Wazazi wazembe wanatoa Elimu kama Urithi, Sheria ya Mirathi inakataa Elimu sio Urithi, Biblia inataka baba kuacha Urithi

Wazazi wazembe wanatoa Elimu kama Urithi, Sheria ya Mirathi inakataa Elimu sio Urithi, Biblia inataka baba kuacha Urithi

Mbona unajitekenya na kucheka? Si umeongelea urithi kiafrica Africa? Waafrica wanazaa watoto wengi bila kujari rasilimali za kuwakuza! Bado elimu ndo mkombozi na mbadala!

Elimu sio Urithi mbona unakichwa kigumu Mkuu!

Hivi unaweza wapa watoto chakula ati ndio useme Urithi,
Elimu ni basic need Kwa mtu inayomsaidia kutumia Rasilimali.

Mzazi unapaswa uache Urithi WA rasilimali ambazo mtoto atazitumia kuendesha maisha yake baada ya kupewa elimu.
 
Mlee mtoto katika njia nzuri na ipasayo
Mpe elimu kama haki yake ya msingi
Mfundishe kupambana/ kujitegemea katika kujitafutia mali zake asitegemee urithi tu

cc Smart911
Tusitoke nje ya mada
Swala la kumfundisha mtoto kupambana au kutegemea urithi is UP TO YOU kama mzazi, Point ni wazazi wanatakiwa kuwatengezea watoto mifumo ya kurithi kitu cha kuendelea kuzalisha fedha au mali si kutoa sababu za kusema ELIMU NDIO URITHI...naona wenzetu kama waarabu wamefanikiwa katika hilo.

Rejea kitabu cha Mwanzo Katika biblia Yule mtoto alieomba urithi kwa babake akaenda kutumia mali ovyo kisha alirejea...ALIOMBA URITHI KWA BABA YAKE KAMA HAKI YAKE NA AKAPEWA.
 
Sijui hata mada yako unaielewa! Kwaeli!


hoja yangu ni kwamba Elimu sio Urithi

Hivi unaweza wapa watoto chakula ati ndio useme Urithi,
Elimu ni basic need Kwa mtu inayomsaidia kutumia Rasilimali.

Mzazi unapaswa uache Urithi WA rasilimali ambazo mtoto atazitumia kuendesha maisha yake baada ya kupewa elimu.

Elimu bila Rasilimali ni Sawa na mdomo pasipo Meno.
 
Kuna familia moja baba alikuwa fundi cherehani na mama anauza genge walikuwa wanaishi gongolamboto miaka ya 1980s. Walikuwa wanaishi nyumba ya kawaida sana ndogo kiasi kwamba watoto walikuwa wanalala sebuleni. Na sisi tulivyokuwa tunaenda kuwatembelea kutoka kijijini tulikuwa tunalazwa sebuleni tena kwenye mkeka asubuhi sana mnaamka! Huyo mzee alikuwa mkali kuwaamsha watoto kwenda shule! Alikomaa nao hao watoto kwa shule za serikali mpaka wote wakapata shahada na wengine wakabakizwa chuo kuwa lecturer! Sasa hivi hiyo familia ni tajili kwasababu watoto waliwahamisha wazazi wao na kuwajengea mjengo huko tegeta eneo kubwa! I salute elimu! Shikamoo elimu! Masikiniwanalishwa uongo kuwa elimu sio kitu! Waache watakuwa walinzi kwenye magate ya walioshiba!
 
Haya sasa! Hayp mashamba makubwa ya kuwakatia watoto wakalime bado yapo? Hata kama yapo bado yanarutuba ya kuotesha na kuzalisha chakula cha kushiba? Bado elimu ndo urithi mbadala wa mashamba! Ukimpa elimu atasoma na kuelewa ulimwengu wa sasa na kama anajitambua atajitafuta nakujipata!
Kwamba hujui kwamba kuna ardhi yenye rutuba Tanzania?
 
Mjumbe naona unataka tuendelee kukaa na Watoto wetu kwenye viuno bila kuwaleta Duniani 🤗

Tukijitahidi sana tufanye kama wenzetu Kataa Ndoa wafanyavyo, kufunga Ndoa na Sabuni na Kopo la mafuta 😜

----------
Umefanya vizuri kutukumbusha, ila Kwa kuongezea ni vyema Kwa Dunia ya sasa kuwapa watoto urithi wote wa Elimu pamoja na Mali.

Unaweza kuwaachia mali, lakini Kwa kukosa kwao Elimu Dunia wanaweza kufeli kuziendeleza.

Binafsi nataka nifate nyayo za Mzee Ngoma pale Mwenge ama Mzee Mengi, pamoja na kuwaachia Mali Watoto wao lakini pia aliwekeza kwenye Elimu zao.

Watoto wa Mzee Ngoma ndiyo Madaktari pale Hospitali ya Mama Ngoma, Mwenge

Vivyo hivyo Watoto wa Mzee Mengi ndiyo Wasimamizi na Waendeshaji wa biashara za Baba yao.

Biblia pia inasema kwenye Kitabu cha Mithali 1:5 "Mwenye Hekima asikie na Kuongezewa Elimu....."

Pia kwenye Mithali 4:13 "Mkamate sana elimu, usimwache aende zake"

Kuhitimisha hili, ni kuwa wakati tunawaandalia Urithi wa Mali Watoto zetu ni vyema tusiache kuwaandaa pia KiElimu.
 
Mkuu MKATA KIU

Kwanza kabisa andiko hili ni zuri, ila huenda kuna kitu kidogo naona hakipo sawa.

Umezungumzia kipindi wazee wetu walikuwa wakiwaachia urithi watoto wao na kipindi cha sasahiv wazazi wetu wakitupa elimu.

Mosi, unaongelea vipindi tofauti hapa,kipindi hicho wazee wa wazee wetu hata elimu ilikuwa ni jambo gumu, hivyo mtoto anakuwa katika kusimamia mali za mzee wake.mfano kuchunga ngo’mbe na mashamba, kijana tangu akiwa mdogo mpaka anakuwa mkubwa anafundishwa ni namna gani ya kusimamia mali ya kwao.

Hivi sasa ni kipindi cha teknolojia tunapatiwa elimu mbadala wa yale yaliyofanyika miaka ile. Elimu ina upana wake, kuna watu wanasomea injinia, ufundi wa magari, majengo, udereva na vitu vingi.

Kama mtu yupo na ujuzi fulani kutokana na elimu tayari ni urithi huo.
Lakini mifumo mibovu ya elimu ya sasa inatengeneza “entitlements mentality” hasa kwa sisi vijana.

Tukitegemea kwamba tutapomaliza shule tutapata favor ya kuwa sehemu fulani sababu ya elimu yetu.

Huwezi kumfananisha kijana aliyeshinda home tangu mdogo akisimamia ngo’mbe na kukosa elimu na aliyeshinda darasani hajui hata ngo’mbe anachungwa vipi.

Elimu ni urithi.
 
Mkuu MKATA KIU

Kwanza kabisa andiko hili ni zuri, ila huenda kuna kitu kidogo naona hakipo sawa.

Umezungumzia kipindi wazee wetu walikuwa wakiwaachia urithi watoto wao na kipindi cha sasahiv wazazi wetu wakitupa elimu.

Mosi, unaongelea vipindi tofauti hapa,kipindi hicho wazee wa wazee wetu hata elimu ilikuwa ni jambo gumu, hivyo mtoto anakuwa katika kusimamia mali za mzee wake.mfano kuchunga ngo’mbe na mashamba, kijana tangu akiwa mdogo mpaka anakuwa mkubwa anafundishwa ni namna gani ya kusimamia mali ya kwao.

Hivi sasa ni kipindi cha teknolojia tunapatiwa elimu mbadala wa yale yaliyofanyika miaka ile. Elimu ina upana wake, kuna watu wanasomea injinia, ufundi wa magari, majengo, udereva na vitu vingi.

Kama mtu yupo na ujuzi fulani kutokana na elimu tayari ni urithi huo.
Lakini mifumo mibovu ya elimu ya sasa inatengeneza “entitlements mentality” hasa kwa sisi vijana.

Tukitegemea kwamba tutapomaliza shule tutapata favor ya kuwa sehemu fulani sababu ya elimu yetu.

Huwezi kumfananisha kijana aliyeshinda home tangu mdogo akisimamia ngo’mbe na kukosa elimu na aliyeshinda darasani hajui hata ngo’mbe anachungwa vipi.

Elimu ni urithi.

ninachomaanisha mzazi wa zama zozote anawajibika kuacha urithi wa mali kwa mwanae. elimu ni basic need kama kumpa mtoto chakula.

Hivi unaweza wapa watoto chakula ati ndio useme Urithi,
Elimu ni basic need Kwa mtu inayomsaidia kutumia Rasilimali.

Mzazi unapaswa uache Urithi WA rasilimali ambazo mtoto atazitumia kuendesha maisha yake baada ya kupewa elimu.

Elimu bila Rasilimali ni Sawa na mdomo pasipo Meno.

Baba yake Mo dewji kamsomesha Mo dewji IST na chuo kikuu kikubwa duniani.. ila bado akaja kumpa urithi wa mali yaani kampuni ya Mohammed Enterprises
 
Tusitoke nje ya mada
Swala la kumfundisha mtoto kupambana au kutegemea urithi is UP TO YOU kama mzazi, Point ni wazazi wanatakiwa kuwatengezea watoto mifumo ya kurithi kitu cha kuendelea kuzalisha fedha au mali si kutoa sababu za kusema ELIMU NDIO URITHI...naona wenzetu kama waarabu wamefanikiwa katika hilo.

Rejea kitabu cha Mwanzo Katika biblia Yule mtoto alieomba urithi kwa babake akaenda kutumia mali ovyo kisha alirejea...ALIOMBA URITHI KWA BABA YAKE KAMA HAKI YAKE NA AKAPEWA.
Hapo mwisho nimesema vizuri kwamba asitegemee urithi tu mrithishe mali/ vitu pia muelekeze kupambana utamsaidia sana!
Asipokua na akili ya maisha hata huo urithi anaeza u miss use badae akataabika

cc Smart911
 
Baba yake Mo dewji kamsomesha Mo dewji IST na chuo kikuu kikubwa duniani.. ila bado akaja kumpa urithi wa mali yaani kampuni ya Mohammed Enterprises
Mkuu,

Katika mfano wako huu sasa.

Kwanza mo dewji amekulia katika familia ya biashara hivyo practical anaelewa nini anafanya.

Ndicho wanachofanya sasahiv makabila ya wakinga iringa, pia watoto wa wahindi na wachaga.

tatizo si kuacha mali, Tatizo ni jinsi ya kuzisimamia mali.

Mtoto hana basic yoyote kuhusu usimamizi wa mali Halafu baba anaacha mali within 2years unamkuta yupo kijiweni anacheza bao na mali zote kashapoteza.

Tena wapo wengi tumeona tunakua wanashinda kwenye mageti na mbwa wakali lakini wazazi wanapoondoka vyote vinapotea.

Elimu ni urithi hili haliwezi kupingwa.
 
Haya mambo ya urithi sijui blahbkah yako Africa! Ulaya mtoto akifikisha miaka 18 anatakiwa atoke kwa wazazi akapambane! Labda wazazi wakifariki ndo hayo mambo ya next of kin na urithi yanakuja! Mtoto anatakiwa umpe elimu ya kujitambua na kupambana!

Kama nchi gani ya Ulaya ambayo haina hayo mambo. Isijekuwa unaangalia tamthilia ndio unaiita Ulaya
 
Screenshot_20240208-122400.png
 
Back
Top Bottom