah kweli kabisa mkuu, na kuna kundi lilitwa Jamaica Mockers.
 
Sehemu bora kabisa musoma kuwahi kutokea ilikuwa diocese ya musoma( kituo cha matumaini ya vijana).

Kilikuwa kituo bora cha michezo na masomo, vyote vilitolewa bure kabisa kilikuwa kisima cha maarifa, kituo hiki cha kanisa romani cathoric baada tu ya kufungwa ndipo yalipoanza kuibuka makundi ya uharifu na wahuni

Pale ilikuwepo michezo ya aina zote unayoifahamu wewe, maktaba na madarasa ya kufundishia fani mbalimbali ikiwemo uchoraji n.k

Vijana na watu wote walikuwa wanakutana pale kushiriki michezo na masomo hivyo hapakuwa na makundi ya kihuni, zilikuwepo timu za mipira na michezo mingine pamoja na wasomi.

Sijaona kikiongelewa humu mkumbuke na mazuri, msikumbushane matukio ya wahuni tu.
You're the best,buddie..
 
Musoma wajuaji wengi ila wajanja wa maisha wachache, nimekaa musoma miaka kadhaa na Tarime pia, kwa miji ya Mara bora Tarime kuna aina fulani ya maisha kwa mtu mwenye kuitaji kutoka wajita wa musoma maneno mengi sana..

Kuna mmoja niliwai kumtoa jino katika gym ya pale pembeni ya uwanja wa karume.. nilikuwa mgeni kule ila kwa sababu napenda mazoezi nikaulizia nikaelekezwa mahala pa gym.. nimefika siku ya kwanza, pili ya tatu jamaa akaanza kuwa anafuatilia maisha yangu... alifikiri siwezi mfanya kitu nilimpa ngumi moja jino likadondoka mpk leo sitasahau hakuna aliyethubutu kunisogelea maana inaelekea yeye ndo alikuwa nunda pale.

Nilikaa miaka 2 hivi nikahamishwa kikazi. Ila wasichana tu wa kule mwanaume unatongozwa kabisa kulikuwa na hotel moja hivi kubwa tu ipo pembezoni mwa ziwa nimeishau jina, nimekula sana samaki pale na pombe sana. Matajiri wa pale ni akina matayo, hussein sokoni, ila wana maisha ya kishamba sana aise. Mitaa naikumbuka kamyonge, umoja, makoko nk, jamaa, zangu walikuwa huyu aliyegombea ubunge, akina Bailes na wengine nimewasahau. Ila sijawai kutamani kurudi kule.
 
Hii thread imenikumbusha mbali nimewakumbuka marafik zangu..

ila sitamani kuja kuishi tena Musoma
 
Musoma wajuaji wengi ila wajanja wa maisha wachache, nimekaa musoma miaka kadhaa na Tarime pia, kwa miji ya Mara bora Tarime kuna aina fulani ya maisha kwa mtu mwenye kuitaji kutoka wajita wa musoma maneno mengi sana..

Kuna mmoja niliwai kumtoa jino katika gym ya pale pembeni ya uwanja wa karume.. nilikuwa mgeni kule ila kwa sababu napenda mazoezi nikaulizia nikaelekezwa mahala pa gym.. nimefika siku ya kwanza, pili ya tatu jamaa akaanza kuwa anafuatilia maisha yangu... alifikiri siwezi mfanya kitu nilimpa ngumi moja jino likadondoka mpk leo sitasahau hakuna aliyethubutu kunisogelea maana inaelekea yeye ndo alikuwa nunda pale.

Nilikaa miaka 2 hivi nikahamishwa kikazi. Ila wasichana tu wa kule mwanaume unatongozwa kabisa kulikuwa na hotel moja hivi kubwa tu ipo pembezoni mwa ziwa nimeishau jina, nimekula sana samaki pale na pombe sana. Matajiri wa pale ni akina matayo, hussein sokoni, ila wana maisha ya kishamba sana aise. Mitaa naikumbuka kamyonge, umoja, makoko nk, jamaa, zangu walikuwa huyu aliyegombea ubunge, akina Bailes na wengine nimewasahau. Ila sijawai kutamani kurudi kule.
Wanaotaman kuish kule ni watu wa hukohuko Kuna kaz niliwahi kuipiga chin kwasababu tu napachukia huko
 
Nakumbuka enzi hizo kwenda Disco Toto Tembo Beach kila sikukuu za Mwisho wa mwaka, Wasanii wakija Karume Stadium tunasubiria mda wa fungulia mbwa ndipo tuingie wakati kiingilio ni 1000 tu watoto.

Watu maarufu kama Tajiri mwenye mbwembwe Nyakiteri, Dereva wa mbio za magari Mama's, Hussein Sokoni, Redio yetu pendwa Victoria FM hapo utawakuta wakina Boke Wambura, Maregesi Girishon, Emmanuel Chibasa, Issa Nundu, mzee wa Mafua Robson Wangaso na wengineo, mitaa ya Nyasho hapo ndilo chimbo la kujipatia mavazi.

Fujo za Musoma Tech na Songe hadi kupelekea Songe kuwa ya wadada, Mitaa maarufu kama Mukendo, Iringo, Mwigobelo, Majita Road bila kusahau vibaka wa Magamaga, na kila likizo tunakutana tuition Mwembeni hapo utakutana na watoto wa Isenye, Ikizu na sisi wa Bweri Makatani.
Hivi kipindi hiki Esther Bulaya alikuwa kishazaliwa?
 
Back
Top Bottom