Wauzaji wa bidhaa za forever living mnaboa sana!

Me mpenzi wangu alijiunga bila kunambia jion anarudi na hizo story ananishawish ninunue pafyum laki na nusu sijui na vinininini? Nikamwambia unahitaji mtaji ufanye biashara ya maana niambie ila sio huu upumbavu na kujivua akili
 
Walinitoa mbagala mpaka Millenium tower sina hata hamu nao wale jamaa.Hivi kwa mtazamo wa kawaida unaweza kuuza product ya laki 3 kwa mkaazi wa mbagala,
Hawangalii aina ya wateja wala
 
Hahahaha nlikitana na mdada mkali bank flan hv kumsalimia tu nikajibiwa Kwa bashasha nkajua zali mwsho wa siku si tukabadilishana no kilichofuatia hata siendelei

mkuu hata mimi nlikutana na mdada mmoja mkali saaana quality centre nikaongea nae vizuri kweli kweli nikajua huyu

nagegeda tukawa tunachati fresh sana baada ya kama week hivi kaniambia kuna seminar ya biashara Etina pale

niende,nikaone niende kwenye seminar ya biashara ya mtoto afurahi kufika pale mtu amepanda anasema kuna Safari ya UK

ukileta watu wa nne wajiunge forever aaaargh shite
 
Hahahaha watu wa forever wana Hatar sn
 
Nakumbuka nikiwa chuo kuna dada alinikokota mpaka makumbusho na hakunambia ni semina ya kitu gani.
Bahati nzur tulifika kwa kuchelewa, nlikuwa na njaa sana nkala chips kavu nikatembea kwa mguu mpaka mwenge.

Siku nyingine yule dada kanijia na mavidonge nkamwambia ayanywe mwenyewe ila sio mimi.
 
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] kumbe ishakutokea mimi chuo alikuwepo dada mmoja mzuri nikawa nataka nimwage mistari asianze kuniletea mahubiri ya foreverforever alinipiga kibuti nikashindwa kuadapt gemu yake kabisa!
 
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] kumbe ishakutokea mimi chuo alikuwepo dada mmoja mzuri nikawa nataka nimwage mistari asianze kuniletea mahubiri ya foreverforever alinipiga kibuti nikashindwa kuadapt gemu yake kabisa!
Acha tu aisee, mi mwenyewe alinambia ni surprise nikajua leo nakula ubwabwa kwa mkono.
Nlipoona mwisho wake nlikasirika japo sikutaka kumwonesha wazi na nauli yangu nikapoteza bure, nliishia tu makiss mengi...
 
Ivi ile mifano ya presentation zao ni kweli? Yaan ukikutana na mwongeaji na akikutolea mifano km unapesa siku ileile unajiunga...
Nakumbuka mwaka 2014 lecture wangu wa chuo alitualika baadhi ya wanafunz km wa5 kwenye semina pale makumbusho kumbe na yy kaingzwa kwenye hii biashara ss kufika pale ndio kukuta mdada mkali hatariiiiii anaprezent hiyo na kutoa mifano kedekede ya waliofanikiwa safar zao za njee kwenye mashamba ya hzo dawa yaan kila sehemu kafka yule dada na magar yao ya dhaman enz hizo ilikuwakuingia ni lak7 nikafikiriaa kidogo nipeleke ada akil za kuambiwa nikachanganya na zakwangu nikasema hapana nw it's not a right time mpaka nimalize chuo ili niwauzie makazn huko maana wanafunz hawez kununu lipstik moja elf40
Kuna dogo mmoja akajiunga na yule aliye muunga akamwahid km unakonection za watu weng miez 6tu utakuja chuo na Harriya au Morano na tht tm Diamond alikuwa amemnunulia Wema Morano hahahahahaha dogo aliacha mpaka chuo kwajil ya kusaka wateja mtaan na masemina yao ila nw kaona ni utumwa karudia chuo sehemu nyngne
 
Teh forever juice inawekwa kwenye maji yenye iodine yanabadilika rangi na kuwa meupe
Mafuta ya samaki yanawekwa ndani ya kikaratasi hivi kinayeyuka unaambiwa ndio hivo Mafuta mwilini yanayeyuka
Hata kama..... Mie uongo wao unanichefua hata bidhaa sizitaki teh na hiyo hela ya kununua make up elf 70 sina
 
Mi sitaki wasikia na wakinisumbua nawaandikia bango mpangoni
 
Iliwahi nikuta kwa GNLD kama uwa wanaambizana yani. Nilitoka ile wanaanza tu kuelezea products zao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…