Watumishi wengi wa Serikali hawana tija. Mishahara inapotea bure

Watumishi wengi wa Serikali hawana tija. Mishahara inapotea bure

Unakuta mtumishi wa serikali anaingia kazini saa 2 asubuhi. Saa 3 anatoka kwenda mtaani kutafuta chai...anarudi ofisini saa 5 au 6 mchana. Anavuta muda ikifika saa 7 mchana anatoka kwenda kutafuta chakula cha mchana. Anarudi saa 8 mchana. Saa 9 huyo anaondoka zake. Ni watumishi wengi sana wa Umma wana hii ratiba kila siku, kila wiki, mwezi na miaka kadhaa... Cha ajabu mwisho wa mwezi mshahara unaingia.

Viwango vya mishahara na faida au output ya mtumishi wa Umma havilingani kabisa. Mtu anaweza kukaa miaka 3 hadi 5 au 10 hajawahi kufanya kazi yoyote kabisa. Lakini unamkuta kachomekea, kaulamba mkanda nje.

Halafu unakuta mtu ana elimu nzuri kabisa.

Hii nchi dah.
Uko sahihi kabisa, vilaza ni wengi sana Serikalini wamekaa tu hawana issue kabisa maofisini
 
Hata wababa wengi wa familia wanaziba nafasi bure tu.

Imagine mida kama hii mtu anashindwa kuhudumia familia unamkuta yupo kwenye mitandao.

Tena amechomekea vizuri na ukimuona kama mtu vile
😅
😂🤣
 
Wivu ni kitu kibaya sana katika maisha ! Ukiona mtumishi amekaa bila kazi ujue kashatimiza wajibu wake ! Kama ni kero mbalimbali za umma wapo wa kuzisemea kwenye umma na huleta kwa watu wa chini na kufanyia kazi. Siyo kila mda mtumishi anakuwa busy ofisini kuna wakati kazi ambazo amepewa anakuwa ameshazimaliza kwanini asipumzike .
Mleta mada ana wake mtu anaye muwinda ila ameshindwa tu kumtaja🤣
 
Tatizo serikalini hakuna targets kwa mfanyakazi na hawafanyiwi tathmini kwakua hawasign KPI na ndio wanakwamisha sana Taifa hizi performance na mafanikio tunayoona kwenye sekta binafsi wafanyakazi wake wana sifa sawa kabisa na hawa waserikali ni kwakua wamesoma vyuo hivi hivi lakini utamaduni wakifanya kazi kwa malengo ndio unawatofautisha
Upo sahihi kabisa.

Huko private pia mtu akiweka mpangokazi wake anawezeshwa kwenda kutekeleza majukumu yake fresh kabisaaa,unatarajia hapo mtu hataacha kuipenda kazi yake mkuu?
 
Nakubaliana kabisa na wewe.

wengine wanatembelea maV8 kabisa lakini kazi kupiga misele tu huko uraiani kujifanga wako busy kumbe wanawaza upigaji tu.
 
Solution Ni kuwa na Watumishi wanaotosha.

Baada ya Hapo, kila mtumishi apewe haki yake kama mshahara, extra duty, sehemu ya kuishi, nauli au usafiri, na chakula wakati wa kazi.

Mshahara uwe classified katika mafungu, Mshahara, extra duty, nyumba, matibabu ( housing allowance ) n.k

KILA mtu akishapata haki yake, then una haki ya kumdai na wewe UTUMISHI ULIOTUKUKA.

Vinginevyo ASHUGHULIKIWE.
And the thread is closed
 
Serikali ibadiri mfumo wa kuajiri.

Seniour positions zote ziwe zinatangazwa watu wanaomba na kuwa interviewed.
Ajira ziangalie sana skills, exposure, level ya shule, exposure ijikite zaidi kwenye makampuni binafsi makubwa yakimataifa..

Serikali iwe makini sana na kuajiri kamlete, hata kama ni form four au six, basi wapimwe uelewa na viwango pia vya ufaulu vya hiyo form four na six viangaliwe...ajira za mjomba,shangazi nk ziangaliwe sana na watu makini..

Ajira za uteuzi zipunguzwe kwa kiasi kikubwa na baadala yake nafasi zitangazwe kwa sifa maalum watanzania waombe, washindanishwe na best candidates wapewe nafasi mfano IGP, RPC's, RC, DC's, UCEO wa mashirika ya umma.
 
Unakuta mtumishi wa serikali anaingia kazini saa 2 asubuhi. Saa 3 anatoka kwenda mtaani kutafuta chai...anarudi ofisini saa 5 au 6 mchana. Anavuta muda ikifika saa 7 mchana anatoka kwenda kutafuta chakula cha mchana. Anarudi saa 8 mchana. Saa 9 huyo anaondoka zake. Ni watumishi wengi sana wa Umma wana hii ratiba kila siku, kila wiki, mwezi na miaka kadhaa... Cha ajabu mwisho wa mwezi mshahara unaingia.

Viwango vya mishahara na faida au output ya mtumishi wa Umma havilingani kabisa. Mtu anaweza kukaa miaka 3 hadi 5 au 10 hajawahi kufanya kazi yoyote kabisa. Lakini unamkuta kachomekea, kaulamba mkanda nje.

Halafu unakuta mtu ana elimu nzuri kabisa.

Hii nchi dah.
Halmashuri ndio hz ishu zipo nenda tanesco kazkaz
 
Watu wanafanya kazi kulingana na kipato wanacholipwa.

Sasa mtu unamlipa Tsh 419,000 na Take home 350,000/-

Hakuna allowance yoyote ya nyumba, chakula Wala usafiri Wala extra duty.

Sasa wewe unataka afanye kazi kama Yuko Jela.

Kwani Utumishi wa umma Ni ADHABU???
Ila kweli pesa Ni kiduchu sna mnazopokea
 
Mtoa mada umeandika kwa hisia hasira sana. Si bure, inawezekana ukawa mhanga wa vyeti feki.
 
Unakuta mtumishi wa serikali anaingia kazini saa 2 asubuhi. Saa 3 anatoka kwenda mtaani kutafuta chai...anarudi ofisini saa 5 au 6 mchana. Anavuta muda ikifika saa 7 mchana anatoka kwenda kutafuta chakula cha mchana. Anarudi saa 8 mchana. Saa 9 huyo anaondoka zake. Ni watumishi wengi sana wa Umma wana hii ratiba kila siku, kila wiki, mwezi na miaka kadhaa... Cha ajabu mwisho wa mwezi mshahara unaingia.

Viwango vya mishahara na faida au output ya mtumishi wa Umma havilingani kabisa. Mtu anaweza kukaa miaka 3 hadi 5 au 10 hajawahi kufanya kazi yoyote kabisa. Lakini unamkuta kachomekea, kaulamba mkanda nje.

Halafu unakuta mtu ana elimu nzuri kabisa.

Hii nchi dah.
Kwani wewe wakati huo wewe unakuwa unafanya kazi gani. Suala la kukaa mtaani kuhesabu wangapi wanakuja kunywa chai mtaani halitakusaidia. Kwa maana nyingine wewe hauko tofauti na jao unaowaona mtaani. Kama ungekuwa na kazi ya kufanya tusingetegemea ukutane nao mtaani hivyo wewe mwenyewe ni jipu.
 
Unakuta mtumishi wa serikali anaingia kazini saa 2 asubuhi. Saa 3 anatoka kwenda mtaani kutafuta chai...anarudi ofisini saa 5 au 6 mchana. Anavuta muda ikifika saa 7 mchana anatoka kwenda kutafuta chakula cha mchana. Anarudi saa 8 mchana. Saa 9 huyo anaondoka zake. Ni watumishi wengi sana wa Umma wana hii ratiba kila siku, kila wiki, mwezi na miaka kadhaa... Cha ajabu mwisho wa mwezi mshahara unaingia.

Viwango vya mishahara na faida au output ya mtumishi wa Umma havilingani kabisa. Mtu anaweza kukaa miaka 3 hadi 5 au 10 hajawahi kufanya kazi yoyote kabisa. Lakini unamkuta kachomekea, kaulamba mkanda nje.

Halafu unakuta mtu ana elimu nzuri kabisa.

Hii nchi dah.
Ukitaka asitoke kwenda kutafuta chai au chakula, mpe chai na chakula hicho hapo hapo kazini ili awe na nusu saa tu ya kula na kurudi kazini....

Pamoja na criticism hii, hata hivyo, mwisho wa siku malengo utendaji hufikiwa bila shaka kwa sababu hatumpimi mtu kwa muda anaotumia kunywa chai au kula chakula...

Mfanyakazi anapimwa kwa deliverance yake, kwamba amefanya kwa ufanisi (effectively) kile alichotakiwa kukifanya kwa muda unaotakiwa...?
 
Kiasi chake mtoa mada ana hoja ya msingi kwa mantiki zifuatazo.

Unakuta mtu yupo idara ya kilimo na mifugo katika kata fulani, elimu yake ikiwa ni diploma, basi anaamua kwenda kusoma zaidi kwa maana ya degree na hata PhD. Sasa baada ya kuhitimu masomo ya juu nilitegemea mtu Kama huyo Basi aje na mbinu mbadala za kuinua kilimo hususani maeneo zinakofanyika shughuli za kilimo, sasa badala yake yeye anapanda cheo anakuwa mtu wa kusoma ripoti ofisini tu, na siyo tena yule aliyekuwa akishinda field na wakulima na wafugaji.

Mimi nadhani hata watu wanaoomba kwenda kusoma, waeleze wameona changamoto gani ktk kazi husika ambayo wanadhani wakienda kusoma wakirudi watakuja kuitatua. Siyo Kama ilivyo sahizi wengi wanaenda kusoma ili wapande vyeo, mishahara na wapunguziwe kazi.

Kama taifa tunahitaji watu ambao wapo tayari kutumia elimu zao vizuri kwa masilahi mapana ya taifa.
 
Tatizo serikalini hakuna targets kwa mfanyakazi na hawafanyiwi tathmini kwakua hawasign KPI na ndio wanakwamisha sana Taifa hizi performance na mafanikio tunayoona kwenye sekta binafsi wafanyakazi wake wana sifa sawa kabisa na hawa waserikali ni kwakua wamesoma vyuo hivi hivi lakini utamaduni wakifanya kazi kwa malengo ndio unawatofautisha
You are right..

Lakini pia kuna utofauti Mkubwa wa challenges & motivation factors kati ya mfanyakazi wa sekta binafsi na ya umma...

Hebu twende na mifano michache. Hapa tuna mfanyakazi (askari) wa kikosi cha Zimamoto. Gari la maji ya kuzimia moto liko pale. Kunatokea emergency ya moto somewhere near where you are living. Wafanyakazi wapo lakini vitendea kazi hakuna. Gari halina mafuta ya kuliendesha. Au haliwezi kabisa kutembea kwa sababu halijawa serviced kwa muda mrefu. Ukiuliza unaambiwa hakuna fedha ya mafuta wala service kwa sababu serikali haijatoa hela....!!!

Katika mazingira haya mfanyakazi akilala tu kazini au akienda kutafuta chakula kwa masaa 6 utamshangalia nini? Na hata ukimpa KPI bila vitendea kazi utapata matokeo gani...?

Aidha, katika sekta ya umma ni ngumu sana kuwa na wafanyakazi wenye moyo wa kujituma kwenye public sector kama kunakuwa na utofauti mkubwa wa viwango vya madaraja ya malipo kwa watu walio na kiwango sawa cha elimu tofauti ikiwa ni huyu ni mwalimu, mwingine askari na mwingine daktari nk nk...

Nenda kwa wanasiasa kuanzia ngazi ya mawaziri, wakuu wa idara, maDC, MaRC, wabunge nk nk yaani wamejipangia mishahara na marupurupu makubwa kiasi cha mara 100 au hata 200 cha kiwango cha mshahara wa mwalimu Grade A au Nesi mwenye stashahada...

Na wakati mwingine huyu mbunge au DC au RC anazidiwa kwa mbali sana kielimu na hawa ambao anawasimamia na kuwatungia sheria na sera mbalimbali....

Kinachotakiwa siyo hiki cha kulalamika. Ni kufanyika kwa mageuzi makubwa ktk sekta ya utumishi wa umma. Kusiwe na tofauti kubwa kivile kwa malipo kama ilivyo sasa, kwamba kuna mwingine analipwa 400,000 kwa mwezi na kuna wengine wanavuta hadi 30,000,000....!!

This is completely not fair at all. Katika mazingira haya lazima tu kuwe migogoro mingi msingi wake ukiwa ni tofauti ya kimaslahi miongoni mwa watumishi wa umma...
 
Unakuta mtumishi wa serikali anaingia kazini saa 2 asubuhi. Saa 3 anatoka kwenda mtaani kutafuta chai...anarudi ofisini saa 5 au 6 mchana. Anavuta muda ikifika saa 7 mchana anatoka kwenda kutafuta chakula cha mchana. Anarudi saa 8 mchana. Saa 9 huyo anaondoka zake. Ni watumishi wengi sana wa Umma wana hii ratiba kila siku, kila wiki, mwezi na miaka kadhaa... Cha ajabu mwisho wa mwezi mshahara unaingia.

Viwango vya mishahara na faida au output ya mtumishi wa Umma havilingani kabisa. Mtu anaweza kukaa miaka 3 hadi 5 au 10 hajawahi kufanya kazi yoyote kabisa. Lakini unamkuta kachomekea, kaulamba mkanda nje.

Halafu unakuta mtu ana elimu nzuri kabisa.

Hii nchi dah.
Na vipi Kama majukum yake anakua ameyatimiza unataka akae anaangalia meza?
 
Hata wababa wengi wa familia wanaziba nafasi bure tu.

Imagine mida kama hii mtu anashindwa kuhudumia familia unamkuta yupo kwenye mitandao.

Tena amechomekea vizuri na ukimuona kama mtu vile
Chacha unataka vuka mipaka⛹️
 
Siku hizi Hata Dodoma hawakai tena wanarudi DSM alhamis yaani na hawajali wala nini!wanakuambia mama mwenyewe anatembea na sisi acha tuzurure!
In short watumishi wa umma ni majanga
 
Back
Top Bottom