Hakuna basi ya Newforce/Golden Deer yenye uwezo wa kumfukuza Sauli hata siku moja.
Niwarudishe nyuma kidogo,enzi stendi ya mabasi ipo pale Ubungo,Newforce/Deer aliamua kukimbilia Shekilango kwa basi za Mbeya/Tunduma tu na kwa safari za Songea alibakia palepale terminal Ubungo,lengo kubwa kimkakati ilikuwa ni kumkimbia Sauli, Newforce/Deer akaamua kuanzia ligi pale nje ambapo hakuna foleni kubwa ya kutoa mabasi asubuhi,na bado alikuwa anapelekewa moto japo anaanzia nje.
Mchina pumzi fupi,hawezi ligi,na mara nyingi sana hao Newforce/Deer ili akae kwenye mkeka wa Nsalaga huwa hashushi abiria pale Chimala,mashine inapita kama ya wizi wakati Sauli anashusha na bado atapelekewa moto kolikoli hadi kufika pale Nsalaga/Uyole ambapo mikeka ya Mbeya inachukuliwa.
Sheikh Rama wa DPK,au Linyama wa DPK pia zamani DJQ,wanaelewa kabisa moto wa Sauli na kama kumla wanavizia sehemu za kushusha abiria,wapo tayari wakukodie bodaboda ikurudishe ili tu akae juu kwenye mkeka.
Mchina akipata chuma ya maana ulimi lazima uende nje,mnakumbuka BOMBASTIC ya Kisbo chini ya usimamizi wa Bob dere Bubu (baadaye akahamia kwenye CONFIDENTIAL CQX)ya Kahama ilivyomsumbua Newforce/Deer safari za Mbeya?
Shortly ni kuwa anayemuweza Sauli ni KLM,au Rungwe na zile Gemilang zake japo nayeye ameshaziuza nyingine kwa Sauli.
Kuna mwamba yupo benchi sasahivi,anaitwa Mwanyilu,huyu hadi kamanda Muslimu anamfahamu kwa kupeleka mioto.
Sauli inauwezo wa kupanda kitonga huku inapiga alarm ya overspeed,sio hatari tu bali ni zaidi ya hatari wakuu.
Sent from my SM-A107F using
JamiiForums mobile app