Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Wazee wa ‘Road Trip’ mpo?

Na mpaka leo hajaipatia dawa ile Evo na kabla hajapumua kuna mwamba mwingine toka Mwanza nae kaingiza Evo matata kuliko ile ya kwanza,ni mapenzi na ujana kwa sheria hizi JMT na aina ya barabara zetu sioni sehemu ya kumwaga moto kuzidi 240kph
Hahahah Evo hadi wajapan wamezipiga ban maana zimezidi kiwango cha fujo 😂😂😂! Hawataendelea kuzizalisha tena.
 
Hii bila shaka ni Morogoro Road kama si Iringa road

😊😊😊

Na hapa je....?

6B86E628-EDEC-400F-91A9-4C1B3333A743.jpeg


😜
 
Huu mwaka usiishe kabla hatujapiga trip moja ndefu....

This is a deal done Bataringaya 😋.

Just set a date on your schedules and don’t forget to set the reminder about the trip.

Jiandae kulishwa matunda ukiwa unaendesha. Ila ikifika zamu yangu usinichokoze tafadhali, uvumilivu wangu ni sifuri nikichokozwa 😜.

Have you ever been in Kapilimposhi...!???
 
Nimecheka sana manake umenikumbusha mbali mnoo 😁 😁 😁 .Kuna mzee alishanisimulia chanzo cha kuacha kunywa bia za kampan na marafiki.Huyu mzee alipark gari mtaroni akiwa amelewa usiku karibu na petrol station,Sasa ameamka asubuh anatafuta gari aende kazini,gari halionekani ila ufunguo anao,anakwambia ilifikia hatua akatafuta gari kwenye suruali 😁😁😁,ghafla washkaji zake wanampigia simu mbona kaegesha gari mtaroni karibu na petrol station ndo akili zikamrudi na kukumbuka
Kuna dereva alitelekeza gari la ofisi vichakani baada ya kuzidiwa na kvant akatafuta boda akarudi kulala. Asubuhi maboss wake wanampigia hapokei cm.. basi wakajua kapata shida wakatafuta gari kwa GPS wakalikuta vichakani. Dereva kalala home kwake hana habari saa 2 asubuhi sijui ile soo ilishaje uko ofisini maana Gari yenyewe Landcruiser hardtop.
 
Back
Top Bottom